JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................359-360
Sura ya: 359
Chester akakaa kwenye sofa lililopo mkabala na Lisa. Kulikuwa na tabasamu angavu usoni mwake, lakini macho yake yalitoa mchomo mkali wa hasira. “Nipe kitabu asilia cha nyimbo.”
"Inaonekana Cindy alikuja kulalamika kwako." Lisa alitabasamu kwa utulivu. "Ni nini kizuri unakipata kwa mwanamke mnafiki kama huyo?"
"Ana mapungufu mengi, lakini bado ni mwanamke wangu," Chester alisema, "Lisa Jones, usiende kinyume nami. Familia yako ya Ngosha haiwezi kumudu matokeo ya kumkasirisha tajiri namba tatu wa nchi hii. Hujatosheka tu kwa kusharirisha nyuso za watu wengine usiku huu?”
Lisa alitabasamu kwa dhihaka. "Chester Choka, kama kijana tajiri namba tatu wa nchi, macho yako ni mabaya sana. Unapaswa kubadilisha miwani yako."
Macho ya Chester yaliangaza kwa ukali. "Uvumilivu wangu una mipaka yake, Lisa."
“Suala kati yangu na Cindy linaweza kuchukuliwa kuwa chuki ya zamani. Sikutaka kueleza yaliyopita, lakini… ni kosa lako kwa kuwa mkali sana, Dokta Choka.” Lisa alitabasamu kwa ujeuri. "Kwa neno moja tu, ulimfukuza baba yangu katika hospitali yako."
Chester aliganda na kukunja uso. "Sikujua kuhusu hilo."
“Hata ungejua, ungemruhusu Alvin afanye hivyo. Inaeleweka kwamba nyinyi watatu ni ndege wa manyoya yanayofanana.” Lisa alisimama, macho yake mazuri yakionekana kuwaka kwa hasira. “Unataka nikupe kitabu cha nyimbo asilia? Dokta Choka, lazima uwe unaota. Unafikiri mimi ni mmoja wa wafanyakazi wako? Hakika, ikiwa unataka kuiondoa familia ya Ngosha, endelea. Sitajali hata kidogo. Sio kama sina pesa hata hivyo. Hata hivyo, ngoja nikukumbushe. Usiende kutafuta mchawi na kurudi nyumbani ukiwa umerogwa. Mtazame Alvin sasa.”
Chester, ambaye hakuwahi kamwe kushindwa waziwazi hapo awali, alikasirika sana hivi kwamba akavuta sigara mfululizo.
“Chester Choka, miaka mitatu iliyopita, nilishukuru sana kwamba ulipata daktari wa kumuokoa baba yangu, lakini baada ya kugundua kuwa Charity aliruka baharini na kufa, nilipoteza kila sehemu ya shukrani niliyokuwa nayo kwa ajili yako. Ulimchukia mwanamke asiye na hatia na bado unamchukulia mwanamke kama Cindy kama hazina. Lazima kuna shimo kwenye ubongo wako." Baada ya Lisa kumaliza kuongea, alitoka bila kugeuka nyuma.
Nyuma yake, Chester alipiga mkono wake kwa hasira na glasi ya mvinyo ikaanguka chini. Uso wake ulikuwa umekakamaa kwa hasira.
Rodney akapigwa na butwaa. Kati ya hao watatu, ni Chester pekee ndiye angetabasamu na kuficha machungu yake moyoni mwake. Kwa kawaida hakuwahi kuonyesha kama alikuwa na furaha au hasira. "Hapana, Lisa alisema nini kilichokukasirisha?" Rodney aliuliza swali lililoambulia ukimya tu.
Hata hivyo, Alvin alicheka na kutabasamu kidogo. “Angalau sasa unajua kwanini mimi hukasirishwa sana na huyo mwanamke.”
"Chester, usiwe na wazimu." Rodney alimfariji. "Kwa neno moja tu, sio shida kwako kuangusha familia ya Ngosha na Mawenzi Investments."
“Unadhani familia ya Ngosha ni kuku kwenye soko la mbogamboga? Hawawezi kuuawa kwa neno moja tu.” Chester alimtazama kwa ukali. “Si rahisi kihivyo. Lisa Jones wa sasa hana doa dhaifu.”
Alvin alipigwa na butwaa, Rodney akasema, “Hilo haliwezekani. Mtu anawezaje kutokuwa na doa dhaifu?"
"Labda mtu hatakuwa tena na maeneo dhaifu baada ya kupoteza kila kitu," Chester alisema kwa kufikiria.
Alvin alikunja uso. Moyo wake ghafla ukahisi kukosa raha. Aligeuka nyuma kwa umati wa watu na kumtafuta Lisa bila kujua, lakini alimuona tu akiondoka pamoja na bwana mdogo wa familia ya Malugu.
Kupitia madirisha ya sakafu hadi dari, aliweza kuwaona watu hao wawili wakizungumza na kucheka huku wakitoka pamoja. Alikaribia kuisaga kwa mikono glasi ya mvinyo mikononi mwake.
Dakika tano baadaye, hakuweza kukaa tena. Alimwambia Rodney amrudishe Sarah baada ya karamu na akatoa udhuru wa kuondoka mapema. Alilifuata gari la Bwana Malugu mpaka waliposimama kwenye sehemu ya kuegesha magari mbele ya majumba ya Karen Estate. Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa nusu saa, bado hakumuona Lisa akishuka kwenye gari.
Taa za gari zilikuwa zimewaka, lakini hakujua walikuwa wanafanya nini.
Walikuwa na mazungumzo gani kwa muda mrefu hivyo? Inaweza kuwa…
Alvin alipofikiria kuwa Lisa na Erick Malugu wanaweza kuwa wanafanya jambo lile lile lililotokea kati yao siku kadhaa zilizopita kwenye gari, moyo wake ulianza kumuuma papo hapo. Alishindwa kuvumilia akatoa simu yake ili apige.
Hazikupita hata dakika kumi, polisi mmoja aliendesha gari na kugonga kioo cha gari la Bwana Malugu.
“Kuna jambo?” Erick alishusha dirisha.
Ofisa huyo aliwatazama mwanamume na mwanamke waliokuwa ndani ya gari, akisema kwa mshangao, “Mtu fulani aliripoti kwamba mnafanya biashara isiyofaa kwenye gari.”
Ni aina gani ya biashara zisizofaa ambazo mwanamume na mwanamke pekee wanaweza kufanya ndani ya gari? Maneno ya Erick na Lisa yakawa mazito kutoka vinywani mwao.
Lisa aliuliza kwa mshangao. "Haya umeona kuna biashara gani inayoendelea hapa?"
"Samahani." Afisa huyo alimlaani mtu aliyewaripoti. Mtu huyo lazima awe mwendawazimu.
Afisa huyo alipoondoka na Erick akijiandaa kuendelea na mazungumzo, gari la maji lilipita ghafla likimwaga maji kwa fujo. Kwa vile dirisha lilikuwa limeachwa wazi, Erick, aliyekuwa ameketi upande huo, alilowa maji. Alikasirika sana hata uso wake ukawa mbaya ghafla.
Lisa alizuia kicheko chake na kusema.“Samahani, naona bora urudi nyumbani ukaoge,”
"Ndio, labda kuegesha gari langu hapa kumemkwaza mtu." Erick alitabasamu kwa jazba. Alikuwa mtu mwerevu. Lisa alikuwa na wafuatiliaji wengi usiku huo, lakini ni yeye tu ndiye aliyepata nafasi ya kumpeleka nyumbani, kwa hivyo lazima kulikuwa na wanaume wengi waliomwonea wivu.
“Hapana, lazima nimemkosea mtu. Huenda kuna mtu ambaye atakuja kunisababishia matatizo baadaye.” Lisa alimkabidhi kitambaa na kutoka kwenye gari kuelekea kwake.
Akiwa anakaribia kubonyeza lifti, ghafla mkono mkubwa uliibuka kutoka nyuma na kuzuia kitufe cha lifti. Kisha, harufu ya kupendeza ya mtu aliyemzoea ilimfunika kutoka nyuma.
Lisa hakutazama juu na akasema kwa kawaida, "Baada ya shida uliyotuletea, bado haujatosheka tu?"
“Nimewaletea shida gani?” Kicheko cha kejeli cha mtu huyo kilisikika juu yake. Ilionekana kana kwamba hakukubaliana kabisa.
Lisa akageuka na kuinamisha kichwa chake. "Uliripoti polisi kwamba nilikuwa na 'biashara zisizofaa' kwenye gari na ukatuma mtu wa kummwagia maji Bwana Malugu. Usiseme kuwa si wewe.”
"Kwanini nifanye mambo ya kipumbavu hivyo?" Alvin alijifanya kama amesikia mzaha na kuvaa tabasamu la kejeli. Asingekubali kufanya jambo kama hilo hata kama angepigwa hadi kufa. Ingekuwa ni kujifedhehesha sana.
"Lazima kuna mtu aliwaona mmekaa kwenye gari muda mrefu na akaripoti kwa polisi kwa nia njema." Macho ya Alvin yalipita kwenye sehemu kubwa ya kifua chake iliyo wazi. “Jiangalie. Umevaa hivi na unakaa kwenye gari na kijana mhuni kama Erick Malugu. Huogopi kwamba watu watakuita hujiheshimu?”
"Kwa hiyo ikiwa mimi sijiheshimu? Tayari tumeachana, kwa hivyo hayakuhusu, ndiyo maana ninakuita mmbea." Lisa aliunyosha mkono wake na kubonyeza kitufe cha lifti.
Alvin aliutazama mgongo wake mzuri na kuhisi moyo wake ukimuuma kwa chuki. “Unafikiri Bwana Malugu atafanya nini akijua kwamba tulilala kwenye gari langu siku chache zilizopita?”
“Labda atanionea huruma zaidi. Baada ya yote, wewe ndiye unakaribia kutulia na kuanzisha familia.” Uso wa Lisa ulikuwa umejaa dhihaka. “Alvin Kimaro, huoni kuwa wewe ni msumbufu? Tayari tumeachana, na ni wewe uliyenilazimisha kusaini talaka. Sarah na wewe mnafanya taratibu za kupandikiza mimba, lakini bado unaendelea kunifuatilia. Usiniambie kwamba huwezi kuniacha niende, au labda…Unamtaka Sarah, lakini unanitaka na mimi pia.” Alimsogelea ghafla. Sauti yake ya kuroga ilikuwa kama sumaku.
Alvin alimsukumia mbali kwa nguvu na kumdhihaki, lakini umahiri wake wa kucheza piano na uimbaji wake wa ajabu usiku huo uliangaza akilini mwake ghafla—pamoja na kumwona akicheza na wanaume wengine na kumwona akiongea na kucheka na wanaume wengine…Ghafla aligundua kuwa alikuwa ametumia zaidi ya usiku huo kumwangalia.
Walikuwa wametia saini karatasi za talaka. Lisa alikuwa huru kabisa. Angeweza kuwa na yeyote anayetaka kuwa naye. Hata hivyo, wakati Bwana Malugu na yeye walipokuwa ndani ya gari kwa muda wa nusu saa tu, alitaka kukwaruza moyo na mapafu yake na kuyatoa nje! Alijua kuwa hakutakiwa kuendelea kuwa hivyo. Ingemuumiza Sarah, na haikuwa haki kwake pia. Hata hivyo, Alvin hakuweza kujizuia.
Sura ya: 360
"Kwani kuna ubaya kuwa na nyie wote?" Alimshika Lisa mabegani na kumkandamiza ukutani, macho yake yakiwa yanawaka moto. “Lisa, lazima nikubali kwamba wewe ni mwanamke wa kuvutia sana. Ni mimi ambaye sikukufahamu vya kutosha hapo awali.”
Kisha, akalazimisha kumbusu Lisa mdomoni, lakini, Lisa aligeuza kichwa chake na kukwepa. Midomo yake iliangukia kwenye shavu lake na harufu nzuri ya mwili wake ikamshika na kumfanya ashindwe kujiondoa.
“Alvin Kimaro, unakumbuka jinsi ulivyowaagiza kwa hasira walinzi wako kunikandamiza chini na kunilazimisha kutoa cheti cha ndoa wiki iliyopita? Unakumbuka jinsi ulivyonilazimisha kusaini karatasi za talaka? Bado unakumbuka jinsi ulivyokuwa jeuri wakati huo?"
Lisa alisema kwa upole huku akionyesha huzuni. “Kweli uliponibeba siku ile kutoka kwenye gari sikuwa nimelala. Nilihisi tu kama ni ndoto na sikuthubutu kuamka. Baada ya wewe kuondoka, nilifikiri juu ya mambo mengi na kuhisi kuwa labda bado kulikuwa na nafasi kwa ajili yetu. Lakini siku iliyofuata, ulikuja kwangu kutoa talaka. Hukuniachia hata chembe ya heshima. Wewe…” Karibu na mwisho, sauti yake iligoma, lakini bado alijifanya kuwa na nguvu.
Mwili wa Alvin ulikuwa mgumu. Mwili wake ulionekana kuwa na kikomo, na kumfanya ashindwe kujisogeza.
Lisa alimsukumia mbali. "Baada ya hapo, nilikuona na Sarah ulipokwenda kufanya upandikizaji wa mimba hospitalini. Kwa vile umeamua kuwa naye, kwanini huwa unarudi kuniumiza? Kati yangu na Sarah, mimi ndiye jalala la hasira zako na tamaa zako za ngono. Ulisema unanitaka, lakini kati yetu sisi watatu, ni lazima nikubali tena na tena kwamba ni mimi pekee ndiye ninayeumia zaidi. Hakuna anayeweza kujifanya kana kwamba hana wivu, sivyo? Lakini nikimuumiza Sarah, unanipiga na kunikaripia tena.”
Lisa alijiinamia na kulia ghafla bila kujizuia. Alvin alimtazama na ghafla akahisi uchungu ukimjaa kifuani. Kwa kweli, alijua pia kwamba alikuwa akimtendea kinyume na haki. Hata hivyo, alikuwa alishikilia sana msimamo wake na kudharau ushawishi wa mwanamke huyo kwake.
"Simama." Alvin alinyoosha mkono kumshika, lakini, Lisa alimsukumia mbali kana kwamba alikuwa na wazimu. “Ondoka. Sitaki kukuona. Niache na maisha yngu, sawa? Sitaki kujihusisha na wewe na mkeo tena.” Aliangua kilio cha uchungu tena na tena.
Mwili wa Alvin ulijhisi kuganda. “Sawa, nitaenda.”
Aligeuka taratibu na kutoka nje ya mtaa huo hatua moja baada ya nyingine. Hapo awali, alikuwa akifikiri kwamba anachukizwa na Lisa. Hakuwahi kufikiria kwamba hata siku moja angeweza kuguswa naye.
Wakati mwingine, alimchukia sana hadi akakosa raha kabisa, lakini kwa sababu fulani, kamba za moyo wake zilipigwa kwa namna fulani. Ilikuwa ni huruma kwamba alikuwa amechelewa kukutana naye.
Alvin alikaa kwenye gari na kuwasha simu yake. Kwenye skrini kulikuwa na picha ya Lisa ambayo alikuwa ameihifadhi kutoka kwenye mtandao siku chache zilizopita. Aliificha mahali fulani kimya kimya.
Usiku kucha, Alvin alikaa kwenye maegesho ya magari ya Karen Estate na kuvuta sigara. Hakujua kuwa wakati huo tasnia ya burudani ilikuwa imetikisika.
Saa saba usiku, menejimenti ya Cindy ilifanya mkutano wa dharura na hatimaye wakatoa tangazo rasmi kwa umma. [Bila kujua, imepita miaka mitano tangu niingie kwenye tasnia ya burudani. Mwaka huo, 'Pepo ya Ndoto' ilinifanya kuwa maarufu kote Afrika Mashariki. Kwa kweli, kwa miaka mingi, nimekuwa nikimshukuru kimya kimya mtu mmoja moyoni mwangu na huyo ni rafiki yangu mzuri, Lisa Jones. Yeye ndiye aliyeniandikia album nzima ya 'Pepo ya Ndoto'. Ninashukuru sana kukutana na rafiki kama yeye katika maisha yangu. Alikuwa akijiweka kimya na hakutaka kujionyesha, lakini kwa kuwa sasa anajulikana kwa umma, sitaki kuficha kipaji chake tena. Ninataka kumpa zawadi ambayo nilitunukiwa wakati huo. Hii ni tuzo yake. Lisa, nakupenda.]
Baadaye, Cindy alichapisha tuzo kadhaa na picha aliyokuwa amepiga akiwa na Lisa shuleni. Katika picha, wawili hao walikuwa wakitabasamu sana na wakionekana kuwa na urafiki wa ajabu.
Wanamtandao walilipuka.
[Kwa hiyo Lisa na Cindy walikuwa marafiki wakubwa. Tizama toka wakiwa shuleni walikuwa warembo kweli!]
[Si hivyo tu. Aliandika hata nyimbo za Cindy. Ni zaidi ya urafiki!]
[Hakuna mtu atakayezungumza kuhusu kipaji cha muziki cha Lisa? Hivi, kuna jambo lolote ambalo hawezi kufanya? Kwa kweli, Lisa shikamoo!]
[Cindy ni mkarimu sana. Amemkumbuka rafiki yake wa karibu na kuelezea alivyomsaidia?]
Lisa alipoamka asubuhi na kuona maoni ya wanamtandao, alitabasamu.
Kama alivyotarajia, Cindy angefanya kitu haraka ili kulinda hadhi yake ndogo iliyokuwa imebaki isije ikapotea yote.
Alitoa simu yake bila haraka na kumpigia Sam. "Sam, umemaliza nilichokuomba ufanye?"
“Bila shaka. Unadhani mimi ni nani? Ninatawala Dar Es Salaam. Ni kazi ndogo sana kupata kitu chochote kutoka kwa Janet Kileo. Kwa jinsi familia ya Kileo ilivyo dhaifu sasa, Janet ananitazama kama anamtazama babu yake—”
“Unaweza kunitumia sasa hivi?” Lisa alikatiza majigambo yake.
“Hakika. Una akili sana. Huenda Cindy alisahau kwamba aliacha mambo mengi mabaya alipokuwa akijaribu kuwalambalamba Lina na Janet huku Dar Es Salaam.” Sam alimtumia rekodi.
Lisa mara moja aliipachika chini ya chapisho la Cindy kwenye Facebook.
[Asante kwa kufunua ukweli, Cindy Tambwe, lakini nilikuwa mdogo
na mjinga nilipokuwa pamoja nanyi zamani. Sikujua jinsi ya kuwasoma watu wakati huo. Baada ya mambo mengi kutokea, sithubutu kukuchukulia kama rafiki tena.]
Wanamtandao walipakua na kusikiliza rekodi ambayo Lisa alichapisha kwa udadisi.
Kwenye rekodi hiyo ya simu, sauti ya Janet ilisikika ikisema, “Huogopi kwamba Lisa atagundua unakula chakula cha jioni na mimi? Sisi ni maadui wakubwa."
Sauti ya Cindy kisha ikajibu, “Kwa hiyo ikiwa atagundua? Kwa hali yake ya sasa, hatoki katika ulimwengu sawa na mimi.”
Janet akajibu, “Hiyo ni kweli. Nilisikia kutoka kwa Lina kwamba familia ya Jones ilimfukuza na hana hata mahali pa kukaa sasa. Alikuomba msaada?"
"Alinipigia simu, lakini sikuipokea."
"Haha, vizuri. Hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa. Akikuomba kumkopesha pesa, usifanye hivyo.”
“Bila shaka, sitafanya hivyo. Lakini Pamela huyo mjinga hakika atafanya hivyo.”
Rekodi iliisha ghafla. Hata hivyo, ilitosha kwa wanamtandao kujua rangi halisi za Cindy.
[Hiyo ni sauti ya Cindy kweli?]
[Ni hakika. Ni sawa kabisa na uimbaji wake wa kawaida na sauti yake kwenye vipindi vya Runinga.]
[Kwa hivyo rekodi ilikuwa baada ya Cindy kuwa maarufu. Alimdharau Lisa na kukataa kupokea simu za Lisa au kumkopesha pesa wakati alihitaji msaada zaidi? Ooh! My God, hata yeye ni binadamu? Alichapisha post yake na kusema kwamba Lisa na yeye walikuwa kama dada usiku wa manane. Huo ni unafiki mkubwa!]
[Bora na nyie watu mmegundua kuwa yeye ni mnafiki. Nimekuwa nikisema mara kadhaa hapo awali kwamba Cindy ana nyodo sana. Hana maana na anadharau watu, anajifanya kama yeye ni mungu wa kike.]
[Hata aliwaita wengine wajinga kwa kumkopesha Lisa pesa. Ana utu kweli? Ikiwa Lisa asingemwandikia nyimbo, angekuwa hapo alipo leo?]......ITAENDELEA......
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.
