JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................357-358

Sura ya: 357

Punde, Alvin alikuja upande wa Jack. Aliuliza kwa sura ya huzuni, "Lisa kakuambia nini?"

Jack alimulika simu yake kwa Alvin huku akitabasamu. "Hawezi kula chakula cha jioni na mimi kwa sababu anaenda kwenye miadi yake na Bwana Malugu usiku wa leo, kwa hivyo amenihamishia milioni 40."

Wakati huo, Alvin alijionea huruma mwenyewe jinsi alivyokuwa amekasirika, kukasirika na kukasirika. Lisa alipata pesa hizo kutoka kwake na akamgawia Jack mara moja. Je, alimchukulia kuwa boya?
Subiri, alikuwa ana miadi na Erick Malugu baadaye? Alvin hakuweza kutulia tena.

Baada ya Cindy kumaliza wimbo wake, alisimama taratibu. Alitoka nyuma ya piano na kuinama. Kulikuwa na duru ya makofi ya radi katika ukumbi wa karamu. Wakati huo, Cindy alifurahi sana. Alijua kuwa machoni pa watu hao kutoka jamii ya hali ya juu, alikuwa mtu mdogotu ambaye haonekani. Lakini, alijulikana kwa kila mtu kuwa alikuwa na kipaji adimu usiku huo.

Muda huohuo, alimuona Lisa akielekea kwake taratibu. Ni wawili tu ndio walikuwa wamesimama katika eneo ambalo vyombo vya muziki viliwekwa. Kwa wakati huo, kila mtu alikuwa amemtazama Lisa mrembo na mlimbwebde. Tabasamu la Cindy likalegea.

"Lisa, umekuja mahali pabaya? Hapa ni mahali pa kucheza piano." Cindy alilazimisha tabasamu na kusema kwa sauti ya upole.

“Sikjakosea hata kidogo. Wewe si umemaliza kucheza wimbo wako? Nimezungumza na mratibu. Nataka kujaribu ujuzi wangu.” Nguo ya Lisa iliyojaa almasi ilifuata nyuma yake alipokuwa akiiendea piano na kuketi mbele yake.

Mwili mzima wa Cindy ukakakamaa. Aligeuka nyuma kwa haraka na kusema, “Lisa, watu ambao wako hapa leo si watu wa kawaida tu. Hata mwanamuziki maarufu, Nandy, yuko hapa pia. Si mahali ambapo unaweza kufanya mzaha wako. Ikiwa unataka kucheza piano… unaweza kucheza ukirudi nyumbani.”

“Unadhani nitajiaibisha?” Lisa alitabasamu bila kufafanua.

Cindy akabaki amebana midomo. Hiyo ilipaswa kuwa kinyume chake. Yeye pia alikuwa anamfahamu vizuri Lisa. Lisa alikuwa na talanta ya kipekee katika muziki hapo awali. Walikuwa wamesoma piano na gitaa pamoja wakiwa shule ya sekondari. Wote walisoma kwenye shule ya ‘Dar es Salaam Independent Schools’ kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Lisa aliweza kujifunza kila kitu haraka na mara nyingi alisifiwa na walimu.

Lisa alikuwa akivutiwa sana na muziki kipindi hicho. Ni vile tu alitegemea kuwa mrithi wa kampuni ya familia yao Kibo Group, iliyojihusisha na mambo ya ujenzi, ndipo ilimlazimu kwenda kusomea Uinjinia wa mambo ya kubuni majengo, alipomaliza kidato cha sita. Vinginevyo angekuwa msanii mkubwa tu kwa kipaji chake. Na hata alitunga nyimbo na kumwandikia Cindy baada ya hapo. Lakini, Cindy hakuweza kupima ujuzi wake wa sasa.

Lakini Lisa asingeweza kufanya jambo lisilowezekana mbele ya umati ule wa watu maarufu. Cindy alihisi kutokuwa na utulivu moyoni mwake.
Wakati huo, wageni walianza kuzungumza juu yake pia. Macho yao yaliweka alama ya dhihaka huku wakimtazama Lisa.

Baada ya yote, Cindy alikuwa amemaliza kufunika kwa show kali. Ikiwa Lisa angeimba baada yake, bila shaka angeonekana mzaha.

Melanie alijifanya kana kwamba ana wasiwasi na kusema, “Dada, hii si karamu ya familia ya Ngosha ambapo unaweza kufanya chochote unachotaka. Isitoshe wewe ndiye mrithi aliyeteuliwa wa familia ya Ngosha sasa. Unapaswa kutunza heshima ya familia ya Ngosha.”

"Hiyo ni sawa." Joan Halua alichukua nafasi hiyo na kuunga mkono maneno ya Melanie.

Sarah alipoona kwamba kila mtu amezungumza, alisema kwa upole, “Hii ni kuhusu kucheza piano. Ni tofauti na kubuni majengo, baada ya yote. Una maoni gani, Alvinic?" Alimvuta mwanamume yule mrefu na mtanashati kando yake.

Alvin alikunja uso. Alikuwa amemsikia Lisa akiimba na kucheza gitaa hapo awali. Kwa kweli alikuwa mzuri sana. Angempoteza Cindy, na sauti yake ilisikika vizuri zaidi kuliko ya Cindy alipocheza gitaa. Lakini, hakuwa na uhakika kama ingekuwa hivyohivyo pia ikiwa Lisa angeimba huku akicheza piano. Baada ya yote, kwa kweli hakuwa na uhakika na uwezo wa mapafu ya Lisa na uzoefu wake. Ikiwa mambo yangeenda ndivyosivyo, Lisa angejidhalilihsa kabisa.

"Sina uhakika." Alikaza midomo baada ya kusema hivyo. "Ni suala lake mwenyewe."

“Mwache ajiaibishe ikiwa anataka,” Rodney alisema kwa kejeli, “Nafikiri anajaribu tu kujionyesha baada ya kusifiwasifiwa na wengine kwa siku chache. Anadhani yeye ni mzuri kwa kila kitu.”

'”Namhurumia kweli. Anafikiri kwamba anaweza kumshinda Cindy? Cindy ndiye diva wa Afro-pop."

"Usijali. Mwache afanye kama anataka. Yeye ndiye mrithi wa Ngosha Corporation, kwa hivyo umwacheni avurunde ili tupate sababu ya kumnanga hapo baadaye. Tutamsema hadi atamani kufa.”

Mbele ya maongezi ya umati, Lisa alitabasamu kwa unyonge na kukandamiza key ya piano, na kufanya jumba la karamu litulie.
Alirekebisha kipaza sauti na kusema kwa sauti ya kupendeza, “Huu ni wimbo mpya niliotunga. Leo itakuwa mara yangu ya kwanza kuucheza na kuumba, hivyo natumai kila mmoja atausikiliza.”

“Ana kichaa? Hata alitunga wimbo wake mwenyewe.”

"Labda anamuonea wivu Cindy na anataka kumshinda, lakini Cindy ni mwimbaji haswa."

"Siku hizi, kila mwanamke kijana kutoka kwa familia tajiri anataka kutengeneza nyimbo yake. Muziki umevamiwa kwa kweli.”

Kila mtu aliponong'ona masikioni mwa mwenzake, mlio wa muziki wa furaha ukiambatana na sauti ya key za piano ulisikika polepole.

"Nakuambia, 'simama hapo',
“Ndege inaruka juu ya anga ya buluu,
"Ninakwenda safari,
"Ninakwenda safari ya mbali.
"Machozi yananidondoka kifuani mwangu,
"Mahusiano haya hayataisha,
"Tunafuatilia ndoto zetu za siku zijazo pamoja,
"Huu sio mwisho, ni mwanzo mpya."

Umati ulitulia taratibu na kusikiliza kwa makini wimbo huo mpya. Wimbo huo wa furaha ulikuwa na kidokezo cha huzuni ambacho kilirejelea kuagana. Mara moja uliwakumbusha watu miaka yao ya chuo kikuu ambapo walilazimika kuwaaga wapendwa wao ili waweze kufuata ndoto zao wenyewe. Ilikuwa huzuni kidogo iliyochochea mioyo yao.

Alvin alimtazama yule mwanamke aliyekuwa anang'aa pale jukwaani huku akiwa haamini. Kichwa chake kilikuwa kimeinama chini, lakini mwili wake ulitoa mwanga ambao hakuna mtu angeweza kuuzuia.

Siku zote alikuwa hivi, akimshangaza mara kwa mara. Haishangazi alikuwa amepanda jukwaani akiwa na ujasiri kama huo. Ustadi wake wa piano na sauti vilikuwa bora zaidi kuliko za Cindy.
Sarah aliyaona macho ya Alvin ya kutamanika na nusura aingiwe na wazimu. Alifikiri kwamba Lisa angejifanya mjinga. Hii ilitokeaje? Miaka mitatu iliyopita, alikuwa amemponda Lisa kwa urahisi kama mchwa.
Miaka mitatu baadaye, wanaume wote nchini walikuwa wakimwona Lisa kwa sura mpya.

Cindy aliyekuwa amesimama pembeni ya Lisa alifedheheka sana hadi uso ukabadilika na kuwa mweupe. Hakuna aliyemjua Lisa kuliko yeye kwenye muziki. Ndio, hii ndiyo aina ambayo Lisa alikuwa amefanya vyema. Baadaye, wimbo uliisha kwa noti ya mwisho.

"Ajabu!" Msanii Nandy akiwa ameambatana na mumewe, alitangulia kupiga makofi. Wimbo huo uliimbwa vizuri, ulichezwa vyema, na hata kupangwa vizuri.

"Bi Jones, ni kweli ulitunga wimbo huu?" Bwana Lojas kutoka Times Media aliuliza kwa mshangao.

"Niliandika muziki na maneno mwenyewe." Lisa alisimama na kumuinamia Nandy. "Bi. Mfinanga, hongera, nimesikia mengi kuhusu wewe.”

”Nandy alijawa na sifa tele kwake. "Inasikitisha kwamba kipaji chako hakisikiki tena, Bi Jones. Tunaweza kurekodi nyimbo moja pamoja? Najuana na watu wengi katika tasnia ya muziki na wanaweza—”

“Asante kwa wema wako, Bi. Mfinanga, lakini muziki sio ndoto yangu. Ni hobby yangu tu,” Lisa alikataa kwa upole. "Kwa kawaida huwa na mambo mengi na nina shughuli nyingi sana."

Bwana Lojas alicheka. "Bi. Nandy, hujui hili, lakini Miss Jones pia ni mbunifu maarufu wa majengo.”

“Hiyo ni ajabu." Nandy alifichua sura ya kupendeza.

Wakati huo, Joan ghafla alisema, “Bi Jones, ulinakili wimbo wa Cindy? Wimbo wako unafanana sana na 'Pepo Ya Ndoto’, wimbo maarufu wa Cindy."

Kila mtu alishtuka, na mtu mwingine akaongezea, "Ni kweli hata mimi nimekumbuka..."

“Bi Jones, haiwezekani kuwa umeiba, sivyo?” Jerome alidhihaki kwa nia mbaya.

Sura ya: 358

Mara tu kauli hiyo ilipotolewa, macho ya kila mtu yakatua kwa Lisa.
Cindy alionyesha uvumilivu na usemi wa ukarimu, akisema, "Kwa kweli, sio kweli. Ukisikiliza kwa makini, wimbo aliotunga Lisa una mahadhi mepesi kuliko wimbo wangu, 'Pepo Ya Ndoto'. Ina mtindo tofauti pia."

Lisa alimtazama Cindy. Kila mtu aliweza kusikia maana iliyojificha katika maneno ya Cindy. Ilikuwa ni kukiri kwa njia isiyo ya moja kwa moja kwamba Lisa alikuwa amenakili Cindy, lakini ni mtindo wa wimbo tu ndio ulikuwa tofauti. Kwa maneno aliyosema, alijionyesha kuwa mkarimu sana huku akimponda chinichini.

Kwa hakika, wakati uliofuata, Joan alisema, “Bi Tambwe, unaweza kuwa mkarimu, lakini hupaswi kuendekeza wizi. Ukibadilisha na kupanga upya nyimbo chache za kigeni na kusema kuwa umeunda wimbo huo mwenyewe, si itakuwa dhuluma kwa waundaji asilia?”

Melanie naye alionyesha sura ya aibu. "Lisa, ingawa sisi sote ni washiriki wa familia ya Ngosha, huwezi kukosa akili."
Kabla Sarah hajazungumza, tayari kila mtu alikuwa akimlenga Lisa. Moyo wake ulikuwa na furaha sana aliponong'ona masikioni mwa Alvin, "Alvin, ni kweli aliiba?"

Uso mzuri wa Alvin ulikuwa umepoa sana. Hakuna aliyeweza kukisia alichokuwa akifikiria.

Rodney hakuweza kujizuia na kusema, “Haijaibiwa kabisa, lakini inafanana kwa angalau 60%. Ni kama nilivyosema. Hawezi kutunga. Mwishowe, bado alinakili kutoka kwa Cindy. Sijui ni nani aliyempa jeuri ya kupanda jukwaani na kujaribu kumwaibisha Cindy. Anamchukulia kila mtu hapa kama mjinga?"

Sara alifurahi aliposikia maoni hayo. Ingawa sura yake ilikuwa ya wasiwasi, moyo wake ulikuwa na furaha.

Mbele ya shutuma zote, Lisa alitabasamu na kucheza kwa starehe wimbo mwingine ambao hakuna mtu aliyewahi kuusikia hapo awali. Wimbo huu ulikuwa wa kutuliza zaidi. Lakini, sauti yake kama ya mbinguni ilisikika kwa mtindo wa kitamaduni.

Wimbo ulipoisha, alicheza wimbo mwingine. Nyimbo hizi zilikuwa na mitindo tofauti na hakuna mtu aliyewahi kuzisikia hapo awali. Baada ya kucheza na kuimba nyimbo hizo, umati ulibadilisha tena mawazo yao na kuanza kumwangalia Lisa kwa jicho la kitofauti.
.
Cindy alihisi wasiwasi moyoni mwake ukizidi kuwa na nguvu.
Joan alifoka, “Kila mtu anazungumza kuhusu wizi wako. Mbona unacheza nyimbo tena? Haijalishi unacheza vizuri kiasi gani, haiwezi kuficha ukweli kwamba umeiba.”

Lisa alimpuuza na badala yake akamtazama Nandy. “Una maoni gani kuhusu nyimbo mbili za mwisho? Je, zinafanana na nyimbo zozote huko nje?”

Nandy akatikisa kichwa. "Ni si msanii tu, bali mfuatiliaji mzuri wa muziki pia. Nyimbo hizi sijawahi kuzisikia popote. Ni nyimbo mpya kabisa."
“Bw. Campos, unaonaje?” Lisa aliwatazama wale watu waliozungumza kwa ukali zaidi hapo awali.

Jerome alisema kwa upole, “Tulikuwa tunazungumza kuhusu wimbo wako wa kwanza. Ingawa nyimbo zinazofuata hazijafahamika, ni nani anayeweza kuwa na uhakika kwamba hujanakili nyimbo za kigeni?”

“Ndiyo maana nilimuuliza Nandy kwanza. Unafikiri yeye asingeweza kuthibitisha hili kwa hadhi yake?” Lisa alirudi kwa utulivu.

Hadhi ya Nandy katika tasnia ya muziki iliheshimiwa. Haijalishi nafasi ya Jerome katika ulimwengu wa biashara ilikuwa ya juu kiasi gani, hakuthubutu kumkanusha waziwazi Bi. Nandy. Jerome akanyamaza kimya.

Lisa alisimama taratibu na kuyahamishia macho yake mazuri kwa Cindy. Alitabasamu ghafla, akauliza, "Unaonaje, Cindy?"

Cindy alishangazwa sana na swali la Lisa. “Unacheza vizuri sana. Endelea na kazi nzuri.”

Lisa akaachia mkoromo wa kicheko na kufinya macho huku akitabasamu. “Hata sasa hutaki kueleza kwanini wimbo wa kwanza ulifanana na wimbo wako, ‘Pepo Ya Ndoto’? Ni kwa sababu nyimbo zote katika albamu ya 'Pepo Ya Ndoto', iwe mashairi au mahadhi yake, zote ziliandikwa na mimi."

Kwa tamko hilo, watu wote waliingia katika ghasia. Umati wa watu ulitupa macho yao kwa Chester bila kujua. Kila mtu alijua kwamba Cindy alikuwa mpenzi wa Chester. Alikuwa akimlinda kwenye duara miaka yote hii, akimdekeza kama yai kwenye kiganja cha mikono yake. Kwa Lisa kumwiaibisha Cindy sasa, hiyo ilikuwa ni sawa na kumpiga Chester usoni. Chester aliwasha sigara na kukunja uso sana.

Cindy alichanganyikiwa. "Unasema nini?"
Rodney alifoka mara moja, “Lisa Jones, nadhani umepandisha wazimu kweli! Nyimbo hizo ziliandikwa na Cindy, sio wewe! Unawezaje kukosa aibu?"

“Ndio, unajua Cindy ana kipaji gani? Kwanini akuhitaji kumwandikia nyimbo?” Joan naye alipiga kelele.

Lisa alipuuza shutuma hizo na kusema, “Wimbo wa kwanza katika albamu ya 'Pepo Ya Ndoto', uliitwa 'Watatu Pamoja'. Ulihusu urafiki wangu na Cindy, na mtu mwingine wa tatu. Tulikuwa marafiki wazuri wakati huo. Mwaka huo, ndoto ya Cindy ilikuwa kuwa mwimbaji, kwa hiyo nilitoa nyimbo zangu nane bora nilizotunga mimi mwenyewe na kumpa Cindy bila mkataba. Kwanini nilicheza nyimbo mbili za mwisho mapema? Nyimbo hizo mbili ndizo nyimbo zangu za hivi punde zaidi. Nilitaka tu kuonyesha kila mtu uwezo wangu. Sikuwa na nia ya kumchafua Cindy hata kidogo.”

Uso wa Cindy ulikuwa umepauka, na alionekana kama anakaribia kulia. "Lisa, ni kwa sababu unataka kuwa mwimbaji? Ni sawa, ninaweza kukutambulisha kwa wanamuziki, lakini hutakiwi kukanyaga sifa yangu.”

Lisa alitabasamu na hata hakumtazama. “Hamkutakiwa kuwa na haraka ya kunishtaki. Kwa bahati nzuri, kitabu changu cha nyimbo bado kipo. Baadaye, nitapiga picha zake na kuziweka kwenye mtandao. Hata hivyo, kuna zaidi ya nyimbo nane katika kitabu changu cha nyimbo. Kuna nyimbo 18. Wale wanaojua muziki wanaweza kufurahia polepole. Unaweza pia kuja kwangu kununua hakimiliki ya nyimbo zangu zingine, lakini sitazitoa bure wakati huu, kwani…” Baada ya kunyamaza, alimkazia macho Cindy. “…baadhi ya watu hawashukuru kwa vitu ambavyo wamepewa kwa nia njema. Kuna watu wengi wasio na shukrani duniani.”

Cindy karibu kuanguka. Alijua kabisa mtunzi wa nyimbo hizo ni nani.
Hata hivyo, hakuwahi kujali kuhusu hilo. Ilikuwa ni kwa sababu, wakati huo, Lisa hakuwa tishio kwake. Ilikuwa tu kitabu cha nyimbo, kwa hiyo kila mtu angefikiri kwamba Lisa alikuwa akimwonea wivu.
Hata hivyo, kwa msimamo wa Lisa kulikuwa na haja ya kumuonea wivu Cindy? Lisa alikuwa binti wa kifalme wa familia ya Ngosha, familia iliyomiliki ardhi nyingi zaidi nchini Kenya. Sambamba na utukufu wake kama mbunifu mashuhuri wa kimataifa, bila shaka wengine wangeamini maneno yake zaidi.

Lisa alimaliza kuongea na kuinama. "Nilicheza tu piano kwa leo ili kufanya karamu iwe ya kupendeza zaidi kwa Times Media, lakini sikutarajia kusababisha usumbufu mwingi. Samahani zangu za dhati, Bwana Lojas.”

“Ni sawa, Miss. Jones. Ulicheza vizuri sana, haswa nyimbo mbili za mwisho. Mabosi wengi kutoka kwenye kampuni za muziki wapo usiku wa leo, kwa hivyo ninaamini kwamba wapo watakaojitokeza ili kununua hakimiliki ya nyimbo hizo hivi karibuni.” Lojas alikuwa mwerevu na alikuwa ameona mambo mengi ya aina hii kwenye tasnia hapo awali.

Hapo awali alimthamini Cindy, lakini alibadilishwa kabisa na maneno ya Lisa.Hata hivyo, bado alipaswa kuzingatia sifa ya Chester. Alisema huku akitabasamu, “Kila mtu ajisevie chakula. Utapata nguvu ya kusikiliza hotuba yangu jukwaani ikiwa utakula vya kutosha.” Umati ulitawanyika taratibu.

Kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa bado wanajadili kile kilichotokea.

“Oh, Bwana Cedo Kadenyi, wewe ni mtayarishaji wa muziki. Nini unadhani; unafikiria nini?"

"Kile Lisa Jones alisema kina uwezekano mkubwa kuwa kweli. Angalia tu nyimbo zake mbili. Ni nzuri sana. Akiachia moja anaweza ku pata tuzo ya muziki kwa urahisi."........ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.