JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................361-362
Sura ya: 361
Jua la mchana la uvivu liliangaza kutoka dirishani na kuangukia kwenye sura nzuri ya Lisa.
Akainama kutazama simu yake na kutabasamu kwa upole. Hata sauti yake ilikuwa laini. “Kwa hiyo mtashukia Dar es Salaam?”
"Ndiyo mpenzi, nimepata ndege ya moja kwa moja." Pamela alijibu upande wa pili wa simu. “Unaweza kutusubiri Nairobi. Sitakaa sana Dar, ni siku moja au mbili tu.”
“Hapana. Nitaenda kuwapokelea Dar, ni siku nyingi hata hivyo sijaenda kwenye jiji la nyumbani.” Lisa alinyamaza na kuinua kichwa chake, akionekana kuwa katika hali nzuri. “Msafiri salama, utawapa hai hao malaika wangu.”
•••
Ndege kutoka Marekani ilitua kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport, majira ya saa tatu usiku. Lisa alisubiri kwa zaidi ya dakika kumi kabla ya kumuona Pamela akitoka akiwa na wapenzi wake wawili.
Lucas alikuwa amevaa shati la rangi ya bluu la mtindo wa Kiingereza. Ingawa mwili wake ulikuwa mdogo, sura yake ndogo iliyopendeza kupita kiasi iliwafanya watu waliokuwa wakipita hapo kumtazama.
Kwa upande wa Suzie alikuwa amekaa juu ya sanduku alilokuwa akiburuta Pamela. Mabutu yake mawili ya nywele kichwani yaliyumbayumba kwa kupendeza. Watoto hao wawili walipomwona Lisa, walifurahi sana. Suzie aliruka chini mara moja kutoka kwenye sanduku na kumkimbilia kwa furaha.
“Mama, mama…”Suzie akaruka mikononi mwake mara moja, na kumganda mama yake kama luba.
Moyo mdogo wa Lisa ulilainika na machozi yalikaribia kumtoka. Tangu wazaliwe, hakuwahi kutenganishwa na watoto hao wawili kwa muda mrefu.
“Mama.” Lucas alijizuia zaidi, lakini macho yake pia yakawa na machozi.
"Sweetie, njoo hapa." Lisa alinyoosha mikono yake na kuwakumbatia.
"Jamani, ni bora kuwa na watoto wangu wa kuzaa mwenyewe. Yaani mlipomwona mama yenu tu mimi tena basi,” Pamela alitania, “Mimi nawanunulia peremende kila siku lakini mnanisahau mara tu mnapomwona mama yenu.”
Suzie aliukunja mabega yake. “Godmother, fanya haraka na wewe uzae watoto tupate kaka na dada mdogo.”
“Asante kwa baraka.” Pamela alipiga kelele.
Lisa alisimama na kutabasamu. “Pole kwa safari na karibu tena nyumbani. Nimewaandalia chakula kitamu sana cha jioni. Nisingekuwa na watoto tungeanzia bar”
Pamela akacheka. "Hakika, twende." Pamela alipokuwa anataka kuondoka ghafla sauti ya mshangao ikasikika nyuma yao.
“Pamela, ni wewe?” Ingawa ilikuwa imepita miaka mitatu, bado aliikumbuka vyema sauti hiyo.
Pamela aligeuka na kuwaona Patrick na Linda wakitoka nje ya geti.
Baada ya kutengana kwa miaka mitatu, Patrick alionekana mtu mzima zaidi na alionekana mpole kuliko hapo awali.
Kwa upande wa Linda, hakuwa amebadilika sana. Alikuwa amevaa tisheti nyeupe na sketi iliyofika magotini. Mikono yake miwili ilikuwa imeuzunguka mkono wa Patrick kiundani. Ilikuwa wazi kwamba walikuwa wapenzi.
Hata hivyo, Patrick alionekana kumsahau Linda aliyekuwa pembeni yake na kumtazama tu Pamela bila kupepesa macho. Jeans yake ya rangi ya blue mpauko ilifafanua vyema miguu yake minene iliyonyooka, na mwili wake wa juu ulifunikwa na fulana nyepesi ya kijivu. Shati la drafti lilikuwa limefungwa kwenye fundo kwenye kiuno chake, likifunua kiuno chake kidogo.
Ngozi yake ilizidi kung’aa kwa weupe wa asili na nywele zake zilikusanywa nyuma ya kisogo na kufungwa kufichua mashavu yake yenye dimpozi. Macho yake yalikuwa makubwa na yenye kung’aa, yalimfanya aonekane mtu wa makabila mchanganyiko. Miaka mitatu ilikuwa imeacha alama kwenye uso wake, lakini ilimfanya kuwa kijana zaidi na mrembo.
Patrick alionekana kusahau mpaka kupumua. Kando yake, Linda alisema kwa mshangao, “Pamela, ni wewe kweli. Umerudi? Tulikuwa na wasiwasi sana juu yako wakati huo tulipoona picha na video zako chafu mtandaoni. Uko salama?"
Patrick aliganda. Ndio, sasa alikumbuka. Miaka mitatu iliyopita, kulikuwa na habari kwamba Pamela alijirahisisha kwa Thomas Njau. Kisha Thomas alimfanyia mambo ya kisodoma na kurekodi video ambayo aliisambaza mtandaoni kwa watu kuona. Japo video hiyo haikuwa na uthibitisho wa kutosha kwamba aliyekuwa akifanyiwa kitendo hicho ni Pamela, teknolojia ilifanya kazi yake na kuuaminisha umma kuwa mwanamke huyo alikuwa ni Pamela. Habari chafu mara nyingi husambaa haraka, ndiyo maana tukio hilo la Pamela lilienea kwa kasi.
Muda mfupi baadaye, kulikuwa na habari kwamba alienda ng’ambo ili kukwepa aibu iliyomkuta. Macho ya Patrick ghafla yalijawa na karaha na tamaa.
Pamela kiasili hakuonyesha mabadiliko yoyote machoni mwake, akacheka tu na kusema. “Linda, unanipaka chumvi kwenye vidonda vyangu mara tu unaponiona, kwani hakuna habari nzuri za kuongelea hadi ukumbushie tukio baya kama hilo? Bado wewe ni wa ajabu tu kama zamani."
Sura ya Linda ilibadilika kidogo huku akijifanya ameziba mdomo kujionyesha kuwa amejawa na hatia. "Samahani-"
“Usiombe msamaha,” Patrick alisema kwa upole, “Kwa kuwa ulithubutu kufanya mambo kama hayo, kwanini unachukia yakiongelewa na wengine?”
Pamela aliinamisha kichwa chake. Huyu ndiye mwanaume ambaye hapo awali alikuwa akimpenda sana. Lakini, kwa sababu tu ya habari za uwongo, angeamini uwongo wa Thomas kuliko yeye.
Lisa hakuweza kujizuia. “Patrick Jackson, Pamela alikuwa nawe kwa muda mrefu lakini bado humfahamu vya kutosha?”
“Namfahamu vizuri sana.” Patrick alisema kwa dharau. “Nilipokuja kumtafuta mara ya kwanza huko Nairobi, alimbusu mwanaume mwingine hadharani tena mbele yangu. Ni wazi kwamba mtindo wake wa maisha umekuwa mchafu baada ya kufika huko.”
"Patrick, usiseme hivyo." Linda akahema. "Pamela huenda alikuwa akijaribu kukukomoa wakati huo. Thomas Njau ni Mkurugenzi wa Kampuni kubwa tu, hata hivyo. Huenda alikuwa akijaribu kutafuta mtu aliye na hadhi ya juu ili akuonyeshe, lakini iliishia… kumrudisha nyuma. Hata hivyo, Pamela, nataka kukukumbusha. Wakati mwingine unapotafuta mwanamume, bado unapaswa kuzingatia tabia yake.”
Pamela alitumbua macho kwa kuchukia. “Uko sahihi. Sikuangalia tabia ya mtu wakati wa kupata mpenzi wangu wa kwanza. Wakati huo, nilisema kwamba rafiki yake wa utotoni ambaye aliendelea kumsumbua alivutiwa naye, lakini hakuniamini. Tazama sasa. Kwa kweli waliishia kuwa wapenzi."
Uso wa Linda ulijawa na aibu, akamtazama Patrick ambaye naye alikosa cha kusema.
Pamela aliinama chini na kusema, “Nilimwambia mpenzi wangu huyo wa kwanza kuhusu hilo lakini alinilaumu na kusema hakuna kinachoendelea. Sasa nikifikiria juu yake, kwa kweli najilaumui sana. Nilipaswa kuondoka mapema. Badala yake, niliishia kuchelewesha uhusiano wa kimapenzi wa mtu fulani kwa miaka mingi sana. Mimi ni mjinga sana."
Rangi kwenye nyuso za Patrick na Linda zilibadilika mfululizo.
Linda aliuma mdomo wake na kusema kwa hatia, “Pamela, umeelewa vibaya. Amini usiamini, sikuwa na hisia zozote na Patrick wakati huo, lakini baada ya wewe kuondoka, nilihisi kwamba alikuwa na huzuni sana. Baadaye, nilipokuwa nikimriwadha, sikuweza kujizuia kumpenda.”
“Huzuni?” Pamela alipigwa na butwaa.
“Ndiyo, nilikuwa na mfadhaiko sana.” Patrick alisema kwa sauti ya chuki. “Nilitapeliwa na mwanamke mnafiki kama wewe kwa miaka mingi sana,”
Pamela alishtuka sana hata ubongo wake ulikuwa umevurugika. "Pia nilikuwa kipofu kabisa kwa kupoteza miaka mingi ya maisha yangu na mtu wa kuchukiza kama wewe. Hapo zamani, nilifikirije kuwa wewe ni mpole na mwenye upendo? Nilikuwa kipofu kabisa.”
Pamela hakuweza kuwa na wasiwasi tena na akamshika mkono Lucas na kuondoka.
"Subiri, huyo ni mtoto wako?" Patrick akatazama kwa udadisi.
Pamela alitaka kukiri kwamba alikuwa mtoto wake, lakini Lucas alizungumza kabla yake, “Yeye ni aunty yangu.”
Linda alisema, “Sijawahi kusikia habari za Forrest kufunga ndoa. Je, ni mwanae wa haramu?”
Sura ya: 362
“Oh jamani, mmesahau? Mtindo wangu wa maisha ni mbaya sana, hivyo ni kawaida kwangu kupata mtoto mmoja au wawili wa haramu,” Pamela alitabasamu na kucheka.
Lakini, uso wa Patrick ulibadilika sana. “Ni kweli ni mwanao wa haramu?”
“Mjinga wewe,” Lucas alimdhihaki, “zaa na wewe wa kwako umwite mtoto haramu, mimi siyo mtoto haramu!”
“Unasemaje wewe mtoto? Nitakufinyaaa!” Patrick alikasirishwa na maneno ya yule mtoto na kukaribia kumshika.
"Jaribu tu kumwekea mkono wako uone." Pamela alishika mkono wake.
Patrick ambaye alikuwa mrefu kuliko yeye alishangazwa na maumivu ya mkono wake. Akamkazia macho Pamela, lakini alimtazama tu kwa dhihaka. Alipatwa na mshtuko kidogo alipokumbuka kwamba alikuwa akimwangalia kila mara kwa kumwabudu. Moyo wake ulimuuma ghafla.
“Patrick Jackson, natumai kwamba tutakapokutana tena wakati ujao, usithubutu hata kunisalimia. Watu husema kwamba mapenzi ya kwanza ni mazuri, lakini mimi nakuona unachukiza kama nzi.” Pamela aliuachia mkono wake na kuondoka na Lisa.
Walipotoka, Patrick aliendelea kumtazama nyuma. Alimchukia waziwazi, lakini miaka yote hii, hakuwahi kufanikiwa kumfuta moyoni mwake.
“Patrick, uko sawa?” Linda kwa haraka akaja na kumshika mkono huku akimtazama kwa karibu.
"Si chochote." Patrick alikuwa hayupo.
Linda alipomuona hivyo alichukia kwa siri.
Ndani ya gari. Lisa alicheka akisema, "Patrick bado anakupenda sana. Bado aliendelea kukutazama tulipoondoka."
"Kwa hiyo?" Pamela alichungulia dirishani. “Baada ya tukio la Thomas, kila mtu alinisuta na kunisema sana. Huyu mpenzi wangu wa zamani pia alinitumia ujumbe akisema sijiheshimu.”
“Usijali Pamela. Sisi sote tumeteseka kwa kitu kimoja. Sote wawili tulikumbana na wahuni kwenye mapenzi yetu, wewe Linda na mimi ni Sarah” Lisa alilalamika.
“Hakika. Sitarudia tena makosa." Pamela alijipa moyo. Alikataa kuwa na bahati mbaya hivyo tena.
"Sawa, natumai utakuwa bora kuliko mimi," Lisa alisema kwa dhati.
“Godmother, usijali. Ukishindwa kupata mwanaume mzuri, nikikuwa mkubwa nitakulinda,” Lucas alisema kwa uvivu.
"Lucas wangu ni mtu mtamu sana." Lisa alimkumbatia na kumpiga busu, na kufanya masikio yake kuwa mekundu.
"Mama, mama, na mimi nataka pia." Suzie alimkumbatia na yeye pia akataka busu.
“Kwanza kabla ya yote shosti nimezikumbuka kweli chipsi vumbi za uswazi na nyama za kuku, tuanweza kuzipata wapi sasa hivi?” Pamela aliuliza ghafla.
“Muda wowote unapata, lakini nyumbani nimewandalia chakula cha jioni kitamu sana…” Lisa alimwambia.
“Sawa, tupite uswazi basi nichukue hata vimiguu vya kuku tu kupoza hamu hamu.” Pamela alisisitiza.
Lisa akawapeleka sehemu moja huko Msasani. Hapo palipatikana kila aina ya chakula cha uswahilini, haswa chpisi, mishikaki, nyama za kuku, mihogo na vingine kama hivyo.
Wale watoto wawili walifurahia sana chipsi na nyama za kuku. Walikula na kujilamba hadi matumbo yao yakakosa nafasi kabisa.
Suzie aliinua mdomo wake mdogo mwekundu na uliojaa mafuta, na mkononi akiwa ameshikilia vipapatio vya kuku vilivyokaangwa, akisema, “Hatimaye ninaelewa kwa nini Godmother huzungumza kila mara kuhusu chakula cha nyumbani, kumbe ni kitamu hivi?”
“Ni kitamu eeh?” Lisa aliuliza akitabasamu kwa bintiye.
“Ni kitamu sana. Sitaki kurudi Marekani tena. Nataka kubaki hapa na kula chipsi na kuku kila siku.” Suzie alisema huku akilazimisha kubugia vipande vya chipsi vilivyojazwa tomato sauce.
“Sawa mwanangu.” Lisa alihisi maumivu ya moyo.
"Sitaki kurudi pia," Lucas alisema kwa uso uliotulia,mdomoni akiwa amerundika minofu ya kuku wa kukaangwa. "Nataka nikae na wewe nikulinde."
Sauti za watotowale zilimfanya Lisa acheke, lakini akasema kwa uzito, “Hamtaweza kukaa huku mkiwa bado wadogo. Baba yenu akiwajua atawaiba na kuwapeleka mbali na mimi, au nyie mnapenda kwenda kukaa na mama mbaya wa kambo?”
"Ndio," Pamela aliyekuwa busy muda mrefu akifakamia nyama za kuku wa uswazi alisema ghafla, "Mama yenu anawapenda sana, lakini baba yenu ni mhuni, hana huruma kabisa."
Watoto hao wawili waliinamisha vichwa vyao, wote wawili wakiwa kimya kwa muda.
Baada ya kumaliza kula, Lisa aliwapeleka Masaki, mtaa wa Buzwagi ambako alinunua lile jumba la kifahari la Alvin siku za mwisho kabla hajaondoka kwenda Nairobi. Jumba lilikuwa kubwa na tulivu na muda wote lilikuwa likitunzwa na Jumbe, kijana wa kazi ambaye muda wote aliliweka jumba hilo katika mazingira nadhifu.
Siku inayofuata, Lisa aliamka mapema na kuandaa kifungua kinywa cha kupendeza kwa wapenzi wake wadogo.
"Wapenzi, mama atapumzika pamoja nanyi leo. Baadaye nitawapeleka beach kwenye uwanja wa michezo, sawa?" Lisa alisema kwa upole.
“Sawa.” Suzie akawa na furaha.
"Mama nataka uninunulie mpira." Lucas alisema aliokuwa akichungulia dirishani kwenye bustani kubwa iliyokuwa nje.
"Unavyotaka mwanangu."
Muda huohuo, Pamela alitoka nje ya chumba cha wageni akiwa amevalia nguo za kupendeza. Alijipaka vipodozi vyepesi usoni, na nywele zake ndefu zilishuka mabegani mwake. Alikuwa amevalia viatu vya visigino virefu."
"Watoto wangu, ninaonekana mrembo?" Pamela akasogea kwenye meza ya chakula
Suzie alipiga makofi. “Wewe ni mrembo sana. Wewe ni mzuri kama yule mwanamke anayeimba kwenye tv."
“Ooh! Msichana wangu wewe ni mzuri sana. Nitakuzawadia chokoleti." Pamela alitupa kipande cha chokoleti juu.
Lisa alimtazama Pamela kwa jicho la kumsifia pia na kuchombeza. “Kama usingesema kuwa unaenda kuhudhuria kongamano linalofanywa na SE Group, ningefikiria kuwa unaingia kwenye shindano la urembo.”
"Unajua nini? Nimesubiri wakati huu kwa muda mrefu sana. Tukio la leo ni muhimu sana kwangu kuanza zoezi langu la kulipiza kisasi kwa Rodney Shangwe wa Osher Corporation. Alinifukuza hapo awali, lakini hah! Siwezi kusubiri kuona macho yake ya huzuni na majuto sasa,” Pamela alisema huku kichwa chake kikiwa juu.
“Sawa, fanya haraka kula. Ondoka ukimaliza, usije ukaachwa na ndege.”
Lisa alisema huku akizuia kicheko.
“Ni masaa mawili tu kutoka Dar hadi Nairobi. Mkurugenzi wa SE Group ametuma ndege binafsi kuja kunichukua, sina presha. Kongamano halitakuwa na maana ikiwa mimi sitahudhuria.” Pamela alijigamba.
•••
Katika Jumba la kifahari la Rodney Shangwe.
Baada ya mpishi kutoa kifungua kinywa, msaidizi wa Rodney alimpa ratiba na kusema, “Bwana Shangwe, mwanakemia wa kimataifa wa vipodozi, Nicole, atakuwa akizungumza jukwaani kwa ajili ya kongamano la SE Group saa saba mchana wa leo. Ungependa kwenda? SE Group imetuma mwaliko.”
Rodney alikunja uso na kukoroma. "Huyu jamaa, Bwana Erick Malugu, ameweza kumwalika Nicole?"
“Ndiyo.” Msaidizi akapumua. "Lakini, Nicole ni wa kushangaza sana. Tumemwalika aje Kenya mara nyingi sana lakini amekuwa akikataa kila mara. Nilifikiri kwamba haipendi Kenya, lakini sikutarajia angekubali ghafla kuja wakati SE Group, mpinzani wetu kibiashara, alipomwalika. Osher ipo juu kuliko SE katika kiwango cha hadhi na brand. Watu wenye akili wangechagua kushirikiana nasi badala yake.”
Rodney alikitumbukiza kichwa chake katika mawazo mazito. "Je, Nicole amesaini mkataba wa ushirikiano na SE?"
"Hapana, lakini inasemekana kwamba Nicole anakuja Kenya wakati huu kutia saini mkataba na SE. Nilisikia kwamba ana fomula ya kipodozi cha kuzuia kasoro za ngozi na kuimarisha ngozi mikononi mwake. Itakuwa shida ikiwa zitanunuliwa na SE. Baada ya yote, bidhaa zilivumbulia na Nicole miaka hii zimekuwa bidhaa maarufu ulimwenguni kote na hadi 80% ya watumiaji wanarudi kununua bidhaa hizo tena.”
Baada ya kuambiwa hayo, Rodney alihisi kuudhika. "Wataalamu wa vipodozi katika kampuni yetu wote hawana maana. Tunawekeza pesa nyingi sana kwao kila mwaka, lakini hawajawahi kufanya chochote cha kuridhisha.”
Msaidizi wake alikunja midomo yake na kusema, “Mkurugenzi wa Idara ya utafiti na maendeleo humsifia kila Pamela Masanja, mwanamke aliyewahi kufanya kazi Osher miaka minne iliyopita. Alikuwa na kipaji kikubwa, lakini inasikitisha kwamba—”
"Nyamaza." Rodney alimtazama msaidizi wake kwa ukali. “Pamela Masanja ni mwanamke asiyefaa. Hakuna kitu cha kusifia juu yake. Wataalamu wa vipodozi kama yeye wanaweza kupatikana kote nchini. Sitaki kumsikia!”
"Hiyo ni sawa. Pamela Masanja hakika hayuko kwenye kiwango sawa na Nicole.” Msaidizi alikubali kwa kichwa alipoona bosi wake akiwaka.
"Hata iweje, hatuwezi kuruhusu Nicole kushirikiana na SE Group." Rodney aliinuka ghafla. “Nipatie hiyo kadi ya mwaliko. Nitaenda kwenye kongamano la SE na kukutana na Nicole mimi mwenyewe. Nikienda kibinafsi, bila shaka atalazimika kunionyesha heshima fulani.”.....ITAENDELEA...
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.
