JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP..........................0628924768

SEHEMU YA................................252-253


Sura ya: 252


Lisa alikaa kimya kwa muda. Kisha, akasema, “Uliajiri mpishi akutengenezee haya yote, sivyo?”

“Hapana, nilitumia asubuhi nzima kukutengenezea chakula cha mchana nyumbani,” Alvin alisema, “Wewe ulikuwa ukinipikia huko Dar es Salaam. Sasa, ni zamu yangu kukukirimu.”

Lisa alidhihaki, “Alvin Kimaro, wewe ni stadi kwa kuigiza. Ulikuwa pia ukifanya hivi ulipokuwa ukiishi na Sarah zamani?”

"Iwe unaamini au la, nimekupikia tu kwa sababu nakupenda." Alvin akamtengea chakula. "Kula." 

"Sili." Lisa alikataa kijeuri

“Lisa, huna akili timamu. Je, wewe pia hukuwa na mpenzi wa zamani?”

“Sawa, nitatafuta mvulana anayefanana na Ethan anihudumie nyumbani kwangu. Hiyo ni sawa?" Lisa alimtazama. Hakika, aliona kutoridhika machoni pake na akacheka. "Unaona, umewahi kujiweka katika viatu vyangu kufikiria juu ya hali hiyo?"

“Samahani,” Alvin aliomba msamaha kwa dhati. Kwa kweli alijihisi kukosea  kuhusiana na suala la Maurine. "Sitarudia tena."

"Alvin, hakuna nafasi nyingine tena," Lisa alisema kwa msisitizo.

“Usiseme hivyo mpenzi.” Alvin akajiweka sawa kwenye kiti. "Ikiwa hutakula, basi sitaondoka."

Lisa alimkazia macho. Hakujua amfanyeje mtu yule ili amwelewe.

“Kuwa mstaarabu.” Alvin alikuwa akigonga juu ya uso wa meza na ghafla akasema, "Mbona unakuwa kama mtu asiye na macho? Kwanini huoni kwamba ninakupenda?” Alvin alitabasamu kwa umaridadi. 

"Inawezekana sina macho ya kuona mapenzi ya kinafiki." Japo Lisa alitia kichwa ngumu, bado maneno ya kupendeza ya Alvin yalikuwa yakimwingia kidogokidogo.

Midomo yake ikafunguka tena ili kusema kitu, lakini Alvin akaiminya haraka kwa mkono wake. “Usiongee.” Alvin alihema kwa nguvu na kusema. “Unajua moyo wangu wote umejaa mapenzi yako. Unataka nifanye nini unielewe?"

“Unataka ufanye nini? Kufa tu!” Lisa alichukua glasi ya maji na kunywa ili kuondoa hasira iliyomkaba kooni mwake. “Sitaki uongee tena.” 

“Sawa, sitasema lolote usiponiruhusu, nitakusikiliza.” Alvin aliweka sura ya utii.

Lisa alikuwa karibu kumfukuza Alvin, lakini alikosa sababu ya kumtimua. Hakuwa tena Alvin yule mwenye kiburi na jeuri kama alivyokuwa zamani. Hakutaka kula chakula chake, lakini alikuwa na njaa sana, hivyo ilimbidi kushika uma na kijiko na kuanza kula chakula. Hakikuwa kitamu sana, lakini ladha yake ilikuwa inaruhusu kupitika mdomoni.

Alvin akaegemeza kidevu chake kwenye mikono yake. “Hatimaye ninaelewa kwanini ulifurahia kunipikia hapo awali. Kuona mtu ninayempenda anakula chakula nilichotengeneza inanifurahisha sana.”

Lisa alinyamaza. Alifurahia kumpikia lini? Hapo mwanzo, alimpikia ili kujipendekeza kwa nia ya kuwa shangazi wa Ethan. Baada ya hapo, ni yeye ndiye aliyemlazimisha.

“Nipe simu yako. Nataka nitoe namba yangu kwenye blacklist.” Alvin alinyoosha mkono wake.

"Hapana." Lisaaligoma.

'Basi nitaichukua kwa nguvu." Alvin alisimama, umbo lake refu likionekana kutawala. Lisa akakosa ujanja na kumtupia simu yake.

Alvin aligonga skrini mara chache na kujiondoa kwenye blacklist ya simu yake na Whatsapp. Baada ya kumrudishia simu, alichukua simu yake na kuigonga mara kadhaa pia.

 Muda si mrefu simu ya Lisa ikaita kwa mtetemo. Aliitazama na kulikuwa na taarifa: [Ni Wako Pekee alikutumia ujumbe.]

Ni Wako Pekee?… Lisa alibubujikwa na mshtuko.

“Umeupokea ujumbe wangu? Hilo ndilo jina langu jipya la Whatsapp.” Alvin akamtazama.

"Unajaribu kumaanisha nini hapa?" Lisa alikuwa katika ukungu.

"Nakupenda."

Lisa alikumbuka kwamba alipokuwa akijaribu kumvutia siku za nyuma,  aliweka jina lake la Whatsapp kama 'Alvlisa'. Hapo awali alikuwa ametulia lakini kukumbuka hilo kulimfanya uso wake kuwa na aibu.

"Angalia status yangu." Alvin alimkumbusha.

Lisa akaifungua huku akitetemeka. Ilikuwa imeandikwa hvi: [Kama kukupenda ni kifungo cha maisha, basi nakubali adhabu hiyo kwa hiari]

Akiwa kama wakili, hilo ndilo lilikuwa tamko la kimahaba ambalo  angeweza kulifikiria. Alvin aliinamisha kichwa na kukohoa. "Umeipenda?".

Lisa aliinamisha kichwa chake na kutabasamu kwa aibu. Alipoinua kichwa chake moja kwa moja aliweka kiganja chake kwenye shavu la Alvin.

"Unafanya nini?" Alvin aliuliza kwa mshangao.


"Nakuangalia kama una homa." Lisa alijibu. Hakuamini kama Alvin alitamka maneno yale akiwa mzima,.

Uso wa Alvin ulisinyaa ghafla. "Inatosha, nilitumia usiku kucha kujaribu kufikiria hii. Kwa mtu kama mimi, dakika moja inatosha kuniingizia kipato cha dola 10,000. Jiulize nimepoteza kiasi gani kwa ajili ya hilo.”

Lisa alikoroma moyoni. Je! alikuwa akimaanisha kwamba alipoteza mamilioni ya dola kwa ajili yake?

"Usijali. Wewe huwezi kulinganishwa na pesa, wewe ni mke wangu wa thamani sana." Alvin akafunga kontena la chakula. “Njoo nyumbani mapema leo usiku. Nitakupikia chakula cha jioni.”

“Asante, lakini hakuna haja. Nimefanya miadi ya kwenda kwenye spa na Charity.”

Alvin alikunja uso na kumtazama tena. Alipotaka kuongea tu, Lisa alimkatisha, “Najua unataka kunizuia nisiende nae tena na kumsema vibaya. Samahani, lakini yeye ni rafiki yangu sasa. Kwangu mimi ni mwadilifu, mkarimu, mpole, mwema, na ana mambo mengine mengi mazuri.”

Alvin alitaka kupasua kichwa chake na kukitikisa. “Nadhani amekuvuruga ubongo. Mwanamke huyo si mzuri kama unavyofikiaria.”

“Nilimruhusu kwa hiari yangu mwenyewe anivuruge ubongo. Una shida gani na hilo?" Lisa alitabasamu bila kufafanua. “Utawaambia rafiki zako wazuri kunifedhehesha tena?”

“Unamaanisha nini kusema hivyo?” Alvin alikunja uso.

“Mara ya mwisho, sikufanya chochote zaidi ya kumwomba Maurine aondoke, lakini rafiki yako mzuri, Rodney, alikuja kwenye kampuni yangu na kunifokea kama mtoto mdogo.” Lisa aliongea kwa huzni, lakini uso wake ulikuwa umejaa kejeli. “Sasa nikiambatana na Charity labda watakushauri unitaliki.”

Macho ya Alvin yaliingia giza. Hakujua kuhusu hilo.

“Alvin, nataka uondoke. Usinisumbue tena. Sitaki kuandamwa kama kichaa na rafiki zako. Wanaweza hata kufikiria kuwa mimi nilikufuata wewe kwa sababu ya maslahi yangu binafsi. Mimi nimeridhika na maisha yangu.” Lisa alikuwa akipitia nyaraka zake huku akiongea.

Ndita zilikunjamana kwenye uso wa Alvin kiasi kwamba zingeweza kumminya inzi hadi akafa. Hakujua mawazo ya Chester, lakini Rodney alikuwa kama vile Lisa alivyomdhania kuwa.

Alvin akasogea mbele na kumshika Lisa  mkono. Lisa aliinua kichwa chake. Alimuona akiitoa simu yake na kupiga namba ya Rodney. Hata akaweka simu kwenye kipaza sauti.

Simu ilipounganishwa, sauti ya Rodney ilisikika kwa uzito na uwazi. “Alvin, nilikuwa karibu kukupigia simu. Je, Lisa alihack akaunti yako? Jina lako 'Ni Wako Pekee' lilinichukiza sana hivi kwamba nilitapika chakula changu chote cha jana usiku."

“Sikudukuliwa. Niliibadilisha mimi mwenyewe.” Alvin alitamani Rodney angekuwa karibu ili ampige ngumi hadi afe. “Acha porojo zako. Hebu nikuulize, ulienda Mawenzi Investments na kumkoromea Lisa?"

“Huyo mwanamke amekuambia nini? Anaweza kuacha—” 

Alvin akamkatisha. Macho yake yalizidi kuwa makali sana. “Ulimwambia nini?”

“Sikusema lolote. Sikumbuki, lakini nilimuonya aache kumnyanyasa Maurine na kwamba asifikirie kuwa yuko juu  kwa sababu tu amekuwa Bi. Kimaro—”

“Rodney Shangwe…” Alvin alikunja vibaya uso wake na kusema neno baada ya neno, “Lisa na mimi kugombana ni mambo yetu wenyewe. Huna haki ya kusema lolote kuhusu hilo. Isitoshe, ikiwa una wasiwasi sana kuhusu Maurine, unaweza kumchukua na kumtunza jinsi unavyotaka.”


"KIM International haihitaji faida kama hizo. Familia za Campos na Kimaro ni jamaa tuliounganishwa kwa ndoa. Miradi hii ndiyo maamuzi niliyofanya wakati huo nilipotaka kuisaidia familia ya Campos. Babu yako anajua hili pia—”

“Basi unaweza kumtafuta babu yangu. Kwanini ujisumbue kunitafuta mimi?” Alvin alitabasamu kwa kejeli.

Uso wa Lea ukabadilika. “Babu yako amestaafu. Ninakukumbusha usifanye mambo bila huruma. Vinginevyo, msinilaumu kwa kukosa huruma kwako.”

“Sijui unamaanisha nini kwa maneno hayo, lakini…” Alvin ghafla alichukua rimoti na kuwasha skrini kubwa ukutani. Nyuso za wanahisa wachache wa KIM International zilionekana wazi kwenye skrini. “Samahani mama. Nilikuwa nikifanya mkutano kwa njia ya video na wanahisa. Wamesikia kila kitu ulichosema hivi punde.”

Mkurugenzi Kennedy, ambaye alikuwa mkubwa kati ya wanahisa, alisema, "Makamu Mkurugenzi Lea Kimaro, ikiwa tutachukua hizo bilioni 80, tunaweza kuzigawanya kati yetu na kila mmoja angekuwa na milioni mia chache. Bila shaka, tunajua kwamba wewe ni tajiri na hujali. Lakini sisi tunahitaji pesa."

Mkurugenzi Martin alisema kwa kejeli, “Tunaelewa kwamba familia ya Campos ni familia ya mume wako, kwa hivyo tuliwafumbia macho watoto walioongoza KIM International wakati huo. Lakini hatukujua kamwe familia ya Campos ilikuwa imechukua bilioni 80. Huu ni ujinga sana.”

Mkurugenzi Morris aliguna. “Hii siyo haki, huwezi kuipa  familia ya Campos shilingi bilioni 80 bila sababu. Siku zote umekuwa upande wa familia ya Campos, hatukubali hata kidogo.”

Mkurugenzi Kennedy akaongezea, “Mwanao, Willie, alitia saini mradi mwingine na familia ya Campos tena muda si mrefu na akatoa asilimia tano ya faida kwao. Kwa bahati nzuri, Bwana Alvin Kimaro alikatisha ushirikiano nuo. Vinginevyo, familia ya Campos ingepata zaidi ya maelfu ya mabilioni.”

Mkurugenzi Morris alisema, "Tunahitaji esa zetu zirudi, ama tutachukua maamuzi mgumu."

Uso wa Lea ulibadilika ghafla nakuwa mpole, na mwili wake ulikuwa ukitetemeka. Alikuwa amesimamia KIM International kwa miaka makumi kadhaa, na hii ilikuwa mara ya kwanza kwa wanahisa kumkosoa. "Mabwana, ninakubali kwamba niliisaidia Campos Ltd. hapo awali, lakini haiwezekani kwamba walichukua kiasi cha bilioni 80. Haya yote yamezushwa tu na Alvin.”

Mkurugenzi Kennedy alitabasamu. “Sidhani kama madai haya yalitungwa na mtu yoyote yule. Familia ya Campos wanajulikana kwa tamaai, kwa hivyo labda hata wewe ulikuwa gizani.”

"Hapana!" Lea hakuamini hata kidogo.

Alvin aliinua kichwa chake kuelekea kwenye skrini na kusema, “Sawa, wanahisa. Nitamwelewesha mama yangu vizuri.”

 "Asante, Bwana Mkubwa Kimaro." Hangout ya Video iliisha.

Mason alikunja uso na kusema, “Alvin, unawezaje kumtendea mama yako hivi? Atakabiliana vipi na watu wengine kuanzia sasa?” 

Alvin akatabasamu. "Uncle, kama ningekuwa wewe, ningesema hivi ili kumsitiri mke wangu, 'Mpenzi wangu, ili usijisikie vibaya, tutarudisha tu shilingi bilioni 80 kwa KIM International'.

Mason alikuwa mdogo kama pilitoni kutokana na aibu. Shilingi bilioni 80 hazikuwa pesa ndogo. Haikuwa rahisi kiasi hicho kuzitoa kirahisirahisi tu.

“Mpenzi wangu…” Mason alitaka kumbembeleza Lea lakini akamkatisha.

“Sawa, Alvin anajaribu kukuweka kwenye hali ngumu. Naelewa." Lea alimvuta Mason. “Twende zetu.”

Alipofika mlangoni, Lea aligeuka nyuma. Sauti yake ilikuwa ya huzuni aliposema, “Alvin, nitakumbuka kofi hili la uso ulilonipa leo. Kuanzia sasa, usiniite 'Mama'. Hatuna uhusiano tena.”

Katika maegesho ya magari, Mason Campos aliegemeza kichwa chake mikononi mwake kwa shida na hakusema neno. Lea aliuma mdomo na kusita. Akatoa kadi kwenye pochi yake na kumpa. "Nina shilingi bilioni 60 hapa. Unaweza kuingiza kwenye Kampuni ya Campos ili kuimarisha mzunguko wa pesa.”

"Mpenzi wangu ..." Mason alimtazama kwa hatia na huzuni. "Siwezi kuchukua hii."


Sura ya: 253

 

"Alvin, hii ni mara ya pili unanikoromea kwa sababu ya mwanamke huyo." Rodney alikasirika pia. “Maurine ni binamu wa Sarah. Sarah hayupo hapa tena. Ninafanya hivi ili kulinda familia yake.”

"Ndio, siku zote nilifikiria hivyo pia. Ndiyo maana niliachana na kanuni zangu kwa ajili ya Sarah tena na tena. Miaka yote hii Thomas amefanya maovu mangapi?!” Alvin alikiri kwa masikitko. "Miaka minne iliyopita, alisababisha kifo cha binti asiye na hatia. Ushahidi wote ulielekeza kwake, hata hivyo nilivumilia Kenya nzima kunikosoa na kupigania kesi kwa ajili yake. Baada ya kesi hiyo, nilichukia kazi yangu na kujiondoa kutoka kwa jumuiya ya wanasheria. Miaka yote hii, Zigi amekuwa na kisasi na mimi, na wewe unajua hilo.” Rodney alikuwa kimya.

Alvin alimshika mkono Lisa kwa nguvu. “Nilimtetea Thomas kwa miaka minne, na hata niliwatetea Sarah na kaka yake na mama yao walipokuwa wakinyanyaswa na mama yao wa kambo. Hata hivyo, hilo limesababisha matatizo katika ndoa yangu. Lisa hanielewi vizuri hatimaye. Siwezi kuwa na uhusiano na Sarah maisha yangu yote. Si haki kwa Lisa.”

Rodney alikunya sura yake bila kuridhika. “Kwa hiyo, haya ndiyo mapenzi uliyomwahidi Sarah? Inaonekana kama Sarah si chochote tena kwako.”

“Sarah tayari amekufa. Pengine… ulimpenda zaidi kuliko mimi?” Mwili wa Rodney ulisisimka. Alvin aliendelea. “Kama bado unapenda kuwa rafiki na ndugu yangu mzuri, natumaini utamheshimu mke wangu.” 

Alvin alikata simu na kumtazama moja kwa moja Lisa ambaye alikuwa ameduwaa. Ubongo wake ulikuwa umechanganyikiwa.

Hapo awali alikuwa amesikia kwamba Alvin alikuwa wakili mkubwa nchini Kenya, lakini ghafla alitoweka kwenye tasnia hiyo kwa muda. Ilibainika kuwa ni kwa sababu ya Thomas. Si hivyo tu, ina maana pia Rodney alimpenda Sarah? Lisa aliona mapichapicha tu kwenye akili yake.

“Lisa, nakuomba tuache yaliyopita na tugange yajayo, sawa?” Alvin alisema kwa umakini huku akimshika Lisa.

Akili ya Lisa ilipotea kwa muda, lakini haraka akautoa mkono wake. Hakuweza kujua ni sentensi gani kati yake ilikuwa ya kweli au ya uwongo.

'Ni sawa. Bado tuna wakati." Alvin akasimama. “Unaweza kuendelea na kazi yako. Sitakusumbua tena.” Baada ya kuongea alifunga mlango na kuondoka.

Lisa alikaa hapo kwa muda mrefu, lakini hakuweza kusoma hata neno moja kwenye nyaraka zilizokuwa mbele yake.

Baada ya kutoka Mawenzi Investments, Alvin aliendesha gari hadi hospitali kwa ajili ya kutiwa dripu. Hali ya ugonjwa wake haikuwa shwari, hivyo angeweza tu kudungwa dawa kwa ajili ya kutuliza.

Sindano ilipodungwa tu, Lea aliingia kwa hasira. “Alvin, ni kweli uliagiza idara ya sheria kudai shilingi bilioni 80 kutoka kwa Kampuni ya Campos?! Unataka kuwamaliza? Nadhani unaanza kuwa na kichaa cha pesa sasa."

Mason alisimama nyuma ya Lea, akitabasamu. “Najua unanilaumu kwa kuwa pamoja na mama yako. Ni sawa kwa kuwa hunipendi, lakini familia ya Campos haina hatia. Alvin, nakuomba, achana na kampuni ya Campos.”

"Mason, usimbembeleze." Kuona mwanaume aliyempenda anambembeleza mwanaye, moyo wa Lea ulimuuma sana.

Alvin alitabasamu kwa huzuni. "Uncle Mason, unataka niseme zaidi? Nimeona matapeli wengi kama wewe wanaojifanya wakarimu kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu. Ni ajabu sana mama yangu hajagundua njama zako kwa miaka yote aliyoishi na wewe.”

Uso  wa Mason ulikauka. Lea alikuwa anakaribia kupandwa wazimu kutokana na hasira. “Chunga mdomo wako! Mason hajawahi kukufanyia chochote kibaya. Nilikuwa najua una akili kumbe nilikuwa na najidanganya. Si tu kwamba huna akili, huna adabu, huna heshima na huna utu.”

Alvin aliongea kwa msisitizo. “Kivipi mimi sina utu? Kwa kudai haki ya familia ya Kimaro? Shilingi bilioni 80 kwa hakika ni faida ambayo ni haki ya KIM International kutokana na miradi yetu ya pamoja na Campos Ltd kwa miaka yote hii. Taarifa ya akaunti yangu imeandikwa kwa uwazi. Wao ndio hawakutupa hizo pesa. Ninadai pesa za KIM International zirudishwe, na bado unanikaripia. Mama, ninafanya hivi kwa manufaa ya KIM International.”


"KIM International haihitaji faida kama hizo. Familia za Campos na Kimaro ni jamaa tuliounganishwa kwa ndoa. Miradi hii ndiyo maamuzi niliyofanya wakati huo nilipotaka kuisaidia familia ya Campos. Babu yako anajua hili pia—”

“Basi unaweza kumtafuta babu yangu. Kwanini ujisumbue kunitafuta mimi?” Alvin alitabasamu kwa kejeli.

Uso wa Lea ukabadilika. “Babu yako amestaafu. Ninakukumbusha usifanye mambo bila huruma. Vinginevyo, msinilaumu kwa kukosa huruma kwako.”

“Sijui unamaanisha nini kwa maneno hayo, lakini…” Alvin ghafla alichukua rimoti na kuwasha skrini kubwa ukutani. Nyuso za wanahisa wachache wa KIM International zilionekana wazi kwenye skrini. “Samahani mama. Nilikuwa nikifanya mkutano kwa njia ya video na wanahisa. Wamesikia kila kitu ulichosema hivi punde.”

Mkurugenzi Kennedy, ambaye alikuwa mkubwa kati ya wanahisa, alisema, "Makamu Mkurugenzi Lea Kimaro, ikiwa tutachukua hizo bilioni 80, tunaweza kuzigawanya kati yetu na kila mmoja angekuwa na milioni mia chache. Bila shaka, tunajua kwamba wewe ni tajiri na hujali. Lakini sisi tunahitaji pesa."

Mkurugenzi Martin alisema kwa kejeli, “Tunaelewa kwamba familia ya Campos ni familia ya mume wako, kwa hivyo tuliwafumbia macho watoto walioongoza KIM International wakati huo. Lakini hatukujua kamwe familia ya Campos ilikuwa imechukua bilioni 80. Huu ni ujinga sana.”

Mkurugenzi Morris aliguna. “Hii siyo haki, huwezi kuipa  familia ya Campos shilingi bilioni 80 bila sababu. Siku zote umekuwa upande wa familia ya Campos, hatukubali hata kidogo.”

Mkurugenzi Kennedy akaongezea, “Mwanao, Willie, alitia saini mradi mwingine na familia ya Campos tena muda si mrefu na akatoa asilimia tano ya faida kwao. Kwa bahati nzuri, Bwana Alvin Kimaro alikatisha ushirikiano nuo. Vinginevyo, familia ya Campos ingepata zaidi ya maelfu ya mabilioni.”

Mkurugenzi Morris alisema, "Tunahitaji esa zetu zirudi, ama tutachukua maamuzi mgumu."

Uso wa Lea ulibadilika ghafla nakuwa mpole, na mwili wake ulikuwa ukitetemeka. Alikuwa amesimamia KIM International kwa miaka makumi kadhaa, na hii ilikuwa mara ya kwanza kwa wanahisa kumkosoa. "Mabwana, ninakubali kwamba niliisaidia Campos Ltd. hapo awali, lakini haiwezekani kwamba walichukua kiasi cha bilioni 80. Haya yote yamezushwa tu na Alvin.”

Mkurugenzi Kennedy alitabasamu. “Sidhani kama madai haya yalitungwa na mtu yoyote yule. Familia ya Campos wanajulikana kwa tamaai, kwa hivyo labda hata wewe ulikuwa gizani.”

"Hapana!" Lea hakuamini hata kidogo.

Alvin aliinua kichwa chake kuelekea kwenye skrini na kusema, “Sawa, wanahisa. Nitamwelewesha mama yangu vizuri.”

 "Asante, Bwana Mkubwa Kimaro." Hangout ya Video iliisha.

Mason alikunja uso na kusema, “Alvin, unawezaje kumtendea mama yako hivi? Atakabiliana vipi na watu wengine kuanzia sasa?” 

Alvin akatabasamu. "Uncle, kama ningekuwa wewe, ningesema hivi ili kumsitiri mke wangu, 'Mpenzi wangu, ili usijisikie vibaya, tutarudisha tu shilingi bilioni 80 kwa KIM International'.

Mason alikuwa mdogo kama pilitoni kutokana na aibu. Shilingi bilioni 80 hazikuwa pesa ndogo. Haikuwa rahisi kiasi hicho kuzitoa kirahisirahisi tu.

“Mpenzi wangu…” Mason alitaka kumbembeleza Lea lakini akamkatisha.

“Sawa, Alvin anajaribu kukuweka kwenye hali ngumu. Naelewa." Lea alimvuta Mason. “Twende zetu.”

Alipofika mlangoni, Lea aligeuka nyuma. Sauti yake ilikuwa ya huzuni aliposema, “Alvin, nitakumbuka kofi hili la uso ulilonipa leo. Kuanzia sasa, usiniite 'Mama'. Hatuna uhusiano tena.”

Katika maegesho ya magari, Mason Campos aliegemeza kichwa chake mikononi mwake kwa shida na hakusema neno. Lea aliuma mdomo na kusita. Akatoa kadi kwenye pochi yake na kumpa. "Nina shilingi bilioni 60 hapa. Unaweza kuingiza kwenye Kampuni ya Campos ili kuimarisha mzunguko wa pesa.”

"Mpenzi wangu ..." Mason alimtazama kwa hatia na huzuni. "Siwezi kuchukua hii."......ITAENDELEA.....


Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.