JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA................................210-211
Sura ya: 210
Lisa alioga baada ya kurejea nyumbani na kukimbilia kwenye maktaba na kukagua kompyuta ndogo ya Alvin.
Kila idara ya kampuni yake ilikuwa imemtuma barua pepe yenye data za mauzo za bidhaa katika mikoa mbalimbali. Alichanganyikiwa haraka baada ya kukagua ripoti kwa ufupi. Asingeweza kupinga kuitafuta kampuni ya Alvinarah mtandaoni. Matokeo yalimshangaza sana!
Kampuni ya Alvinarah lilianzishwa chini ya miaka mitano iliyopita, lakini, thamani yake ya soko tayari ilikuwa imepita Shilingi za Kenya bilioni 200.
Kando na hilo, biashara kubwa yenye faida katika Alvinarah Corporation na KIM International ilikuwa katika miradi ya marighafi za ujenzi, kama vile simenti, jipsamu, chokaa na vitu kama hivyo. Bila shaka, nafasi ya KIM International katika sekta hiyo haikutetereka. Licha ya hayo, kampuni ya Alvinarah iliweza kujitokeza kutoka kwa ushindani na kudhibiti zaidi ya robo ya faida katika sekta iliyotajwa hapo juu.
Kwa maneno mengine, Alvin alikuwa ameanza mpango huu kwa siri yapata miaka mitano iliyopita. Je, alitarajia kwa muda mrefu kwamba angeachwa na familia ya Kimaro? Papo hapo, Lisa alihisi kutetemeka kupita ndani yake.
"Unapeleleza kampuni ya Alvinarah?" Sauti ya Alvin ilisikika nyuma yake ghafla.
Lisa alishtuka, akafunga laptop haraka. Hisia ngumu ilijidhihirisha moyoni mwake baada ya kumuona mtu nyuma yake ambaye alijitokeza bila kutarajia.
“Tayari nimeona skrini. Shani alikuambia kuhusu hilo?” Aliegemea meza kwa umaridadi.
"Ndio. Lakini kwa sababu nilimuuliza kuhusu hilo, "Lisa alisema mara moja kwa kuogopa kwamba Alvin angemlaumu mlinzi wake.
"Sio mbaya kwamba unaonyesha kujali kuhusu mume wako." Akainama huku akitabasamu usoni. "Lakini unaweza kuniuliza chochote ambacho unatamani kujua badala ya kukitafuta mtandaoni."
“Aaahmm..” Lisa aliinua midomo yake, lakini hakujua la kuongea.
Akampigapiga kichwani. "Unafikiri ninaogopa kwa kuanzisha kampuni ya Alvinarah kwa siri miaka mitano iliyopita kwenda kinyume na KIM International?"
“Si kweli? Ninaelewa umuhimu wa kujiandaa kwa siku za dhiki.” Lisa alijibu.
"Wewe ni mgeni, kwa hivyo labda hujui kuwa KIM haikutumaiwa kuwa biashara yenye faida zaidi ya makampuni yote. Ilianza kwa kujikongoja na ilifanya vibaya katika tasnia ya ujenzi. Mgogoro wa kifedha ulitokea baada ya mimi kuchukua kampuni, kwa hivyo sikuwa na chaguo ila kuimarisha nafasi yake katika tasnia ya ujenzi. Lakini mimi nilikuwa mwenyekiti tu. Kwa maneno mengine, mimi ni kama mfanyakazi mwingine tu. Ilinibidi nitengeneze mpango mbadala…Nilianzisha Alvinarah ili kuua ushindani wa nje na kuipa kampuni KIM nafasi ya kuongoza soko”
Aliendelea kusema, “Kama ningefanikiwa kurithi KIM International, Alvinarah angeendelea kuwepo katika nafasi ya pili milele na hakuna ambaye angemjua bosi halisi nyuma ya kampuni hiyo.”
“Lakini wewe si mwenyekiti tena wa KIM International. Je, unapanga kuiongoza Alvinarah kuiangusha biashara ya familia yako?" Lisa aliuliza.
“Timu nzima iliyokuwa inafanya kazi katika mradi wa utafiti wa teknolojia mpya ya cement na jipsam katika KIM International tayari imejiuzulu na hivi karibuni watakuja kunifanyia kazi Alvinarah. KIM International itaondolewa hivi karibuni bila kuwa na wahandisi wasomi na wenye uzoefu. Sekta ya ujenzi inabadilika haraka kila siku inayopita.”
Lisa ghafla alijiona mjinga sana. Alidhani Alvin ameachana na KIM International kwa ajili yake. Hata hivyo, yeye pia alishangazwa na hatua hiyo ya ujasiri. Kweli, kama ilivyotokea, tayari alikuwa na mpango mbadala mahali. Asingeweza kamwe kuondolewa kutoka juu ya ufahari wake. Labda angeweza kuwa na nguvu zaidi baadaye. Hilo lingetokea, kweli angekuwa tajiri mkubwa nchi nzima bila kuzuiwa na mtu mwingine yeyote.
“Mbona unaniambia haya? Je, huogopi kwamba ninaweza kufichua siri hiyo?” Lisa aliuliza kwa wasiwasi.
"Hapana, hauwezi, kwa sababu wewe ni mke wangu." Alimnyanyua kutoka kwenye kiti, akaketi mwenyewe, na kumweka kwenye mapaja yake.
Lisa alishusha macho yake chini ili kuficha kejeli machoni mwake. “Mke?'
Sahau. Jina la Alvinarah ni lako na la mwanamke mwingine.”
“Alikuwa mke zamani, sasa mke wangu ni wewe.”
"Alvin, hujisikii kuwa na hatia kidogo unaponiambia maneno haya?” Aliuliza ghafla kwa sauti ya kawaida. “Kama ilikuwa zamani kwanini sasa usibadilishe?’
Lisa aliona hisia zisizofaa ambazo zilijitokeza kwenye uso wa Alvin kabla ya kutabasamu kawaida. "Itaamuliwa baada ya majadiliano ya ndani ya mimi na wewe."
“Tusilizungumzie hilo tena. Hii ni nini?" Alipunga kadi ya mwaliko mkononi mwake.
ALvin alikumbuka kuiacha kwenye meza baada ya kurudi nyumbani. "Melanie alinialika."
"Alinialika na mimi pia." Alvin alicheka kabla ya kusema, "Anafikiria anaweza kuturusha roho kwa kuolewa na Jerome Campos."
Lisa alikosa la kusema. Mwanamke huyo hata alimwalika mpenzi wake wa zamani. Ilionekana kana kwamba siku hiyo ingekuwa ni siku ya kuvutia.
“Vema… Si lazima uende. Ipuuze tu.” Alvin akaitupa kadi ya mwaliko.
"Na wewe je?" Alimtazama machoni.
"Nitaitembelea familia ya Campos." Alvin alijibu kifupi.
Mwanga wa mshangao uliangazia katika macho ya Lisa. "Unafikiri familia ya Campos inahusika katika matukio ya hivi majuzi?"
"Ndio, haswa video hiyo kutoka kwenye Yatch. Jack hana uwezo wa kufanya hivyo peke yake. Nadhani familia ya Campos ilimsaidia,” Alvin alisema huku akipapasa vidole vyake. Alifurahi kumuona akiwa amevaa pete yao ya ndoa. "Zingatia kazi yako na acha nishughulikie hili."
“Hapana, tayari nilimuahidi Melanie kwamba nitakuwepo.” Aliinua kichwa chake juu kwa kumaanisha.
“Usiende…” Alvin alikunja uso.
Lisa aliruka kutoka mapajani mwake. “Unaogopa nitakudhalilisha kwa sababu ya sura yangu si ndiyo? Au labda una wasiwasi kwamba kwenda kwenye hafla za umma na mwanamke mbaya kama mimi kunaweza kukufanya kuwa kituko?”
"Lisa Jones ..." Sauti ya Alvin ilidhihirisha kutofurahishwa kwake. “Hivyo ndivyo unavyonifikiria mimi? Sitaki uende kwa sababu ninataka kukulinda dhidi ya Melanie. Nina hakika unajua nia yake mbaya.”
"Lakini ulemavu wangu ndo umeshatokea. Ina maana ni lazima niepuke matukio ya hadhara maisha yangu yote?” Alibembeleza uso wake kwa ufupi. "Hadhi yako ya heshima inamaanisha kutakuwa na hafla nyingi za kijamii zinazokungoja katika siku zijazo. Nini kinatokea watu wanapouliza kuhusu mke wako? Una mpango wa kunificha chumbani milele? Kwa upande mwingine, je, natakiwa kubaki nyumbani na kutazama unapojitokeza kwenye hafla na wanawake warembo tofauti kila wakati? Ikiwa ndivyo, basi unapaswa kunitaliki sasa hivi, sitaweza kuvumilia.” Baada ya kusema hivyo aligeuka na kuondoka.
Wimbi la kufadhaika lilimpitia Alvin. Amfanyeje mwanamke huyu ili ajue kwamba anampenda?
Lisa alipanda kitandani mara baada ya kukanyaga chumbani. Hakuwahi kukosa utaratibu wake wa kutunza ngozi wakati wa usiku hapo awali lakini kwa muda huo aliona haikuwa lazima tena.
Muda mfupi baadaye, Alvin alipanda kitandani na kumkumbatia kwa nyuma. Sauti yake ilijawa na unyonge. “Tafadhali usiwe na wazimu.
nitahudhuria tukio hilo pamoja nawe kesho. Ni wakati mzuri wa kutangaza kwa jamii ya watu matajiri wa Nairobi kwamba wewe ni mke wangu.”
Lisa aligeuka kumtazama na kuona mapenzi yakimiminika kutoka kwenye macho yake gizani. “Lakini… naonekana mbaya. Watu wanaweza wakakucheka.”
ALvin alibana pua yake kwa kuichezeachezea. "Ulikuwa ukinifokea tu kwa kukuzuia kwenda, lakini sasa unajidharau tena, maana yake nini?"
Lisa aliuma mdomo kwa kuchanganyikiwa. Alijua kweli alikuwa anajipinga mwenyewe. Hakuwa na wasiwasi kuhusu maoni ya wengine lakini maoni yake… bado yaliathiri hisia zake.
“Msichana mpumbavu, ni lazima nikuambie mara ngapi kwamba haijalishi sura yako bali nakupenda wewe kama Lisa?” Alvin alinong’ona kwa upole, “Sikutaka uende kwa sababu naogopa unaweza kukosa furaha. Sijali kuhusu wengine wanafikiri nini. Kitu pekee ambacho ni muhimu kwangu ni kile unachofikiria."
Sura ya: 211
“Lakini… ikiwa uko tayari kukabiliana na watu pamoja nami, basi nitahudhuria mikusanyiko yote ya baadaye pamoja nawe huku nikikuweka kwa karibu."
Alvin alisisitiza kila neno kwa uzito kana kwamba alikuwa akisema nadhiri zake kanisani. Lisa alihisi kitu kikimsonga. Alikuwa mwanamke wa kawaida tu. Hakuweza kupinga kuguswa hasa wakati maneno matamu yalipotoka kinywani mwake, licha ya kuhisi kuwa Alvin alikuwa anaigiza tu kumpenda. Alihisi kutomwamini lakini wakati huohuo mvuto wa kutatanisha aliouonyesha Alvin ulipita kwenye hisia zake.
“Inaonekana kama itabidi nithibitishe upendo wangu kwako kwa vitendo."
Midomo ya Alvin ilijikunyata na kuwa tabasamu la kutatanisha kabla ya kumbusu midomo yake.
“Hapana…” Lisa alifadhaika alipotambua alichokuwa anataka kufanya. Alikuwa amepatwa na kiwewe tangu usiku ule wa kwanza.
"Msichana mzuri, wewe kwangu ni tunu ya thamani, kwa hivyo lazima nikupe hali ya usalama." Akamshika kiuno chake chembamba na kumvuta karibu. Aliachia tabasamu kali na kutamka katika hali ya kujiamini, “Nakuahidi sitakuumiza tena.” Lisa alijikuta akizama kwa sauti yake ya upole.
Siku iliyofuata, Alvin alitoka bafuni baada ya kuvaa na kumkuta Lisa bado amejilaza kitandani. Midomo yake ilionekana laini na nyororo. Alibaki amefumba macho huku akisitasita kumtazama.
"Nguruwe mvivu, jua limetoka na ni wakati wa kuamka. Mbunifu wa mitindo atakuwa hapa baadaye kidogo kukuletea vazi utakalo vaa jioni.” Kwa upole akampa busu kwenye paji la uso wake.
Hapo awali Alvin alikuwa ameajiri mwanamitindo mashuhuri kutoka Afrika Kusini kwa ajili ya kubuni gauni la Melanie la kuvaa siku ya harusi hiyo. Sasa kwa kuwa hakuwa tena na Melanie, alipindua tu oda hiyo na kumpa Lisa badala yake kwa sababu Lisana Melanie waliendana kwa umbo na kimo.
“Wewe ndiye nguruwe mvivu,” Lisa alifumbua macho yake na kumkemea.
Hata hivyo, macho yake yalikuwa yamejawa na mapenzi. Akacheka. Ingawa sura yake ilikuwa tofauti, macho yake bado yalikuwa yanavutia kama hapo awali.
"Mpenzi, ngoja nikusaidie kutafuta nguo ya kuvaa." Alvin alitembea kuelekea kwenye kabati la nguo.
“Sitaki msaada wako. Naweza kufanya mwenyewe.” Lisa alimsukuma.
Akiwa kwenye chumba cha kubadilishia nguo, Lisa alichanganyikiwa baada ya kuona uso wake kwenye kioo. Alvin alikuwa amethibitisha kwa matendo yake jana yake usiku kwamba hakujali kuharibika kwake usoni, lakini hakuweza kuamini kwa sababu hata yeye wakati mwingine ilikuwa ngumu kujikubali. Ilibidi akubali kwamba alipata hali mpya ya amani baada ya kusikia maneno ya kutia moyo ya Alvin jana yake usiku.
Mbunifu mitindo alifika mida ya saa nne asubuhi akiwa na gauni la jioni la rangi ya samawati lisilo na bega. Lilionekana la kawaida lakini lilimbadilisha kabisa Lisa. Nguo hiyo ilifunikwa na almasi ndogo ndogo zilizofanana na nyota zinazoanguka kutoka angani. Alitoka nje ya chumba cha kubadilishia nguo kama binti wa kifalme kutoka kwenye jumba la ufalme, kila hatua yake ilikuwa ya kuvutia na yenye mvuto wa ajabu.
Mbunifu mitindo huyo pia alimtengeneza nywele zake katika mikunjo mikubwa ya mawimbi na nywele ndefu za mbele zikifunika nusu ya uso wake. Macho yake ya pande zote yalionekana ya kupendeza sana chini ya mikunjo hiyo. Mabega yake yalifunuliwa na vazi lile lisilo na mabega, yakionekana kuwa safi.
"Bibiye, nataka uonekana wa ajabu leo. Gauni hili la jioni limebuniwa na Bonny King, mbunifu bora kutoka Afrika Kusini. Sio tu kwamba linagharimu zaidi ya milioni 5 za Kenya, bali pia ni la pekee duniani kote.” Mbunifu mitindo yule alimwambia Lisa kwa husuda. Lisa alishangaa kidogo. Hakutarajia gauni hilo kuwa la asili na gharama kama hivyo.
"Nilisikia Miss Ngosha alikuwa akipanga kuvaa hii kwa sherehe ya uchumba wake lakini sio kitu ambacho unaweza kununua kama mboga mboga hata kama una pesa," mbunifu huyo alisema huku akitabasamu. "Bila shaka utakuwa kitovu cha umakini wa watu katika sherehe usiku wa leo."
Kusema kweli, Lisa alifurahishwa sana na jitihada za Alvin.
Saa tano kamili asubuhi Alvin alifika nyumbani kutoka kazini kumchukua Lisa. Akasogea mbele kumshika mkono, na macho yake yakang'aa kama nyota za anga la usiku. "Nimelipenda sana vazi hili la jioni."
"Asante kwa kunijali mume." Lisa alisema huku akiinua macho.
Wakiwa njiani kuelekea Mombasa ambako sherehe za uchumba zingefanyika, gari lilisimama kwenye makutano ya barabara, likisubiri taa ya kijan iwaruhusu kupitai. Lisa ghafla aligundua kitu nje ya dirisha na akahisi moyo wake ukipiga. “Paki pembeni ya barabara. Ninataka kununua kitu kutoka kwenye duka la dawa."
"Unahitaji nini? Nitakwenda kukununulia.” Alvin alimtazama machoni.
“Um… dawa za kupanga uzazi,” alijibu bila wasiwasi.
"Hakuna haja, tunaweza kufikiria kuwa na watoto," Alvin alisema kwa sura ya umakini, "nakuahidi nitakuwa baba mzuri."
“Aaah Bwanaa..Muda bado Alvin…” Lisa alihisi uhusiano wao haukuwa thabiti kwa kupata watoto. Isitoshe, bado alilazimika kushughulikia matatizo mengi. “Sitaki watoto sasa. Mimi bado ni mtoto katika umri huu,” alisema huku akigeuza uso wake pembeni. Sauti yake ilisisitiza maamuzi yake.
“Sawa. nitakuletea dawa.” Gari lilisimama kando ya barabara. Alvin aliingia kwenye duka la dawa peke yake. "Nipatie vidonge vya Vitamini C na vidonge vya kudhibiti uzazi."
Muuzaji kwenye duka la dawa alimletea alichoomba. Hapo hapo, Alvin alibadilisha vilivyo ndani ya chupa mbele ya muuzaji. Muuzaji alikosa la kusema.
Baada ya kuingia ndani ya gari, Alvin alimkabidhi Lisa vidonge na chupa ya maji. "Nitakuacha utumie wakati huu lakini dawa kama hizi sio nzuri kwa afya yako. Nitatumia kinga wakati ujao.”
“Next time…?!” Lisa alimtazama kwa aibu Alvin baada ya kumtazama Hans aliyekuwa amekaa mbele. Alvin hata hakuhisi aibu.
“Mpenzi wangu, si jambo la kuonea aibu. Sisi si mume na mke?” Alvin alitabasamu kwa kujiachia. Lisa alikataa kujibu akihofia mazungumzo yangekuwa mabaya zaidi.....ITAENDELEA....
Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
