JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................134, 135


Sura ya 134


Hapo awali, Lisa alihisi mashaka kidogo, lakini baada ya kusikia sauti ya Kelvin, alihisi kwamba alikuwa na mawazo potofu. Kelvin alikuwa muungwana sana. Asingeweza kamwe kueneza picha kama hizo.


“Amekasirika sasa. Ukimpigia simu utazidi kumkasirisha zaidi.” Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Si ulisema siku ile uliharibu kamera? Kwa nini…”


"Niliiharibu. Hata niliiangalia wakati huo hakukuwana picha zozote." Sauti ya Kelvin ilionyesha jinsi alivyokuwa na huzuni. "Nadhani kamere zilikuwa zinahamisha picha wakati zikirekodi. Nilikuwa mzembe. Niligundua kuwa picha hizo mtandaoni zilisambazwa na ripota baada ya kupewa na Lina.”


Lisa alitabasamu kwa hasira. Alikuwa amemdharau Lina. Picha hizi zilikuwa za uchochezi sana.


“Samahani.” Kelvin aliomba msamaha tena. “Sijali kwa vile mimi ni mwanaume, lakini itaathiri sana sifa yako. Ikiwa kuna chochote ninachoweza kukufanyia, nijulishe tu na nitajaribu niwezavyo kukusaidia.”


"Asante. Nina simu kutoka ofisini ninayohitaji kuipokea. Tuongee baadaye.” Lisa haraka akakata simu kwa Kelvin na kupokea simu kutoka kwa msaidizi wake, Tunu.


“Mwenyekiti Jones, njoo ofisini haraka. Uvumi kuhusu kashfa yako unavuma na laini ya simu ya kampuni inashikiliwa na waandishi wa habari. Inabidi ushughulikie jambo hili haraka iwezekanavyo.”

“Sawa, nitakuja mara moja.” Lisa hakujali tena na kubadilisha nguo zake haraka kabla ya kushuka.


Alipotoka nje, aligundua kwamba Shani hakuwepo na hakumfuata tena ili kumlinda. Moyo wake ukaingia giza. Alvin ndiye alikuwa amepanga Shani amlinde. Sasa kwa kuwa alitaka kumuacha, alimfukuza Shani pia.


Baada ya kufikia kwenye kampuni hiyo, waandishi wengi walikuwa wamesimama mlangoni. Aliingia kutoka kwenye viwanja vya maegesho. Alipopanda ghorofani, watendaji kadhaa walikuwa tayari wakimsubiri ofisini.


"Mwenyekiti Jones, kuna wanamtandao wengi kwenye mtandao wanaokukaripia kwa kuwa... 'wazi' sana…” Paji la uso la Freddie Ngololo lilijawa na jasho baridi. Tayari alikuwa ametumia neno lenye ukakasi sana. “Kwa kifupi, hali si nzuri sana na sifa yako kama mwenyekiti wa kampuni naogopa kusema kwamba inaathiri sana.


Uso wa Lisa ambao tayari ulikuwa umekunjamana ulizidi kuwa mbaya. Mara nyingi alisoma magazeti ya udaku mtandaoni na alijua vyema uovu wa watumiaji wa mtandao dhidi ya wanawake katika kashfa kama hizi.


"Je, idara ya PR ina mawazo yoyote?" Lisa aliuliza huku akikuna kichwa.


Meneja Mkuu Ngololo alisema, “Idara ilifanya mkutano mapema asubuhi. Tunafikiri njia bora ni kutangaza rasmi kuwa wewe na Kelvin Mushi ni wapenzi ili kushusha joto. Kwa kweli, hata wafuatiliaji wa habari hii wanasema Kelvin Mushi na wewe mnaendana sana na mnalingana vyema katika hali ya kijamii. Hakika utapokea mwitikio chanya kutoka kwa watu mitandaoni na kashfa hii itageuka kuwa baraka kwako.”


"Ndiyo…Ndiyo!" Meneja wa idara ya PR alitabasamu haraka na kusema, “Wakati huo, tunaweza pia kuipandisha hadhi Mawenzi Investments, Kwa taswira yako kama mwenyekiti wa bodi, na taswira ya Kelvin Mushi kama mwenyekiti wa Golden Corporation, mnaweza kuwa mabalozi wazuri wa kampuni.” Watendaji walikubaliana na wazo hili.


Kadiri Lisa alivyozidi kusikiliza ndivyo alivyozidi kukosa la kusema. "Hapana, tayari nina mpenzi."


Meneja Mkuu Ngololo alianguka kwa aibu. “Sawa… Lakini ulipigwa picha ukiwa na Bwana Mushi. Ukikataa, itakuwa mbaya kwa picha yako, na kila mtu atakudharau kwa kuwa na maisha ya faragha yasiyo na uaminifu. Ikiwa suala hili halitashughulikiwa vyema, sura ya Mawenzi Investments itaathirika pakubwa.”


"Niliwekewa madawa ya kulevya wakati huo. Unaweza kueleza moja kwa moja kwenye tovuti rasmi.” Lisa alisimama na kuwatazama watendaji hao kwa macho makavu. "Hii ni kampuni ya mali isiyohamishika. Maadamu mali zetu zimejengwa kwa ubora mzuri, bado tunaweza kupata nyota zilizo na picha nzuri za kututangaza. Ikiwa kweli tumeathiriwa, basi haiwezi kusaidia. Siwezi kumuumiza mpenzi wangu kwa sababu ya kampuni, kama vile baadhi yenu hamtawaacha wake zenu kwa ajili ya faida. Kila mtu ana msingi wake."


Umati ukanyamaza. Baada ya nusu dakika ya kimya, Meneja Mkuu Ngololo alitikisa kichwa. "Tutafanya kama Mwenyekiti Jones anavyosema."


Baadaye, ukurasa wa Facebook wa Mawezni ulichapisha taarifa kwa umma.

[Picha zilipigwa zaidi ya mwezi mmoja uliopita. Mwenyekiti Jones alifanyiwa njama na kulishwa madawa ya kulevya. Kwa bahati nzuri, Kelvin Mushi alionekana kwa wakati na kumuokoa Mwenyekiti Jones, lakini hakuna kilichotokea kati ya pande hizo mbili. Wawili hao bado ni marafiki wa karibu sasa. Tunatumai kila mtu ataelewa na ataacha kujadili suala hilo.]


Kisha, Kelvin binafsi ali’share chapisho hilo.


[Wakati huo, Mwenyekiti Jones alikuwa ameleweshwa dawa za kulevya, lakini aliokolewa haraka na kulowekwa kwenye bafu baridi. Ni mwanamke mwenye heshima sana. Natumai kuwa watu hawatamwelewa vibaya na kumtusi kwa sababu ya picha chache.]


Baada ya chapisho kupakiwa, athari ilikuwa nzuri ya kushangaza.

Watu wengi walimsifu Kelvin kwa kuwa mungwana na msikivu, na Lisa kwa kuwa hodari na jasiri. Baadhi ya watu hata waliwashauri na kuwaambia wawe wapenzi badala ya marafiki. Walisema walikuwa ni kapo zinazofaa zaidi katika ulimwengu wa biashara.

•••

Katika kampuni ya sheria, Jennings Sollicitors, Ofisi ilionekana kuwa na giza la ukiwa. Alvin alikuwa amekaa siku nzima kwenye simu yake. Asubuhi, kila mtu alimkemea Lisa, lakini upepo ulibadilika ghafla mchana. Kila mtu alipiga kelele kwa Lisa kuungana na Kelvin.


Aliibomoa simu yake pale pale kwa hasira. "Hivi watu kwenye mtandao siku hizi hawana kitu cha maana cha kufanya? Eti hawa wawili wanaendana vizuri? Hivi ni vipofu?”


Hans aliyekuwa amesimama pembeni aliitazama ile simu iliyosambaratika akiwa hoi. Angelazimika kununua simu mpya tena. Hakujua hata idadi ya simu ambazo Alvin alikuwa amevunja tangu awe na Lisa.


“Bwana Kimaro, watu kwenye mtandao wote ni wavivu sana. Usiwajali.” Hans alimpoza kimawazo.


Alvin alikodoa macho. Hakutaka, lakini alikuwa amesoma yale ambayo watu walisema kuhusu Kelvin Mushi kuwa na mapenzi makubwa kwa Lisa, na Lisa kuwa na hisia nzuri kwa Kelvin. Kulikuwa na watu wanaotunga hadithi ya mapenzi ya kipuuzi kuhusu kupendana kwao kwa siri.


Tumbo la Alvin liliwaka kwa hasira. Akaketi na kufungua laptop yake, vidole vyake vikiruka kwenye keyboard. Dakika chache baadaye, Hans aligundua kuwa habari ya Kelvin na Lisa ilikuwa imetoka kwenye habari zanazovuma mtandaoni! Ilishangaza! Bwana Kimaro kweli alikuwa amedukua akaunti ya facebook ya Mawenzi moja kwa moja.


“Alvin...” Mlango wa ofisi ulifunguliwa ghafla na Sam Harrison akaingia. Alipomwona Alvin ambaye alionekana kama mfalme wa pepo, alitetemeka. “Nilifanya uchunguzi. Usiku huo, Lina Jones aliingia na watu wachache na alionekana kwenye jumba hilo la hoteli. Wakati huo, pia alimwagiza meneja wa hoteli hiyo kwamba hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia katika chumba alichopanga.”


Alvin alikodoa macho. Ilionekana kana kwamba tukio hilo la Lisa lilikuwa ni njama. Hata hivyo, jinsi alivyokuwa amembusu Kelvin kimahaba bado ilimkasirisha.


"Umegundua ni wakati gani Lisa na Kelvin waliondoka?" Aliuliza kwa huzuni.


"Asubuhi," Sam alikohoa kwa upole na kusema kwa sauti ya chini, "Walitoka asubuhi baada ya kubadilisha nguo." Maneno hayo yaliposikika, Alvin aliivunja kompyuta moja kwa moja.


Mwanamume na mwanamke katika chumba pamoja, na mwanamke hata kulishwa madawa ya kulevya. Inawezekanaje kuamini kwamba hakuna kilichotokea kati yake na Kelvin?


Sam alimtazama kwa huruma. Kusema kweli, pia hakuamini kabisa kwamba Lisa hakuwa na hatia. “Sawa… Lisa pia ni mwathirika katika hili… Nilisikia kwamba Lina Jones aliingia na walinzi wawili wakati huo. Kama Kelvin Mushi asingetokea, matokeo yangekuwa mabaya zaidi.”


"Unamaanisha nini? Unasema ninapaswa kumshukuru Kelvin Mushi?” Macho jeuri ya Alvin yalimtoka. "Mwishowe, yeye ndiye mjinga. Anaendelea kuanguka kwa hila za familia ya Jones mara kwa mara. Baadaye, alijaribu hata kunihadaa na kuwa marafiki na Kelvin. Ananichukulia kama mjinga”


Sam alikuna ncha ya pua yake na kusema. “Hata hivyo, tayari nimekuchunguzia. Ni juu yako ikiwa unataka kuachana naye au kuendelea naye.”

Alvin hakuwa na mahali pa kutoa uchungu wake. Aliwasha sigara na kumwambia Sam. "Twende tukanywe vinywaji vichache na mimi leo usiku."


Sura ya 135


Usiku huo, Alvin alikunywa glasi baada ya glasi ya pombe. Sam hakuweza kumzuia. Uvumilivu wa pombe wa Alvin ulikuwa mkubwa, lakini alikunywa sana usiku huo na cha kushangaza alilewa kidogo.


"Nimemkumbuka Sarah ghafla." Alitazama usiku nje ya dirisha na kunong’ona, “Kati ya wanawake wote waliobahatika kuingia kwenye maisha yangu, ndiye pekee aliyekuwa na moyo wake wote kwangu. Hakukuwa na udanganyifu na hakukuwa na usaliti. Kwa nini alikufa?”


Sam alishika glasi yake, maumivu makali yakimtoka moyoni.

Kile ambacho wengine walikiona kwa Alvin kilikuwa ni Kilima cha juujuu kilichoonyesha ufahari wake, lakini Sam alijua kwamba Alvin alikua bila mapenzi ya wazazi wake. Ndani ya moyo wake alikuwa ni mtu asiyejiamini sana katka suala zima la mahusiano. Hata alipokuwa akisoma shule, waliomwendea walikuwa na ajenda za siri na kumfanya aingiwe na mashaka makubwa. Wakati huo, Alvin aliumia sana.


Kama rafiki yake, Sam ghafla alijuta kumwita Dar es Salaam. Hakutarajia kwamba moyo wa Alvin, ambao siku zote ulikuwa umeganda, ungehamaki ghafla. Sam aliongozana naye kunywa hadi Alvin akalewa sana. Ilikuwa ni mara ya pili Sam kumuona Alvin akiwa amelewa kiasi hicho.


Kwenye meza ya vinywaji, simu mpya ilitetemeka kila mara. Lisa alikuwa akimpigia simu Alvin mara kwa mara. Sam alichukua simu na kuitikia. Sauti ya Lisa ilisikika kutoka upande wa pili. “Uko wapi? Mbona umechelewa sana? Njoo nyumbani, tutayaongea tu yataisha sawa…"


"Alvin amelewa." Sam akamkatisha.


"Nakuja kumchukua mara moja," Lisa alisema kwa hofu.


"Hakuna haja. Hutaweza kumbeba hata hivyo. Nitamrudisha mimi mwenyewe.”


Baada ya simu kukatika, Lisa alisubiri mlangoni. Kulikuwa na mvua usiku huo tena, na matone ya mvua yalidondoka nje na kulowanisha kila kitu. Nusu saa baadaye, Sam aliegesha gari lake. Alipumua kwa huruma na upole baada ya kumuona Lisa akiwa amesimama kwenye upepo wa baridi.


Baada ya gari kuegeshwa, Lisa alifungua mlango wa siti ya nyuma. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Alvin akiwa amelewa sana. Uso wake mzuri ulionyesha wazi kuwa alikuwa amelewa, na alionekana kupoteza fahamu pale kwenye siti ya nyuma. Yeye na Sam walimsaidiana kumwingiza Alvin hadi chumbani pamoja. Lisa alimtazama Sam huku akihisi mnyonge. “Bwana Harrison, asante. Mimi…”


“Ni sawa, Alvin aliniambia niachunguze jambo hili. Najua hukukusudia.” Sam alikuwa na maumivu ya kichwa. Pia hakujua la kusema. “Nitaondoka sasa hivi.”


Lisa aliona kuwa Sam alikuwa akimchukulia tofauti na hapo awali. Hakucheka na kutabasamu kama alivyomfanyia siku za nyuma. Alikua na huzuni kidogo kwa sababu yake. Alijua kwamba hakutaka kuzungumza naye sana, lakini hakuweza kujizuia kuuliza, “Bwana Harrison, unajua Alvin anachofikiria kuhusu hili?”


"Lisa, mwanaume yeyote angechukizwa na hilo," Sam alisema bila kuficha, "Ungemwambia Alvin juu ya hili mapema. Sasa kwa kuwa imejulikana bila wewe kusema, kusema kweli inatia uchungu sana.”


Uso wa Lisa ulipauka. “Hakuna kilichotokea kati yangu na Kelvin. Ni kweli."


“Ni bure kuniambia hivyo. Unahitaji Alvin akuamini.” Sam akatikisa kichwa na kuondoka.


Lisa alibaki ameduwaa kwa muda. Alielewa nini Sam alimaanisha. Alvin hakumuamini. Afanye nini? Alikuwa anampenda kweli sasa. Hakutaka kumuacha. Alimtazama sana yule mtu pale kitandani. Huenda ikawa ni kwa sababu alikuwa amekunywa pombe kupita kiasi na hakujisikia vizuri, hivyo tumbo lake pia likawa na usumbufu. Aliendelea kupapasa tumbo lake. Kiyoyozi cha kuongeza joto kiliwashwa mle chumbani na hakuwa amevua koti lake, kwa hiyo jasho likatoka upesi kwenye paji la uso wake. Lisa alichota beseni la maji ya baridi. Alivua koti lake, akafungua kola ya shati lake, na kuufuta uso wake mzuri kwa taulo.


“Sarah…” Mwanaume huyo alimshika mkono ghafla, na manung’uniko ya chinichini yakatoka kwenye midomo yake myembamba. Lisa aliganda kana kwamba ndoo ya maji baridi imemwagwa juu yake.


Sarah? Huyo alikuwa nani? Je, alikuwa mpenzi wake wa zamani?

Lisa aliuvuta mkono wake kutoka kwenye mshiko wake kwa nguvu. Mkono wa mtu huyo ulishika hewa, na akamwita tena, “Sara”.


Aligeuka na kukaa pembeni ya kitanda. Macho yake yalikuwa mekundu, na moyo wake ulikuwa umechomwa kana kwamba alikuwa akichomwa kisu. Inauma!


Asubuhi iliyofuata, Alvin aliamka na hangover. Kichwa chake kilimuuma, na tumbo lake lilihisi kukosa raha pia. Alitazama mazingira na kugundua kuwa alikuwa katika chumba chake cha kulala katika nyumba yake. Kwanini Sam alimrudisha pale? Kwa kweli hakutaka kukutana na Lisa kabisa. Hata hivyo, alikuwa amekunywa pombe kupita kiasi jana yake usiku na alikuwa akijisikia vibaya sana muda huo.


Alipotazama huku na kule, ghafla aliona kikombe cha maji ya uvuguvugu na vidonge viwili vya tumbo vimekaa kando ya kitanda cha kulalia. Macho yake meusi yalimtoka. Alihisi ni Aunty Linda ndiye aliyemwkea dawa hiyo. Alichukua dawa huku moyo wake ukiwa umechanganyikiwa. Alishuka tu baada ya kunawa na wakati tumbo lake lilihisi vizuri kidogo.


Shangazi Linda alipokuwa akifanya usafi alimuona Alvin akishuka. Alitabasamu. "Bi Kimaro anakuandalia kifungua kinywa sasa hivi."


Alvin akaenda kwenye meza ya chakula. Kulikuwa na nyama na nguruwe iliyochomwa, supu ya kuku wa kienyeji, maziwa fresh, maziwa, juisi ya limao...


Mlango wa kuteleza wa jikoni ukafunguliwa, na Lisa akatoka na chungu cha mtori. Alivaa gauni la rangi ya waridi na aproni iliyofungwa kiunoni mwake. Nywele zake zilikuwa zimefungwa kama mkia wa farasi, na kufunua uso wake mdogo na safi. Ilimfanya aonekane mpole na mtulivu.


"Ulikunywa sana jana usiku, kwa hivyo ni bora ukaanza kwa kula kitu chepesi asubuhi. Mtori ni rahisi kusagwa na hautakuwa mzigo kwenye tumbo lako.” Lisa alisema huku akivuta bakuli la mtori na kuliweka mbele yake.


Alvin aliutazama ule mtori kisha akamtazama Lisa. Taswira ya yeye kushika shingo ya Kelvin na kumbusu kwa nguvu ghafla ilionekana akilini mwake. Kamba ya uvumilivu moyoni mwake ilionekana kukatika kwa nguvu. Alinyanyuka na kuumwaga mtori moja kwa moja kwenye pipa la takataka. Kisha akamtazama kwa macho ya jeuri. "Vitu unavyopika ni vichafu."


Uso wa Lisa ulibadilika ghafla. Baada ya muda mrefu, alipepesa macho yake ambayo yalikuwa yakitoka kwa machozi. “Kwa kuwa unafikiri mimi ni mchafu, kwa nini nisiondoke?” Kwanza likuwa ameita jina la mwanamke mwingine alipolala, hata hivyo. Kwa kweli, labda hakumpenda sana.


Alvin aliganda alipomsikia hivyo. Macho yake yaliyokuwa na damu kwa mbali yalimtazama ghafla. “Unataka kuondoka? Unataka kwenda kwa Kelvin kukaa naye sasa? Kila mtu kwenye mtandao anawaambia nyinyi wawili mnafaa kuwa pamoja. Nyinyi ndio wanandoa wanaofaa zaidi katika ulimwengu wa biashara.”


"Hapana." Lisa hakuweza kulala usiku kucha kwani alijiona hana nguvu. “Naondoka kwa sababu hutaki kuniona.”


"Hata kama unanichukiza, unatakiwa kukaa katika nyumba hii," Alvin alifoka kwa hasira, "Maadamu nipo karibu, unaweza tu kuota kuwa na Kelvin. Acha nikuambie, Lisa Jones, kwa kuwa umenichokoza, usifikirie hata kuniacha nikiwa mzima!”

Kisha, akaondoka.


Lisa alitabasamu kwa uchungu. Hivi, alikuwa bado mzima? Tayari alikuwa amepoteza moyo wake kabisa.....ITAENDELEA.......


Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.