JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP.........................0628924768
SEHEMU YA...............................120, 121
Sura ya 120
Baada ya kumwona Lisa mapema, Willie alimtazama kwa shauku. Hakujua kamwe kuwa Lisa aliyekuwa amemsikia mapema alikuwa mwanamke mwenye sura nzuri kama hiyo. Uzuri wake ulionekana kuwa wa aina yake miongoni mwa mamia ya wanawake aliokuwa amekutana nao.
"Halo, Bi Jones." Willie alinyoosha mkono wake kwa kumpa salamu. Lisa pia alishangaa kwamba Lina aliwezaje kupata ushirikiano na mtu kutoka kwa familia ya Kimaro. Lisa hakuwa na la kufanya zaidi ya kunyoosha mkono wake bila kupenda, akijua kuwa hawezi kukataa salamu yake bila sababu.
Nani alijua baada ya Willie kumshika mkono, alichora miduara kwenye kiganja chake kwa utani kwa kutumia kidole chake kidogo na kumchoma kichokozi Lisa. Mabadiliko kidogo yalionekana katika uso wa Lisa. Alijaribu kujinasua kutoka kwa mguso wake, lakini kwa makusudi Willie alimshika kwa nguvu na kumzuia.
"Bi Jones, unataka kunishika mkono wangu hadi lini?" Willie alitabasamu kwa ujanja.
Lina mara moja akainua mdomo wake na kusema, "Unafanya nini, Lisa?" Hapo hapo Lina akamvaa Lisa na kumwanzishia varangati, akidhani kwamba Lisa alijaribu kumchombeza Willie.
Waandishi wa habari waliosimama kwenye ukingo wa zulia jekundu walichukua picha za watatu hao mara moja. Pamoja na dada wawili kutoka kwa familia ya Jones wakipigana juu ya mtu maarufu wa familia ya Kimaro, lilikuwa tukio ambao lingetengeneza kipande cha habari nzuri.
“Kwanini hukumuuliza alichonifanyia pia?" Akiwa na tabia ya utulivu, Lisa hakuwa na jeuri wala kujidharau. “Hivi nyie mnafikiri kwamba mimi kama mtu anayesimamia Mawenzi ningemtongoza mpenzi wa binamu yangu bila aibu? Samahani, hata hivyo si mpenzi wako. Ninavyokumbuka, Stephen ndiye mpenzi wako, sivyo?”
Waandishi wa habari walianza kushangaa. “Kweli? Stephen ni mpenzi wa Lina kweli, lakini kwa nini alikuja na Willie leo?”
“Sasa kwa kuwa alikutana na Willie, inawezekana kwamba anajaribu kumtosa Stephen?”
“Hilo linawezekana. Hapo awali alikuwa mchumba wa Ethan, lakini Ethan alipokabiliwa na wakati mgumu, mara moja alimbwaga kwa kushutuma za usaliti.”
“Ni fedheha iliyoje! Willie anavutiwaje na mwanamke wa aina hii?"
Uso wa Lina ulikuwa mweupe kama karatasi wakati huo. Willie hakutambua kwamba Lina alihusishwa na habari nyingi mbaya. Aliishia kujiingiza kwenye matatizo.
Bila bughudha, Lisa alijiondoa kwa nguvu kutoka kwa Willie na kugeuza mkono wake kwa maumivu. "Ulinibana mkono wangu kwa nguvu sana hadi unauma, Bwana Kimaro."
Mkono wake, ambao hapo awali ulikuwa wa kawaida, ulikuwa mwekundu wakati huo. Waandishi wa habari waliposogea karibu, waliweza kuiona ngozi yake nyekundu vizuri. Macho ya Willie yakaangaza kwa dharau mara moja. Hawakutarajia mtu kutoka kwa familia ya Kimaro angekosa haya.
Siku zote Willie alikuwa mtu wa kupenda kunyenyekewa na wengine. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kudhalilishwa na mwanamke hadharani. Macho yake yalionyesha uhasama, lakini alitabasamu kwa unyonge.
"Samahani kwa kukuumiza bahati mbaya." Akamsogelea Lisa hadi karibu na kumnong’oneza, “Utanijua mimi ni nani, Lisa.”
Alipomaliza tu kuongea, aliingia moja kwa moja ndani ya hoteli hiyo. Na Lina alimfuata haraka. Lisa alipoutazama mgongo wa Willie, alihisi kana kwamba alikuwa amelengwa na nyoka mwenye sumu kali. Alikuwa na hasira ya kuzama.
Willie alipanda lifti uso wake ulikuwa na hali ya huzuni. Akiwa ameingiwa na mawazo ya wasiwasi, Lina alisema kwa utulivu, “mpenzi, natumai hautajali kuhusu hilo. Lisa anajidai na anajigamba kwa kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kampuni na kufanya mambo yasiyo ya kiungwana.”
“Yeye ni nani wa kufanya hivyo? Yeye ni mwenyekiti tu wa kampuni, kufumba na kufumbua anaweza kukuta kiti hicho kina mtu mwingine.” Willie alikuwa akifuka kwa hasira.
"Kwa kweli, yeye si kitu ikilinganishwa na wewe. Labda ni kwa sababu ana mpenzi mwenye nguvu, na yeye ni mwaminifu sana kwake.” Baada ya kukaa siku chache na Willie, Lina alijua kuwa Willie alipenda sana kusifiwa.
Kwa hakika, macho ya Willie yalionyesha kupendezwa kwake dakika tu aliposikia hivyo. Alipenda sana wanawake ambao muda wote walikuwa wakimsifia, kumbembeleza na kumpetipeti. Zaidi ya hayo, ukizingatia jinsi Lisa alivyokuwa mkali muda si mrefu, alifanana na waridi lenye miiba na alionekana mrembo zaidi kuliko Lina.
Alipoona hali ya kuvutia machoni pake, Lina alitabasamu na kusema, “Ninaweza kumfanya alale nawe kama utapenda.” Lina alisema bila aibu. Kwa kuwa amekuwa akidhalilishwa na Willie kama mbwa kwa muda waliokuwa pamoja, alitaka Lisa pia aonje adha hiyo.
"Wewe ni mwanamke mbaya sana." Willie alimpiga jicho la mshangao.
"Furaha yako ndiyo muhimu kwangu. Hutaki kumfundisha somo?” Lina aliuliza kwa kupendeza.
Willie aliinua macho yake. Aliwasha sigara kisha akasema kwa uovu, “Wale walionidhalilisha wote waliishia katika hali mbaya sana. Lisa pia anastahili kujuta!”
•••
Sherehe kuu ya kumbukumbu ya kampuni ya Mawenzi ilianza rasmi. Lisa alipaswa kuwa kivutio cha tukio hilo, hata hivyo, wageni wote walimzunguka Willie, Jones, na Lina badala yake.
Kwa macho ya wengi, familia ya Kimaro ilionekana kuwa ya hadhi ya kipekee. Ingawa Willie hakuwa mzao wa moja kwa moja wa Kimaro, uwepo wake jijini Dar es Salaam ulikuwa na nguvu ya kutosha kupata heshima kutoka familia kubwa za kitajiri.
Chris Maganga akajongea kuelekea kwa Lisa na kumuuliza. "Jones Masawe aliwezaje kujenga uhusiano na Willie Kimaro?"
"Nadhani Lina alilala naye." Lisa alifanya dhana ya kuridhisha. Tayari aliweza kuona tabia mbaya ya Willie kupitia tukio fupi alilokutana nalo mlangoni wakati wanaingia.
Sura ya dharau iliosha usoni mwa Chris. “Babu na bibi zako walikuwa na sifa ya uungwana na uadilifu, hii tabia chafu yenye aibu ameitoa wapi dada yako?”
“Ni kwaida yake kujua ndani ya kila suruali ya mwaname aliyefanikiwa kuna mdudu gani.” Lisa kichwa kilimuuma. Hapo awali, alikuwa na uwezekano mkubwa wa kumvutia kila mtu, lakini mwonekano wa Willie ulimfunika kabisa. Willie alikuwa amevutia umakini wa wasanii, waalikwa, wakurugenzi wa kampuni na wasimamizi wakuu.
Kwa wakati huo, wakurugenzi wawili wa bodi ya kampuni ya Mawenzi, Amiri Gumbo na Mzee Levy walimwendea na kumwambia. "Lisa, ulipaswa kuwa wa kwanza kutoa hotuba kwenye jukwaa usiku wa leo. Lakini baada ya kujadiliana na wakurugenzi wengine, tuliamua kumwacha Bwana Kimaro aanze kwanza, akifuatiwa na Jones kisha—”
“Nyie watu ni wazima kweli?” Chris alipandwa na hasira. “Bwana Kimaro hata hajui kinachoendelea katika kampuni yetu, wao huja kuchukua faida tu. Unahitaji kujua kuwa usiku wa leo ni sherehe ya kumbukumbu ya Mawenzi Investments. Pia, kwa nini Jones anapanda jukwaani kabla ya mwenyekiti? Hii haina maana.”
Mkurugenzi Amiri alijibu kwa aibu, “Angalia Bwana Kimaro ni nani. Ukweli kwamba amejitokeza kwenye sherehe ya ukumbusho wa Mawenzi Investments unaonyesha kwamba anatufikiria sana. Zaidi ya hayo, yuko tayari kupanda jukwaani kutoa hotuba, ambayo ni heshima yetu kubwa. Bei ya hisa za kampuni yetu itaongezeka kesho. Kuhusu Jones, ni Bwana Kimaro ambaye alimwomba azungumze. Ana uhusiano wa karibu naye. Huwezi kunilaumu kwa hili.”
Uso wa Lisa ulibadilika kidogo. “Itakuwaje kama sikubaliani?”
"Hapana," Mkurugenzi Levy alijibu kwa njia ya moja kwa moja, "Sote tulifikia uamuzi huu kwa ajili ya kampuni. Lazima ukubaliane nao.”
Lisa alicheka. "Ikiwa Willie ataamua kumpendekeza Jones kuwa mwenyekiti, nyinyi pia mtakubaliana naye? Je! ni Sheryl au Kimaro ambaye alianzisha Mawenzi Investments?"
"Tunafanya hivi kwa ajili ya matarajio ya kampuni," Mkurugenzi Levy alisema kwa kukerwa, "Kwa kuzingatia hali ya familia ya Kimaro, utajiri wa familia yao una thamani ya mamia ya mabilioni ya shilingi.” Mkurugenzi Amiri alikubali kwa kichwa pia.
Saa mbili na nusu usiku, Willie alipanda jukwaani na kutoa hotuba, akifuatiwa na Jones Masawe…
Sura ya 121
Saa tatu usiku, Lisa alikuwa kwenye chumba chake cha mapumziko baada ya kumaliza kutoa hotuba yake. Alisimama kwenye kioo akipaka lipstick yenye rangi ya hudhurungi kwenye midomo yake maridadi, huku akitafakari hotuba aliyotoka kuitoa punde.
Lina akaingia ghafla. Akiwa na tabasamu la ufidhuli, alisema, “Pengine hukutarajia kwamba hivi karibuni ungeweza kupoteza nafasi yako ya uenyekiti ambayo ndiyo umeipata hivi punde, sivyo?”
"Wewe bado hujabadilika kabisa Lina." Lisa aligeuza kichwa chake na kukutana na macho ya Lina. “Kwanza, ilikuwa Ethan, ikifuatiwa na Stephen na sasa Willie. Umelala na wanaume wangapi zaidi kabla ya hawa? Wewe ni zoazoa, cha wote, au chakula cha wageni?”
Kauli fupi kama hiyo iligusa ujasiri wa Lina ghafla na kusababisha damu yake kuchemka. “unanionea wivu, huh? Sasa ninakupa nafasi hii pia. Ni heshima kubwa sana kuweza kulala na Willie Kimaro sivyo? Nadhani utafurahia pia, yupo vizuri kwa bedi.”
Mara tu alipomaliza kuzungumza, Willie aliingia ndani ya chumba akiwa amevimba kama mbogo.
"Bwana Kimaro, nitakusaidia kulinda nje." Lina alifunga mlango wa chumba mara baada ya kusema hayo.
“Unataka kufanya nini?” Lisa alijaribu kukimbia, lakini Willie alimshika mkono. Kukiwa na mlango kati yao, alisikia sauti ya mlango ukiwa unafungwa.
Wimbi la wasiwasi lilimkumba Lisa. Shani hakuwemo chumbani wakati huo. Alimwambia abaki tu nje kwenye gari kwani hakutarajia tukio kama hilo kutokea wakati wa hafla ya ndani ya kampuni.
“Niache niende, Kimaro.” Lisa alimuuma Willie kwa nguvu.
Willie aliachia mkono wake kwa maumivu kisha akacheka. “Hakika wewe ni mjanja. Hiyo inavutia. Napenda wanawake wachangamfu kama wewe.”
“Una kichaa?” Lisa alishangaa, “familia ya Kimaro ni moja ya familia zenye heshima kubwa. Sikutegemea kama kuna mtu mwenye kuchukiza na mchafu kama wewe katika familia yenu, au wewe si mtoto halisi wa familia ya Kimaro?” Lisa alikosoa.
“Endelea kunikosoa. Kadiri unavyonikosoa, ndivyo nitakavyokuletea taabu zaidi.” Willie alidhihaki. “Wakurugenzi wa kampuni yako wote wananichukulia kama mheshimiwa. Jones Masawe ameniomba nimsaidie kupata nafasi ya mwenyekiti kesho. Ninaweza kusema kitu kwa urahisi na kukufanya upoteze nafasi yako mara moja. Unajua nina nguvu ya 25% ya hisa za kampuni. Kwa hivyo, nitafikiria upya ikiwa utanihudumia vizuri usiku wa leo.”
Akiwa na mawazo, Lisa alijifanya kuwa na hofu na kusema, “Hii ni kweli?”
“Bila shaka.” Willie alifoka, akijua kuwa Lisa tayari alikuwa anaingia kwenye anga zake.
"Lazima unisaidie, Bwana Kimaro," Lisa alidakia na kusema kwa huruma, "naweza kukufanyia chochote."
“Vizuri sana kwa kuwa umeelewa. Unajua kilicho bora kwako. Njoo hapa basi.” Willie alifungua mikono yake.
Lisa akajitupa mikononi mwake. Harufu ya kuburudisha ya mwili wake ilijaza pua yake. Kwake, umbo lake lilikuwa bora zaidi kuliko la Lina. Moyo wa Willie ulikuwa unawaka. Alipotaka kumkumbatia kwa nguvu, alipigwa na nguvu kubwa.
Willie akainama kwa uchungu. Lisa alikuwa amechukua kalamu ya chuma kutoka kwenye mkoba wake na kumchoma nayo Willie kwa nguvu kwenye mbavu. Kalamu hiyo ilikuwa na kichwa chembamba kilichopenya kwenye nyama kama risasi. Willie aliganda kwa maumivu na hakuweza kusogea hata kidogo.
Lisa alivua viatu vyake virefu na kumpiga usoni na mwilini kwa visigino vikali vya viatu vyake. Alimpiga hadi chini, na akaishia kuwa kama samaki aliyetolewa baharini na kuwekwa nchi kavu, asiweze kusogea hata kidogo. Baada ya kuona amefanikiwa kumdhibiti Willie yeye mwenyewe, Lisa hakuwa na haja hata ya kumpigia Shani.
Baada ya kumpiga Willie, Lisa alishtuka kuona uso wake umevimba. Alifikiria kwa muda na kugundua kuwa alihitaji kumfanyia zaidi ya hivyo, na akamvua nguo zake pia.
“Unataka kufanya nini?” Willie alilalama kwa uchungu. Siku zote ndiye aliyekuwa akiwavua nguo wanawake. Yeye kamwe hakuwahi kufikiri kuwa kuna siku nguo zake zingekuja kuvuliwa na mwanamke. Macho wake yalidhihirisha ukali. Alitamani kumpasuapasua Lisa lakini hata hivyo hakuwa na nguvu hata kidogo ya kupinga kwani alipigwa vibaya viatu vya mbavuni na usoni.
Baada ya kumvua nguo, Lisa alichukua simu yake na kumpiga picha zaidi ya kumi kutoka pembe tofauti. Alimtisha kwa njia ya dharau, “Ikiwa utathubutu kuniletea matatizo kuhusu kilichotokea leo, nitatupia picha zako hizi chafu mtandaoni. Hebu tuone kama familia ya Kimaro inajali utu wao.”
“Wewe…” Willie alikasirika. Katika kipindi cha miaka 25 ya maisha yake, hakuna hata mwanamke mmoja aliyekuwa na ujasiri wa kumfanyia hivyo. “Nakuonya! Nitakushughulikia, Lisa."
“Na mimi nitakushughulikia pia.” Lisa alimjibu kwa dharau. “Ni mara yangu ya kwanza kuona mwili mbaya kama huu. Unakera na kuchukiza kama nini!"
Lisa akampa kidole cha kati na kuziitupa nguo na simu ya Willie dirishani. Baada ya hapo, alimburuta hadi chooni na kumfungia humo. Kisha Lisa alitoroka kupitia dirishani ili kumfanya Lina asielewe chochote.
Willie alilala kwenye sakafu baridi ya choo kile akiwa uchi. Hata baada ya kutumia muda mrefu kuomba msaada kwa sauti dhaifu, hakuna mtu aliyekuja kumsaidia.
Ni baada ya nusu saa kupita ndipo alianza kupata nguvu. Alitetemeka huku akinyanyuka na kuufungua mlango kwa nguvu. Baada ya kusikia kelele, Lina alikimbia kwa uangalifu kuelekea kwenye chumba hicho na kufungua mlango.
Pindi alipouona tu uso wa Willie uliojeruhiwa, alipiga kelele kwa mshtuko. “Imekuwaje tena mpenzi…”
“Nyamaza, mpuuzi wewe!” Willie alimpiga Lina kibao cha usoni na kumpiga mateke machache dhaifu kwa hasira. “Nilikuwa nakuita sasa hivi. Ulikuwa kiziwi?”
“Usinipige, mimi sikusikia. Niliogopa kukusumbua, na nilikuwa nimesimama mbali sana… Ohoo-hoo!” Lina alipiga magoti na kumsihi. Mwanaume huyo alitisha sana alipokuwa na Lina, utadhani si yeye aliyekuwa kama panzi mbele ya Lisa muda mchache uliopita.
"Potea, wewe huna maana kabisa!" Willie alianza kutetemeka tena. Kwa hasira alifoka na kuapa, “Lisa, nikishindwa kukuua, nitakula mavi yangu!”.....ITAENDELEA......
Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
