JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................118, 119


 Sura ya 118


Katika hoteli moja ya kifahari, Stephen Kileo na dada yake Janet walikuwa wakimfanyia mapokezi ya heshima mtu mmoja maarufu aliyeketi katikati ya kochi. Mtu huyo alikuwa ni Willie Kimaro ambaye alikuwa ametoka Nairobi. Willie na Alvin walikuwa mtu na binamu yake. Familia ya Kimaro ilikuwa familia ya kifahari sana na utajiri wa kutupwa. Ilimiliki makampuni mengi hapa Tanzania na Kenya, yakiwemo ya mawasiliano, Vyombo vya habari, usafirishaji na hata vituo vya mafuta ya magari. Pia walimiliki hisa kwenye makampuni mengine makubwa nchini ikiwemo Mawenzi Investiments. Ni vile tu Alvin hakuwa tayari kujionyesha kwa watu kama alitokea kwenye familia hiyo ndiyo maana watu wengi hawakumjua kiundani. Hata hivyo Kimaro ni jina la ukoo kwa familia nyingi za kichaga hivyo ilikuwa rahisi sana kwa Alvin kuficha uhusiano wake na familia yake.

“Bwana Kimaro, ngoja nikutambulishe kwa mpenzi wangu, Lina.” Stephen Kileo alikuwa ameambatana na Lina. "Baba yake, ambaye ni mwanahisa mkubwa katika kampuni ya Mawenzi Investiments, amekuletea zawadi usiku wa leo."

Usiku huo, Lina alivaa nguo ndefu ya rangi isiyokolea iliyokazia mikunjo ya mwili wake maridadi. Ingawa hakuwa mrembo kama Lisa, alikuwa amependeza sana. Familia ya Jones ilichukuliwa kuwa mojawapo ya familia za juu zilizo na ‘mbegu’ nzuri. Alikuwa amejipodoa ipasavyo usiku huo. Alipotabasamu kwa upole, hakika alionekana kama malaika aliyeshuka duniani kwa bahati mbaya.

Macho ya Willie Kimaro yaliangaza kwa hisia. Lina alikuwa na mawenge sana na wanaume matajiri. Ikiwa angeweza kumvutia kimapenzi mwanamume yule kutoka familia maarufu ya Kimaro, asingekuwa na muda na watu kama Stephen Kileo tena.

Lina alimfuata kwa tabasamu la kichokozi. “Willie, familia yangu ingependa kukupa zawadi hili. Mkufu wa dhahabu wenye kidani cha jiwe la thamani la Tanzanite kutoka Mererani, umenakshiwa na sonara maarufu hapa jijini, Enjipai Jewellery."

Alipomaliza tu kuongea, alifungua boksi. Macho ya Willie yakaangaza. “Woooh! Kidani hiki kina thamani ya mamilioni ya pesa, sivyo?”

“Sio muhimu sana, ilimradi tu unaipenda," Lina alijibu huku akijaribu kumfurahisha.

“Hahaah! Kwa kweli sikutegemea. Nakupenda sana wewe!” Willie alisugua kidani kwenye sehemu ya juu ya pua yake. Haikujulikana kama alimaanisha kuwa anampenda Lina au kidani.

Ghafla, kimya kikatanda kwenye chumba kile cha kifahari cha Hoteli maarufu. Macho ya kila mtu yalikuwa kwa Willie. Stephen alitabasamu kwa utulivu, na mara akanyanyuka yeye na Janet wakatoka nje. Kisha Lina alikaa na Willie kwa muda wote wa usiku. Aliimba na kuzungumza naye. Kwa vile alikuwa mzuri katika kukonga nyoyo za wanaume, mara alimfanya Willie acheke kimoyomoyo.

Baadaye Lina alielekea mapokezi mara moja. Dakika alipotoka nje ya kaunta, alimuona Stephen akisubiri nje.

“Asante kwa usiku wa leo, Stephen. Natumai Willie anaweza kuisaidia familia yangu kurejesha nafasi ya mwenyekiti wa Mawenzi Investiments.” Lina alitabasamu huku akizungusha mkono wake kiunoni kwa Stephen. 

"Natumai atasaidia." Stephen alitabasamu bila huruma. “Kwa hiyo Willie na wewe—”

Lina akamkatisha mara moja, “Usinielewe vibaya. Unajua kuwa wewe bado ndiye ninayekupenda. Sasa hivi, Kimaro bado nina maongezi naye—”

“Ninaelewa. Sina wazo lolote baya kuhusu hilo.” Stephen alimpiga piga nyuma ya mkono wake. "Ni wakati tu familia yako itakaporejesha kiti chake cha uenyekiti wa kampuni ya Mawenzi ndipo familia zetu zote mbili zinaweza kufanya maendeleo zaidi na kufikia mambo bora zaidi."

"Ni vizuri umeelewa." Lina hakuwa akimfikiria kabisa Stephen moyoni mwake tena baada ya kuona Willie amekaa mkao wa kueleweka.

"Kilicho muhimu zaidi kwa sasa ni kumfurahisha Willie Kimaro." Stephen alipitisha vidole vyake kwenye nywele zake. “Nitakusubiri.” 

“Asante.” Lina alijibu kisha akarudi na keti kando ya Willie tena. Wakati huo, Willie aliweka mkono wake kiunoni mwake na kuanza kumpapasa kama alivyotaka.

Saa tano usiku, Willie alikuwa amelewa. Stephen alimuomba Lina ampeleke chumbani akapumzike.


Sura ya 119


Baada ya Lina na Willie kuondoka, Janet alimwambia Stephen kwa mshtuko, “Umerukwa na akili, Lina si mpenzi wako? Kwa nini hukunitambulisha mimi kwa Willie? Bila shaka ningeifaidisha familia yetu ikiwa ningekuwa binti-mkwe wa familia ya Kimaro.”

“Willie hakuvutiwa nawe,” Stephen alijibu kwa dharau huku akiwasha sigara.

Janet alipandwa na hasira. "Unamaanisha nini? Machoni pako, mimi si mrembo kama Lina, huh? Kwanza mimi sikukulia kijijini kama yeye—”

“Ninafanya hivi kwa faida yako.” Stephen akamkatisha. “Willie ana tabia chafu ya kulala na wanawake hovyo, hajali hata kama ni mpenzi au mke wa mtu.” 

Janet alipigwa na butwaa. Stephen aliongeza, “Wewe ni dada yangu wa damu. Ikiwa kuna njia rahisi ya mafanikio makubwa, bila shaka ningekupendelea wewe kwanza. Hata hivyo, Willie ni mhuni na malaya sana. Amewahi hata kuua mwanamke.”

"Una uhakika?" Janet akatetemeka.

“Ni kweli kabisa. Isingekuwa jamaa yetu ambaye anafanya kazi kama msaidizi wake, nisingelijua hilo.” Stephen alisimama taratibu na kusimama. “Vinginevyo, kwa nini unadhani nilimpa Lina nafasi kubwa namna hii? Yeye hana heshima pia.”

Stepehen alitulia kidogo kisha akaongeza tena, “Lakini usijali. Willie atashukuru kwamba nilimpa nafasi ya kuwa karibu na Lina. Katika hali hiyo, nitapata fursa ya kuwa rafiki wake wa karibu. Nitatumia nafasi hiyo kuinufaisha familia yetu kibiashara.” Mara Janet akaridhika.

Asubuhi iliyofuata Lina aliporejewa na fahamu, alishtuka baada ya kumuona mwanaume aliyekuwa pembeni yake ambaye alikuwa akimtumbulia macho. Huku kila kitu kilichotokea jana yake usiku kikimulika akilini mwake, alihisi kana kwamba alikuwa ameenda kuzimu kwa mara nyingine tena. Mtu huyo alikuwa anatisha, kwa kweli. Kifupi alikuwa mnyanyasaji. Wakati huo, Lina alikuwa ameumizwa vibaya sana kutokana na kuingiliwa kinyama kinyume na maumbile.

“Umeamka?” Willie alipogeuza kichwa chake na kumwangalia Lina, mtetemeko ulimtawala mwili mzima.

 “Umenifanyaje hivi?” Lina aliuliza kinyonge huku akishika sehemu zake zilizokuwa zinawaka kwa maumivu.

“Kwanini? Hujaridhika na mimi?" Willie aliwasha sigara, macho yake yakimeta kwa chuki.

"Hapana." Lina alilazimisha tabasamu. Kwa kuwa alikuwa ameyataka mwenyewe kulala naye, alifikiri kwamba haikuwa na maana tena kujutia yaliyomkuta. Aliuma meno na kujifanya kuwa na haya. Aliongeza, "Ni furaha yangu kuweza kulala na wewe, Mpenzi Kimaro."

'Ni vizuri kwamba umefurahia. Kwa kweli wewe mtoto ni mtamu sana.” Willie alivuta sigara, akimwangalia Lina kwa udadisi. "Ilikuwa mara yako ya kwanza kufanya jana usiku?"

Lina alipigwa na butwaa. Alikumbuka kwamba alikuwa amefanyiwa upasuaji wa plastiki kurudisha bikra yake kimakusudi ili kumfurahisha Stephen endapo kama wangekutana kabla ya hapo. Hakutarajia kwamba angelala ghafla na Willie jana yake usiku. Inavyonekana, Willie hakuelewa jambo hilo.

“Ndiyo-Ndiyo.”

"Sikutarajia." Willie akamgusa kidevu chake. "Huogopi kwamba Stephen atachukia?"

"Kama nilivyosema, ni heshima yangu kuweza kulala na wewe kwa usiku kucha nikizingatia hadhi yako nzuri," Lina alijibu kwa kujiamini.

Aliposikia hivyo, Willie aliangua kicheko. “Inavutia. Nakupenda sana. Nitakuwa Dar kwa muda, na utanisindikiza katika muda wangu wote hapa.”

“Sawa.” Lina alilazimisha tabasamu. "Nashangaa ni mradi gani uliokuleta hapa Dar, bila shaka ni mkubwa sana!"

“Oh. Kando na kuhudhuria hafla ya Mawenzi, Kampuni ya teknolojia chini ya familia ya Kimaro ingependa kuwekeza katika sekta ya viwanda. Nimekuja kutazama fursa.” 

Lina aliuliza kwa tahadhari, “Utawekeza kiasi gani?”

"Pengine mamia ya mabilioni ya shilingi. Hakuna kikomo kwa kiasi, ukomo utategemeana na fursa itakayopatikana.” Willie alijibu kwa kawaida.

Roho ya Lina ilimruka. Ikiwa Mawenzi Investments ingeweza kufanya kazi kwenye mradi huu, Jones na hadhi yake ingeinuliwa.

"Mpenzi Kimaro, nadhani ungetaka kufanya kazi na kampuni ya ndani kwenye mradi mkubwa kama huu..."

"Mawenzi Investments ana nia ya kushiriki katika hilo, huh?" Willie alitoa tabasamu la nguvu.


“Mpenzi, ningependa kushirikiana nawe kwa ajili ya mradi huu, lakini nimefukuzwa kutoka kwenye kazi yangu huko Mawenzi Investments. Baba yangu pia amenyang’anywa cheo cha uenyekiti wa Kampuni” Akiwa amekata tamaa, Lina alitoa tabasamu la uchungu. "Baba yangu na mimi wote tupo hatarini ..."

"Naweza kukutatulia chochote mradi tu ufanye wajibu wako vizuri katika kuniweka sawa." Tabasamu likaangaza usoni mwa Willie. "Wanawake wote wanaonizunguka hawajawahi kushindwa kupokea thawabu nzuri kutoka kwangu."

"Kwa hali hiyo, hakika nitakutendea vizuri." Kwa dhamira mbaya, alimbusu kwa hiari yake mwenyewe.

Muda mfupi baadaye, kilio cha Lina kilisikika kutoka chumbani kwa mara nyingine tena. Willie alimgeuza tena na kuanza kumshughulikia kinyama. Akiwa analia kwa uchungu, alijiwazia, 'Lisa, ninateseka sana sasa kwa ajili yako. Hakika nitakulipa na riba katika siku zijazo!”

•••

Mwaka ulikuwa unaelekea ukingoni. Maadhimisho ya kumbukumbu ya Mawenzi Investments yaliadhimishwa katika hoteli ya nyota saba.

Sio tu kwamba Mawenzi Investments alialika watu mashuhuri wachache kwa usiku huo, lakini idadi kubwa ya wafanyabiashara wenye nguvu pia walikuwa wamejitokeza.

Ilikuwa ni saa moja kamili jioni ambapo Lisa akiwa ni mwenyekiti aliyeteuliwa hivi karibuni, aliwasili katika hoteli hiyo. Lisa aliendesha polepole hadi hotelini kwa gari aina ya Range Rover.

Mlango wa gari ulipofunguliwa, alionekana akiwa amevalia gauni refu jeusi la mtindo wa zamani na akiwa ameshikilia mkoba wa zamani uliopambwa. Kwa kawaida si rahisi kuwa kivutio cha watu kwa mtu aliyevaa nguo nyeusi. Hata hivyo, Lisa alibaki mrembo na mzuri akiwa na uso wake mwanana na wa kuvutia na mdomo uliokolea lipstick nyekundu iliyofanana na waridi linalochanua.

Waandishi wa habari walianza kuchukua kamera zao ili kupiga picha zake. Kwa wadhifa wake na utambulisho wake, angeweza kuchukuliwa kuwa C.E.O mwanamke mwenye umri mdogo na mrembo zaidi jijini Dar es Salaam. Lisa akapiga pozi kwa ajili ya picha, lakini muda mfupi baadaye, kelele za ghafla zikasikika kando yake kutoka kwa waandishi wa habari.

“Fanya haraka utazame! Je, hili si toleo la pekee la Bugatti Veyron L'Or Blanc?"

“Nilisikia limetengenezwa kwa chuma cha titanium. Linagharimu zaidi ya Shilingi milioni mia saba!"

“Angalia namba ya usajili, ni private number. KIMARO! Inashangaza.”

“Kweli inashangaza. Ni nani huyo? Yuko hapa kuhudhuria sherehe ya ukumbusho wa Mawenzi Investments?”

“Tazama! Mlango unafunguliwa.”

Akiwa amezungukwa na sauti za watazamaji, mwanaume mmoja aliyevalia suti ya bluu iliyokolea alitoka kwenye kiti cha dereva. Sifa zake zilitamkwa, na tabasamu la kishetani lilionekana usoni mwake.

Kulikuwa na vifijo kutoka kwa waandishi wa habari katika umati huo.

"Yeye ni mzuri sana!"

“Namfahamu yeye ni nani. Yeye ni Willie kutoka familia ya Kimaro."

"Familia ya Kimaro? Familia yenye utajiri zaidi hapa Tanzania?”

“Ndiyo. Ni hiyo familia ya Kimaro! Wanakaaga Nairobi.”

"Mungu wangu. Mawenzi Investments wana uhusiano na familia ya Kimaro?”

Katikati ya majadiliano ya umma, mlango wa abiria ulifunguliwa. Akiwa amevalia gauni jekundu, Lina alitoka nje ya gari kwa kuvutia huku akiushika mkono wa Willie. Sauti ikazidi kuvuma tena kutoka kwa umati.

“Huyu ni nani?”

"Lina, binti ya Jones Masawe ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa bodi ya Mawenzi Investments."

“Kwa hiyo yuko kwenye uhusiano na Willie. Anajaribu kugeuka kutoka kuwa mkulima hadi kuwa binti wa kifalme, huh?

"Kwa kuwa sasa ana uhusiano na familia ya Kimaro, familia ya Harrison na familia ya Zongo sasa watamheshimu Jones."

Maneno hayo yalimfanya Lina azidi kuridhika. Ilifaa kujipendekeza na Willie kama mtumwa kwa siku chache ili apate taji la utukufu na heshima siku za baadaye. Alipogeuza macho yake, alitokea kumwona Lisa aliyekuwa mbele yake akiwa anamshangaa bila ukomo.

Akiwa amekunja midomo ya waridi, Lina alimshika Willie mara moja na kuelekea kwa Lisa. "Halo, Lisa. Willie, huyu ni dada yangu, ambaye pia ni Mwenyekiti na CEO wa Mawenzi Investments.”......ITAENDELEA......


Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.