JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................116, 117


Sura ya 116


“Ni rahisi sana kupata tena mamlaka," Stephen Kileo alisema ghafla. 

Wakishangazwa na maoni hayo, Jones na familia yake walimtazama kwa makini. “Stephen, tuambie haraka wazo lako. Sisi ni familia,” Lina akasema mara moja, “Mara tu Lisa atakapoanguka madarakani, tutaoana mara moja.”

Stephen alikodoa macho na kusema; "Willie Kimaro kutoka familia ya Kimaro anakuja Dar kwa ukaguzi wa miradi waliyowekeza hapa jijini. Kma tutaweza kumfurahisha, tunaweza kumtumia kuwamngusha Lisa.”

Macho yao yote yakang'aa. Willie Kimaro alitoka familia tajiri ya Kimaro. Yeye na Alvin Kimaro walikuwa watoto wa kaka na dada, yaani mtu na binamu yake. KIM International, ni kampuni ya familia ya Kimaro na ilikuwa ikimiliki asilimia 25 za hisa za Mawenzi Investments. Kwa maana hiyo ilikuwa na nguvu kubwa kwenye bodi ya wakurugenzi. Kama kweli KIM International ingeungana na Jones Masawe kumwangusha Lisa, basi angeondolewa kwenye nafasi yake ya Mwenyekiti na mtendaji mkuu wa Kampuni ya Mawenzi.

Mgawanyo wa hisa katika Kampuni ya Mawenzi ulikuwa ni 30% kwa Lisa, 30% kwa Jones Masawe na 25% kwa KIM International, 10% Chris Maganga na 5% zilizobaki zilimikiwa na wanahisa wengine wadogowadogo. Kwa hiyo wanahisa wakubwa walikuwa wanne, Lisa, Jones Masawe, KIM Internatonal na Chris Maganga. kama wawili kati yao wangeungana basi ilikuwa rahisi kumwangusha mwingine, ndiyo njia aliyotaka kutumia Jones Masawe, kutafuta njia ya kuungana na KIM International kumwangusha Lisa.

Jones alitetemeka kwa fadhaa. "Familia ya Kimaro ndiyo inamiliki KIM International. Ingawa Willie si mzao wa moja kwa moja wa familia ya Kimaro, tutaweza kumtumia kuunganisha nguvu yetu mradi tu tufahamiane na familia ya Kimaro. Ikitokea hivyo, hatutasumbuliwa na Lisa tena.”

"Ni wazo zuri sana." Stephen aliitikia kwa kichwa. “Sifahamiani na Willie lakini najuana na msaidizi wake. Kwa kuwa msaidizi wa Willie nipo naye vizuri, nitajitahidi anisaidie kuwa karibu naye na kuwatambulisha nyinyi kwake. Ili kumteka kwa urahisi mnatakiwa kuandaa zawadi ya kumfurahisha. Willie anavutiwa na vito vya thamani, na pia wanawake warembo!"

“Asante Stephen. Ninajuta kutokutana na wewe mapema. Wewe ndiye ninayeweza kukutegemea kwa sasa.” Lina alimtazama kwa hisia za kuguswa.

"Ni jukumu langu kukusaidia. "Stephen alijaribu kuficha chukizo lake kwake. 

••••

Ndani ya Mawenzi Investiments, saa kumi na mbili za jioni, Lisa alipozima taa na kutoka nje ya ofisi, mjukuu wa mmoja wa kwakurugenzi wa bodi ya Mawenzi, Amiri Gumbo alikuwa nje akimsubiria na alipomuona alimsalimia kwa shauku.

“Lisa, unatoka kazini. Ningependa kukukaribisha kwa chakula cha jioni kwenye hoteli maarufu ambayo hutoa chakula kizuri…” 

Lisa alikuwa mwisho wa akili yake. Tangu alipoanza kupata tena mamlaka katika kampuni, wakurugenzi wa bodi wote walijaribu kujipendekeza kwake kwa kuwatambulisha watoto wao na wajukuu zao kama washirika wake watarajiwa.

"Nashukuru, lakini nilipanga kula chakula cha jioni nyumbani ... " Lisa alimtosa kwa upole.

“Ngoja basi nikupeleke nyumbani.” Kijana yule aliongea kwa shauku. “Mkoba wako unaonekana kuwa mzito. Acha nikusaidie kuubeba.”

Kabla hajaugusa, Shani alishika mkono wake. Macho ya mwanamke huyo yalimtoka kwa ukali, jambo lililomfanya kijana yule ashtuke. Alikuwa amesikia kwamba mlinzi wa Lisa alikuwa mkatili na hasa stadi wa kupiga watu makofi. “Ikiwa utafanya hivyo kwa mara nyingine, sitasita kukuvunja mkono,” Shani alimwonya kwa ukali.

Kijana yule alirudi nyuma kwa aibu. "Unajua mimi ni nani? Sawa, hata hivyo wewe ni mlinzi tu. Ulinzi ni kazi gani? Hata mbwa anaweza kulinda, kwa hiyo mimi siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa.” Kijana yule aliropoka tu kwa aibu ya kuadhibiwa na mwanamke.

Wakati huo lifti ilikuwa tayari imefika. Kiijana huyo alipoona Lisa anaondoka akamfuata akiwa na maneno ya kuvutia. “Lisa, umesikia kuhusu mkufu wa Malkia? Kuna stori kuwa miaka mingi iliyopita, mfalme alimpa malkia wake mpendwa mkufu. Mtu yeyote ambaye atavaa mkufu huo atafikia furaha katika uhusiano wake. Mkufu huo utauzwa kwa mnada hivi karibuni kule Mlimani City. Nitakununulia, sawa?"


"Hapana Asante. Sihitaji.” Lisa alijibu kifupi. Kijana yule alionekana kumganda kama jojo iliyong’ang’ania kwenye nguo ambayo ilikuwa vigumu kuiondoa.

Mara tu Lisa alipotoka nje ya jengo hilo, aliona mtu aliyemfahamu vizuri akiwa amesimama kwenye mraba. Alijawa na mchanganyiko wa mshangao na furaha. Taa za rangi mbalimbali ziliwaka polepole usiku. Alvin, ambaye alisimama kando ya geti kuu, alikuwa amevalia suti nyeusi na koti la rangi ya parachichi kana kwamba alikuwa ametoka kushiriki katika Wiki ya Mitindo ya Paris. Alionekana mtanashati sana, na sura yake ilikuwa ya kuvutia kweli. Hata hivyo, macho yake meusi yaliangaza kwa huzuni dakika moja alipomwona mtu aliyemfuata Lisa kwa nyuma.

"Alvlisa, kwa nini uko hapa?" Lisa hakugundua mawazo ya Alvin. Alimkimbilia na kuzungusha mikono yake kwenye kiuno chake kwa furaha.

Unyogovu ndani ya macho yake ulipungua polepole. Alimwangalia yule kijana kwa macho mabaya. "Inaonekana nilikuja kwa wakati mbaya, ona sasa nimevuruga miadi yako."

"Yeye ni nani, Lisa?" Yule kijana naye alikasirishwa na Alvin. Huku wote wawili wakiwa wamevalia kifahari, jinsi Alvin alivyokuwa na umbo bora na maridadi ilimfanya yule kijana aonekane mtu wa chini sana.

Alvin alikaa kimya. Aliinua uso wake huku akimwangalia Lisa, akiwaza ni namna gani atamtambulisha kwa mwanaume huyo.

“Ni mpenzi wangu,” Lisa alijibu moja kwa moja. "Ninajua nia ya babu yako, Mzee Amiri Gumbo, lakini tayari ninampenda mtu mwingine. Tafadhali pia mwambie babu yako kuwa nina shughuli nyingi hivyo asitume tena vijana wake kuja kunisumbua. Sina wakati wa kukaa kuongea na vijana wadogo kama nyinyi."

Hakutaka kukata tamaa, yule kijana mjukuu wa Mzee Amiri alisema, “Wewe ni mjanja. Afadhali ufikirie kwa busara. Ukiolewa na familia ya mkurugenzi katika kampuni, itatusaidia sote wawili. Kwa maoni yangu, mpenzi wako hana kitu kingine isipokuwa sura ya mauzo tu. Yeye si mpenzi mzuri kwako.”

Uso wa Alvin ukaingia giza huku mikono ya Shani ikianza kumuwasha na kuchezacheza kwa nguvu, akisubiri tu ruhusa ya bosi wake ili agawe kichapo. Shani alimtazama kijana yule kana kwamba ni mtu wa ajabu sana.

“Asante kwa ushauri wako, lakini ndiye ninayempenda. Nimeanguka katika kumpenda bila matumaini, na ndiye anayestahili upendo wangu. Tafadhali ondoka sasa hivi.” Lisa alimfukuza kwa namna ya kudharirisha sana.

"Kwa kweli hujui ni nini kinachokufaa." Kijana yule alimkodolea macho Lisa kabla hajaondoka kwa kukata tamaa.

Lisa akashusha pumzi. Aligeuza kichwa chake na kukutana na macho ya Alvin yaliyochangamka. Alishtuka kwa kufikiria maneno ambayo alikuwa ametoka kusema yangekuwa yamemuudhi. “Nilitaka tu asiendelee kunisumbua. Usielewe vibaya…”

“Kwani umekosea nini?” Alvin aligeuka ghafla. Akayakazia macho yake huku akitoa tabasamu la busara. “Ina maana unanipenda bila matumaini?”

“Tatizo lenu wanasheria kila kitu lazima mtafsiri.” Lisa akacheka.

“Hili lipo wazi wala halihitaji tafsiri, kwamba unanipenda tu lakini huna matumaini yoyote na mimi, sivyo?” Alvin alidadavua na kumchosha kabisa Lisa. Lisa akakosa la kusema.

Ukimya wake ukamfanya Alvin atabasamu. "Ingia kwenye gari."

Lisa alimwambia Shani aondoke na gari lake kisha yeye akaingia kwenye gari la Alvin. Gari ilisafiri hadi barabara kuu na ili kuondoa upweke, Lisa alijaribu kuanzisha mazungumzo mengine. "Umekula?" 

Tumbo la Alvin lilinguruma hata kabla hajajibu. Baada ya kimya cha sekunde mbili, Lisa alicheka. "Ni saa kumi na mbili tu sasa hivi. Mbona tayari una njaa? Hukula chakula cha mchana?” 

“Chakula cha ofisini hakikuwa na ladha nzuri,” Alvin alisema kwa hasira, “Ni muda mrefu umepita tangu unipikie. Unafikiri kwamba kuvunjika kwa mkataba ndiyo mwisho wa makubaliano? Kumbuka bado sisi ni wanandoa.”

"Nina mengi kwenye kichwa changu sasa hivi." Lisa alihisi kuchoka kabisa. “Nitatayarisha kifungua kinywa ili uende nacho ofisini kila asubuhi, sawa?”

"Unanichukulia kama mwanafunzi?" Alvin alimkazia macho. Sekunde chache baadaye, aliongeza, "Sawa basi, utakavyopenda mwenyewe." Lisa alikosa la kusema.


Ni mabadiliko ya haraka kama nini katika maisha ya Lisa ndiyo yaliyomnyima raha Alvin. Tangu aanze kufanya kazi huko Mawenzi Investiments, hakuwahi kumwandalia chakula kitamu kama zamani, Alvin ali’miss sana mapishi yake.

“Nisikilize. Tukifika nyumbani usiku huu, ninataka kula nyama ya choma ya nguruwe, saladi ya…”

Lisa alimshika mkono na kupiga kelele za furaha kabla hajamaliza sentensi yake. “Tulia…Acha! Wacha nikupeleke tukale vyakula vya uswahilini usiku wa leo. Ghafla natamani miguu ya kuku, shingo, vichwa, firigisi na vipapatio vya kuku vilivyokaangwa, mihogo ya kuangwa na kachumbari...”

“Una kichaa? Unawezaje kunilazimisha kula takataka za aina hii?" Alvin alishtuka na kukasirika sana hata ndita zake zilikuwa zimejikunja.

“Umekosea kusema hivyo. Watu wengi wanaishi kwa kula aina hii ya chakula, sawa? Weka vizuri kauli zako. Hata kama hupendi lakini mimi nina hamu ya firigisi za kuku zilizokaangwa. Kama mume wangu ni wajibu wako kunisikiliza, haya ndiyo makubaliano yetu mapya!”

Lisa aliendelea kukuna mikono yake. Wakati mkataba ulipovunjika na makubaliano mapya yalipoanza kutumika, msimamo wao katika uhusiano haukuwa kama zamani na ilimbidi Alvin amsikilize. Sasa, angeweza kufanya chochote alichotaka na kula chochote alichotamani na roho yake.

Alvin hakuwa na la kufanya zaidi ya kuendesha gari hadi Coco Beach na kuegesha kando ya barabara. Wawili hao waliingia kwenye vibanda vya wakaanga nyama za kuku pamoja.


Sura ya 117


Msongamano wa wateja wengi waliokuwa wakiingia na kuondoka pale Coco Beach pamoja na harufu ya nyama vilimyima kabisa amani Alvin. Alikosa raha hadi akakunja uso.

“Nenda ukachukue kiti. Chukua kiti hicho kiko wazi..." Lisa alimwambia Alvin aliyekuwa amesimama tu akishangaashangaa. Lisa alionekana kutokuwa mgeni sana kwenye mazingira kama hayo.

Lisa alinyoosha kidole kuwelekeza Alvin kwenye meza tupu ambayo ndo kwanza mteja alikuwa ametoka. Takataka za mabaki zilizokuwa mezani hazikuwa hata zimesafishwa.

"Sitakaa hapo mimi." Alvin alimpiga Lisa jicho kali. Lisa akamfuata na kumsisitiza. Maneno ya Lisa ya kubembeleza yalimfanya Alvin akose la kusema. Kwa hayo, akasogea pale na kuketi kwa kusitasita.

Dakika kumi baadaye, Lisa aliandaa mlo kamili wa familia, ambao ulijumuisha firigisi na kila sehemu ya kiungo cha kuku vikiwa vimekaangwa, mihogo ya kukaangwa, kachumbari na aiskrimu.

“Kula hii firigisi ya kuku, ni tamu.” Lisa alinyakua kipande na kumlisha kwa shauku. Alvin akakwepesha na kusukuma mkono wake pembeni.

"Ngoja nikuonyeshe kitu." Alvin akatoa simu yake na kusogeza hadi kwenye ukurasa unaoonyesha habari mbaya kuhusu nyama za kukaangwa hovyo mitaani. Kisha, akampitishia Lisa.

Baada ya kuangaza macho kwenye picha mbaya ya sahani ambayo ilikuwa na vipande vichache vya vipapatio na zaidi ya miguu kumi ya kuku, Lisa alijawa na karaha. "Alvin, huwezi kupata madhara kwa kula chakula hiki mara moja tu."

"Vitu vya aina hii vina kiasi kikubwa cha viambato vya sumu. Baada ya leo, huruhusiwi kula aina hii ya chakula tena. Wewe hata si mtoto.” Alvin alidhamiria.

Lisa hakuweza kuwa na wasiwasi juu yake. Aliinamisha kichwa chini na kupiga msosi kisawasawa. Baada ya kula vipande kadhaa, aligundua kuwa vingine vilikuwa na ladha mbaya, na badala yake akaviingiza kinywani mwa Alvin.

Huku mdomo wake ukiwa umejaa chakula ghafla, Alvin alimtupia jicho la hasira. Lisa alijifanya kuwa mwadilifu. “Si wapenzi wa kiume hutakiwa kula chochote ambacho wasichana wao huwalisha? Angalia wanandoa kando yetu. Ndivyo wanavyofanya pia.”

Wapenzi vijana walioketi kando yao walikuwa wanafunzi wa chuo kikuu. Baada ya msichana kukerwa kidogo na kipande cha nyama alichokuwa anatafuna mdomoni, alimpa mpenzi wake. “Haina ladha nzuri. Unaweza kula?”

Mpenzi wake naye akajibu, "Unafikiri naweza kusema hapana?"

Lisa naye alikoroma kwa wivu. “Kwanini hutaki kula firigisi niliyoiuma, unanionea kinyaa, huh? Kumbe hunipendi?” Alvin alishindwa cha kusema.

Lisa aliyekaa mkabala naye alikunja uso huku akimwangalia. “Jinsi ninavyowatamani. Ninapenda kuwa kwenye uhusiano kama huo."


"Nyamaza." Huku akifungua mdomo, Alvin alichukua kipande cha kuku kilichobaki mkononi mwake na kukiuma.

Kwa wakati huo, Alvin bado hakuweza kumwelewa Lisa hata kidogo. Alikuwa akimtii, lakini kwa nini kulikuwa na badiliko kubwa hivyo ndani yake sasa? 

Baada ya hapo, walimaliza kula firigisi zote za kukaanga, na hata ice cream iliyobaki. Hawakutambua kuwa kuna mtu alikuwa amewapiga picha kwa siri na kuiweka kwenye group whatsapp la kikundi cha wanasheria wenzake na Alvin.

Sam alikuwa akipata nyama choma katika mgahawa mmoja wa kisasa alipoona picha hiyo. Karibu apaliwe na minofu ya nyama. Haraka alisevu picha hiyo na kuisambaza kwenye makundi mengine aliyokuwa na marafiki zake.

Chester: [🤩Macho yangu yananidanganya? Alvin angewezaje kuingia Coco Beach?] 

Rodney: [Damn! 🤪Sijawahi kuona Alvin akila firigisi za kukaangwa uswazi. Huyu ni Alvin kweli?🙄🙄🙄]

Sam: [Nooooo. Hii ni kweli. Mwanasheria mwenzetu kutoka kampuni yetu alimpeleka binti yake huko Coco beach na kumwona Alvin akila vipande vya nyama ya kuku wa kukaangwa kwa furaha pamoja na Lisa.]

Chester: [🤮🤮🤮Hiyo ni mbaya sana, si hadhi ya Alvin. Utakaporudi, nitakupokea kwa mlo wa hali ya juu wa Kijapani.] 

Rodney: [Nakubali. Rudi haraka, Alvin. Nitamwomba mmoja wa wapishi wakuu Kenya akuhudumie.]

Sam: [🤥Nathubutu kuweka dau la milioni tano kwamba Alvin hawezi kuhangaika kuhusu nyinyi. Nina hakika hatajali kula hata Losholi la kimasai ama kichuri cha kikurya mradi tu Lisa yuko karibu naye.]

Ni pale tu Alvin alipotoka kwenye eneo la ufukwe huo ndipo alipogundua fujo zilizokuwa zikiendelea kwenye group hilo la whatsapp. Alifadhaika sana na kujawa na hasira.

Baada ya kuingia kwenye gari, Lisa alimsogelea na kumbusu mdomoni. Macho yake meusi angavu yaliwasilisha hisia za furaha na mahaba. “Asante, Alvilisa. Nimefurahia sana chakula cha jioni ya leo." 

Alvin hakuonekana kufurahia kabisa. "Kwa hiyo unajaribu kunifanya nisahau kuhusu jambo hili kwa njia hii, huh? Unajua kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuingia Coco Beach usiku wa leo na kula chakula cha ajabu?”

Lisa alihisi kuwa Alvin alikuwa anajifanya tu kuchukia. Wakati mwingine, wanawake hutawala kwa urahisi tu. Mara baada ya kugundua kuwa Alvin alifurahia kitu alichomfanyia, alimwongezea dozi ili kumlainisha kabisa. Aliuma mdomo wake wa waridi, kisha, akaweka mikono yake shingoni mwake na ulimi uliojaa mate na akambusu tena.

Safari hii, Alvin alimshika kichwa na kumpiga busu refu. Alipoanza kuvuta pumzi za uchovu ndipo alipomwacha apumue........ITAENDELEA.....


Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.