JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................122, 123


Sura ya 122


Alvin, ambaye alikuwa na mkutano wa video katika chumba chake cha maktaba, alisikia sauti ya gari kutoka chini. Wakati huo alikuwa anasikiliza mipango mbalimbali ya maendeleo ya miradi yake. "Mpango huu hauwezekani. Njoo na mwingine." Alipomaliza tu kuongea, alikatisha mkutano na kuelekea chini.


Akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa, Lisa akaingia mlangoni. Alisahau hata kubadili viatu vyake. Alvin alikodoa macho na kutazama gauni lake refu jeusi. Alionekana kuvurugwa tofauti na alivyoondoka.


Akiwa amekunja uso, Alvin alimtupia macho ya mshangao na udadisi Lisa. Alipoyaelekeza macho yake chini, ghafla aliona ufa kwenye pindo za gauni lake.


“Mbona nguo yako imetatuka?” Macho yake meusi yalikuwa yakimtazama kama mshale.


Alipojitazama tu chini ndipo alipogundua. Labda nguo hiyo ilikuwa imeshikana na kitu chenye ncha kali alipotambaa nje ya dirisha kutoka kwenye chumba kile cha hoteli. “Nilinasa sehemu kwa bahati mbaya.” Lisa aligeuza macho yake, hakutaka ajue kwamba alikuwa amemchokoza Willie Kimaro. Hata hivyo hakujua kabisa kama wana uhusiano wa aina yoyote. Kwa mawazo yake, Alvin alikuwa wakili tu, na asingekuwa na uwezo wa kuwa na uhusiano wowote na familia tajiri ya Kimaro. Alijua ni majina ya ukoo tu ndiyo yamefanana.


"Una tabia mbaya ya kunitazama kila wakati unaposema uwongo." Alvin alishika kiuno chake chembamba kwa nguvu, macho yake meusi yakionyesha hisia kali ya ukali. “Ulihudhuria sherehe ya ukumbusho usiku wa leo, sivyo? Nani alikuletea shida?”


“Hakuna aliyenifanya chochote. Haya, nani anaweza kunigusa wakati mimi ni mwenyekiti?” Lisa alimsukuma na kwenda juu. “Naenda kuoga."


"Usinifiche Lisa." Alvin akamvuta kuelekea kwake tena. “Angalia jinsi ulivyokosa amani kwa sasa. Afadhali unieleze ukweli kama unanichukulia kama mume wako.”


Lisa alipiga kelele, na macho yake yakawa mekundu licha ya yeye mwenyewe kupenda. “Nimemkosea mtu ambaye sikupaswa kumkosea katika ulimwengu mzima wa kibiashara. Alvlisa, kama… Ikiwa… mtu huyo ananilenga, usithubutu kufikiria kunisaidia. Afadhali unikane kabisa kuliko kunisaidia vinginevyo utapoteza kila kitu. Yeye si sawa na Clark Zongo…”


Alvin aliinua macho yake na kuuliza. “Unaamaanisha nani huyo anaweza kunitisha mimi?”


"Willie Kimaro, kutoka familia ya Kimaro." Lisa alisema huku akihema. “Biashara zao kubwakubwa zimetapakaa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki yote, pia wanamiliki asilimia 25 za hisa za Mawenzi.”


Alvin alishindwa cha kusema. Hilo lilimshangaza sana. Tangu lini Willie, yule bwana mdogo mpuuzi tu, akawa mtu ambaye kwa hakika anaogopwa kiasi kile na matajiri wa Dar es Salaam? Ina maana Lisa hakumchukulia yeye  kama mtu mwenye nguvu? Anyway, halikuwa kosa lake kwa sababu alimficha utambulisho wake halisi.


“Umeshtuka sana?” Lisa alituliza baada ya kumuona Alvin akiwa kimya sana, hivyo mara moja akamfariji. “Lakini usijali. Kwa bahati nzuri, nilikuwa na kalamu ya chuma kwenye mkoba, alipojaribu kunivamia chumbani nilimchoma na kalamu kwenye mbavu akaanguka, nikampiga sana na visigino vya viatu. Kisha, nilimvua nguo zake na kumpiga picha…”


“Ulimvua nguo?” Macho ya Alvin yalionyesha hasira na huzuni, na kusababisha hali ya mazingira kuwa tata ghafla.


"Ah ... nilikuwa najaribu kumtisha tu akae mbali na mimi, nimemwambia akijaribu kunifuatilia wakati mwingine nitamdharirisha mtandaoni." Kwa kupoteza, Lisa alieleza, “Sikuwa na la kufanya. Unafikiri nitakuwa nimekosea sana?”


“Una akili?” Alvin alishusha pumzi ndefu huku akihofia kuwa angepatwa na wazimu. “Kwa hiyo umeona na nanihii yake?”


Akiwa chini ya macho ya hatari ya mwanaume huyo, Lisa alikuna kichwa na kukohoa kidogo. " Eeh..Aah..Hapana. Inachukiza. Yeye ni ngozi na mifupa tu, na umbile lake si zuri kama lako pia. Kinyume chake, wewe ni mrefu na umejengwa vizuri. Ninapokutazama, ninavutiwa na wewe. Kukutazama kwa mara ya pili kunanipaga wazimu kwe—”


“Nakupandisha wazimu?” Macho meusi ya Alvin yalimtoka huku akivaa tabasamu la sifa.


Lisa alijisikia mkanganyiko wa kimawazo. Akijihisi hana cha kusema, alimwambia, “Sasa si wakati wa kuzungumzia jambo hili…”


“Nipe simu yako.” Alvin alinyoosha mkono wake kuelekea kwake.

Mara moja akampitishia simu yake. Alvin alipozitazama zile picha alizidi kusononeka. Muda mfupi baadaye, alihamishia picha hizo kwake na kuziondoa zote kwenye simu ya Lisa.


“Haya, kwanini umezifuta…” Lisa alikosa raha.


"Kama mwanamke wangu, huoni aibu kuweka picha za mwanamume mwingine kwenye simu yako?" Akiwa anamwangalia kwa ukali, alionya, "tena umepiga picha ukiwa umezingatia kabisa sehemu zake za siri!" Lisa alikosa la kusema. Aliinamisha kichwa chini bila kutamka neno lolote.


“Nenda ghorofani ukalale. Usifikirie mambo kupita kiasi kwani tayari umempiga picha kama hizo. Familia ya Kimaro inajali sana hadhi yao, hawawezi kukuacha salama pindi utakapozisambaza picha hizi.” Alvin alisema kile ambacho hakumaanisha kumfariji.


“Kweli?” Lisa alikuwa na shaka juu yake. "Lakini sidhani kama Willie ni mtu anayejali hadhi ya familia yake. Anastahili kutendewa vibaya kama hivyo. Nilimpiga vibaya sana.”


“Hujui ni kiasi gani wanaume wanajali utu wao ikilinganishwa na wanawake. Wewe si mwanaume, kwa hivyo hutaelewa. Naamini hatakuwa na ujasiri wa kukutafuta. Umelishughulikia jambo hili vizuri sana,” Alvin aling’oa risasi na kuendelea kueleza kimafumbo.

Ni mara chache alimpongeza Lisa. Kwa hivyo Lisa alishtuka kidogo aliposikia pongezi zake. Labda Alvin alikuwa sahihi. Huenda alikuwa haelewi kabisa wanaume.


"Baada ya kusema hivyo, usivue nguo za mwanaume tena." Baada ya kutulia, Alvin alimuonya kwa huzuni, "Bila shaka, isipokuwa mimi tu." Lisa alishindwa cha kusema na kubaki anacheka tu.


“Nenda ukaoge. nitakusaidia kwa hilo.” Alvin hakujali macho yake ya kusema, akauweka mkono wake kiunoni na kumbeba juu juu moja kwa moja.


“Sitaki." Lisa alipiga kelele kwa aibu. Alikuwa ameweka wasiwasi na hofu nyuma yake.


Usiku, ilimchukua Alvin muda kutafuta usingizi wake bila mafanikio. Mwishowe aliamua kushuka chini, akaingia kwenye gari na kuondoka kwenye nyumba yake ya kifahari.

•••

Usiku wa manane, Willie alirudi hotelini baada ya kufungwa majeraha yake hospitalini. Kwa hasira kali, akatoa simu yake ili apige.


"Kwa ndoano au kwa hila, nyinyi watu lazima mumtie Lisa kuzimu. Sitaki kusikia anaendelea kuishi mbwa yule.”


Alipomaliza tu kuongea, mlango ukasikika ukigonwa kwa nguvu. “Ni nani huyo mwenye kelele anayebisha saa za usiku hivi? Una hamu ya kifo, huh?" Willie alikimbia kuelekea mlangoni ili kuufungua, lakini akafunikwa na gunia. Ghafla, mtu fulani alianza kumpiga.


Mtu huyo alikuwa mkatili na mkali. Aliendelea kuupiga teke mwili wa Willie kwa nguvu. Wakati gunia liliipofunuliwa. Mtu mrefu na mpana aliingia ndani. Mwanaume huyo alikuwa amevalia sweta nyeusi. Vipengele vyake vya kuvutia vilipoainishwa chini ya taa zenye giza kwenye chumba, Willie alihisi hofu na hali ya hatari iliyouzunguka mwili wake.


“Alvin… Hapana, ninamaanisha kaka Alvin. Kwa nini… Kwa nini uko hapa?” Willie angeweza kumtambua mara ya kwanza. Kwake, mtu huyo alifananishwa na shetani. Alikuwa mwanaume pekee katika familia nzima ya Kimaro ambaye Willie alikuwa anamuogopa.


"Umekuwa ukifanya kazi na Jack Kimaro hivi karibuni lakini hukujua nilipo?" Huku mikono yake ikiwa mfukoni, Alvin aliingia ndani kwa majivuno na kumkanyaga Willie kifuani.


Willie alitetemeka kwa hofu. “Kaka Alvin, sijui unasemaje. Ndiyo, ni Jack ambaye amekuwa akisimamia KIM International hivi karibuni, lakini… Lakini sote tunafahamu kuwa uwepo wako katika kampuni ni wa umuhimu mkubwa. Kwa kweli, wewe ndiye bosi wa KIM International.”

"Ujuzi wako wa kuongea maneno ya kuhadaa umeongezeka. Hivi ndivyo unavyofanya mbele ya Jack pia?" Alvin alimpiga teke Willie kidevu kwa madaha kwa kutumia ncha ya kiatu chake. “Bado ninakumbuka mambo yote ambayo baba yako alifanya. Alimsaidia Jack kushusha cheo changu.”

“Hapana, kaka Alvin. Sote tunakungoja.” Willie aliogopa sana kufanya kelele yoyote.

"Mnaningojea wapi wakati umekuja Dar es Salaama kimyakimya kukagua biashara na kufanya mipango ya kupanua uwekezaji?" Sura ya dharau iliosha usoni mwa Alvin. "Mnajaribu kubadilisha teknolojia za kimsingi za kampuni wakati mimi sipo karibu, huh?"


Sura ya 123


Huku akiendelea kumkaripia kwa hasira, Alvin alikanyaga kifua cha Willie. "Leo, umeonekana kuwa wa kushangaza sana huko kwenye sherehe za Mawenzi, huh? Kwa tabia zako chafu, unawezaje kuthubutu kuanzisha fujo huko hotelini? Huenda usijali kupoteza sifa yako, lakini familia ya Kimaro inajali sana hadhi yake. Unajichukulia kama bosi wa KIM international na kisha unatumia nafasi hiyo kufanya mambo ya hovyo ya kushusha hadhi ya kampuni?"


“Kaka Alvin, najua ni kosa langu. Sitafanya tena,” Willie aliendelea kumsihi kwa woga.


"Hapana. Nadhani wewe ni jasiri sana. Unathubutu hata kujaribu kupata kipande cha mapenzi ya mwanamke wangu.” Alvin alicheka kwa huzuni.


Willie alipigwa na butwaa. "Lina ni mwanamke wako?"


"Sitavutiwa na mwanamke mchafu wa aina hiyo." Alvin akainama taratibu na kuchuchumaa. Macho yake ghafla yakageuka kuwa makali sana.


Akiwa amepigwa na mawazo, Willie akauliza kwa mshangao, “Unamaanisha… Lisa…?”


“Ni vizuri kwamba unamkumbuka. Sipendi kudhani kwamba nilimuonea mtu asiye na hatia baada ya kumalizana na wewe.” Alvin akajiweka sawa.


Willie alifahamu mbinu ambayo Alvin angetumia. Akiwa amechoka, mara akatambaa kwa shida. Alipiga magoti sakafuni na kumsujudia Alvin. “Pole, kaka Alvin! Kwa kweli sikujua. Ni kosa langu. Nilikuwa kipofu. Tafadhali niruhusu niachane na…”


Alvin alimpiga teke kali hadi akajibamiza ukutani. Willie alitema damu iliyojaa mdomoni. "Kwa kuwa huwezi kudhibiti hiyo sehemu yako ndogo ya mwili, wacha tuiondoe kabisa..." Alvin akapiga hatua kuelekea kwake.


"Hapana." Willie alitetemeka kwenye buti zake. “Kaka Alvin, sitarudia tena. Ukiharibu, bibi yangu ataumia moyoni kwani ananipenda. Pia Babu atakasirika.”


"Sawa, niambie ninachoweza kufanya ili nifikirie kukusamehe." Alvin alimkanyaga kwa nguvu kwenye ‘jongoo’ lake.


Machozi yalitiririka usoni mwa Willie kutokana na maumivu. Akiwa ameshikilia sehemu ya chini ya suruali ya Alvin, aliomba na kusihi, “Hapana, hapana. Naweza kufanya vile unavyotaka. Nitapiga magoti na kuomba msamaha kwa Lisa kesho.”


“Sawa. Kumbuka ulichosema.” Alvin aligeuza kichwa chake na kumwambia mtumishi wake wa chini, “Kwa vile anafurahia kufanya wanawake vibaya, vua nguo zake na umpeleke kwenye kibaraza. Wacha apigwe na upepo baridi wa baharini usiku kucha, labda ataikumbuka siku ya leo kila atakapokuwa anafikiria kufanya ujinga.”


Mtetemeko ulishuka kwenye uti wa mgongo wa Willie. Kabla ya hapo, Lisa alikuwa amemvua nguo na kumwacha amelala kwenye sakafu ya choo kwa muda wa nusu saa, na kumfanya ashikwe na baridi. Mbaya zaidi alikuwa anaenda kupigwa na upepo wa baharini kwa usiku mzima. Ilikuwa ni saa sita usiku na dakika kadhaa. Wawili hao walikuwa wakatili kwelikweli.


“Kaka Alvin, nitaganda hadi kufa.” Willie alijitetea.


“Usijali. Kwa kuzingatia kuwa wewe ni binamu yangu, sitakuacha ufe. Ambulance ya hoteli hii iko kwenye standby hapo chini. Utaokolewa mara moja ukibaki na pumzi yako ya mwisho." Alvin akampiga bega huku akimkumbusha kwa sauti ya upole. Kwa hayo, aligeuka na kuondoka.


Willie alikuwa kwenye hatihati ya kuanguka. Aliapa kwamba hatamchokoza Lisa tena.

•••

Saa mbili kamili asubuhi, Lisa alipokuwa akiandaa kifungua kinywa jikoni, alipokea simu kutoka kwa Chris Maganga. "Lisa, wakurugenzi wanataka kufanya mkutano mkuu wa dharura leo asubuhi." Chris alieleza. “Wanadai kwamba ulimpiga Bwana Kimaro jana usiku, kwa hivyo wanaomba ufukuzwe kwenye nafasi yako ya mwenyekiti. Pia, ikiwa hautapiga magoti na kuomba msamaha kwa Bwana Kimaro, watakuondoa kwenye bodi ya wakurugenzi pia."


Lisa aliondoa apron yake mara moja. “Nakuja sasa hivi.” Alipokata simu, alielekea mlangoni kama upepo.


“Kifungua kinywa changu kiko wapi?” Akiwa amevalia nguo za kulalia nyeusi, Alvin alitokea akishuka chini kivivu huku akipiga miayo. Haijalishi alivaa nini, alikuwa akivutia tu kwa macho kutokana na umbile lake lenye nguvu.


"Kuna jambo la dharura limetokea ofisini. Shangazi Linda atakuja kukuandalia.” Lisa alibadilisha viatu vyake haraka na kukimbilia nje ya jumba hilo. Ndita za Alvin zilijikunja sana. Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu apate kifungua kinywa kilichoandaliwa naye.


Saa mbili na nusu asubuhi Katika chumba cha mkutano, wakurugenzi wote walikuwa na nyuso za huzuni na zenye hasira. Kwa kutajwa kwa Lisa, walitamani kumla.


"Chris ndiye wa kulaumiwa kwa jambo hili. Kama asingemtetea Lisa na kuwa mwenyekiti, Mawenzi Investments isingeiudhi familia ya Kimaro."


“Amerukwa na akili? Alithubutu vipi kumpiga Willie? Kimaro ni familia mashuhuri, na kwa wazi hatuwezi kumudu kuwachokoza.”

"Nilisikia mtu ambaye alimuudhi Willie kabla ya huyu alikuwa bilionea kutoka Kenya. Familia yake ilifilisika kwa usikummoja tu.”


“Ndiyo. Willie anatisha."


Katikati ya majadiliano ya wakurugenzi, Jones Masawe alishusha pumzi ndefu. “Yote ni makosa yangu. Sikupaswa kumruhusu Lina kumleta Willie jana. Lakini nilisikia Willie alikuja hapa kwa ajili ya ukaguzi, na nilikuwa na matumaini kwamba Mawenzi Investments ingeweza kufanya kazi na KIM International.”


“Kweli. Ikiwa tungeweza kushirikiana na KIM International, ingeinufaisha sana Mawenzi Investments.


“Tulikosea. Tungemfanya Jones kuwa mwenyekiti.”


“Najutia uamuzi wangu pia. Sikupaswa kumpigia kura Lisa wakati huo.”


Akihisi mnyonge, Mkurugenzi Amiri alisema, “Sasa kwa vile mambo yamekuwa hivi, hatuna chaguo ila kumwondoa katika nafasi yake ya mwenyekiti kwa ajili ya matarajio ya Mawenzi Investments. Labda Jones ndiye pekee anayeweza kutusaidia kukabiliana na dhoruba wakati huu. Baada ya yote, binti yake ana uhusiano wa karibu na Willie.


Jones alipunga mkono kwa unyenyekevu. “Sina hakika kama naweza kusuluhisha hili. Baada ya kusema hivyo, Bwana Kimaro anampenda sana Lina. Ataenda naye popote aendako. Una maoni gani, Lina?"


Akivumilia maumivu kutoka kwenye majeraha yake ya sehemu za siri yaliyosababishwa na Willie jana yake, Lina alilazimisha tabasamu tamu. "Bwana Kimaro ananipenda sana. Hata aliniambia mambo mengi kuhusu mradi huo.”


Kila mtu alishangilia kwa furaha. Mkurugenzi Amiri alisema, "Ni mpango wetu sasa. Jones atakuwa mwenyekiti wetu mpya.”


Lisa aliusukuma mlango na kujipenyeza ndani. Macho ya wazi na makali yaliwakumba wakurugenzi wote. “Kwangu, ninyi nyote ni wakurugenzi wa Mawenzi Investments, ambao pia mnachukuliwa kuwa wazee wangu. Nilimpiga Willie jana usiku, ndiyo! Lakini kuna yeyote kati yenu aliyeniuliza kwa nini nilifanya hivyo?” Kila mtu alipigwa na butwaa.


Lisa aliongeza kwa hasira, “Jana usiku, Willie alinifungia kwenye chumba changu cha hoteli na karibu kunibaka. Lina alisimama nje ili kumsaidia kufuatilia hali ya nje. Kwa sababu ya njama yao chafu, mimi, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, nilikuwa karibu kuharibiwa. Kwa nini? Kwa sababu Willie ni mjanja na hajali kabisa. Hakuwa tu anajaribu kunidhalilisha mimi bali pia Mawenzi Investments nzima.”


'Hilo ni jambo lisilo na akili kwa Willie," mkurugenzi alinong'ona.


“Vipi Lina anathubutu vipi kufanya vile?! Hiyo inatisha.”


“Sikufanya hivyo. Lina alisimama mara moja. “Wewe ndiye uliyetaka kumtongoza Bwana Kimaro, lakini hakuwa na hamu na wewe. Anaweza kupata mwanamke yeyote anayemtaka kwa urahisi. Kwa nini atake kujilazimisha kwako?”


Jones alisema kwa mzaha, “Hata waandishi walikupiga picha ukiwa umemshika Bwana Kimaro kwa mkono wake kwenye lango la hoteli jana usiku. Hata hivyo, Bwana Kimaro alidai kuwa ulimvua nguo.


"Ni aibu kama nini!"


"Ni aibu kubwa kuwa na mkurugenzi kama huyu Mawenzi Investments." Kila mtu alimtazama Lisa kwa dharau.


Mkurugenzi Amiri alikunja uso na kusema. “Acha kujitetea. Umeingia kwenye matatizo makubwa wakati huu. Tunataka tu kuilinda Mawenzi Investments. Kwa kuwa lilikuwa ni kosa lako, unapaswa kubeba jukumu. Kusema kweli, huwezi tena kukaa katika kampuni tena.”


Mdomo wa Lisa ulitetemeka kwa kejeli huku macho yake yakionyesha sura ya jeuri. "Kwa hivyo mnapanga kunifukuza kutoka kwenye bodi ya wakurugenzi?"


Jones alitabasamu kwa dharau. “Hilo ndilo jambo pekee tunaloweza kufanya. Afadhali ufungashe na kuondoka sasa hivi.”


Lisa alidondosha macho yake. Alikuwa amechanganyikiwa kabisa na kampuni hiyo. Wakati huo, mfanyakazi mmoja alikimbia ndani na kupiga kelele, "Willie yuko hapa! Sasa yuko chini, na anataka kukutana na Mwenyekiti Jones.”.....ITAENDELEA.....


Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.