JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................572-573
Sura ya: 572
Alvin alipokuwa akisikiliza, moyo wake ulimuuma sana hadi akakaribia kukosa hewa. Ilibainika kuwa mateso ambayo Lisa na watoto walipitia yalikuwa mengi kuliko vile alivyofikiria. Si ajabu kwamba alimchukia kiasi hicho. Alikuwa hafai kabisa. Yeye ndiye aliyemkemea Jack, lakini kwa kweli, hakuweza hata kujilinganisha na Jack.
Hans alisema, “Bwana Mkubwa, kusema kweli, matendo yako wakati huo yalinikera pia. Siijali ikiwa ulipenda kuwa pamoja na Sarah, lakini kwanini ulilazimika kumuumiza Miss Jones kwa njia hiyo? Ulitaka hata kumnyang'anya watoto wake. Ulizidisha mno.”
Alvin aliona aibu zaidi. Kufikiria nyuma, alikuwa mbaya sana. Ni kana kwamba alikuwa amepagawa wakati huo. Ikiwa Lisa angekuwa mbele yake, bila shaka angepiga magoti na kutubu.
“Kwa kweli, nimejua kuwa Suzie ni binti yako tangu mwanzo. Hata hivyo, sikukuambia kwa sababu nilijua nikifanya hivyo, bila shaka utamtumia mtoto huyo kumtishia Miss Jones au hata kumpokonya mtoto kutoka ubavuni mwake. Hilo litakuwa si la haki kwake.”
Hans alisema kwa majuto, “Bwana Mkubwa, ninatumai kwa dhati hutampokonya watoto kutoka kwake. Huna hata fununu kuhusu shida ngapi Bi Jones alipitia kwa watoto hao wawili. Hata hukuwalea. Pesa zako zote zilitumika kwa Sarah. Tangu Bi Jones alipokuwa mjamzito, hujafanya lolote zaidi ya kumsumbua Bi Jones na kuweka ujauzito wake hatarini.
"Bwana Mkubwa, najua nimevuka mipaka kwa maneno yangu, lakini hivi ndivyo nimekuwa nikitaka kusema kwa miaka mitatu iliyopita."
"Hans, sikulaumu." Alvin alizungumza kwa ukali, “Kinyume chake, ninashukuru kwa ajili yako. Asante. Usijali. Sitawanyakua watoto. Sina haki ya kufanya hivyo. Lakini katika siku zijazo, nitachukua maisha yangu yote kuwafidia watoto hawa wawili.”
Hans akashusha pumzi kubwa ya ahueni.
Kisha, Alvin ghafla akasema, “Chukua gari unipitie hapa shule ya chekechea. Twende kumtembelea Bw. Garson.”
Hans alipigwa na butwaa. "Nilidhani hautakuwa na hamu ya kwenda ..."
"Kwa kweli sina hamu ya kwenda, lakini ... Najua nina majukumu zaidi juu yangu sasa." Pembe za mdomo wa Alvin bila fahamu ziliinuliwa na kutabasamu kwa upole. “Nina watoto wawili. Nataka kufanya kazi kwa bidii kwa ajili yao.”
Alitazama shule ya awali nyuma yake. Alipofika, alihisi kama anga linaanguka, lakini alipoondoka, aliona matumaini ya siku zijazo.
Akiwa njiani kwenda kumchukua Alvin, Hans aliwaza na kuamua kumpigia simu Lisa. Lakini, hakupokea. Alihisi alikuwa katikati ya mkutano.
Baada ya hapo, alimpeleka Alvin hadi Hoteli ya Kimataifa ya Fortuna, ambako mwenyekiti wa Garson Inc. alikuwa akiishi. Hans alikuwa amewasiliana na msaidizi wake hapo awali.
Baada ya kuingia ndani ya hoteli hiyo, Alvin alimuona Jerome na msaidizi wake wakitoka ndani. Uso wa Jerome haukuwa mzuri, lakini aliachia kicheko cha kejeli alipomwona Alvin.
"Hauko hapa kumtembelea mwenyekiti wa Garson Inc. pia, sivyo?"
Jerome alimpa Alvin jicho la dhihaka na kusema kwa dharau, "Hata umepata ujasiri wa kuonana na mtu kama huyo, kwanini usichukue kioo na ujiangalie wewe mwenyewe unavyofanana kwanza?
Hans alitembea kwa hasira, lakini Alvin akamzuia. “Jerome, ninakuomba ujizuie kidogo. Si kila wakati ambapo utapata bahati ya kumpata mtu akufanyie kazi ngumu.”
Mtazamo katika macho ya Jerome ulibadilika. Akadhihaki. "Alvin, ulipata bahati mara ya mwisho. Utakufa kwa mikono yangu siku moja.”
Alvin hakujibu maneno yake. Badala yake, alimtazama Jerome kwa kiburi, kana kwamba alimtazama paka mdokozi. "Jerome, nitamaliza madeni yote kati yetu hivi karibuni."
"Ha, mawazo gani ya kupendeza. Je, unadhani KIM International inaweza kuinuka tena kwa kuanzisha ushirikiano na Garson Inc.? Katika ndoto zako. Ngoja nikuambie. Mwenyekiti wa Garson hatakutana na wewe, kwa hivyo hakuna haja ya wewe kwenda juu na kumsumbua pia.” Jerome aliashiria kwa meneja wa chumba cha wageni kuja baada ya kuzungumza.
"Bwana Campos, kuna chochote ninaweza kukusaidia?" Meneja akaja mara moja na kuuliza kwa kujaribu kumfurahisha Jerome.
"Mtu huyu anataka kwenda kwenye chumba cha Garson na kumsumbua mgeni wako wa VIP. Unapaswa kumtazama kwa karibu. Usimruhusu anyemelee,” Jerome alisema huku akitabasamu.
Hans alisema kwa hasira, "Tayari tumepanga miadi."
“Miadi? Na mtu kama wewe?" Jerome alicheka kwa kejeli. "Wacha kudanganya. Familia nyingi tajiri za Kenya zilikuja kumtembelea mwenyekiti huyu, lakini zote zilikataliwa. Nani atakuamini ukisema una miadi?”
Meneja alikunja uso mara baada ya kusikia hivyo. “Tafadhali msiwasumbue wageni wa VIP wa hoteli yetu. Ondokeni mara moja.”
“Umesikia hivyo? Mnatakiwa kuondoka.” Jerome alianza kuwafukuza pia. “Meneja, sidhani kama wanataka kuondoka. Ni afadhali kuwaleta walinzi waje na kuwafukuza.”
Hans alikasirika, na Alvin, ambaye mwanzoni alikuwa katika hali nzuri, alikasirika pia. Akiwa amevalia suti nyororo, Alvin alioonyesha hali ya hasira kali huku macho yake yakipita kama picha ya X-ray. Meneja alitetemeka bila kuelezeka.
Wakati huo, mtu mwenye umri wa kati alitoka kwenye lifti. Alipomwona Alvin na wengine, alitabasamu na kusema, “Bwana Kimaro, mbona hujapanda? Mwenyekiti wetu anakusubiri.”
Alvin alishtuka baada ya kumuona mtu huyo. "Ni wewe?"
Mtu huyo alikuwa ni dereva wa Rolls-Royce ambaye aligongana naye alipokuwa akiendesha gari na Suzie kwenye gari siku kadhaa nyuma. Ilionekana kama mtu kwenye kiti cha abiria alikuwa mwenyekiti wa ajabu wa Garson Inc.
“Ndiyo, ni mimi.” Dereva akatabasamu huku akimtazama Jerome na wengine.
Jerome alimtambua pia. Huyu ndiye mtu aliyemzuia alipokwenda kumtembelea Garson muda mfupi uliopita. Kwa mawazo kwamba mwenyekiti wa Garson Inc. alikuwa anaenda kukutana na Alvin, uso wake uligeuka kwa hasira. “Kwanini ulisema mwenyekiti wa Garson Inc hakuwepo nilipotembelea sasa hivi? Je mwenyekiti wako haelewe kuhusu Alvin ni nani? KIM International sivyo ilivyokuwa. Wamefikia mwisho wao sasa. Sisi, familia ya Campos, kwa sasa ndio familia kuu nchini Kenya.
Dereva alimtazama bila kujali kabla ya kusema kwa tabasamu, “Bwana Campos, umekuja mara nyingi sana, na kila wakati, mwenyekiti wetu amekataa kukutana nawe. Huelewi kuwa kusema hayupo ni kisingizio tu cha kuokoa heshima yako?”
"Watu wengine hawajifikirii sana." Alvin alimtazama Jerome.
Macho ya Jerome yalikuwa yanawaka kwa hasira. “Sawa, mwambie mwenyekiti wako kwamba afadhali asijutie hili katika siku zijazo.” Baada ya hapo, aliondoka kwa hatua ndefu.
Meneja wa hoteli alikuwa amekwama baada ya kuona Jerome akishushiwa hadhi yake na Alvin kuthaminiwa. "Samahani. Nilifikiri…”
“Kwa kuwa unatii maagizo ya Jerome vizuri, hufai kuwa meneja hapa. Unapaswa kwenda kufanya usaili wa kazi katika kampuni ya Campos. Hans alicheka. "Nitaripoti kwa mkuu wako."
Baada ya Hans kuzungumza, alipanda ghorofani pamoja na Alvin.
Walipofika kwenye mlango wa chumba cha bosi huyo, dereva alimsimamisha Hans. "Samahani. Mwenyekiti wetu atakutana na Bwana Kimaro pekee.”
"Subiri hapa." Baada ya hisia ya shaka kuangaza machoni mwa Alvin, akaingia ndani.
Sura ya: 573
Juu ya sofa nyeusi la ngozi aliketi mtu mnene katika suti ya giza bluu. Mtu huyo alionekana kama alikuwa na miaka arobaini. Sifa zake na muhtasari wake ulikuwa wa kiume sana, lakini ilikuwa ni aibu kwamba alikuwa na kovu usoni mwake. Kovu hilo lilifanya upande mmoja wa uso wake uonekane mbaya, na upande mwingine wa uso wake ulikuwa mzuri.
Wakati huo, kulikuwa na sigara kati ya vidole vya mtu huyo. Macho yake meusi yalimtazama Alvin kupitia ule moshi.
Alipomuona mtu huyo kwa mara ya kwanza, Alvin alifikiri kwamba mtu huyo alikuwa amemfahamu, lakini hakukumbuka.
"Tumekutana hapo awali?" Alvin aliuliza kwa kuhema.
Yule mtu akacheka. Alizima sigara kwenye sinia ya majivu na kusema kwa sauti ya ukali, “Tunafahamiana vizuri sana. Jina langu la mwisho ni Tikisa, Mike Tikisa. Bado unakumbuka?"
Mike Tikisa? Lilikuwa jina ambalo Alvin hakuwahi kulisikia kwa muda mrefu.
Ilikuwa ni muda mrefu sana kwamba karibu kumsahau mtu huyo. Alisahau kwamba asingezaliwa duniani kama si mtu huyo. Katika siku zake za ujana, alisali ili mtu huyo arudi. Hata hivyo, alingoja na kungoja hadi alipohuzunika. Mwishowe, angeweza tu kuendelea na maisha yake kwa kujitegemea yeye mwenyewe.
Alvin alimtazama mtu aliyekuwa mbele yake. Kielelezo chake kilikuwa shwari, lakini hisia zilitoka moyoni mwake. Muda mrefu baadaye, alisema kwa shida sana, “Kwanini umerudi? Kwa muda mrefu nimekufikiria kuwa umekufa.”
Hatia kali ilitanda kwenye macho ya Bwana Tikisa. "Alvin, samahani ..."
“Si lazima uombe msamaha. Sina baba. ” Alvin alimkatisha ghafla. Macho yake yalikuwa kuangaza kwa ukali. "Baba yangu tayari alikufa nilipokuwa mdogo." Aligeuka na kuelekea mlangoni baada ya kusema.
Hakutaka hata kutumia wakati mwingine katika nafasi sawa na mtu huyo.
Isitoshe, mambo mengi sana yalikuwa yametukia siku hiyo. Ghafla, alikuwa na mwana na binti. Hata baba yake, ambaye alikuwa ametoweka kwa zaidi ya miaka 20, alikuwa amerudi. Ha?! Alitaka tu kutulia peke yake kwa muda.
"Alvin, ilibidi niondoke wakati huo. Nisingeondoka, ungepoteza maisha yako.” Mike aliongea kwa huzuni ghafla nyuma ya Alvin.
Alvin alisimama. Kisha, alitazama nyuma na kumtazama Mike kwa kuchanganyikiwa.
Mike alipumua kabla hajaenda upande wa Alvin na kupiga mabega yake. "Mwaka huo, Mason alinitisha. Nisingetoweka, angekuuwa. Yaya aliyekutunza alikuwa ni mtu wake.”
Alvin alishtuka. "Je, yayaunayemzungumzia ni Aunty Willa?"
“Mm.” Mike akaitikia kwa kichwa.” Nilifikiria kukuchukua niende nawe, lakini familia ya Kimaro ilikuwa na nguvu, na sikuwa na nguvu wala ya ushawishi wakati huo. Ningewezaje kuwa na uwezo wa kwenda kinyume na familia ya Kimaro? Isitoshe, nilikuwa na mama mzee. Nilitaka kumleta Bibi yako ng'ambo ili atulie kwanza, kisha nifikirie njia ya kuwasiliana nawe baadaye. Hata hivyo, nilipofika ng’ambo, watu wa Mason walinifuata.”
Alvin alishangaa. Hakutarajia Mason amekuwa akipanga njama na kula njama tangu zaidi ya miaka 20 iliyopita. “Kwanini ilikuwa ni lazima akuwinde? Je, mama yangu hakukubali kuwa naye kwa hiari?”
"Kwa sababu nilivuruga mipango yake." Mike alisema kwa kutatanisha, “Zaidi ya miaka 30 iliyopita, Lea, Mason, na mimi tulikuwa katika shule moja. Mama yako alikuwa mrembo wa shule wakati huo. Alikuwa mungu wa kike katika mioyo ya kila wavulana wakati mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu kutoka kwa familia iliyokuwa na kipato cha kati. Nilimfahamu mama yako kwa sababu sote tulijiunga na baraza la wanafunzi.
“Lakini, hali ya kifedha ya familia ya Mason ilikuwa bora kidogo kuliko yangu. Wakati wa tafrija, Mason alimywesha divai ya mama yako…”
Uso wa Alvin ulikunjamana. "Lakini mama kila wakati alisema kuwa ni wewe uliyetumia dawa kumlevya wakati huo ..."
"Sijawahi kufikiria kuchukua fursa ya ulevi kumpata mama yako hata kidogo, sawa?" Mike alisema kwa upole, “Ilikuwa ni mpango wa Mason, lakini kwa bahati mbaya mimi ndo nilikunywa glasi hiyo ya divai, na Mason alishikiliwa na mtu mwingine wakati huo pia, na mimi nikaishia kushiriki na Lea. Baada ya hapo, tulikupata, na familia ya Kimaro ilinitaka nimuoe Lea.”
Alvin alikunja uso.
Alijua kuhusu ndoa iliyotokea baadaye. Ingawa familia ya Mike haikuwa nzuri kifedha wakati huo, alikuwa amefaulu mtihani wa kuingia chuo kikuu mwaka huo. Baada ya kujiandikisha katika chuo kikuu, matokeo yake yalikuwa juu ya wastani, na alishinda tuzo nyingi kubwa. Kwa kuwa sifa yake haikuwa mbaya, familia ya Kimaro ilikubali ndoa yao.
"Kwa hiyo umevuruga mipango ya Mason?"
“Mm. Mike akaitikia kwa kichwa. "Mason alitaka sana kuoa katika familia ya Kimaro. Lakini, tamaa yake ilivurugika kwa sababu yangu. Alimpenda Lea kwa dhati wakati huo, hivyo alinichukia sana. Na ingawa mimi na Lea tuligombana baada ya kuoana, hatungeachana ikiwa asingekuwa na nia ya kuendelea za Mason. Jambo ambalo sikuweza kuvumilia zaidi ni kwamba Lea alipata ujauzito wa mtoto wa Mason ndani ya muda mfupi.”
“Ni nini kilitokea ulipokuwa ng’ambo?” Alvin aliendelea kuuliza.
Baada ya kuulizwa hivyo, chuki kubwa ilitanda machoni pa Mike. "Nilipata kovu hili kutoka wakati huo. Nusu ya uso wangu ilikuwa karibu kuharibiwa, lakini nilichochukia zaidi ni kwamba bibi yako aliwasimamisha watu hao kwa kuhatarisha maisha yake ili kuniokoa. Mwishoni…
alikufa.”
Baada ya Mike kuongea, aliinamisha kichwa chini, akawasha sigara na kuivuta kwa muda mrefu.
Alvin alikunja ngumi akiwa haamini.
Hakuweza kukumbuka sura ya bibi yake wa upande wa baba kutoka enzi za ujana wake kwa sababu alikuwa kwenye familia ya Kimaro muda mwingi.
Hisia yake pekee kwake ilikuwa kwamba alikuwa bibi mwenye upendo. Hakujua kuwa aliuawa na Mason. Aligundua ni kwanini alikuwa tayari na chuki kubwa na familia ya Campos muda mrefu uliopita.
Mike aliendelea kusema, “Baada ya hapo, ili kuepusha kufuatiliwa na Mason, sikuthubutu kutumia pasipoti yangu. Niliishi kama ombaomba kila siku. Nililala kwenye uchochoro na kula mabaki ya vyakula. Wakati fulani, nilifanya kazi zisizo halali kwa ajili ya wengine, na hata nilinyimwa mshahara wangu. Nilikuwa msomi mzuri, lakini niliishi maisha ya taabu sana.”
Koo la Alvin liliguna kwa uchungu.
Siku zote alifikiri Mike alimtelekeza na alikuwa akiishi kwa raha ng'ambo.
"Je, Mason alifanikiwa wakati huo?"
“Ndiyo. Jambo la kuchukiza zaidi ni kwamba Mason alikuwa mzuri sana katika kujificha. Takriban Kenya nzima ilimchukua kama muungwana mwenye maneno laini, na kwamba Lea na sanaa vilikuwa kipenzi cha maisha yake.” Mike alicheka kwa kejeli. “Machoni pa watu wengine, mimi nilionekana ni mwanamume asiye na haya ambaye ningefanya lolote kumdhuru mama yako. Haijalishi jinsi nilivyomweleza Lea, aliendelea kufikiria kuwa nilikuwa najaribu kumchokoza na kuharibu uhusiano wake na Mason. Hakuna aliyeniamini.”
“Baba samahani…”.....ITAENDELEA.....
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA..
