JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................403-404

Sura ya: 403

Lisa alichanganyikiwa hadi akawageukia wanandoa wale pembeni. Alishtuka na kukumbuka kitu tangu zamani. Yeye na Alvin pia walikumbana na maneno kama hayo hapo awali walipokula kwenye ufukwe wa Coco Beach huko Dar es Salaam.

Akiwa anawaza hayo, ghafla akasikia sauti ya mhudumu. “Bibiye, uko sawa? Mwanamume uliyekuja naye amezimia nje ya mlango wa choo."

Lisa alitazama upande wa bafuni ambapo kundi la watu walikuwa wamekusanyika. Alikimbia na kusukuma umati wa watu, na kumuona Alvin akiwa amepoteza fahamu.

“Alvin… Alvin…” Alimvuta na kuita jina lake kwa muda mrefu, lakini alipokataa kuitika, alipiga simu kuita ambulensi haraka. Muda si mrefu gari la wagonjwa lilifika na kumpeleka Alvin hospitali.

Suzie alionekana kuwa na wasiwasi. "Mama, nini kimetokea kwa baba mchafu? Kwanini alizimia ghafla?”

Lisa alikunja uso. Alishuku kuwa huenda Alvin alikumbuka kitu baada ya kusikia mazungumzo ya wanandoa hao mapema,kwa hiyo kumbukumbu zake zikamrudia kwa nguvu na kukizidia kichwa chake. Lakini, mwanasaikolojia hapo awali alisema kuwa ni 0.1% tu ya watu waliolazwa akili wanaweza kupona. Wengine wanaweza kupata nafuu lakini wakawa mazuzu.

Wakati huo, mlango wa Emergence Room ulifunguliwa na daktari akatoka. “Bwana Kimaro amenaguka kutokana na uchovu. Inavyoonekana hajalala kwa siku chache. Ninaamini amekaa kwa muda mrefu bila kupumzika, na kusababisha ugonjwa wa neva wa ubongo ambao ulisababisha kuzirai.”

Lisa alikosa la kusema. Mwanzo alifikiri kwamba Alvin alizimia kwa sababu alichochewa na kumbukumbu za zamani. Naam, ilionekana alikuwa amefikiria mbali sana.

Wakati huo, Chester na Rodney pia walifika. Alvin alipopelekwa hospitali, watu waliokuwa kwenye chumba cha dharura walikuwa wamemjulisha Chester. Rodney alikuwa pamoja naye, hivyo wawili hao walifika pamoja.

Hata hivyo, Rodney alipomwona Lisa nje, alipandwa na hasira. "Lisa Jones, kwanini uko hapa? Wewe ni kama mzimu unaomsumbua Alvin. Je, unajaribu kumrejesha Alvin kwako kwa sababu harusi yake na Sarah imeghairiwa kwa muda? Ninakuonya, bora ukae mbali na Alvin.”

“Mbona wewe ni mkali sana?” Suzie alimkazia macho Rodney kwa hasira.

"Watoto wadogo kama wewe wanapaswa kujiepusha na masuala yanayohusu watu wazima.” Rodney alimkazia macho Lisa. "Kuna wanaume wengi chini ya anga, kwanini unamng'ang'ania Alvin tu? Je, huoni aibu kuwa mchepuko?”

"Mchepuko?" Lisa alicheka. “Sawa, nina makosa hata nifanye nini. Sikupaswa kupiga 000 na kumleta Alvin hapa. Ningemwacha afe badala yake.”

“Wewe ndiye ulimleta hapa?”

“Kumbe? Alvin akiamka kumbuka kumwambia anilipie gharama za matibabu. Sina mpango wa kutumia pesa zangu kumtibu mume wa mtu.” Lisa alisema kwa ujeuri na kumbeba Suzie moja kwa moja. Alihisi kwamba IQ yake ingepungua ikiwa angeendelea kuzungumza na Rodney.

“Usidhani sijui unataka Alvin akulipe ili umpigie baadaye. Alvin atafunga ndoa na Sarah, acha kuota!” Rodney alimfokea nyuma yake. Kisha, akatoa simu yake na kutaka kumpigia Sarah.

Chester alichukua simu yake na kumfokea, “Huwezi kumwacha Alvin awe na amani na utulivu? Hukusikia alichosema daktari? Alvin hajalala kwa siku kadhaa na yote ni kwa sababu ya Sarah. Hajalala vizuri tangu tukio lile na Sarah.”

“Ninamwita Sarah ili amtunze,” Rodney alieleza, “hawawezi kuendelea hivi, inabidi waelewane.”

"Lakini inabidi ungoje hadi Alvin apate nafuu kidogo. Ataumwa na kichwa akimuona tena Sarah sasa hivi.” Chester alikasirika. “Si unajua kwanini hapokei simu zetu tena? Ni kwa sababu hataki kusikia tukizungumza kuhusu Sarah. Mpe muda.” Rodney alikasirika na hakuweza kusema chochote kingine.

Alvin alipoteza fahamu kwa siku nzima kabla ya kuamka. Alipofumbua macho, ni Chester pekee aliyekuwa amekaa wodini. “Rafiki nakuomba upumzike vya kutosha baada ya hapa. Sitaki kuhudhuria mazishi yako ikiwa utakufa ghafla,” Chester alitania.

Alvin alisugua kichwa chake. “Kwanini nipo hapa?” Alikumbuka mara ya mwisho alikuwa na Suzie na Lisa, wakila mgahawani katika bustani ya burudani.

“Haujapumzika kwa siku nyingi, jambo lililopelekea kuzirai kutokana na kushindwa kufanya kazi kwa mishipa ya ubongo. Lisa ndiye aliyekuleta hapa. ” Chester akamtazama pembeni. “Badala ya kusema ulikuwa umezimia, ni bora kusema ulilala kwa sababu ulikuwa umechoka sana. Unafikiri umetengenezwa kwa chuma?”

Alvin alifumba macho yake kimya kimya.

“Sawa, una njaa? Nitampigia Hans— ”

Alvin akamkatisha Chester ghafla. "Nakumbuka ulisema kwamba nilikula Coco Beach na Lisa hapo awali."

"Ndio, mbona unaniuliza ghafla?"

"Je, niliwahi kwenda na mwanamke mwingine yeyote hapo awali?" Alvin aliuliza.

“Ningejuaje?” Chester alihisi kutokuamini. "Lakini sidhani. Kwanini?”

"Si chochote." Alvin, mara moja akaketi. Akatupa shuka la hospitalini na kubadili nguo na viatu. “Nisaidie utaratibu wa kuagwa. Naondoka.”

"Alvin Kimaro." Chester alikasirika sana. "Unaweza kuichukulia afya yako mwenyewe kwa uzito?"

“Sasa sijambo. Niko sawa." Alvin alifungua mlango.

Maya, ambaye alikuwa akingoja mlangoni, mara moja alisema, “Bwana Mkubwa, unaenda wapi? nitakupeleka.”

“Kwanini uko hapa?” Macho makali ya Alvin yalimpita Maya na kuruka kwa woga.

Maya alikuwa mwanachama wa ONA na jukumu lake lilikuwa kumlinda Sarah. Ni mara chache sana angekuja kumtafuta kama Alvin asingemwita. Alikuwa hapo kwa ajili ya kumtazama tu kwa ajili ya Sara.

“Kazi yako sasa ni kumlinda Sarah. ” Macho meusi ya Alvin yalijaa ukali ghafla. “Maya Chande, wewe ndiye mtu wa karibu zaidi na Sarah. Ina maana, hukumuona kabisa alipoenda kwenye ghorofa kila wiki kumtafuta Hisan?”

Maya alishtuka. “Bwana Mkubwa, kwa kweli sikujua. Ingawa ni jukumu langu kumlinda, yeye ana mambo yake binafsi wakati mwingine na siwezi kumuangalia kila wakati. Sikujua kama alikuwa akifanya mambo kama hayo. Lakini usijali, katika siku zijazo, nita—”

"Unahitaji tu kumlinda kwa sasa asije akachukua maamuzi magumu sana. Anaweza kuwa na yeyote anayetaka. Huna haja ya kuniambia kuhusu hilo tena.” Kisha, Alvin akageuka na kuondoka.

Maya alipigwa na butwaa. Alimaanisha nini kwa kusema hivyo? Je, alikuwa anaachana na Sarah kistaarabu? Haraka alimfuata, lakini kabla hajamkaribia, Alvin alimtazama kwa ukali. “Hujasikia nilichosema? Watu wa ONA wote wana majukumu yao. Nitakupigia nikikuhitaji. Hakuna haja ya kunilinda.” Alisema na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Wakati huo, Maya hakuthubutu kumfuata tena kwani aliogopa kuibua mashaka yake.

Nusu saa baadaye, gari la Alvin lilikuwa limeegeshwa chini ya ofisi za Mawenzi Investments. Alvin alipokuwa akijiandaa kushuka kwenye gari, ghafla aONA BMW nyeusi ikiwa imeegeshwa kando ya barabara. Muda si muda, Erick alitoka ndani huku akiwa ameshika maua. Alikuwa akipiga simu kwa Lisa.

Uso wa Alvin ulibadilika na kujawa huzuni huku akiufunga mlango kwa nguvu baada ya kutoka kwenye gari. Alichukua hatua kubwa kuelekea kwa yule mtu.

“Sawa, nitakusubiri,” Erick alisema kwa upole huku kivuli kirefu kikimfunika. Akageuka na kuuona uso wa Alvin wa kupendeza. "Bwana Kimaro, habari." Erick alitabasamu kwa umaridadi. Ingawa mara nyingi hakukutana na Alvin, aONAna naye mara chache sana kwenye karamu mbalimbali za watu mashuhuri alizoalikwa.

Macho makali ya Alvin yalitazama maua ya waridi mkononi mwake. "Hayo ni kwa ajili ya Lisa?"

“Ndiyo, Lisa aliniambia mara ya mwisho kwamba anapenda maua ya waridi— ”
Kabla Erick hajamaliza, maua mikononi mwake yalipokonywa kutoka kwake. Alvin alichukua maua na kuyasukuma moja kwa moja kwenye pipa la takataka lililokuwa karibu naye.

"Alvin Kimaro, unafanya nini?" Hasira ilionekana kwenye uso mzuri wa Erick.

"Kaa mbali na Lisa ikiwa unataka familia ya Malugu kuendelea kuwa kwenye ramani." Alvin alimuonya.

“Huna nafasi ya kuingilia mambo yangu na ya Lisa. Najua ni mke wako wa zamani, lakini nyinyi wawili tayari mmeachana. Huna haki ya kuingilia mambo yake,” Erick alidhihaki.

“Hukunielewa? Usidhani sijui unamfuata Lisa kwa sababu ya utambulisho na hadhi ya familia ya Ngosha. Mwishowe, ni kwa ajili ya familia ya Malugu. Lakini inabidi uelewe, ukiniudhi, nitasema neno moja tu na riziki ya familia yako itakuwa ya shida.” Macho ya Alvin yalikuwa yamejawa na hasira, na sauti yake ya chini ilionyesha kuwa uvumilivu umekwisha.

“Alvin Kimaro, huwezi kumwacha Lisa aende zake? Nani katika mji huu hajui kuwa tayari uko na Sarah Njau? Kama hadhi yako huoni kwamba unajidhalilisha kwa kuendekeza michepuko?” Erick alikuwa kijana asiye na makuu na alikasirishwa na matendo ya Alvin ya dharau.

"Ndio, sina aibu, lakini watu wasio na aibu wanaweza kufanya chochote. Unataka kunijaribu?" Alvin alimtazama kwa macho ya kuchoma.

Erick aliogopa kiasi fulani. Kwa wakuu nchini, Alvin ulikuwa mlima usioweza kupandwa. Akauma meno na kuondoka kwa hasira.

Sura ya: 404

Hata hivyo, baada ya gari hilo kutembea umbali usiozidi mita 200, Erick alimpigia simu Lisa tena. “Lisa, samaki amechukua chambo. Utanishukuruje kwa hili?”

Akiwa amesimama mbele ya dirisha na kutazama chini, Lisa alitabasamu kwa upole. “Nitakuandalia chakula cha jioni siku nyingine.”

“Sihitaji chakula. Unahitaji tu kuja na muundo wa kipekee wa nyumba yangu mpya.” Erick aliguna.

"Bado una ujasiri wa kuniuliza kuhusu muundo wa nyumba? Kama nisingalikuwa ngao yako, familia yako ingalikulazimisha kwenda kwenye miadi ya uchumba.”

“Usiseme hivyo. Si tulikubaliana?”

“Sawa, nitakupa muundo wako baada ya mwezi mmoja.”

Baada ya Lisa kukata simu, midomo yake ilijikunja kwa kejeli. Siku hizo, Nairobi nzima ilifikiri kwamba Erick alikuwa akitoka na Lisa kimapenzi. Hata hivyo, hakuna aliyejua kwamba Erick na yeye tayari walikuwa wanajuana tangu akiwa huko Marekani. Alikuwa amemuona kwa macho yake Erick akiingia na kutoka katika mahusiano na wanaume kadhaa. Ndiyo, wanaume! Mwanaume huyo alipenda mahusiano na wanaume wenzake.

Lisa alimtazama Alvin pale chini. Akitazama chini kutoka ghorofa ya 30, umbo la mwanamume huyo lilikuwa ndogo kama mchwa. Hata hivyo, mchwa huyo hatimaye alikuwa amemeza chambo. Lengo la Lisa lilikuwa ni kumuaminisha Alvin kuwa yeye alikuwa anatoka na Erick, na Alvin tayari alikuwa ameshaamini hilo.

‘Alvin Kimaro, nitakupa ladha ya kuhisi jinsi inavyouma kuona mpenzi wako wa zamani akiwa na mwanamume mwingine.' Lisa alijiapia.‘Sarah Njau, nitakupa ladha ya kuhisi jinsi inavyouma kunyang'anywa mpenzi wako.’ Hata kama Alvin alilazwa kiakili, asingemsamehe.

Alvin alisimama chini kwa dakika kumi kabla ya kumuona Lisa akitoka nje ya jengo hilo akiwa amevalia suti ndogo ya rangi ya chungwa. Nywele zake ndefu zilikusanywa na kubanwa kisogoni, zikifunua hereni ndefu za tassel zilizoning’inia masikioni mwake. Lisa alitazama eneo lile na kwa haraka akamuona Alvin akinyata kuelekea kwake.

“Kwanini uko hapa?” Alimuuliza kwa makusudi.

“Ulikuja kumpokea nani? Erick Malugu?” Alvin alidhihaki, “Lisa Jones, hebu niambie, Erick anapenda wanaume, wewe umempendea nini?”

Macho ya Lisa yalimtoka. Alvin aliwezaje kuyafahamu hayo? Hakuna mtu katika Nairobi ambaye alijua kwamba Erick alipenda wanaume.

Alvin aONA sura ya Lisa iliyoshtuka.Tabasamu likaangaza usoni mwake. Alikuwa ametupa tu jiwe gizani lakini hakuwa na uhakika kama lingempata, lakini bila kutarajia alimwamini. “Hata hivyo, nasema ukweli. Nakushauri ukae mbali naye,” Alvin aliongeza.

Lisa alimkazia macho na kutoa simu yake ili kumpigia Erick.
Alvin akasema, “Erick tayari ameondoka.”

"Alvin Kimaro, ulimfanya nin?" Lisa alimkazia macho.

"Nilimwambia kuwa aache kukufuata, akaondoka bila neno," Alvin alisema kwa dharau. "Yeye ni mwoga kama panya."

Lisa akaguna. Kama asingemfahamu Erick vizuri, angeamini upuuzi wa Alvin. Mtu huyu alisema uwongo bila kuja na ushahidi kwanza.

Alvin alipoona ameacha kuongea na kumtazama kwa sura yake nzuri, akakohoa kwenye ngumi. “Nilikuja hapa kukushukuru kwa kunipeleka hospitali jana. Kwanini nisikufanyie chakula cha jioni usiku wa leo kama shukrani?”

“Asante, lakini sihitaji. Jana nilikupeleka hospitali kwa wema tu na kuishia kuzomewa na marafiki zako wazuri. Walisema kwamba mimi ni kama mzimu unaokusumbua na kwamba ninachukua fursa hiyo kurudiana pamoja nawe. Niliwaambia wakukumbushe unilipe gharama zangu za matibabu, lakini wakasema nilitaka tu kisingizio cha kukupigia." Lisa aliinua mikono yake kwa ujeuri na kumdhihaki, “Ikiwa nitakubali kwenda kula chakula cha jioni nawe, nitayaumiza masikio yangu kwa kwa maneno yao makali tena.”

“Unamzungumzia Rodney?” Alvin alikasirika ghafla. Ikiwa sivyo kwa sababu walikuwa marafiki bora kwa miaka mingi, alitaka sana kumpiga ngumi. "Usisikilize upuuzi wake."

“Alvin Kimaro, sijui unataka nini kutoka kwangu.” Lisa alionekana kukasirika. “Kwa sababu yako, huwa nazomewa na wengine. Je, humpendi Sarah Njau? Mbona huwa unakuja kunitafuta? Je, umesahau kwamba kwenye harusi siku chache zilizopita, wewe binafsi ulisema kwamba utafanya harusi nyingine na Sarah baada ya siku chache? Au ni kwa sababu Sarah alifanya jambo ambalo limekuangusha, ulikuja hapa kwangu kwa kupoza machungu yako? Mimi sio kipozeo chako."

Uso mzuri wa Alvin ulijawa na aibu. Kila neno alilosema Lisa lilianguka usoni mwake kama kofi. Kama mwanamume, aONA aibu.

"Alvin Kimaro, acha kuwapa watu matumaini na kuwafanya wakate tamaa." Lisa aligeuka na kuondoka.

Alvin aliganda. Alipomwona Lisa akiondoka, bila fahamu alimshika mkono. “Jana, tulipokuwa tunakula Mgahawani, baadhi ya kumbukumbu ziliangaza akilini mwangu. Hapo awali… sidhani kama nilikuchukia kiasi hicho.”

Mwili wa Lisa ukawa mgumu. Alikuwa na mashaka hayo jana yake, lakini hakutarajia angekumbuka kitu.

"Haiwezekani mimi na Sarah kuoana tena." Alvin alipoona Lisa amesimama kumsikiliza, aliendelea, "Nimehama kutoka Oasis na kumwacha Sarah peke yake. Sidhani kama nipo tayari kumuoa tena."

"Kwa hiyo unataka kunifanya kama tairi lako la spea? Unakimbilia kwangu kwa sababu tu mambo yako yameenda vibaya kwa Sarah.” Lisa alitupa mkono wake kwa hasira. "Nadhani ni kwa sababu umegundua kuwa mpenzi wako wa utotoni na penzi lako la kwanza sio safi kama ulivyofikiria, kwa hivyo unajuta. Kwa kuwa hakuna wanawake wengine karibu nawe, ulihisi kuchoka na badala yake ukaja kunisumbua.” Kadiri alivyozidi kuongea ndivyo alivyokuwa na hasira. Macho yake yaliwaka moto wa hasira na machozi.

Moyo wa Alvin uliuma sana. Alifungua kinywa chake kwa shida.“Siyo hivyo.”

"Alvin Kimaro, sitaki kuumizwa na wewe tena." Lisa aligeuka na kuondoka.

Alvin alimfuata Lisa. Alipomwona Lisa akirudi kwa uthabiti, alihisi kwamba ikiwa hakuweka wazi mambo fulani, angeweza kumpoteza milele. “Usiende. Kwa kweli, nilikupenda tangu zamani. Hii ilikuwa mara ya kwanza kueleza kikamilifu mawazo yake ya kweli.

Lisa akanyamaza, Alvin akashusha sauti yake kwa huzuni. “Lakini sikuweza kusema kwa sababu nimemfahamu Sarah kwa muda mrefu na nina deni kubwa kwake. Nisingeweza kumwangusha, hivyo ningeweza kuchagua tu kuachana nawe. Sielewi kwanini nilibadilisha mawazo yangu pia. Ninapenda tu kutumia wakati wangu na wewe zaidi. Ninapokuona na Jack au Erick, huwan naumia sana.

“Ndio hivyo?" Lisa aligeuza macho yake mekundu kwake na kumtazama kwa tabasamu la kejeli. "Alvin Kimaro, umechanganyikiwa sana na Sarah. Ulisema kwamba unanipenda, lakini inaweza kulinganishwa na hatia uliyo nayo kwa Sara? Wakati mwingine atakaposema neno dhidi yangu, utaniacha bila huruma tena. Je! kusikia juu ya mvulana ambaye alilia mbwa mwitu na kuwaita wanakijiji kumbe anawadanganya? Na siku alipotokea mbwa mwitu wa kweli hakuna aliyejitokeza kumsaidia kwa sababu wote walijua alikuwa akiwadanganya. Mimi ndiye mwanakijiji katika hadithi hiyo. Sina imani nawe tena.”

"Hapana, ni kweli ... haiwezekani kati yangu na Sarah." Alvin akatikisa kichwa. Baada ya kuzungumza, alihisi utulivu. Alionekana kweli hakumpenda Sara tena. Alikuwa amechoka kila wakati alipokuwa naye. Hata harusi yao ilikuwa imemjaza mfadhaiko.

“Kwa vyovyote vile, sitakuamini. Sitaki kuwa dampo la mafadhaiko yako. Siku mambo yakiwa mazuri kwa Sarah, unaniacha kwa kashfa kama zote. Siku mambo yakikuchachia, unarudi kwangu ukiwa mpole kama njiwa. Hapana, sitaweza tena. Usinifuate tena.” Lisa alimkazia macho na kuondoka kwa kasi akiwa amevalia viatu vyake virefu. Alionekana kana kwamba anaogopa kwamba angemfuata.

Alvin alikasirika. Tayari alikuwa ameeleza hisia zake za kweli, lakini bila kutarajia, hakuitikiwa vizuri hata kidogo. Labda alikuwa amemuumiza sana hapo awali.....ITAENDELEA....

Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.