JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................373-374
Sura ya: 373
“Wewe pia umeona? Lea alicheka kwa uchungu. "Jack, unadhani baba yako ni mtu wa aina gani?"
Jack alifungua kinywa chake kwa sekunde, lakini mwishowe alinyamaza.
Miaka mitatu iliyopita, kila mtu alikuwa amemshuku wakati picha za Alvin katika hospitali ya magonjwa ya akili zilipovuja. Ni Jack pekee ndiye aliyejua kwamba hakuwa na hatia.
Alipojua kwamba habari hizo zilitoka kwa familia ya Campos, alikuwa na zaidi au chini ya kukisia kuwa ni Mason ndiye aliyefanya hivyo. Baba yake anaweza kuonekana mpole na asiyejali mambo mengi, lakini kile kilichoonekana nje kinaweza kuwa si kweli.
Kwa bahati mbaya, haijalishi aliuliza kiasi gani, Mason hakuwahi kujibu maswali yake moja kwa moja. Miaka yote hiyo, Jack alihisi kukosa hewa akifanya kazi katika Kampuni ya KIM. Lakini, Mason hakuwahi kutaja chochote kuhusu kumsaidia hata kidogo. Muda ambao Mason alikaa naye haukuwa mwingi kama ule ambao Mason alitumia na Jerome.
Wakati wowote Jack alipoenda kwa familia ya Campos, watu wa hapo wangekuwa na urafiki wa juu juu tu kwake. Kuna wakati mmoja alitaka kuwa na hisa katika mradi mpya wa baba yake mdogo kwa sababu alifikiri haukuwa mbaya. Hata hivyo, ba’mdogo wake alitoa kisingizio akisema kwamba tayari alikuwa ametoa mradi huo kwa watu wengine kwani haukuleta faida nyingi.
Jack aligundua baadaye kwamba ba’mdogo wake hakufanya mradi huo bali alimwacha mpwa wa upande wa mke wake awe na hisa katika mradi huo. Yeye aligeuka kuwa duni kwa mpwa kutoka upande wa mkewe.
Si hivyo tu, lakini wakati mmoja alipoenda nyumbani kwa familia ya Campos kwa Mwaka Mpya alipokuwa mdogo, aliona kwamba Bibi yake alikuwa na pipi zake za kupendeza katika mfuko wake. Bibi alisema peremende zimeisha alipomuomba, lakini alimwona akimpa Jerome peremende kwa siri. Alikuwa mjukuu wake pia.
Hatimaye alifikiri kwamba labda ni kwa sababu jina lake la mwisho lilikuwa Kimaro. Kwa hivyo, ingawa familia ya Campos ilikuwa hatua kwa hatua kuwa familia ya pili yenye utajiei mkubwa nchini Kenya, Jack bado alijiweka mbali nao.
“Mama mimi ni mtoto wa damu wa baba kweli?” Jack aliuliza swali hilo ghafla.
Lea alipigwa na butwaa kwa muda kisha sura yake ikaingia giza. Akasema, “Wewe ni mtoto wa nani kama si wa baba yako? Unataka kusema nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine?"
“Hicho sicho nilichomaanisha. Sahau, nilikuwa namaanisha hanijali kama mimi ni mwanaye." Jack aliondoka baada ya kusema.
Akili ya Lea ilizunguka kwingine. Hakuweza kujizuia kukumbuka mambo fulani ya zamani. Siku alipopata ujauzito wa Jack, alikuwa ametoka tu kuachana na Mike Tikisa. Alikuwa katika hali mbaya na akalewa. Ni Mason ndiye aliyemrudisha nyumbani baadaye. Bila kujua, alifanya mapenzi na wote wawili kwa nyakati tofauti.
•••
Ndani ya Ofisi za Kampuni ya KIM International.
Baada ya mkutano wake kuisha, Alvin alitazama simu yake na kuona missed call nne kutoka kwa Bibi Kimaro.
Akampigia tena. Bibi Kimaro alimkemea kwa ukali, “Uko busy tu na huyo mwanamke, Sarah? Hupokei hata simu zangu."
"Nilikuwa kwenye mkutano," Alvin alielezea bila hasira.
“Sawa basi. Njoo nyumbani baada ya kutoka kazini. Kutakuwa na karamu kwenye jumba la kifahari usiku wa leo. Mama yako hajakuambia bado?"
“Unafikiri atanipigia simu?”
"Sawa basi," Bibi Kimaro alisema kwa furaha, "Tumegundua kwamba Jack, mdogo wako, ana binti wa nje. Sikujua juu yake mwanzoni, lakini nilikutana nao leo. Ah, mtoto huyo mdogo ni mzuri sana. Usiku wa leo, ningependa kuona kila mwanafamilia wa Kimaro anakuja na kushiriki karamu kwa ajili ya mdogo wangu mpenzi. Wewe kama anko wake, lazima uwepo. Lazima uandae zawadi na kumtunza pesa ya mfukoni pia."
"Jack ana binti wa nje ?" Alvin akashangaa. Alijisikia faraja isiyo ya kawaida. Ikiwa Jack tayari alikuwa na binti wa nje, Lisa asingefikiria kuchumbiana naye.
"Alikuwa binti wa nje ya ndoa, lakini yeye si wa nje tena. Yeye ndiye bintiye rasmi wa familia ya Kimaro. Yeye ndiye binti mdogo kabisa katika familia.
Bibi Kimaro alimkumbusha Alvin, “Kwa njia, Suzie ana zaidi ya miaka mitatu lakini bado hajafikisha miaka minne. Unaponunua zawadi, zinunue kulingana na umri wake. Pia, acha nikufahamishe kwamba ninamruhusu Suzie atumie chumba ambacho kilitayarishwa kwa ajili ya mapacha hao hapo awali. Hata hivyo hautakitumia sasa hivi.” Alikata simu baada ya kumaliza kuongea.
Alvin aliishika simu yake na kuduwaa kwa muda mrefu. Ikiwa watoto wa Lisa wangekuwa hai, wangekuwa karibu na umri huo pia.
Wakati huo simu yake iliita tena. Sarah ndiye aliyepiga simu. “Alvinic, bado unatakiwa kufanya kazi kwa saa za ziada leo? Si ulikubali kunipeleka hospitali kuchoma sindano baadaye?”
“Sina muda leo. Lazima niende kwa babu baada ya kumaliza kazi yangu, ina naweza nisirudi nyumbani,” Alvin alieleza.
Sarah aliuma mdomo. “Bado unanikasirikia kwa sababu kaka yangu alituma watu kuharibu nyumba ya Lisa? Alvinic, kwa kweli sikujua juu yake. Nilimwonya hapo awali, lakini wakati mwingine hanisikii. Samahani. Sifa yako imeharibika kwa sababu nina mbaya kaka kama huyo…”
"Sarah, acha yaliyopita yawe yamepita. Lakini nakushauri ujiweke mbali naye. Tayari ana uwezo wa kujiokoa,” Alvin alimkatisha. Kusikiliza maneno yake mara moja au mbili kungemfanya amhurumie, lakini, aliposisitiza mara nyingi sana, ilimfanya azidi kumchukia zaidi Thomas.
“ Sawa,” Sarah alijibu kwa aibu.
"Kwa kweli nina jambo la kushughulikia nyumbani kwa babu leo."
Baada ya Alvin kukata simu, alimuomba Hans amuandalie zawadi mtoto huyo.
Wakati Hans aliposikia kwamba Jack alikuwa na binti nje wa miaka mitatu, alishikwa na butwaa.
“Mbona umeduwaa? Nenda haraka.” Alvin alimkazia macho.
Baada ya Hans kutoka nje, mara moja akapata sehemu na kupiga namba ya Lisa. "Bi Jones, binti wa nje wa Jack anaweza kuwa ..."
“Uko sahihi. Ni Suzie,” Lisa alimweleza Hans kila kitu kinyonge.
Hans alipigwa na butwaa.
Hakuna aliyejua kuwa 'kuharibika kwa mimba' kwa Lisa miaka mitatu au minne iliyopita lilikuwa jambo ambalo yeye na Jack waligushi ili kuwaokoa watoto wa Alvin waliokuwa hatarini.
Hapo nyuma, Lisa alikuwa ametokwa na damu nyingi baada ya Alvin kumsukuma. Watoto walikuwa karibu kupotea, lakini bado walinusurika mwishowe. Wakati kila mtu alijua kuwa mimba hiyo imeharibika. Zaidi ya hayo, hata kama Lisa angezaa mapacha hao, bila shaka asingeweza kupata malezi ya watoto hao. Watoto bila shaka wangedhulumiwa ikiwa wangeanguka mikononi mwa Sarah.
Kwa hiyo, alikuwa amewasiliana na Jack. Jack mara moja alimhonga daktari na kumwambia daktari amwambie kila mtu kwamba mimba ya Lisa ilikuwa imeharibika.
Hans alifikiri Alvin angemtaliki Lisa na kumwacha aondoke baada ya kuharibika kwa mimba, lakini hakuwahi kufikiria kwamba Sarah angemchochea Alvin kumpeleka Lisa kwenye hospitali ya wagonjwa wa akili. Yeye na Jack walikuwa na wasiwasi sana katika kipindi hicho cha wakati.
Kama suluhisho la tatizo hilo, waliamua kudanganya kifo cha Lisa baadaye na na kumsafirisha kwenda nje ya nchi ambako watoto wake walizaliwa salama huko Marekani.
Hans hakutarajia kwamba Suzie angerudi kwenye familia ya Kimaro kama binti wa Jack mwishowe. Hii ilikuwa kwa bora pia. Angalau Suzie angeweza kurudi kwa familia ya Kimaro kwa mara moja na asilengwe na Sarah pia.
Kwa kuwa ilikuwa zawadi ya binti mdogo, Hans alienda kwenye duka la watoto mara moja na kununua nguo nyingi na vifaa vya kuchezea ambavyo wasichana wadogo wangependa. Ni wazi, alitumia kadi ya Bwana Kimaro kulipia. Bwana Kimaro alikuwa na deni kubwa mno kwa bintiye.
Sura ya: 374
Saa kumi na mbili na nusu za jioni, gari aina ya Sedan iliingia kwenye nyumba ya familia ya Kimaro. Baada ya Alvin kushuka kwenye gari, Hans alifungua buti. Uso wa Alvin ulibadilika baada ya kuona buti limejaa hadi ukingoni. "Ni nani aliyekuruhusu kununua vitu vingi?"
Hans akapepesa macho. "Yeye ndiye mwanachama mdogo zaidi wa familia ya Kimaro. Nilisikia kwamba Bibi Kimaro amefurahiya sana. Familia ya Kimaro haijachangamka hivi kwa muda mrefu, kwa hivyo nilinunua zawadi zaidi.”
Alvin alishtuka. "Huyo si mtoto wangu hata hivyo."
Kwa kweli, huyo alikuwa mtoto wake, ndiyo maana Hans alimunulia zawadi nyingi vile.
Alvin alipanda ngazi. Alipoingia tu ndani ya jumba hilo, msichana mdogo ambaye nywele zake zilikuwa zimefungwa kwenye mabutu mawili akikimbia.
Aligeuza kichwa chake alipokuwa akikimbia na kusema, “Paka alikimbia. Ninamfuata.
"Usikimbie, kidonda chako bado hakijapona." Lea alikuwa amemaliza kuongea ndipo Suzie alipowavamia miguu ya Alvin na kuanguka chini.
“Mtoto, tazama mbele yako unapotembea.” Alvin akainama na kumsaidia kuinuka.
Suzie aliinua macho na kuiona sura ya Alvin karibu. Ulikuwa ni uso ambao alizoea kuuona kwenye picha na video tu, na sasa alikuwa akiuona laivu. Siku chache zilizopita, Lucas alikuwa amefungua video kwenye mtandao na akamwonyesha. Lakini, baada ya kukutana na Alvin katika maisha halisi, Suzie aligundua kuwa anaonekana mzuri zaidi kuliko alivyokuwa kwenye picha. Hapana, alikuwa mzuri zaidi kuliko ma-uncle wake wote waliokuwa karibu na mama yake.
Suzie alijua kuwa huyo ni baba yake mkorofi. Baba yake mchafu pia alikuwa na mwili mzuri. Shati lake jeusi la kawaida lililochomekewa kwenye suruali ya rangi ya kahawa lilionyesha kikamilifu kiuno chake chembamba na miguu mirefu.
Macho yake yakaangaza mara moja. Ingawa alipaswa kumchukia, alikuwa mzuri sana hivi kwamba hakuweza kupinga kumpenda. Alvin aliinamisha kichwa kumtazama pia yule binti mdogo. Alikuwa na mng’aro wa kitoto kwenye mashavu yake dodo na alikuwa mrembo kama mwanasesere mzuri.
Alivin alihisi mvuto wa ajabu na kumpenda kwa mtazamo wa kwanza. Alipoona kichwa chake kimefungwa bandeji, hakuweza kujizuia kumuonea huruma pia. Ilikuwa ni hisia ya kuvutia. Ni wazi hakuwapenda watoto hapo awali. Labda ni kwa sababu mtoto huyo alifanana naye.
Hakuweza kuelewa. Kwa nini mtoto wa Jack alifanana naye sana?
“Suzie, uko sawa?” Wakati huo, Lea alimkimbilia. Baada ya kumuona Alvin, Lea alishindwa kujizuia kumtazama pia Suzie. Naye akakubali. “Si ajabu Aunty Valerie alisema Suzie anafanana na wewe. Mnafanana kweli.”
“Bibi, niko sawa. Huyu ndiye Uncle Alvin?" Suzie alipepesa macho yake makubwa. "Anko Alvin anaonekana mzuri sana."
"Ndiyo, huyu ni Anko Alvin," Lea alisema huku akitabasamu.
“Anko Alvin, nakupenda sana.” Suzie aligeuka na kulikumbatia paja la Alvin.
Alvin alipigwa na butwaa, na bila fahamu alinyoosha mikono yake kumbeba. Msichana mdogo alikuwa mwepesi sana, na alikuwa na harufu nzuri ya maziwa.
“Bwana Mkubwa, hizi ndizo zawadi ulizomnunulia Binti Mdogo.” Hans alileta rundo la nguo na midori.
"Wow, nazipenda! Zite ni nzuri kwangu. "Suzie alitoka kwenye kumbatio lake. Alikimbia na kutazama nguo na midori. Macho yake yalikuwa yamejipinda huku akitabasamu. Alikuwa akitabasamu kutoka sikio hadi sikio.
Alvin alitabasamu bila kupenda. Alidhani Hans alikuwa amenunua vitu vingi sana hapo mwanzo, lakini ghafla alihisi kuwa hakununua vya kutosha.
“Umenunua hizi?” Lea alimtazama kwa mshangao. "Hiyo ni nadra."
Wakati huo, Suzie alikimbia upande wa Alvin. Akampa ishara kwa kidole. "Anko Alvin, inama kidogo." Baada ya kuinama, Suzie alisimama kwa vidole vyake na kubusu shavu lake. "Asante, Anko Alvin."
Alvin alihisi kana kwamba moyo wake unabanwa na mkono kwa wakati huo. Hakuweza kueleza hisia zake. Alihisi kama… Alimpenda binti yule mdogo sana. Alikuwa na hamu ya kung'oa mwezi na nyota kutoka angani kwa ajili yake ikiwa alitaka.
Hata hivyo… Suzie alikuwa binti wa Jack. Jack, ambaye Alvin alimdharau zaidi tangu alipokuwa mdogo. Ikiwa watoto wake wangekuwa hai, wangekuwa wa kupendeza sana, sivyo?
Alvin akatoa kadi kwenye pochi yake na kuiweka mikononi mwa Suzie. "Hizi ni pesa za mfukoni kwako."
Macho ya Lea nusura yaanguke chini kutokana na mshtuko.
Hakutarajia kamwe Alvin angekuwa na urafiki kwa binti ya Jack. Mbali na hilo, Alvin alimtendea kila mtu kwa ujeuri Suzie labda ndiye pekee aliyepata ukarimu maalum kutoka kwake.
"Hii ya nini? Babu wa baba alinipa kadi pia. Yule Baba Mkubwa alinipa pia, inatosha. ” Suzie alimrudishia Alvin kadi. "Siwezi kuchukua hii."
Alvin alifurahi. Ilionekana kama mama yake alikuwa amemfundisha vizuri. "Ni sawa. Kadi hiyo ulipewa na babu yako, wakati hii umepewa na mimi. Ina maana tofauti. ”
“Suzie, chukua kadi. Anko wako ana pesa nyingi hata hivyo. Usipoteze,” Lea alimkumbusha.
Suzie aliinamisha kichwa chake na kuwaza. Hiyo ilikuwa sawa pia. Angeweza kumpa Lucas moja ya kadi. Ingawa hawakujua kuwepo kwa Lucas, aliweza kuweka sehemu ya kila kitu alichopokea kwa ajili ya Lucas. Isitoshe, je, isingempa faida mama yake wa kambo katili ikiwa asingechukua pesa za Baba yake mchafui?
“Sawa.” Baada ya Suzie kujibu kwa sauti ya kitoto, aliushika mkono wa Alvin. "Anko Alvin, unaweza kwenda kuona paka pamoja nami?"
Lea alidhani Alvin angemkataa kabisa Suzie. Alipotaka kuwakatisha, Alvin alikubali bila kutarajia. Hata alimruhusu Suzie apande mabegani mwake na kumpeleka nje kucheza.
Valerie alitembea huku akila karanga. Alisema, "Wale ambao hawajui bora zaidi watafikiri kwamba wao ni baba na binti."
“Uko sawa.”
Ilikuwa ni usiku sana baada ya tafrija kumalizika. Alvin alikaa usiku kucha katika nyumba ya babu yake. Katika miaka mitatu iliyopita, alienda hapo mara chache sana kwa sababu kulikuwa na athari nyingi za Lisa hapo.
Usiku, alipumzika chumbani kwake. Labda ni kwa sababu aliendelea kuwaza juu ya watoto wawili aliowapoteza hapo awali ndipo hakuweza kulala. Ghafla, sauti ya mtu akigonga mlango nje ilisikika. Aliinuka na kufungua mlango. Suzie alikuwa amevalia seti ya pajama za kupendeza za dubu. Alisimama mlangoni kwa huzuni huku akipepesa macho. "Anko Alvin, tunaweza kulala pamoja?"
"Unaweza kulala na baba yako," Alvin alisema kwa upole.
'Sipendi kulala naye. Anakoroma na kuna kelele nyingi,” Suzie alifoka na kusema kwa namna ya kuchekesha.
“Sawa. “Alvin akainama na kumbeba.
Juu ya kitanda, Suzie alimng'ang'ania kama luba. Punde, alilala fofofo.
Alvin alipomtazama, bila kufafanua alimsikia msichana mdogo akinong'ona 'Baba'.
Moyo wake ulijawa na uchungu. Labda ilikuwa wakati wa kujenga familia yake mwenyewe. Vinginevyo, kwa nini aone wivu kwa Jack kwa kuwa na binti mzuri kama huyo? Baada ya kufikiria upuuzi kwa muda, alilala pia.....ITAENDELEA....
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.
