JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................329-330

Sura ya: 329

Alvin alikula chakula chote kwa muda mfupi lakini bado alikuwa akihisi njaa. Alienda bafuni na kumkuta Lisa akiwa anafua nguo zake kwenye sinki. Bila hata kumuaga, aliamua kuondoka.

Mwanamume huyo aliendesha gari kupita barabara yenye shughuli nyingi na kuona mgahawa maalumu kwa pasta. Aliingia na kuagiza pasta kutoka kwenye menyu lakini alitema chakula baada ya kuonja mara moja tu. “Pasta unayotengeneza ina ladha ya kutisha,” alifoka kwa hasira.

"Umekuja hapa kwa ajili ya kula au kufoka?" Mmiliki wa mgahawa akaruka kwa hasira. "Nimekuwa nikiendesha mgahawa wangu kwa zaidi ya miaka kumi na kila mtu hapa anazipenda pasta zangu. Wewe ndiye wa kwanza kulalamika.”

"Hiyo ni sawa. Pasta za hapa ni bora zaidi katika mtaa mzima." Mmoja wa wateja hakuweza kujizuia kusema.

Alvin hakujua la kusema. Lisa alikuwa amemroga kwenye vyakula alivyompikia? Haikuwa na umuhimu wowote hata kama ingekuwa mmiliki huyo amekuwa akiendesha mgahawa huo kwa zaidi ya karne nzima. Ukweli ulibaki kuwa chakula alichotengeneza Lisa kilikuwa na ladha nzuri zaidi.
•••
Kufika nyumbani, Sarah alimsalimia huku akiwa amevalia nguo za ndani za kuvutia. Alionekana kushangaa kumuona Alvin akirudi nyumbani mikono mitupu.

“Mbona umechelewa nyumbani hivi?” Sarah alihoji huku uso wake ukiwa umemshuka. Kwanza alikuwa amechoshwa na shuruba za Hisan, pili alichoka kwa kuona Alvin akija akiwa mikono mitupu.

"Nilikuwa nikifanya kazi kwa muda wa ziada," Alvin alisema bila kutarajia alipokumbuka kila kitu kilichotokea nyumbani kwa Lisa hapo awali.

“Pole.” Sarah alihisi moyo wake kuzama.

"Lisa alikutishia kwenye mkutano asubuhi ya leo?" Alvin alimuuliza ghafla.

"Ndio." Sarah alijibu huku akikunja sura yake kwa madeko.

Alvin alikumbushwa kitu ghafla. Alikuwa ameenda kumtafuta Lisa ili kumuonya kuhusu tukio hilo lakini bado alisahau kila kitu baada ya kuingia nyumbani kwake.

Hisia ya hatia iliosha juu yake. “Sarah, samahani, mimi—”

“Acha. Najua ulimkubalia Lisa achukue kampuni kwa ajili ya yangu mwenyewe.” Sarah alijitupa mikononi mwake. “Ila nina wasiwasi kwamba Lisa atakuiba. Mkutano wa leo ulipoisha, aliniambia kuwa ataharibu kila kitu ninachojivunia.”

"Kuharibu kila kitu?" Macho ya Alvin yalionyesha kubadilika. "Anafikiri yeye ni nani?"

Sarah akashusha pumzi. “Nilimshauri aachane na mambo hayo lakini hakutaka kunisikiliza. Kuna umuhimu gani wa kukosana na kila mtu? Anahitaji kujua kwamba makampuni mengi yanashirikiana na Mawenzi kwa sababu ya kukuheshimu.”

Wazo likamjia Alvin kichwani huku akimpigapiga Sarah kichwani. “Uko sahihi. Itakuwa majanga kwa Mawenzi Investments ikiwa kampuni zitakataa kufanya kazi naye. Ni juu yake kuamua kama anataka kusaini hati za talaka ili kuokoa kampuni.”

“Alvinic, unafikiria…” Sarah aliuma mdomo wake. "Hii haitakuwa sawa."

"Acha ujinga wewe, kila mtu anajua kwamba tunafunga ndoa mwaka huu. Itakuwaje kwako nisipomtaliki?” Akamkumbatia kwa upole. Mwanamke huyo alitabasamu kwa ujanja mikononi mwake.

Baada ya kuelekea ghorofani, Sarah alimuuliza kwa mtego wakati akibadilisha nguo chumbani. “Alvinic, ni lini utapata muda wa kwenda shopping na mimi? Nataka kununua nguo mpya za ndani."

“Si nilikupa kadi yako ya benki hapo awali? Tumia tu kwa chochote unachotaka." Alvin alimjibu na moja kwa moja akaelekea bafuni.

Sarah alihisi kukosa raha ghafla. Joan alikuwa amekosea, au? Alvin alikuwa akinunua nguo za ndani kwa ajili ya nani kama si yeye mwenyewe? Lisa? Au alikuwa na mwanamke mwingine?

Alfajiri iliyofuata, Sarah alichukua ufunguo wa gari la Alvin kwa siri na kuingia ndani ili kuangalia picha za dashcam. Ndani ya sekunde chache, aligundua kuwa Alvin alikuwa ameendesha gari kwenda mahali fulani paitwapo Karen Estate mara mbili jana yake usiku.

Asubuhi hiyohiyo, Sarah aliendesha gari hadi sehemu ile ile na akashtuka baada ya kumuona Lisa akitoka pale. Ni kweli alikuwa Lisa. Hii ilikuwa nje ya matarajio yake.

Tatizo lilikuwa nini? Tayari Sarah alikuwa amemvuruga Alvin ili amdharau Lisa. Ni lazima angekuwa ni Lisa ambaye alikuwa akimg’ang’ania Alvin. Huyo b*tch! Lazima angemtambua.

•••

Saa mbili na nusu asubuhi, Lisa aliingia kwenye kampuni na kuwakuta baadhi ya wanahisa na wajumbe wengine wa bodi ya wakurugenzi wakimsubiri. Meneja Mkuu Ngololo aliyekuwa amerejeshwa kwenye nafasi yake alionekana kukosa subira akiwa amesimama kando.

"Leo mbona mapema?" Lisa aliwauliza kwa mshangao.

Mkurugenzi Gumbo alisema baada ya kuketi kwenye meza yake, "Unafikiri bado tunaweza kulala vizuri? Makampuni matatu makubwa ya ujenzi ambayo yameshirikiana nasi kwa miaka mingi ghafla yalighairi ushirikiano wao mara moja. Zaidi ya saiti kumi za ujenzi kote nchini Tanzania na Kenya haziwezi kuendelea kufanya kazi leo. Mwenyekiti Jones, ulionekana kana kwamba ulikuwa karibu sana na Bwana Kimaro hivi majuzi, lakini kwanini ghafla hakuna mtu anataka kushirikiana nawe?”

"Ninaamini ni kwa sababu alimkosea Miss Njau jana," Mkurugenzi Williams alisema kwa hasira, "Kampuni hizo za ujenzi zilifanya kazi nasi tu kwa heshima ya Miss Njau na Bwana Kimaro. Lazima walisikia kwamba kuna kitu kibaya kati yenu."

"Tunapaswa kufanya nini? Kampuni imepoteza zaidi ya dola milioni kumi baada ya maeneo ya ujenzi kulazimika kuacha kazi kwa siku moja tu, itakuweje baada ya wiki?” Mkurugenzi Wande aliuliza kwa wasiwasi.

“Hilo si tatizo letu kubwa. Suala ni kwamba wanataka kuacha kushirikiana nasi.” Mkurugenzi Gumbo alionekana kufadhaika.

“Siku zote tunaweza kushirikiana na washirika wengine,” Lisa alijibu.

"Unajua nini?" Mkurugenzi Gumbo alisema bila subira, "Wateja walinunua tu mali zetu kwa sababu ya sifa nzuri za kampuni tunazoshirikiana nazo. Hao ndio njia bora zaidi ya kufanya biashara katika nchi hii. Wateja walinunua mali hizi kutoka kwetu kwa sababu wanaziamini. Kwa hakika watatukimbia ikiwa kampuni zitabadilishwa. Sifa ya kampuni yetu itaharibika wakati hilo litatokea.”

“Hiyo ni sawa. Suluhisho pekee sasa ni kutafuta msaada kutoka kwa Bwana Kimaro au kumwomba Bi Njau msamaha. Mkurugenzi Williams alisema, "Lazima utatue tatizo hili uliloanzisha. Usituhusishe wajumbe wa bodi.”

"Usitulaumu kwa kuchukua nafasi yako usipotatua jambo hili," Mkurugenzi Gumbo akaingilia. "Huwezi kutukasirikia. Tunafikiria tu faida za kampuni. Mwenyekiti mzuri hatazuia ukuaji wa kampuni.”

Lisa aliwatazama tu kwa utulivu. "Nilisema siwezi kushughulikia hili?"

“Una uhakika unaweza?” Mkurugenzi Gumbo hakuonekana kushawishika.

Mkurugenzi Williams alisita kabla ya kusema, "Labda kuna nafasi. Bwana Kimaro anaonekana kama bado anamjali Mwenyekiti Jones.”

"Natumai hautoi ahadi tupu," Mkurugenzi Wande alisema kwa sauti ya kushangaza. "Maeneo ya ujenzi yanaweza kuacha kufanya kazi kwa siku tatu tu."

“Hakika.” Lisa aliitikia kwa kichwa.

“Basi tutakupa nafasi. Ikiwa kampuni za ujenzi hazitaanza tena kufanya kazi baada ya siku tatu, basi tutachukua nafasi yako kama mwenyekiti wa kampuni.” Mzee Gumbo alitoa angalizo.

Baada ya kuondoka kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi, Meneja Mkuu hakuweza kujizuia kuuliza kwa wasiwasi, “Mwenyekiti Jones, unaweza kweli kushughulikia hili? Hali ni tata sana wakati huu."

Sura ya: 330

“Rudi kazini. Nitalishughulikia hili.” Lisa alifungua laptop yake. Amba alimtazama kwa ajabu bosi wake ambaye safari hii alionekana kujiamini isivyo kawaida.

Ndani ya muda mfupi, kila mtu alisikia habari za kampuni tatu kubwa zaidi za ujenzi za Kenya na Tanzania kughairi ushirikiano wao na Mawenzi Investments. Siku iliyofuata, hisa za kampuni hiyo zilishuka kwa pointi nane.

Alasiri hiyo, Lisa alikuwa anakula chakula cha mchana kantini wakati Alvin alipompigia simu. Sauti ya Alvin ilipambwa na kiburi. “Unatakiwa uniombe msaada. Nitasuluhisha suala hilo na kampuni za ujenzi ikiwa utakubali kunitaliki.”

“Usijali. Nitalitatua mwenyewe.” Lisa alimkata stimu kabisa.

Tabasamu la kijeuri lilienea usoni mwake. "Thubutu, hata kama utawaita mabosi wa kampuni hizo na kuwapa rushwa ya ngono hutaweza kutatua jambo hili."

Mwanamke akacheka. “Kweli umedhamilia kunitaliki kwa nguvu zote? Maana si nguvu hizi unazotumia kubadilisha mawazo ya watu.”
"Umejitakia mwenyewe hili." Sauti yake haikuwa ya kirafiki. “Nisingefika mbali kama hukumkosea Sarah na kuendelea kuburudisha ndoto zako hizo nzuri. Ninakushauri usaini hati hizi mapema na kwa utulivu wa akili au sitajali kupoteza wakati wangu kuendelea kucheza mchezo huu na wewe.”

"Inaonekana kama mpenzi wako wa maisha yako amekuwa akikushinikiza sana nikutaliki ili umuoe," Lisa alijibu bila kujali. "Unaweza kuendelea kufanya chochote unachotaka."

Sauti yake isiyo na hasira ilimkera sana Alvin hivi kwamba akakaribia kutupa simu yake chumbani. Hakika, angeweza kuwa mkaidi na kujidai yote aliyotaka kwa muda huo lakini hakuweza kusubiri kuona majuto usoni mwake baada ya siku tatu.

Ilikuwa ni mida ya saa kumi jioni ambapo Lisa alimkuta Meneja Halua kutoka Idara ya Masoko akipapasana na Sarah alipotoka kwenye lifti.
Sarah haraka alisema alipomkaribia, “Lisa, usielewe vibaya. Meneja Halua na mimi tunajadili kazi tu.”

Meneja Halua aliinua macho yake kwa aibu. “Bi Njau, huna haja ya kujieleza. Kwa maana, leo inaweza kuwa siku ya mwisho ya Mwenyekiti Jones katika kampuni hii.”

Lisa alimtupia jicho meneja huyo bila kujali. Kujiamini kwake na uwepo wake wa kutawala ulijaza chumba. Meneja alihisi wasiwasi kwa sekunde ya haraka kabla ya kujifanya ana utulivu wa kutosha.

“Lisa, tulikuwa tunazungumza tu. Usifanye mambo kuwa magumu kwake kwa sababu tu una kinyongo dhidi yangu.” Sarah alijiweka mbele ya meneja.

“Bado unafanya nini hapa Sarah?” Lisa alijibu kwa upole, "Huwezi kuishi siku hata moja bila kuja kufanya show mbele yangu, huh?"
"Sii ... sikuwa…" Sarah alionekana mwenye huzuni ghafla kana kwamba anataka kulia. “Nilisahau kukabidhi baadhi ya nyaraka kwa Meneja Halua nilipoondoka jana. Ndiyo maana niko hapa leo.”

"Meneja Halua, chukua hizo nyaraka na urudi kazini haraka. Bado ni saa za kazi. Sijali kama ungependa kuzungumza na Sarah, lakini una wakati wote wa kuzungumza naye baada ya saa za kazi.”

Lisa hakuweza kujisumbua kushughulika na watu hao na akageuka kwa nia ya kuondoka. Bila kutarajia, ghafla Sarah akablock kwa mbele ili kujigongesha kwenye mabega yake. Mara Sara akajikongoja hatua chache nyuma na kuanguka chini.

“Sarah.” Kivuli kirefu kilikimbia kumsaidia mwanamke huyo asianguke chini. Lisa alielewa kila kitu ndani ya sekunde chache. Alikasirishwa na ulaghai huo wa uwongo kupita kiasi.

“Alvinic, sikujua kama upo hapa,” Sarah alisema mara moja, “Usielewe vibaya. Lisa hakufanya hivi makusudi.”

“Acha kumtetea. Niliona kwa macho yangu kwamba alikugonga kimakusudi.” Alimtazama Lisa kwa hasira. “Hujabadilika hata kidogo baada ya miaka mitatu. Bado ni mkatili kama hapo awali. Fanya haraka na kuomba msamaha, la sivyo?"

“La sivyo nini?” Lisa alikosa la kusema. Miaka mitatu iliyopita, ni yeye ndiye aliyekuwa akinyanyasika bila huruma. Ilikuaje akawa mkatili sasa? Hakukuwa na kitu kingine ambacho angeweza kusema. Lakini, alipitia matukio kama hayo mara nyingi sana kwake kuwa na hasira juu yake tena.

“Alvin, umewahi kusikia kuhusu kitu kinachoitwa kamera za uchunguzi? Unaweza kuangalia ni nani aliye na makosa kwanza kabla ya kutoa shutuma?” Lisa alisema kwa utulivu.

Sarah alionekana kufadhaika lakini Alvin hakuliona hilo hata kidogo. Muda wote alikuwa akimwangalia Lisa kwa hasira. "Unamaanisha kwamba nisiamini macho yangu mwenyewe lakini niamini kamera za uchunguzi ambazo zinaonyesha mtazamo tofauti kutoka kwa pembe tofauti?"

Lisa alisugua kichwa chake. Alitamani sana kumfokea na kumwambia kwamba mtu anaweza kuona mambo kwa macho yake kutoka pembe tofauti pia. Alijiuliza ikiwa huenda Sarah alimlaza akili ili asiwe na akili hata kidogo kila anapokuwa mbele ake.

“Alvinic, achana naye. Twende,” Sarah alimuomba huku akimvuta mkono mwanaume huyo.

Meneja Halua alisema kwa haraka, “Bwana KImaro, hakika unapaswa kumtetea Bi Njau wakati huu. Alikuwa hapa kunikabidhi nyaraka fulani. Alikuwa akinikumbusha maelezo ya ziada wakati Mwenyekiti Jones alikuja kusema kwamba Miss Njau alikuwa akifanya show na kuanza kumkaripia. Bila kutaja alikuwa akimaanisha kuwa tulikuwa tunapoteza muda kwa kupiga gumzo. Yeye hata… Yeye hata…”

“Ongea.” Macho ya Alvin yaliyokuwa yamemkodoa yalijawa na hatari.
Meneja Halua alisema kwa kusaga meno, "Hata alijisifu kuwa nguo za ndani alizovaa leo zilinunuliwa na wewe."

Sarah aliinamisha kichwa huku machozi yakimlenga lenga.
“Naweza kueleza hilo. Sarah, si unajua jinsi ninavyojisikia kuhusu wewe kwa sasa? Ninajisikia vibaya hata nikimtazama tena mwanamke huyu sasa.” Alvin alifadhaika, bila kutarajia kwamba uamuzi wake wa jana usiku ungemuumiza Sarah.

Ghafla, akampa Lisa jicho la kutoboa ngozi. Wafanyakazi waliokuwa wamekusanyika kuangalia zogo hilo walionekana kushangaa.

Kama ilivyotokea, Bwana KImaro hakuwa na hisia kwa Mwenyekiti Jones tena. Hata alichukizwa naye. La hasha, walipaswa kujaribu zaidi kumfurahisha Sarah badala ya kumuunga mkono Lisa. Baadhi yao walijutia sana uchaguzi wao wa kumuunga mkono Lisa.

Lisa hakuwa na neno la kujibu. Sio tu kwamba alikuwa hana la kusema, lakini pia alijisikia kucheka kwa upuuzi ule. Alijiona mjinga kwa kutorekodi mazungumzo yao mapema. Tazama, watendaji wa kampuni yake walikuwa wakishirikiana na Sarah kumshtaki.

“Lisa, hata mimi nilifikiria kukusaidia kwenye tukio la kampuni za ujenzi zilizokususia kwani zamani tulikuwa mke na mume. Lakini sitafanya hivyo tena.” Sauti ya Alvin ilikuwa baridi kama barafu. “Kuanzia leo na kuendelea, nitahakikisha watu wote wanajua kuwa sina uhusiano tena na Mawenzi Investments. Isitoshe, yeyote ambaye atathubutu kukusaidia atakuwa akipambana na mimi moja kwa moja.” Kisha, akatoka nje ya kampuni bila kuangalia nyuma huku akiwa amemshikilia Sarah kwa karibu.

"Bwana KImaro, tafadhali subiri." Mkurugenzi Gumbo na wengine haraka walimfuata. Hata hivyo, Alvin aliwapuuza kabisa na kuingia kwa kasi kwenye gari lake.

Wajumbe wa bodi walikasirika na kurudi mbio kumkaripia Lisa, “Sijui unataka kufanya nini lakini kwanini uishushe kampuni pamoja nawe? Angalia ulichofanya! Neno moja tu kutoka kwa Bwana KImaro na hakuna mtu atakayethubutu kufanya biashara nasi tena."

“Mtu kama wewe hastahili kuwa mwenyekiti. Ondoka hapa!” Mkurugenzi Wande alipiga kelele.

Wafanyakazi na wanahisa wengine pia walianza kuzungumza nyuma yake.
“Anafanya nini hapa? Kampuni ilikuwa ikipanda chini ya uongozi wa Mwenyekiti Njau. Hata nilipata mamia ya maelfu ya dola katika bonasi za mwisho wa mwaka katika miaka ya hivi karibuni.”

"Ni bahati mbaya sana kwamba tumekwama na mwenyekiti wa aina hii."
"Sawa, tunapaswa kuuza hisa zetu hivi karibuni na kuwekeza mahali pengine kabla hatujachelewa."

“Sasa kwa vile umesema, basi lazima nijitayarishe pia.”.....ITAENDELEA...

Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.