JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................309-310
Sura ya: 309
Sarah alibofya ulimi wake na kusema, “Kwanini nikudanganye? Lisa hakuweza kukubali ukweli kwamba mimi na Alvinic tuko kwenye uhusiano. Zaidi ya hayo, kaka yangu pia alitaka kumbaka Pamela. Lakini Alvinic hakuweza kuvumilia kumuona akiwa kwenye matatizo, hivyo akamtoa kaka yangu jela na kumzuia Pamela asichunguze suala hilo. Lisa alikasirika sana hivi kwamba alikuwa na ugomvi na Alvinic. Alvinic alimsukuma, na akawapoteza watoto tumboni mwake. Kwa kuwa alikuwa na kiwewe, nilimwambia Alvinic ampeleke hospitali ya magonjwa ya akili kwa matibabu. Pamoja na sindano na dawa zote alizopewa, alijiua mwishowe.”
Alitamka kila neno kwa kawaida sana. Hata hivyo, maneno hayo yalisikika masikioni mwa Charity kama bomu.
Thomas alitaka kumbaka Pamela? Lisa alijiua? Ingawa Charity hakuwajua Pamela na Lisa kwa muda mrefu, aliweza kutambua kwamba ni watu pekee waliomwamini kwa dhati pindi anapopata matatizo. Lakini, angalia jinsi walivyoishia.
"Sarah, kwanini unakuwa mkatili kiasi hiki?" Charity alikasirika sana hadi macho yake yakawa mekundu, na mwili wake ukatetemeka. Kama kusingekuwa na dirisha la nondo lililowatenganisha wawili hao, angetoka nje na kumchukua Sarah na kumfanyia kitu kibaya sana.
"Mimi ni mkatili zaidi kuliko unayoweza kunifikiria." Sarah aliridhishwa na jinsi Charity alivyoonekana kuwa na wasiwasi sasa. “Lisa alipokutembelea mara ya mwisho, hakukuambia kuwa wazazi wako wamekufa?”
Bam! Habari hizo zilikuja kama pigo jingine kwa Charity. Alitikisa kichwa kwa nguvu. "Lazima utakuwa unanidanganya!"
"Nilimweka mama yako chini ya ‘hypnosis’ nyepesi. Baada ya mimi kuondoka, alianguka kwenye sinki la kuogea na akafa kwa kupoteza damu nyingi kwa sababu hakuna aliyemuokoa. Baba yako alipojua kuhusu hilo, alipata mshtuko wa moyo na akafa. Usitarajie kama watakutembelea maisha yako yote.”
Sara aliangaza vibaya. Aliongea kwa upole kiasi kwamba ni wawili tu waliweza kumsikia. "Lakini ilipofika wakati wa mazishi ya mama yako, niliutoa mwili wa mama yako kwenye jeneza na kuubalidilisha kuwa wa mbwa."
"Sarah, wewe si binadamu." Damu ya Charity ilikuwa ikichemka.
Aliendelea kupiga nondo za dirisha mithili ya mwendawazimu, akitaka kumuua Sarah vibaya sana. Hata hivyo, upesi polisi walimzuia.
Charity alipiga kelele kama mnyama wa porini, na uso wake ulijaa machozi. Kwanini Mungu alikuwa akimpendea hivyo?
Alichoishia ni kuwa gerezani, na rafiki na wazazi wake walikuwa wamekufa. Sasa, alikuwa peke yake kabisa. Hata hivyo, muuaji alikuwa huko nje akiwa huru kaisa. Katika kipindi chote alichokuwa gerezani, Charity hakuwahi kulia kwa huzuni hivyo bila tumaini na bila kufarijiwa. Polisi hawakuwa na la kufanya zaidi ya kumwangusha na kupoteza fahamu.
Charity alipozinduka alijikuta amelala kwenye kitanda cha magereza. Macho yake ya kupendeza yalibadilishwa na kuwa kama shimo la giza lisilo na mwisho. Alitaka kulipiza kisasi. Alitaka kulipiza kisasi dhidi ya kila mtu aliyemkosea.
Sarah Njau, Alvin Kimaro, Chester Choka, Thomas Njau… Alichokuwa akingoja ni muda tu!
•••Nusu mwaka baadaye•••
Mara tu Chester alipomaliza upasuaji wa saa tatu, msaidizi wake alimsogelea ghafla. "Nilipokea habari kwamba Charity aliruka baharini na kukimbia wakati wafungwa walipokuwa wakilima shamba lao huko Bagamoyo. Polisi wamejaribu kumtafuta baharini kwa siku tatu, lakini bado hawajampata.”
Chester alijitenga kwa muda. Kisha, taratibu akavua miwani yake na kugeuka kuelekea dirishani. Akawasha sigara.
"Charity hawezi kuogelea."
"Unashuku kuwa amekufa?"
"Unafikiri nini kitatokea kwa mtu ambaye hawezi kuogelea, anarukia baharini?" Chester akavuta sigara yake.
Ghafla, alikumbuka sura ya Charity wakati alipokutana naye kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka kumi na saba. Alikuwa amesimama chini ya jua na sare za shule, shati jeupu na sketi damu ya mzee. Ngozi yake ilikuwa laini. Charity alikuwa kidato cha sita wakati huo na Chester tayari alikuwa mwanafunzi wa udaktari akitokea familia tajiri jijini Nairobi.
Siku hizo, wasichana walikuwa na haya sana walipomwona. Charity pekee alimtazama kimya na kwa mbali kwa macho yake safi. Wakati huo, Chester alikuwa na hamu kubwa ya kuvunja usichana wa binti huyo. Charity alikuwa mpole na alionekana kumpenda sana Chester.
Lakini nyuma yao kulikuwa na mtu ambaye hakuufurahia hata kidogo uhusiano wao huo. Mtu huyo alikuwa Sarah Langa. Sarah alimchukia Charity kwa sababu tu alikuwa binti wa mama yake wa kambo. Chuki yake alihakikisha inasambaa hadi kwa Alvin, ambaye alikuwa ni mpenzi wake kipindi hicho. Na Alvin, bila kujua nia na makusudi ya Sarah, akameza chambo na kueneza chuki hiyo hadi kwenye genge lote la marafiki zake, Rodney na Chester, ambao walijikuta wote wakimchukia Charity kwa sababu ya chuki zilizoenezwa na Sarah.
Hatimaye Charity akamkosa Chester aliyempenda sana. Tangu wakati huo Chaster hakumpenda tena Charity na alimchukia kila alipomuona. Kila alipopata mafanikio, walimchukulia kama mafanikio hayo yalikuwa ni haki ya Sarah. Charity alipambana kwa juhudi zake lakini vikwazoalivyokutana navyo kwa sababu ya Sarah havihesabiki.
Sura ya: 310
•••Miaka mitatu baadaye. Marekani•••
Lisa aliondoa bendeji usoni mwake polepole mbele ya kioo, akionyesha sura yake ndogo na ya kupendeza. Kisha akagusa ngozi yake maridadi. Baada ya kupitia miaka michache ya matibabu, ngozi yake iliyoonekana mara chache iligeuka kuwa laini na nyororo.
Isingekuwa rahisi kusema kwamba alionekana kama msichana mwenye umri wa miaka 18 pia. Sura yake, japo ilibadilika kidogo, Daktari Ramoskutoka Cuba aliyesimamia upasuaji wake, alijitahidi sana kuirejesha katika mwonekano wake wa awali.
"Wow, wewe ni mzuri sana, mama." Lisa alimwambia maneno hayo msichana mdogo mrembo aliyeinama kwenye mapaja yake na kumtazama kwa furaha, kisha akamgeukia na mvulana mdogo aliyekuwa akikimbia kimbia mbele yake. "Duh, angalia ni nani aliyepita na sura yake ya kuvutia mbele yangu?" Mvulana yule akakimbilia nyuma yake alionekana mwenye furaha. "Hakuna mtu anayeweza kuzaa mvulana mzuri kama mimi."
Lisa akasugua uso wake. Kutokana na sura yake changa na yenye kupendeza, hakuna mtu ambaye angeamini kwamba tayari alikuwa amepitia matatizo makubwa huko nyuma, na sasa ana sura mpya, na watoto wawili wazuri wenye afya.
“Lakini mimi sifanani na Mama hata kidogo. Lazima nionekane kama baba yangu mchafu.” Msichana mrembo alitabasamu.
Lisa naye akanyamaza. Kulikuwa na msemo kwamba binti atafanana na baba wakati mwana atafanana na mama.
Hakika ilikuwa sahihi. Ingawa Suzie na Lucas walikuwa mapacha, hawakufanana hata kidogo.
“Uko sahihi. Unafanana na baba yako mchafu, lakini wewe ni mrembo zaidi." Pamela akainama na kuzipapasa nywele za msichana huyo mrembo.
“Pamela…” Lisa alimtazama. “Niko tayari kurudi nyumbani. Na wewe je?"
Pamela aliinamisha macho yake chini. “Nitarudi wakati fulani baadaye. Bado nina mradi wa kushughulikia."
Lisa alimtazama kwa huzuni. "Ni sawa. Nyie wote ni Wamarekani sasa. Watoto wangu ni kwa kuzaliwa na wewe ni kwa Green Card. Wakati huu, nitarudi mimi binafsi…”
“Hakuna haja. Tutashungulikia na wewe upate Green Card.” Pamela ghafla akatazama juu na kusema, "Mimi sioni faida ya wewe kurudi iwe Tanzania ama Kenya. Unaweza kupata maisha mazuri hapa hapa kwa uwezo ulio nao. Marekani inawapenda sana watu wenye akili kama wewe."
"Hiyo ni sawa. Lakini lazima nirudi kumalizia kazi niliyoianzisha ya kumlipizia mama yangu kisasi." Lisa alificha sura ngumu machoni pake. “Ofcourse kuna wengine wamejitokeza pia kwenye mkumbo. Sarah na Alvin, lazima warudishe kila kitu kilichochangu."
“Sawa.” Pamela alikubali. “Kuhusu Thomas, nitakuja kudili naye mimi binafsi. Kwa sasa mimi si mnyonge kiasi hicho.”
“Sitaweza kuondoka na watoto hawa wawili pamoja nami wakati huu, kwa hivyo nahitaji uwatunze kwa sasa." Lisa alimsihi Pamela.
“Usijali. Sisi ni marafiki bora.” Pamela aliweka mkono wake kwenye bega la Lisa huku akitabasamu. “Zaidi ya hayo, mimi ni godmother wao."
“Mama, naweza kwenda nawe.” Lucas aliinua kichwa chake na kusema, “Naweza kukusaidia.”
"Mtoto mzuri. Mama anajua unaweza kumsaidia, lakini unahitaji kumtunza Suzie.” Lisa akampigapiga kichwani. "Mbali na hilo, ikiwa familia ya Kimaro itawaona nyinyi wawili, watawang’angania."
“Ndio. Mama yako amejitahidi sana kukulinda.” Pamela aliinamisha kichwa chake na kusema kwa uzito, “Hasa ni kwa sababu baba yako ataoana na mama yako wa kambo mwovu. Mwanamke huyo ni mbaya zaidi kuliko mama wa kambo wa Snow White. Ikiwa atajua kuwapo kwako, atakuiba na kukupeleka kwa mama yako wa kambo akulee kwa mateso.”
Suzie aliogopa sana hadi akakumbatia paja la Pamela. “Basi mimi sitaki kwenda na mama. Sitaki huyo mama wa kambo.”
Lucas alikunja uso. “Sawa. Nitakaa hapa kwa sasa, lakini lazima urudi haraka na kutuchukua."
“Sawa.” Lisa aliitikia kwa tabasamu mwanana. Licha ya kwamba angewa’miss sana watoto wake, ilimbidi arudi.
•••Siku mbili baadaye•••
Aliposhuka tu kwenye ndege wa Jomo Kenyatta, Kelvin Mushi alimwendea mara moja. "Karibu tena, Lisa." Kelvin alikuchukua masanduku yake huku akitabasamu. “Hukuwachukua Lucas na Suzie pamoja nawe?”
“Nimemwomba Pamela kuwatunza. Kelvin…” Lisa alimjibu kwa uchangamfu.
“Ghorofa iko tayari. Ngoja nikupeleke huko sasa.” Kwa hayo, Kelvin na Lisa wakaingia kwenye gari.
Redio kwenye gari ilikuwa ikitangaza habari za ndani. “Kulingana na chanzo cha habari, Mwenyekiti Kimaro, mtu tajiri zaidi nchini Kenya, ametumia dola milioni 20 kununua gauni la harusi la mchumba wake. Inavyoonekana, Mwenyekiti Kimaro ametayarisha vazi hilo kwa miaka miwili. Wawili hao wamekuwa kwenye uhusiano kwa miaka minne na hatimaye wanafunga ndoa.”
Kelvin alimtupia jicho Lisa. Alipoona hali yake ya utulivu ndipo akashusha pumzi ya raha. “Nimesikia habari zake pia. Inaonekana kwamba wanafunga ndoa.”
“Ndiyo hivyo.” Lisa alionekana kutojali lakini hakukasirika hata kidogo. Tangu alipopelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili kwa matibabu, alikuwa ameacha kumpenda Alvin. "Nilikuwa nadhani kwamba wangekuwa wamefunga ndoa kwa muda mrefu."
Kelvin alisema, “Wameishi pamoja kwa muda, jambo linalofanya ionekane kama wamefunga ndoa.”
Lisa alitabasamu. "Hilo halishangazi."
Alvin alikuwa tayari na Sarah kabla ya kuachana na Lisa. Zaidi ya hayo, kwa kuwa alidhani kwamba Lisa amekufa, kwa kawaida angekutana na Sarah. Kuangalia sura yake, midomo ya Kelvin ilitetemeka, na akashikilia ulimi wake.
Saa moja baadaye, gari liliingia katika kitongoji ambapo Karen Estate ilikuwa. Nyumba aliyomnunulia ilikuwa kwenye ghorofa ya nane. Ilikuwa na vyumba vinne vya kulala, kumbi mbili za kuishi, na kibaraza kikubwa. Pia kulikuwa na vyumba viwili vya watoto - chumba chenye mandhari ya bluu-anga kwa mvulana na chumba chenye mandhari ya waridi kwa msichana. Matandiko katika chumba cha bluu yalikuwa na Spiderman, ambayo Lucas aliipenda zaidi, ilhali chumba cha waridi kilikuwa na wanasesere mbalimbali wa Barbie.
Lisa alipigwa na butwaa. Kelvin alimweleza, “Nilifikiri ungekuja na watoto pia. Sikufikiri Lucas na Suzie wangeishi nje ya nchi maisha yao yote. Utavirudisha hivi karibuni au baadaye, kwa hivyo nimeunda vyumba vyao kulingana na mapendeleo yao. Kuna chekechea katika kitongoji hiki, na mazingira ya hapa ni mazuri kabisa. Pia kuna shule ya msingi, shule ya sekondari, na chuo karibu na kitongoji hiki. Zote ni taasisi bora za elimu hapa Nairobi.”
Lisa alikaa kimya kwa muda mrefu baada ya kusikia alichosema Kelvin. Bila kusema chochote, aliguswa. Isingekuwa kwa usaidizi wa Kelvin, Jack, na Hans miaka mitatu iliyopita, angeweza kuwa na wazimu kwa kudungwa sindano za kila siku wodini. Angeweza kugeuka kuwa kweli kichaa na kuishia katika hospitali ya magonjwa ya akili miaka yote.
Hansa, akishirikiana na Sam Harrison, Jack Kimaro na Kelvin Mushi ndiyo waliofeki kifo cha Lisa wakati huo ili kumnusuru yeye na watoto. Baada ya kwenda nje ya nchi, Kelvin aliendelea kumsaidia Lisa na watoto wake.
Angeweza kusema kwa waziwazi kwamba asingekuwa vile alivyokuwa siku hiyo bila yeye. Sasa kwa kuwa alikuwa amerudi, bado alikuwa akimjali na kumfikiria sana.
“Lisa, usifikirie sana. Ninafanya hivi kwa hiari yangu,” Kelvin alisema huku akitabasamu. "Tangu nilipokutana nawe huko Dar es Salaam, moyo wangu hauna mtu mwingine ila wewe. Endelea na unachotaka kufanya, lakini siku zote nitakusubiri wewe pekee.”
"Kelvin, mimi tu ... sidhani kama ninastahili kuwa na wewe." Moyoni, Lisa alihisi hatia sana.
“Ni kwa sababu ya Lucas na Suzie?” Kelvin aliuliza kwa sauti nyepesi. "Machoni mwangu, hao ni malaika wa kupendeza zaidi ambao nimewahi kukutana nao. Hawajawahi kuwa mzigo. Ingekuwa furaha yangu kama ningekuwa baba yao.”
Kwa mara nyingine tena, Lisa aliguswa.
Kila alipokuwa katika hali kama hii, alijikuta akisaidiwa na Kelvin badala ya Alvin. Alijuta kumwangukia Alvin badala ya yeye. Kelvin ndiye alipaswa kumthamini.
“Samahani, Kelvin. Siwezi kukuahidi chochote sasa. Nilirudi safari hii kwa nia moja tu ya kulipiza kisasi,” Lisa alisema kwa ukali.
“Najua. Nimengoja kwa miaka mitatu, na sijali kusubiri tena hata kama itakuwa milele.” Kelvin alipapasa kichwa cha Lisa. "Nenda na ujitayarishe kwa sherehe ya kuadhimisha miaka 30 ya Ngosha Corporation usiku wa leo."....ITAENDELEA.....
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA.
