JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA...............................180-181
Sura ya:180
Baada ya Alvin kumaliza kuzungumza, alichukua koti lake la suti na kujiandaa kuondoka.
"Nadhani unataka tu afe huko ili ukose mtu anayeweza kushindana nawe kwa KIM International," Lea alisema kwa sauti kali.
Miguu mirefu ya Alvin ilitulia na akasema kimya kimya, “Fikiria chochote unachotaka.”
"Alvin Kimaro, majuto yangu makubwa ni kukuzaa kwako. Nilipaswa kukutoa ungali uko mimba.” Sauti ya Lea ilisikika kwa nyuma.
Alvin aliingia kwenye lifti moja kwa moja. Hans alitazama uso wake kwa uangalifu. Hakuwa na wasiwasi kwenye uso wake lakini Hans alijua kwamba kwa mtazamo ule, ulikuwa ni utulivu kabla ya dhoruba. Hiyo ilitokea kila mara Alvin na Lea walipokutana. Wawili hao bila shaka wangepigana, kana kwamba mama na mwana walikuwa maadui wa asili. Hans alihema moyoni mwake. Lea Kimaro alikuwa anapendelea sana.
Dereva akaleta gari, na Alvin akafungua mlango na kuingia ndani kabla ya kujiendesha. Nairobi ni kubwa, lakini ilionekana kana kwamba hakuwa na pa kwenda. Aliamua kuendesha gari hadi New Metropolis Park. Alifungua mlango na kuingia ndani. Jumba kubwa la kifahari lilikuwa kimya bila hata sura. Hapo hapo akampigia simu Lisa. Baada ya kuita mara kadhaa, simu ilikatwa na akajaribu tena mara mbili zaidi na ikawa hivyo hivyo tena.
"Vizuri sana." Alvin aliitazama simu ile, macho yake yakiwa yamejawa na mwanga wa damu.
Katika hoteli, Lisa alikata simu na kushtuka ghafla. Kwa tabia ya kijeuri ya Alvin, je, angefanya jambo baadaye? Lakini, baada ya kungoja kwa nusu siku na kutopokea habari yoyote kutoka kwake, mwishowe alipiga simu ya intercom ya hoteli kuagiza chakula cha jioni.
Saa moja jioni akiwa anajiandaa kula chakula cha jioni, ghafla kengele ya mlango ililia na mlango kupigwa teke na mtu. Alvin akasogea kwa hatua pana na kuubamiza mlango kwa kishindo.
“Umeingiaje?” Lisa alishtuka.
"Kampuni yangu inamiliki hoteli hii, na wewe hujui lolote." Alvin akaitupa kadi ya ufunguo pembeni na kumsogelea hatua kwa hatua. "Nilifikiri kwamba ulijifunza somo lako jana usiku, lakini inaonekana kwamba haujafuzu."
Kivuli chake kirefu kilimwangukia, na uso wake mzuri lakini mweusi ulimfanya Lisa kuogopa. “Mimi…nilitaka kuja, lakini wewe ndiye uliyetuma picha hizo jana usiku kwa Kelvin. Umeenda mbali sana.”
“Nilienda mbali sana?” Alvin alitabasamu kwa unyonge. "Nadhani nina huruma sana kwa kutomtumia picha za jinsi ulivyokuwa unafanya jana usiku."
"Nyamaza!" Lisa aligeuka rangi kutokana na unyonge.
“Nimesema kitu kibaya? Wewe ni mchumba wake lakini ulilala na mimi jana.” Maneno ya kikatili yalitoka kwenye mdomo wa Alvin. “Nadhani ulizaliwa tu kudharauliwa. Hujui hata mapungufu yako mwenyewe na bado unataka kuweka mbele…”
“Paah!” Lisa hakuvumilia tena kumsikiliza na kumpiga kofi zuri tu usoni. Alikuwa akilia machozi ya hasira. Macho yake mekundu yalijaa chuki na hasira kali alipokuwa akimwangalia. Ilikuwa ni sura ile ile aliyopewa na Lea Kimaro muda si mrefu kabla ya hapo.
Alvin alihisi tu kama kifua chake kimechomwa visu vikali. “Unathubutu kunipiga Lisa Jones?” Macho yake yaliyofinywa yalionekana kuwa kama ya shetani.
Lisa alichukua hatua mbili nyuma na kusema, "Alvin Kimaro, tafadhari naomba usinidhuru."
"Lisa Jones, sitakuonyesha tena huruma hata kidogo."
Kilichofuata hapo ilikuwa ni kumbukumbu ya pili isiyofutika katika maisha ya Lisa, ukiacha ile ya jana yake usiku. Miaka mingi baadaye, wakati Lisa angekuwa akikumbuka usiku huo, angeweza kutumia neno moja tu kuelezea: KUTISHA! Lisa alihisi kama ameanguka kwenye shimo baya ambalo likawa ndoto yake mbaya zaidi...
•••
Saa nane za usiku, Alvin aliamka kwa hasira na alichokiona kilimshtua.
Mwanamke aliyekuwa kando yake alikuwa amejikunja kama karunguyeye kwa maumivu. Uso wake ulikuwa umepauka sana na midomo yake ilikuwa na damu.
“Lisa!” Moyo wa Alvin ulipiga kelele. Hata hivyo, mwanamke huyo hakuitikia.
Alvin alishtuka. Alimfunga shuka yule mwanamke kwa haraka kabla ya kumchukua na kumkimbiza hospitali.
Usiku sana katika korido la hospitali ya City General. Alvin alisimama karibu na madirisha ya chumba cha dharura na kujaribu kuwasha sigara, lakini aligundua kwamba mkono wake ulikuwa ukitetemeka. Hata baada ya muda mrefu, hakuweza kuwasha sigara.
"No smoking!" Chester Choka, ambaye alikuwa ni daktari katika hospitali hiyo akiwa amevalia koti jeupe, alimsogelea huku akimtazama kwa macho makali. “Umefanya nini Alvin, kwanini unashindwa kudhibiti hasira zako? Nafikiri uraibu wako wa kuvuta sigara pia umezidi kuwa mkubwa zaidi, bila shaka ugonjwa wako wa hasira za hovyo umeanza kupanda tena.”
"Nilikutana na Lea Kimaro leo na akanifanya kupoteza udhibiti wa hisia zangu." Alvin alichanganyikiwa. "Anaendeleaje?"
“Daktari wa kike hospitalini amemchunguza.” Chester alimtazama. “Wewe ni kichaa kweli. Daktari amesema kwamba Lisa ametoka kupoteza usichana wake na bado anamshtuko wa kisaikolojia. Anahitaji angalau siku mbili hadi tatu za kupumzika, lakini ulimfanya nini?
"Umesema nini?" Alvin alitingisha kichwa kumwangalia Chester.
“Hivyo ndivyo daktari Melisa alisema. Unapaswa pia kujua kwamba Daktari Melisa hawezi kusema uwongo. Ameshughulika na wagonjwa wengi na ana uzoefu mwingi.”
Kila neno alilosema Chester lilikuwa kama bomu lililolipuka kwenye kichwa cha Alvin, likivuma. Kwa hivyo… Lisa na Kelvin Mushi hawakuwa na hatia kweli? Alikuwa amemuelewa vibaya?
“Yeye… Kwa hiyo hakufanya chochote na Kelvin Mushi?” Alvin alihisi kwamba ubongo wake ambao siku zote ulikuwa ‘genius’ ghafla ukawa hautoshi. “Lakini hakukuwa na hata na tone la damu lililotoka siku hiyo, inakuweje bikira awe namna hiyo?”
“Umenikumbusha hadithi za magazetini enzi zile nipo shule” Chester alisema huku akicheka, “....mara oooh! nikaanza mnyonya nini na nini kisha nikaingiza...Binti akalia sana kwa maumivu, nilipomaliza nikakuta shuka lote limelowa kwa damu....”
“Kwa hiyo si lazima iwe hivyo?” Alvin alijawa na mshangao mkubwa.
“Hiyo ni fantancy tu!” Chester aliendelea kumwelimisha. “Bikira haloweshi shuka kwa damu unless katikati ya tendo hedhi ikaanza, au wakati wa tendo binti kuvunja ungo. Hii inawatokea mabinti wadogo wanaolazimishwa kuolewa au wanaobakwa au umefanya kwa fujo sana mpaka ukamjeruhi mtoto wa watu”.
“Kwa hiyo inawezekana Lisa hakutoka damu kwa sababu alishavunja ungo siku nyingi?” Alvin aliuliza kwa hamasa.
“Unaweza kuwa ulimwandaa vya kutosha, akatokwa hofu kabisa kwa hiyo akawa amerelax wakati wa tendo.” Dokta Choka alisema. “Enzi zile ndiyo ilijengeka imani hii, kwamba siku ya harusi, usiku binti baada ya tendo anapachikwa kijitambaa cheupe ukeni ili kujua kama bikira imetoka. Kwamba kukiwa na damu, shangwe! Kikiwa kisafi kilio.... Lakini kumbuka enzi zile mabinti wengi waliolewa wakiwa wadogo na bila mapenzi so technically walikuwa wakibakwa na wengine kuvunjishwa ungo kabla ya siku zao hivyo damu ilikuwa ndio ushuhuda pekee!!”
Dokta Choka aliendelea kumpatia Alvin maelezo mengi ya kitaalamu. “Pale ukeni huwa na kijiutandu ambacho kinaweza kutoka kutokana na shughuli za kimaisha au mtindo wa maisha, michezo na kadhalika. Ukweli ni kuwa, Bikira ni kutokufanya tendo la ngono… Kwa hiyo nikijibu swali lako.... Hapana! Sio lazima damu imtoke mwanamke mara yake ya kwanza kufanya mapenzi!
“Siku inayofuata baada ya tendo anaweza kuona uchafu uliochanganyikana na damu kwenye chupi ikiwa aliumia....inategemea ulimuingilia kwa nguvu kiasi gani.nHali hiyo inaweza kuendela kwa siku mbili-tatu kisha akawa poa, again sio lazima kuwe na damu.”
Maelezo yale ya Dokta Choka yalikuwa yamejitosheleza kabisa na kumfanya Alvin aanze kuhisi hatia nzito moyoni mwake.
Je, hakulewa na madawa ya kulevya na kukaa usiku kucha na Kelvin hotelini? Ina maana siku hiyo hawakufanya chochote kweli?
Daktari Melisa asingeweza kusema uwongo. Ilionekana kana kwamba Alvin alikuwa amemuelewa Lisa vibaya. Alipoyafikiria maneno aliyomwambia hapo awali, alijuta na kujipiga makofi mawili ya usoni. Alikuwa amefanya nini? Usiku ule, je, kweli alijizamisha ndani ya maji baridi ili alale, kama vile alivyosema?
Chester akasema. "Nilipoona picha zake akiwa katika urafiki wa karibu na Kelvin Mushi wakati huo, nilifikiri walikuwa tayari… Nani angefikiria hili lingetokea. Hata baada ya kuchumbiwa kwa muda mrefu, usichana wake ulitenguliwa na wewe badala yake. Unafikiri Kelvin hatakufa kwa majuto?”
Alvin alikunja uso kwa nguvu. Hakujua kama Kelvin angekufa kwa majuto, lakini Alvin alikuwa karibu kufa majuto hayo. Alisimama wodini huku akiwa na hisia hizo za majuto. Alipoona sura ya Lisa iliyopauka, akataka kujipiga makofi mengine mawili.
Mambo ambayo alikuwa amemfanyia yalikuwa ya kinyama tu. Alikuwa akimshutumu kwa kulala na Kelvin lakini daktari alidhibitisha kuwa ubikira wa Lisa ulitolewa na yeye. Wakati huo, kope za Lisa aliyelala kitandani zilitetemeka ghafla. Alvin ambaye alikuwa akiwaza jinsi ya kumkabili mwanamke huyo, alikuwa amekata tamaa.
Lisa alifumbua macho taratibu. Alipomuona Alvin amesimama kando ya kitanda chake, tukio lile la kutisha liliibuka ghafla akilini mwake. Alitetemeka kwa woga na uso wake ulikuwa mweupe wa karatasi. “Usije huku!” Lisa aliogopa sana. Alijaribu kujificha pembeni, na macho yake safi yalijawa na hofu juu yake.
Moyo wa Alvin ulipiga kwa maumivu na kujaribu kumtuliza. “Usiogope, sita…”
“Ahhhh, usinishike!” Lisa akaingia kwenye blanketi kwa woga, mwili wake ukitetemeka kama jani.
“Sitathubutu tena. Sikupaswa kukupiga. Unaweza kufanya chochote unachotaka katika siku zijazo. Ninaogopa sana sasa. Nimejifunza somo langu!” Alvin alijitetea bila kueleweka.
Sura ya:181
"Toka nje…”
“Usijifunike gubigubi utakosa hewa.” Alvin alinyoosha mkono kuvuta blanketi lakini akamwona Lisa akiuma vidole vyake kwa nguvu. Uso wake ulikuwa na michirizi ya machozi.
“Sawa, nitatoka. Nitaomba mtu akuletee chakula kwani usiku kucha haujala.” Alvin alihema na kugeuka kuondoka.
Muda si muda, nesi akaingia. Lisa alipoona Alvin ameondoka, hofu moyoni ikamtoka kidogo, lakini bado mwili ulikuwa ukimuuma sana. Hakuwa na hamu ya kula kabisa na alilala baada ya muda mfupi kidogo.
Alipoamka siku iliyofuata, anga tayari lilikuwa limeangaza. Alvin alisimama mbele ya dirisha na alikuwa kwenye simu, akiongea kwa sauti ya chini. “Sitakuja kwa kampuni leo. Ghairi mkutano huo."
“Lakini Naibu Mwenyekiti Lea Kimaro atahudhuria mkutano wa leo—”
"Nilisema ghairi, kwa hivyo ughairi." Alvin aliamuru.
Alvin akageuka nyuma na kuyaona macho ya Lisa yakiwa yamejaa woga kama ya kulungu. Lisa alikurupuka. Alvin akasogea kitandani na kusema kwa sauti ya upole, “Daktari aliniambia kuwa usichana wako niliutoa mimi kwa mara ya kwanza. Samahani nilikuelewa vibaya hapo awali. Ninaahidi sitatenda kama nilivyofanya jana tena. Unaweza kunisamehe?”
Lisa alipigwa na butwaa. Si ajabu kwamba ghafla alikuwa mpole sana kwake. Alifikiri kwamba hatimaye angemwamni baada ya kuwa ameshuhudia kwa macho yake. Ilibainika kuwa ni kwa sababu daktari alikuwa amemwambia. Alitamani kucheka kwa jinsi ambavyo hakujawa na uaminifu kati ya wawili hao.
“Sawa.” Aliitikia kwa kichwa. “Wewe ni Bwana Alvin Kimaro, nani angethubutu kutokusamehe?”
“Huna lolote lingine la kuniambia?” Alvin alikuwa amepotea kiasi. “Unaweza kunilaumu utakavyo.”
“Kukukaripia? Nani atathubutu kukukemea? Nilikukaripia jana na kuachwa nikiwa hivi. Sitathubutu tena”
Alvin alitabasamu kwa uchungu. Wakati huo, angetumia jitihada zake mwenyewe kuuchochea moyo wake na kumuondoa woga.
Alasiri, Alvin alikamilisha taratibu za kutolewa hoaspitali na kumrudisha Lisa hadi New Metropolis Park. Ilikuwa imepita zaidi ya mwaka mmoja tangu jumba hilo kukarabatiwa, na ilikuwa mara ya kwanza mtu kuishi humo.
Asubuhi, alimwambia Hans kuandaa vifaa vingi vya nyumbani na hata kununua kabati nzima iliyojaa nguo za kike. Gari lilisimama kwenye maegesho, Alvin akainama kumnyanyua. Lisa alimruhusu amsogeze kwa utiifu.
Kilichokuwa muhimu kwake sasa ni kuvumilia. Ni mpaka pale ambapo angejua kuhusu sababu ya kifo cha Sheryl Masawe na kulipiza kisasi, ndipo angeondoka Nairobi. Hakuwa na haja tena na biashara. Alichotaka ni uhuru.
Alvin alimbeba mpaka kwenye sofa na kumfungulia luninga.
“Acha na TV usiku umeingia, kwa hiyo nitaandaa chakula cha jioni.” Lisa alivumilia maumivu na kuinuka.
“Unawezaje kupika namna hii? Usihangaike.” Alvin alimsimamisha na kumshika, hivyo akaketi tena.
"Kukupikia ni jukumu langu." Lisa alikuwa mtiifu kama kijakazi mdogo. "Utakula nini ikiwa sitapika?"
Alvin alikasirika. Zamani hakutaka kitu zaidi ya yeye kuwa mtiifu hivi, lakini sasa Lisa alikuwa mtiifu kwake na bado moyo ulimuuma tena.
"Nitapika." Alvin alivua koti lake na kukunja mikono yake.
Lisa alishangaa. Baada ya kumfahamu kwa muda mrefu, hakuwahi kumuona hata kushika mwiko. Angepikaje?
Alvin kweli hakujua kupika, lakini aliweza kujifunza papo hapo ili tu kumfurahisha Lisa. Kulikuwa na mafunzo mengi kuptia Youtube kwenye simu yake, hivyo aliamni kwamba haiwezi kuwa ngumu kiasi hicho. Baada ya kutumia saa moja kutizama mapishi mbalimbali, hatimaye aliandaa sahani mbili za chips na mayai japo hazikuonekana na sura nzuri. Kulikuwa na samaki pia kwenye friji aliomwagiza Hans awalete akawakatakata na kuwakaanga.
Lisa alitazama sehemu ya nyuma ya mkono wake uliokuwa umebadilika na kuwa mwekundu kwa sababu ulikuwa umetapakaa mafuta ya moto. Ikiwa asingepaka asali mara moja, bila shaka angepata malengelenge kesho yake.
"Kula." Alvin akamtengea sahani ya chips na kumsogezea minofu ya samaki. Viazi vya chips vilikuwa vimekatwakatwa hovyohovyo tu, vingine vidogo kama karanga wakati vipande vingine vikubwa kama biskuti, na ilikuwa wazi kuwa alijikatakata kwenye vidole wakati akimenya viazi hivyo. Hata hivyo, viazi hivyo havikuwa na chumvi hata kidogo. Alikumbuka kutia chumvi kwenye mayai lakini nako ilikuwa imepitiliza na kuyafanya mayai yasilike kabisa japo yalinukia vizuri.
Alvin aliyaonja na kugundua dosari hiyo. Akayasukumia pembeni na kumsogezea kipande kikubwa cha minofu ya samaki. "Kula hii."
Lisa, akaguna mara tu ya kumuonja yule samaki. Ilivyoonekana alitolewa kwenye kikaango akiwa hata hajakauka vizuri hivyo minofu mafuta yote yakanyonywa na minofu, lakini, bado alijilazimisha kula samaki huyo kwa utiifu.
Alvin hakuona mwanzoni, lakini baadaye alijaribu kuonja mnofu na akakuta ladha ya samaki ina mafuta kupita kiasi. Kwa kuudhika, alitupa kwenye pipa la taka ile sahani ya minofu ya samaki. “Inatosha, acha kula. Ni wazi ladha yake ni mbaya. Mbona hukusema lolote?” Sauti yake ilipandishwa kwa hasira, na mikono ya Lisa ikatetemeka. Macho yake makubwa yalijawa na wasiwasi na woga.
Moyo wa Alvin ulimuuma. Alimbeba moja kwa moja kwenye mikono yake, sauti yake ikiwa imejaa mamlaka na kutawala,, alisema, “Lisa Jones, nataka uishi na mimi kama tulivyofanya hapo awali huko Dar es Salaam, sawa?”
Lisa alipigwa na butwaa na kumtazama huku akiinamisha kichwa chake. Macho yake yalitetemeka. "Unatakaje, niishi kwa kujinyenyekeza na kujipendekeza?"
Wakati wakiwa huko Dar es Salaam, walikuwa tofauti na jinsi walivyokutana tena Nairobi. Kipindi hicho Lisa alikuwa akimbembeleza akidhani ni mjomba wa Ethan, alimtii hata aseme nini, akajilazimisha kuacha hasira yake na kuacha mambo yote aliyopenda kufanya ili tu kumfurahisha Alvin.
Alvin alijikaza huku moyo wake ukiwa umejaa uchungu. "Kwa hiyo, huko Dar es Salaam ulikuwa ukijinyenyekeza tu na kujipendekeza, madai yako kwamba ulinipenda yalikuwa ya uwongo?"
"Samahani, nilikosea." Lisa aliomba msamaha bila raha. “Usikasirike.”
“Sina hasira. Nilikuwa namaanisha kuwa unaweza kuishi na mimi pasipo kujinyenyekeza tena. Unaweza kudai chochote, unaweza kukasirika au kufurahi, unaweza kupika au usipike ukipenda, unaweza kufanya chochote unachopenda ukiwa huru kabisa. Unaweza kunitendea kama mpenzi wako. Sitakutendea kama jana tena, naapa!” Alvin akamkumbatia kwa nguvu.
Lisa alitabasamu na kuinamisha macho yake, lakini moyo wake ulikuwa umejaa kejeli. Mpenzi? Alikuwa mpenzi wa Melanie, si wake. Alikuwa ni kama hawara tu au mchepuko.
“Kwa hiyo naweza nikwambia kitu na ukanisikiliza?” Lisa aliuliza kwa wasiwasi.
"Ndio, mradi sio kuhusu Kelvin Mushi." Alvin alifikiria kwa muda na kuongeza, “Sitaki uwe na mahusiano naye tena.”
Lisa alitikisa kichwa na kusitasita kwa muda kabla ya kupata ujasiri wa kutosha kuuliza kwa sauti ndogo, "Je, unaweza kumrudisha Jack Kimaro?"
Alipomaliza, aligundua kuwa uso mpole wa Alvin ulikuwa umebadilika na kuwa baridi na giza kwa kasi inayoonekana kwa macho… Kidogo kama vile usiku…Aliingiwa na hofu na kuogopa. "Nilikosea, sikupaswa kukuomba kitu kama hicho. Chukulia kama nilipitiwa tu. Usinidhuru…”
Hasira iliyokuwa ikienda kukimbilia kichwani kwa Alvin ghafla ikatoweka na mara akarudiwa na fahamu zake baada ya kusikia sauti yake ya hofu. Hakuwa na nia ya kukasirika, lakini hakuelewa kuwa Jack alikuwa kivuli moyoni mwake. Jack alikuwa mwiko kwake.
“Sitakuumiza,” Alvin alimshika mkono na kusema kwa sauti ya upole, akitumaini angetulia.
Lisa alimtazama kwa woga. “Nataka kupanda ghorofani nikapumzike.” Kwa kweli hakutaka kukaa naye tena.
Alvin alimpeleka juu na kumuweka kitandani bila ya Lisa kusema neno lolote. “Hukula vya kutosha. Nitapiga simu hotelini kuagiza chakula. Nitakuja kukuchukua baadaye.”........ITAENDELEA...
Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
