JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP............................0628924768
SEHEMU YA................................145-146

Sura ya 145

Mara tu dalali yule alipomaliza kuzungumza, ghafla aligundua kuwa uso mzuri wa mwanamke yule ulionekana kupauka. Alikaribia kukosa mwelekeo wake. "Uko sawa, mwanamke mzuri?"

“Mimi… nipo sawa.” Lisa akamkabidhi kadi yake ya biashara. "Ningependa kununua nyumba hii ya kifahari, lakini natumai hutafichua utambulisho wangu kwa mmiliki wa awali. Nitakulipa kamisheni pia.”

“Oh, sawa, hakika.” yule dalali alifurahi. Hakutarajia kwamba angeweza kuuza jumba lile kwa kutembea tu hadi mlangoni. Ni kazi rahisi iliyoje.

Baada ya kuingia ndani ya gari, Lisa alitawaliwa na hali ya kuchanganyikiwa. Ghafla, alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa umetoweka. Ingawa alikuwa ametia saini hati za talaka, hakutarajia Alvin angeondoka Dar es Salaam mapema namna ile. Hiyo ilimaanisha kwamba wote wawili wangeweza wasikutane tena kwa vile walikuwa katika miji tofauti. Alikuwa amejitoa katika maisha ya Alvin, lakini kwa nini moyo wake ulikuwa bado unauma kiasi cha kushindwa kupumua? Aliushika Mkufu wa Malkia huku akilia kwa jazba.

Dakika 40 baadaye, alijitokeza kwenye ukumbi wa kampuni ya mawakili ya Jeninnings akiwa na miwani ya jua usoni. Mhudumu wa mapokezi pale mlangoni akamtambua mara moja. Baada ya kumuona mhudumu wa mapokezi alihema kwa huzuni kwani asingeweza tena kuiona sura nzuri ya Mr. Kimaro kila siku. “Unamtafuta Bwana Kimaro? Ameondoka.”

"Namtafuta Sam." Lisa alimsahihisha.

Mhudumu wa mapokezi aliwasiliana na msaidizi wa Sam mara moja. Muda si muda, aliagiza Lisa apande ofisini kwake. Ofisini, Lisa alipitisha boksi la velvet kwa Sam. “Mkufu wa Malkia uko kwenye boksi. Tafadhali mpe.”

"Alvin hataitaka" Sam alisema kwa uhakika, "Itunze tu. Nadhani ataitupa mara atakapoiona.”

“Hebu atupe basi. Bidhaa hii ina thamani ya shilingi bilioni tatu, ambayo ni gharama sana. Sitaki anidai.” Kwa hayo, Lisa aliinuka na kuondoka.

Lisa alipokea simu kutoka kituo cha mahabusu mchana. Ilitajwa kuwa Jones Masawe alikuwa na hamu ya kumuona kwa mara ya mwisho. Hukumu za Jones Masawe na mkewe zilikuwa zimetolewa. Kwa kuwa mama Masawe ndiye aliyekuwa muuaji, alihukumiwa kifungo cha miaka 20. Kwa upande wa Jones Masawe, alihukumiwa miaka kumi tu kwa kuwa msaidizi. Ukizingatia uzee wao, maisha yao yalikuwa yamekwisha. Baada ya kufikiria kidogo, aliamua kuwatembelea.

Alipomwona Jones Masawe tena baada ya siku kadhaa, tayari alikuwa na mvi kana kwamba alikuwa amekua kwa miaka kumi.

“Kwa nini ulinitaka nije?” Lisa aliuliza bila kujali. Tayari hakuwa na hisia naye hata kidogo.

Jones Masawe alijibu kwa huzuni, “Najuta, na nimejisalimisha kwa hatima yangu. Nimehamisha hisa zote za Mawenzi Investments kwako. Ninachotumai ni kwamba utamruhusu Lina atoke kwenye ndoano. Baada ya yote, yeye ni binamu yako, ambaye pia ndiye mwanafamilia wako pekee.”

"Amefanya mambo mengi maovu." Lisa alikunja uso kwa kejeli. "Aliponiumiza, hata alinifikiria kama mimi ni binamu yake?"

Jones Masawe aliuma midomo yake. “Ulimtumia pia mtu kumdhuru? Tangu mimi na mama yake tufungwe jela, hajatutembelea hata kidogo.”

Lisa akabaki ameduwaa. “Pamoja na mambo mengi yanayoendelea kwa sasa, sikupata hata muda wa kumfanyia chochote. Haishangazi kwamba hajaja kukutembelea. Umemlea kwa muda gani? Kwa mtu katili kama yeye ambaye atafanya chochote kufikia malengo yake, bado unatarajia atakuwa na mawazo na wewe? Nina hakika sasa atakukwepa kadri awezavyo.”

Jones Masawe aliyatoa macho yake kwa butwaa. Alichosema Lisa kilionekana kuwa pigo kubwa kwake. Jones Masawe na mkewe walipofikiria, waligundua kuwa Lina ndiye mtu ambaye alikuwa mbinafsi zaidi yao. Wangewezaje kuweka matumaini yao kwa binti huyo? Alikuwa binti yao wa kuzaa, lakini vipi hakwenda kuwaona?

Jones Masawe alilazimisha tabasamu. Kwa kweli, Lisa alikuwa binti mzuri. Hata hivyo, Jones Masawe na mkewe hawakuwahi kumjali kwa sababu tu hakuwa mtoto wao wa kumzaa. “Uko sahihi. Ni kosa langu, Lisa."

"Natumai utajuta gerezani kwa yale uliyofanya." Lisa alisimama na kuondoka kwenye kituo hicho cha mahabusu.

Baada ya kurudi ofisini, alimwomba msaidizi wake amtazame Lina.
Msaidizi haraka alimletea habari kuhusu Lina. "Amepotea kwa siku kadhaa. Hata hakuchukua vitu vya nyumbani kwake. Hakujawa na miamala yoyote katika akaunti yake ya benki pia. Anaonekana kutoweka kimaajabu sana.

Lisa alipigwa na butwaa. Hakutarajia kwamba Lina angetoweka vile vile baada ya kupigana naye kwa muda mrefu. Kwa mwonekano wa mambo, hakukimbia kweli. Labda maisha yake yalikuwa hatarini.

Kwa wakati huo Lisa alifanya kazi huku akimhudumia Kelvin. Kimsingi, mtu angeweza kusema kwamba walikuwa wakiishi pamoja. Alitumia mkesha wa Mwaka Mpya katika jumba la kifahari la Kelvin. Usiku, nyumba ya familia ya Mushi ilikuwa na mwanga mzuri. Lisa alipomsukuma Kelvin aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha magurudumu kutoka chumbani, akakutana na Ethan, Tracy na Sonya waliokuja kula chakula cha jioni. Wote watatu walipigwa na butwaa kumwona. Uso wa Sonya ukawa mgumu mara moja.

"Lisa, huna aibu kama nini kuonekana nyumbani kwetu -

"Nyamaza. Mwite wifi wakati mwingine." Mama Mushi alimsogelea Sonya na kumwambia aondoke. “Atachumbiwa na Kelvin baada ya Mwaka Mpya. Acha kuongea chochote kilichotokea huko nyuma." Alinyamaza kisha akamwambia Ethan, “Lazima umuite ‘Shangazi’.” Wakati huo, Sonya na Ethan walivaa sura ya kustaajabisha.

Lisa alihisi kutokwa na machozi kutokana na hali hiyo kuwa mbaya.
Hili ndilo tukio aliloliota miezi kadhaa iliyopita. Ingawa tukio kubwa lilikuwa limefanyika hatimaye, hakufurahishwa nalo kwa sababu mambo mengi yalikuwa yamebadilika.

"Baba, unatania?" Sonya karibu aingie kichaa. Hapo awali, Lisa alikaribia kuwa ‘binti-mkwe’ wake, lakini Sonya alilazimika kumwita 'wifi' sasa. Je, Mungu alikuwa akimdanganya?

Mzee Mushi alimkodolea macho Sonya. "Sasa ndiye mtu anayesimamia Mawenzi Investments. Hadhi yake ni kubwa kuliko yako. Je, ni vigumu kwako kumwita ‘wifi’?” Sonya alinyamaza mara moja.

Hakuwa mjinga. Ikiwa Kelvin na Lisa wangefunga ndoa, ingefaidisha familia ya Mushi. Zaidi ya hayo, kwa hali ile ya Kelvin, mwanamke yeyote kutoka katika familia mashuhuri bila shaka angekataa kuolewa naye.

Jikoni, Lisa alivaa apron na kuandaa vyakula vya kiasili zaidi. Kwa kuzingatia kwamba mwili wa Kelvin ulikuwa dhaifu, alikuwa amechukua usimamizi kamili wa lishe yake. Ethan alipoingia ndani alihisi kubanwa kifuani kwa kuuona mgongo wa Lisa. Alikuwa anajua upishi wake mkubwa. Mara nyingi alipika vyakula mbalimbali kwa ajili yake wakati ule pia. Hata hivyo, asingepata tena upendeleo huo.

"Lisa, upo tayari kuolewa na mjomba wangu?" Ethan alimsogelea na kutazama umbo lake zuri na la kuvutia chini ya taa.

Lisa aliinamisha kichwa chake, akaweka viungo kwenye sufuria na kusema. "Anahitaji mimi nimtunze."

Ethan alitoa kicheko cha uchungu. “Natamani ningekuwepo siku hiyo. Ningekuwa tayari kukuokoa kutokana na kuchomwa kisu pia…”

"Kama nisingekuwa mwenyekiti wa Mawenzi, usingeniokoa." Lisa aliinua kichwa chake na kumtazama kwa kutokubali.

Uso mzuri wa Ethan ukawa mgumu. “Acha kusema mambo ya namna hii. Mpenzi wako yuko nje anakusubiri.” Lisa alitoka jikoni huku akiongea.

Sura ya 146

Saa sita kamili usiku, fataki ziliangaza anga la usiku. Lisa alimshika Kelvin mkono na kumpeleka kitandani. Alipomlaza kitandani, Kelvin alimshika mkono. Huku fataki zikionekana katika macho yake yenye giza, alionekana kuangaza macho yake vizuri. “Lisa upo tayari kuolewa na mimi kweli? Usijute.”

"Ninaogopa kuwa wewe ndiye utajuta badala yake." Lisa alikunja uso na kusema kwa mawazo, “Ninapanga kuhamisha makao makuu ya Mawenzi Investments hadi Nairobi mwaka ujao. Nataka kujua sababu ya kifo cha mama yangu. Sijui adui zangu wa baadaye watakuwa na nguvu kiasi gani—”

“Nitakusindikiza. Nitaenda hadi miisho ya dunia ili kukusaidia wakati wa maisha yangu,” Kelvin alikatiza sentensi yake kwa sauti ya kudhamiria.

Lisa alibaki kimya kwa muda. Kwa kuzingatia tabia ya Kelvin, hakuweza kuvumilia kumkataza na kumuumiza. "Asante."

Baada ya mwaka mpya, Lisa alielekeza akili yake kwenye kazi.
Mali mpya za Mawenzi Investments ziliuzwa haraka, na kurahisisha mtiririko wa pesa wa kampuni.

Alipokuwa akipakia vitu vyake ili aondoke jioni hiyo, mhudumu wa mapokezi akampigia simu ghafla. “Mkurugenzi Maganga yuko hapa. Alikuja na mtu ambaye anadai kwamba anataka kukutana nawe."
Lisa alipigwa na butwaa. Chris Maganga alikuwa amerudi Mwanza baada ya kumsaidia katika kuimarisha cheo chake kama mwenyekiti, kwa hiyo kwa nini alikuwa amerudi kwa ghafla?

Dakika tano baadaye, mlango wa ofisi ukasukumwa. Chris alitokeza mlangoni na kunyoosha mkono wake kwa heshima. Baadaye, mtu mrefu ambaye alitoa mwonekano wa utulivu na heshima aliingia.
Mwanamume huyo alikuwa na sifa za kuvutia, lakini aliweza kutambua kwamba alikuwa na umri wa makamo kutokana na mikunjo ya macho yake. Wanaume walikuwa watu wazima zaidi katika umri huu.

Chris pia alikuwa na umri wa makamo, lakini mwonekano na sifa zake hazikuweza kulinganishwa na za mwanamume huyo. Mwanaume huyo alipoingia tu ofisini, alimkazia macho Lisa. Macho yake yalionekana kuwasilisha kila aina ya hisia ikiwa ni pamoja na furaha, huzuni, na taabu.

“Mjomba Chris, huyu…” Lisa alijawa na mshangao.

Chris akajibu, "Yeye ni baba yako, Joel Ngosha."

Kichwa cha Lisa kikamlipuka. Alikuwa amemfikiria baba yake mzazi hapo awali. Hata hivyo, kwa kuonekana kwake ghafla sasa, hakuweza kujizuia kuhisi amepigwa na butwaa. Zaidi ya hayo, jina la 'Joel Ngosha' liligonga kengele akilini mwake! Alikuwa mmoja wa wafanyabiashara watanzania kumi mashuhuri zaidi waliofanikiwa nje ya nchi kwa mwaka uliopita. Hapo awali alikuwa amekutana na habari zinazoelezea kwamba Joel alitoka kwenye familia ya kisukuma huko Mwanza na alianza na baishara akiwa Mwanza hadi akafanikiwa kukuza na kuvuka mipaka hadi Kenya. Alikuwa mmoja wa watu wema zaidi huko Nairobi, na zaidi ya hayo, alikuwa mtu mashuhuri mwenyewe.

Iliaminika kuwa familia ya Ngosha haikuwa na nguvu sana mwanzoni. Chini ya uongozi wa Joel katika miaka michache, hata hivyo, waligeuka kuwa moja ya familia tajiri zaidi katika jiji la Nairobi. Mwanaume huyu kwa kweli alikuwa baba yake mzazi. Hakuweza kuamini kabisa.

"Wewe ni picha ya mama yako." Joel aliendelea kumtazama Lisa huku machozi yakimtoka. “Sikutarajia kuwa Sherly angenificha. Hakika alijifungua binti yetu.”

"Sherly alikuwa na matumaini kwamba Lisa angeweza kukua salama," Chris alisema kwa sauti ya chini.

“Uko sahihi. Sikuwa na uwezo wakati huo.” Joel alikunja ngumi akionekana kukumbushia jambo la uchungu. "Kama nisingesikia kuhusu kuteuliwa hivi majuzi kwa mwanamke mchanga, ambaye alikuwa binti ya Sheryl, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, nisingejua uwepo wako."

Mambo mengi sana yalikuwa yamemtokea Lisa ndani ya kipindi kifupi. Licha ya kukumbwa na wimbi la hisia ndani yake, alijituliza baada ya muda mfupi. "Kwa hivyo, kwa nini unataka kukutana nami?" Aliuliza bila kujali na bila kujadili.

Joel alipigwa na butwaa lakini punde si punde alionyesha hali ya kusikitisha. “Tabia yako inafanana na ya Sherry enzi hizo, Lisa. Ningependa kukurudisha kwa familia ya Ngosha ili kufidia malezi yote ambayo umekuwa ukistahili kutoka kwangu kama baba yako kwa miaka mingi.”

“Sidhani kama hilo ni wazo zuri. Tayari una familia yako mwenyewe na una watoto. Mimi si mtoto tena, sitarudi nyuma.” Akiwa amechoshwa na migogoro ya kifamilia, Lisa alikataa.

“Lisa…” sura ya wasiwasi ilivuka uso wa Joel. “Lazima uende nami. Nahitaji kukutazama ili niweze kukulinda. Utambulisho wako utafichuliwa hivi karibuni. Wengi wao kutoka kwa ukoo wa Ngosha wamegundua uhusiano wangu na mama yako wakati huo.”
Lisa alipigwa na butwaa.

Chris kisha akaeleza, “Familia ya Ngosha ina mali nyingi ambazo vijana wengine katika familia wanatazamia. Kwa kuwa wewe ni binti wa Bwana Ngosha, utaingia katika urithi wake siku zijazo. Baadhi ya watu watahatarisha maisha yao kwa ajili ya madaraka.”

Lisa alikasirika na kukosa kusema, lakini hakupendezwa na utajiri wake hata kidogo. Kwa kweli, kuonekana kwa ghafla kwa baba yake kulikuwa kumeweka mzigo juu yake.

“Usiogope bwana Ngosha. Nitamshawishi. Tumtembelee Sheryl sasa.” Chris alibadilisha mada.

Lisa alikubali kuungana nao. Wakati wa safari, Joel alimsimulia hadithi nyingi kuhusu jinsi alivyokutana na Sheryl. Hata hivyo, hakuguswa hata kidogo. Aliuliza, “Kwa nini uliachana na mama yangu wakati huo?”

'Miaka 20 iliyopita, sikuwa na uwezo kiuchumi. Katika uhangaikaji wangu kwa bahati mbaya nikakutana na kulala na mke wangu wa sasa, Nina Mahewa. Baada ya mama yako kujua, aliamuua kuondoka akiwa na mimba yako. Muda si mrefu, nilisikia kwamba amefariki.”

Sura ya uchungu iliosha uso wa Joel. "Kisha, nilianza kuishi maisha yangu katika hali ya mshangao. Nina alipopata ujauzito, nilikubali kumuoa ili niwajibike kwa mtoto.”

Lisa alipokuwa akimsikiliza, alijawa na chuki. Ilikuwa hadithi ya kuudhi iliyoje. Alimuonea huruma mama yake kwa kuwa mwathiriwa. Baada ya kutembelea makaburi, aliondoka kwa kisingizio cha kuwa na kitu cha kuhudumia.

Joel alipomtazama akiondoka, alishusha pumzi ndefu. “Oh, Chris. Inaonekana binti yangu hataki kunitambua.”

"Lisa ameteseka sana katika familia ya Jones mwaka jana," Chris alieleza.
“Ndiyo. Ni kosa langu kwamba nilikuja kujua kwa kuchelewa sana. Lazima nimrudishe kwa familia ya Ngosha. Ninataka kumfanyia kazi na kumtunza vizuri,” Joel alisema kwa hatia.

Asubuhi iliyofuata, Lisa alikuwa na mkutano. Baada ya hapo, alirudi ofisini na tayari Chris alikuwa akimsubiri pale.

"Mjomba Chris, ulishajua mapema kuwa yeye ni baba yangu?" Lisa aliuliza moja kwa moja, "Je, unatarajia kwamba nitarudi kwa familia ya Ngosha pia?"

Chris alikuwa mkweli naye. "Lisa, unaweza tu kujua ni nani aliyemuua mama yako wakati huo ikiwa utarudi kwa familia ya Ngosha. Nimekuwa nikishuku kwamba huenda alikuwa Nina.”

Lisa kichwa kilimuuma. Ilimbidi ahusishwe katika mzozo mwingine wa kifamilia wakati alikuwa amemaliza tu mgogoro mmoja. Uchovu wake ulikuwa hauelezeki.

“Kwa hiyo, wakati huo alikuwa akimwonea wivu mama yangu hivyo akaamua kumuua?”

"Nina ni mtu katili sana. Yeye pia ni binti mkubwa wa familia ya Mahewa. Chris alipumua na kusema kwa unyoofu, “Ni sawa ikiwa hujisikii kuchunguza suala hilo. Kwa kweli, ni miaka mingi imepita tangu mama yako afariki. Zamani zimepita kwa muda mrefu na upepo. Kwa sasa, Joel na Nina wako kwenye uhusiano mzuri. Hata hivyo haitakuwa rahisi kwako kushughulika naye.”

Lisa alinyamaza kimya.

Chris kisha akasimama na kusema. “Nimekuja hapa kukujulisha kuhusu jambo hili. Baada ya kusema hivyo, kumbuka kwamba ikiwa Nina atapata habari kuhusu kuwepo kwako, hakika atakuwa mtu wa kwanza kushughulika nawe. Badala ya kuachwa juu na kuti kavu, afadhali ukae karibu na Joel.”

“Joel ana mke na binti ambaye ameishi nao kwa zaidi ya miaka 20. Mbali na ukweli kwamba nina uhusiano naye wa damu, nitaweza kweli kuwashinda? Lisa alitoa kicheko cha uchungu.

Chris alijibu kwa uzito, “Joel alikuwa akimpenda sana mama yako wakati huo. Amekuwa akimfikiria kwa miaka hii yote. Atakulinda.” Lisa aliposikia hivyo alikaa kimya kwa muda mrefu....ITAENDELEA....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.