JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................130, 131


Sura ya 130


Stephen na Janet Kileo waliwakimbilia wakiwa wamefura. Uso wa Stephen ulijawa na hasira kali. Hakutaka kitu zaidi ya kumnyonga Lisa akiwa hai. Alvin alimvuta Lisa nyuma yake, umbo lake refu na kubwa likitoa ulinzi wa nguvu kwa Lisa.


"Lisa Jones, wewe ndiye ulicheza ile video?" Stephen alifoka kwa hasira. “Sawa, umenikera mno. Ikiwa sitakuua, basi jina langu si Stephen Kileo.”


Janet naye alisema kwa msisimko, “Unajua umemkosea nani? Huyo ndiye Willie Kimaro! Hata kama umemficha uso, hatakuacha kwa kuwa umesambaza video zake kama hizi.”


Lisa aliinua macho yake na kutabasamu kwa dharau. “Umewahi kujiuliza hii video imetoka wapi na ni nani aliyenipa? Au ulifikiri ningethubutu kurekodi kitu kwenye chumba cha Willie Kimaro?”


Stephen na Janet wote walikua hoi kwa wakati mmoja. Muda mfupi baadaye, Stephen akatikisa kichwa. "Hiyo haiwezekani. Video hii huwezi kuwa ulipewa na Wiliie Kimaro. Ulimkosea jana usiku, kwa hiyo tayari anakuchukia. Umepata mtu wa kudukua simu ya Bwana Kimaro? Sawa, wewe ndiye uliyeanzisha hii. Nitampigia msaidizi wa Willie sasa hivi. Msaidizi wake ni rafiki yangu wa karibu sana.”


"Endelea kuota. Huenda hujui kuwa Willie Kimaro aliondoka Dar asubuhi ya leo.” Lisa alitabasamu kwa uso uliolegea. “Hivi mpenzi wako mzuri hakukuambia? Asubuhi ya leo, Willie alikuja Mawenzi Investments na kusema kwamba hatafuatilia suala la jana usiku tena. Willie pia alimdhalilisha sana Jones na binti yake. Sasa, kila mtu katika kampuni anajua Lina Jones alipanda kitanda cha mwanamume mwingine kutafuta kufadhiliwa. Wale wawili baba na binti yake hawana hadhi tena ya kuja kwenye kampuni."


“Usijaribu kunidanganya. Hakuna kitu kama hicho." Stephen hakumwamini hata kidogo. Alipiga moja kwa moja nambari ya msaidizi wa Willie Kimaro. Baada ya muda mrefu, simu iliunganishwa na sauti iliyolaaniwa kutoka upande wa pili, “Stephen Kileo, unawezaje kuthubutu kuwasiliana nami?! Umeniharibia! Hata nilipoteza kazi yangu.”


"Nini kimetokea?" Stephen aliuliza kwa sauti ya kuchanganyikiwa.


"Sijui. Vyovyote iwavyo, Lina Jones na wewe, nyinyi wawili ni mashetwain kabisa, mmemkasirisha sana Bwana Kimaro. Tayari amerejea Nairobi bila kupenda.” Simu ilikatwa kwa haraka.


Stephen aliganda kama sanamu ya mbao. Alimtazama Lisa ambaye alikuwa akitabasamu na ghafla akahisi damu yake ikishindwa kutembea kwenye mishipa. "Ulifanya nini kwa Bwana Kimaro?"


“Sina haja ya kujieleza kwa mtu kama wewe. Stephen Kileo, sikutaka kushughulika nawe, lakini ni kosa lako kumtambulisha Lina kwa Willie. Sasa, sifa yako imeharibika, na nadhani sio watu wengi watathubutu kuwasiliana na familia ya Kileo kwa ushirikiano katika siku zijazo. Unaweza kuendelea na ndoto ikiwa bado unataka kuoa mke kutoka katika familia yenye hadhi sawa na yako.” Lisa akamaliza hotuba yake na kuondoka zake kwa furaha huku akimshika mkono Alvin aliyekuwa kakasirika sana hadi kushindwa kuongea.


Janet aliyebaki nyuma alishika kichwa na kupiga kelele. "Stephen, haya mambo yametokeaje?" 'Yote ni kwa sababu ya ujinga wa Lina. Yule mjinga hata hajitambui kabisa.”


Stephen aliitoa hasira yake. "Sitamsamehe Lina kamwe. Naelekea nyumbani.”


Gari lilikuwa kimya, hewa ya wasiwasi ilitanda kila kona. Alvin akaminya midomo yake myembamba, umbo lake maridadi lkionekana kutulia kama sanamu. Lisa alimtazama kwa siri huku akijaribu kumwongelesha bila mafanikio.


“Bado una hasira? Kwa kweli nililazimika kukabiliana na Lina wakati huu. Nilitamani kutapika kila nilipoutazama mwili wa Willie Kimaro. Sasa, ninachotaka ni kwenda nyumbani na kuutazama mwili wako mzuri ili niweze kuosha macho yangu…”


“Sasa ndiyo unataka kunitazama?” Alvin ghafla alimkazia macho. Lisa akaguna na kukubali kwa kichwa.


"Sawa, nitakuruhusu uangalie usiku kucha." Alvin alikubali ghafla.

Lisa alipigwa na butwaa na kukosa la kusema. Alvin alikunja uso na kumuonya tena. "Ikiwa hii itatokea tena ..."


“Haitatokea tena,” Lisa aliapa, "Ikiwa itatokea, Mungu na aniadhibu nisiuone tena mwili mkamilifu wa Alvilisa maishani mwangu."


"Nyamaza." Alvin alicheka. “Hiyo video bado ipo kwenye simu yako? Nitafuta kila kitu kwenye simu yako tukifika nyumbani. Willie Kimaro ni mchafu sana kijana yule, sijui tabia hiyo kaitoa wapi!"


"Nakubali. Ingawa nimeona kidogo tu, sijisikii vizuri hata kidogo.” Lisa alijifanya kuchukizwa. "Alvilisa, najua huna tabia mbovu kama hii, si ndiyo?"


“Utaijua tu tabia yangu, ikiwa ni nzuri ama mabaya.” Alvin alijibu akicheka.


Baada ya kurudi nyumbani, Lisa alivua Mkufu wa Malkia wa almasi kwa uangalifu baada ya kukaa chini ya taa ya mezani na kuuangalia kwa upendo. “Ni mzuri sana. Hakuna dosari hata kidogo.”


"Nakumbuka ulisema haupendi vito vya mapambo." Alvin alitembea nyuma yake na kumtania, "Hata ulisema ni mtumba tu."

Lisa aliona haya na kusema kwa kigugumizi, “Mimi… nadhani ni ghali sana. Ni shilingi bilioni tatu. Itachukua muda gani kupata kiasi hicho cha pesa?"


"Ethan Lowe alikuwa tayari kutoa bilioni mbili kwa ajili ya mwanamke wake, kwa nini nijali kuhusu kiasi hiki?" Alvin alicheka kwa unyenyekevu. "Kwangu mimi, pesa haijalishi. Muhimu ni kwamba unaupenda."


Lisa akapepesa macho, mara akaelewa kuwa alikuwa akijaribu kushindana na Ethan. Hata hivyo, hiyo haikujalisha. Kadiri alivyokuwa akipambana na Ethan ndivyo ilivyokuwa ikionyesha kuwa anamjali.


“Alvilisa, Ethan kwa kweli hana uhusiano wowote nami. Mimi pia simpendi tena. Ninayempenda ni wewe." Aligeuka na kumkumbatia shingo na kumbusu usoni.


Moyo wake uliuma. Hapo awali, ingawa alipata pesa nyingi, hata hivyo ilionekana kama hazina faida yoyote. Sasa, ilionekana kana kwamba alikuwa amepata maana ya kupata pesa. Midomo yake myembamba ilijikunja huku akimpa sura isiyoeleweka. "Ni hayo tu?"

Lisa alionekana kujua alichokuwa akiongea na kuinamisha kichwa chini.


Alvin alicheka na kumnyanyua. "Si ulisema unataka kunitazama?"


“Hapana…” Uso wa Lisa ukageuka kwa woga. Alikuwa ni hodari wa kusema maneno makubwa, lakini ndani alikuwa ni mwoga kuyatekeleza.


"Kwa hiyo ulikuwa unanidanganya si ndiyo?" Alvin akakisugua kidevu chake taratibu. Sauti yake ilisikika kana kwamba ni sauti ya simba.


Mapigo ya moyo ya Lisa yalimuenda kasi, akazidi kuogopa. Alimsukuma kwa haraka. “Si ulisema hukula chakula cha kutosha wakati wa chakula cha jioni? Nitakwenda kukupikia.” Harakaharaka akamtoroka na kutoa tabasamu la hovyo chini ya macho ya Alvin.


Alvin alipotoka kuoga, Lisa alikuwa amepika chakula chenye harufu nzuri na kumtengea. Hakuwa amekula chakula cha jioni kilichopikwa na Lisa kwa muda mrefu na mara moja akakichukua ili kukionja. Kilikuwa ni chakula cha kawaida tu, lakini hakujua jinsi Lisa alivyokipika maana ladha ilikuwa ya kipekee sana kila wakati. Lisa alimsaidia kukausha nywele zake zilizolowa maji huku akimwangalia akila chakula kile kitamu.


“Upishi wangu bila shaka ni mtamu sana, lakini ulisema hukuupenda nilipokutengenezea mara ya kwanza. Wewe ni mnafiki sana, lakini wewe pia unajua kunipenda sana.”


Alvin aliona aibu. Ilikuwa ni kidogo sana kwa mwanamume kuelezewa kama mnafiki. Alimvuta kwenye mapaja yake na kuonyesha kutofurahishwa. “Unamwita nani mnafiki mkubwa? Hebu thubutu kusema tena?”


“Nakuzungumzia wewe. Bado unakataa kukiri… Mmh…”


Kabla Lisa hajamalizia, busu la kutawala la Alvin likaanguka kwenye midomo yake. Alimbusu bila kupumua, na hatimaye alipomwacha, alimwambia akiwa amemshika mabegani "Ukithubutu kusema tena nakuongeza zaidi ya hili..."


“Wewe ni mnafiki, kwani uongo…” Lisa alirudia tena huku akicheka. Inaonekana alikuwa amefanya kamchezo fulani ka makusudi.


Alvin akamkamata tena na kumpa busu. Wakati huu, alipigwa busu kali zaidi. Mikono yake mikubwa ilimkumbatia kwa nguvu kumzuia asikwepe. Lisa alikuwa na hasira na furaha kwa wakati mmoja. Alvin alikuwa jabari kupita kiasi na hakuruhusu mtu yeyote kuzungumza kwa utani juu yake.


Punde, Lisa alianza kulegea na kuzidiwa na hisia, Alvin alimbeba hadi kitandani. Alvin alikuwa amevaa bukta nyepesi tu alipotoka kuoga. Aliivua na kumtazama Lisa na kusema kwa sauti ya unyonge, “si ulisema unataka kunikodolea macho ili kuosha macho yako? Unaweza kuanza sasa.”


Uso wa Lisa uliwaka moto. Hakuwahi kufikiria kwamba Alvin angekumbuka jambo lile tena.


Umbo lake lilikuwa zuri sana. Hakuwa na misuli kupita kiasi bali mtanashati na mwenye nguvu. Zaidi ya hayo, alikuwa ametoka tu kuoga, hivyo harufu yake ya kiume na harufu ya gel ya kuogea ilimfanya apate hisia nzuri za utamu.


Sur ya 131


Nywele za Alvin zilikuwa zimekaushwa tu na kuachwa zikiwa zimevurugika kwa fujo. Kwenye uso wake mzuri, kulikuwa na hisia zisizo na kikomo za kimapenzi zikitoka kwenye mwili wake wote.


Lisa alimtazama kwa shauku. Wakati huo, alitaka sana kumshukuru Pamela. Ni kosa alilofanya Pamela la kumchanganya Alvin na Kelvin, mjomba wake Ethan, ndilo lililompeleka Lisa kwake. Alikuwa amemsaidia mara kwa mara. Ni yeye pia aliyemfanya awe na ujasiri wa kuishi licha masaibu yote aliyokutana nayo.


Usiku huo, alimpatia Mkufu wa Malkia, kwa gharama ambayo ilimfanya kuwa mwanamke tajiri na aliyevutia kuliko wote Masaki nzima.


“Alvilisa…” Lisa alinyanyuka na kushika shingo yake. Uso wake wa ajabu uliangaza kwa aibu. "Tunaweza ... tujaribu?"


Alikuwa ameamua. Bila kujali kama familia ya Kimaro ingemkubali au la katika siku zijazo, alitaka kumpa Alvin kitu cha thamani zaidi alichostahili.


Alvin aliganda! Yeye alikuwa sugu kwa mambo hayo siku nyingi, na alikuwa hajaenda mbali zaidi pia. Mbona Lisa alikuwa ameamua ghafla…?! Au ni kwa sababu alijua utambulisho wake halisi?


“Kwa nini?” Macho yake mazito yalimtazama kana kwamba alitaka kuona kupitia kwake.


Lisa alikuwa amefunikwa na aibu na hakuona sura yake ya kushangaza. Alikuwa ameuzika uso wake mdogo katika kifua chake. “Kwa sababu nakupenda. Sijawahi kuwa na uhakika wa hisia zangu kama nilivyo sasa.” Lisa alijibu kwa aibu.


Alvin alisugua nywele zake laini na ndefu juu ya kichwa chake kwa udadisi. Hakuridhika na jibu lile. Kulikuwa na wanawake wengi sana waliomzunguka ambao walitaka sana kumrukia kwa sababu tu walijua utambulisho wake halisi, kwamba yeye ni mwanamume tajiri.


“Kwa nini? Je!… hutaki?” Lisa aliona haongei wala hafanyi chochote na akaona aibu. “Usinielewe vibaya, ni moyo tu ndiyo umenituma, sina nia ya kukujaribu na wala sikulazimishi. Kama hutaki basi tuache…” Alimsukuma na kukaribia kuinuka, lakini mwili wa Alvin haukumruhusu kunyanyuka.


"Ikiwa utanishinikiza kwa njia hiyo, basi nitakubali kwa kusita," Alvin alisema kwa sauti.


Lisa alimtazama kwa hasira. “Si lazima ufanye kwa kusitasita. Sikulazimishi na sijali hata hivyo…” Kabla hajamaliza, Alvin akambusu. Wakati huo, alielewa. Haijalishi alikuwa akifikiria nini, ni kweli alimtaka! Zaidi ya hayo, alikuwa amekiri kwake muda mrefu uliopita. Hakukuwa na haja ya kutilia shaka kwamba alimpenda.


Dakika chache baadaye, aliufunga mlango kwa nguvu na kwenda bafuni kuoga tena. Lisa alifoka kwa hasira ya kuachwa akiwa ‘ameiva’.


Dakika 20 baadaye, Alvin alitoka kuoga akiwa na sura tofauti. Hakumgusa tena Lisa wala kuwambia kitu chochote. Moyo wa Lisa uliumia alipofikiria juu yake.


‘Sitathubutu kumwambia katika siku zijazo.’ Alijiapiza kimoyomoyo kwa unyonge. Alikumbatia shingo yake na kuuzika uso wake kifuani mwake. Alikuwa na haya sana hivi kwamba hakuweza kuongea tenakwa muda mrefu.


"Potezea tu kwa leo. Utakuwa mwanamke wangu mapema au baadaye." Sauti ya Alvin alipomkumbatia ilikuwa ya kutetemesha sana.


Wawili hao walipolala, hawakujua kwamba habari kuhusu tukio la hisani usiku huo zilikuwa zimeenea mitandaoni. Kila mtu alijua kuhusu hilo. Wakati huo, katika makazi ya Jones Masawe, Jones kwa mara nyingine tena alipokea simu kutoka kwa wadaku.


“Bwana Jones, umeona sura duni ya binti yako? Hehe, nipe basi binti yako alale nami kwa usiku mmoja na nitafanya kazi nawe kwenye mradi."


"Nyamaza!" Mwili wa Jones ulitetemeka kwa hasira huku akilaani, “Weka kinywa chako ksafi unapoongea na mimi!”


“Hehe, ningewezaje kuwa msafi kuliko binti yako? Nani angethubutu kutaka takataka kama hiyo?"


"F*ck off! Usinipigie tena.” Jones aliivunja simu yake.


Alikuwa ameishi kwa miaka mingi na tayari alitumia nusu ya maisha yake, lakini hakuwahi kufedheheshwa kama ilivyokuwa siku hiyo. Hapo awali, alifikiria kwamba angeipata Mawenzi Investments kwa urahisi, lakini ilienda mbali zaidi na mikono yake. Si hivyo tu, hata alipoteza sifa na heshima yake ya mwisho. Alikasirika sana hivi kwamba alipoteza busara yake. Alichukua ufagio na kwenda juu ili kumpiga Lina.


“Wewe b*tch, yote ni makosa yako! Tangu uliporudi, tulipoteza Kibo Group na sifa yetu. Hata mimi pia nimefedheheshwa katika umri huu. Mjinga sana wewe!”


"Hapana!" Lina alipiga kelele mara kwa mara na kuendelea kujificha. "Baba, nilifanya hivyo kwa ajili ya familia ya Jones. Ni wewe ulinishauri nimfurahishe Bwana Kimaro.”


"Nilitaka umfurahishe kwa zawadi, sio kulala naye, paka wewe!" Jones alipiga kelele. Kadiri alivyokuwa akisema ndivyo hasira zilivyozidi kuongezeka na ndivyo mikono yake ilivyozidi kuwa matata.


“Una kichaa? Ni binti yetu!” Mama Masawe aliingia ndani na kumsukuma. Alipoona sura ya Lina iliyochubuka na kupigwa, alilia kwa huzuni.


“Afadhali nisiwe na binti kama yeye!” Jones alimnyooshea kidole na kumkaripia, “Ningejua kwamba haya yangetokea knisingekurudisha kabisa. Ikiwa sio wewe kurudi, ningekuwa na ugomvi na Lisa? Ikiwa hukunitia moyo, ningemuua mama yangu kwa mikono yangu mwenyewe? Isingekuwa wewe hata Lisa angeingia Mawenzi Investments angenisikiliza na kuniacha niwe mwenyekiti.”


Lina aligeuka rangi, na mwili wake ukatetemeka huku akijilaumu mwenyewe.


Mama Masawe hakuweza kumsikiliza tena. Alimkumbatia Lina kwa nguvu na kupiga kelele, “Inatosha! Ni wazi Lisa ndiye aliyetulazimisha kufikia hatua hii, lakini bado unamlaumu na kumpiga Lina. Unataka tu kumalizia hasira yako kwa kumuonea mtu mwingine."


“Bado una ujasiri wa kusema hivyo? Binti mzuri uliyemlea mwenyewe hana haya wala aibu. Ninachojutia zaidi ni kwamba nilikuoa na kumzaa!”


"Sawa, kwa kuwa unajuta, tutaondoka!" Mama Masawe alilia na kuushika mkono wa Lina kabla ya kutoka nje. Muda si muda, nyumba nzima ikawa tupu na ya kutisha......ITAENDELEA....


Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.