JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................802-803
Sura ya: 802
Msaidizi aliendesha gari na kumtazama Matthew aliyekuwa kimya nyuma yake mara kwa mara. "Bwana Mkubwa, tulidanganywa?"
Uso mzuri wa Matthew ulikuwa na huzuni sana. Sio tu kwamba alidanganywa, lakini alishuku kwamba alikuwa ameanguka kwenye mtego wa Lina na wazazi wake.
Matthew zaidi alikaa juu ya jambo hilo, hasira ikiwa juu yake. Katika hatua hii, alikataa kumtambua Lina kama dada yake. Subiri. Madai ya Lisa kwamba Lina hakuwa dada yake yanaweza kuwa ya kweli. Mwanaume mtukufu kama yeye angewezaje kuwa na dada mwenye karaha namna hii? Sheryl pia asingeweza kuzaa binti wa tabia kama hiyo. Baada ya kusema hivyo, vipi kuhusu matokeo ya mtihani wa DNA? Huku akiwa amechanganyikiwa, msaidizi alifunga breki.
“Unajua kuendesha gari?” Matthew alishindwa kujizuia.
“Samahani bwana mkubwa. Bibi kizee alitokea mahali hapo sasa hivi, na karibu nimgonge. Ngoja nishuke nikaangalie.” Msaidizi akafungua mkanda wake wa usalama kwa haraka na kutoka nje ya gari.
Bibi kizee mwenye mvi alikuwa amelala njiani. Msaidizi akaenda kumsaidia mara moja. “Bibi, uko sawa...”
Kabla hajamalizia sentensi yake, kisu kiling’aa na kumchoma kifuani. Huku mgongo wake ukiwa umemtazama Matthew, akili ya msaidizi ilipotea mara moja. Alitaka Matthew akimbie haraka, lakini hakuweza kusema neno lolote.
“Kila kitu kiko sawa?” Matthew alishuka, akamuona msaidizi wake akiinama. Baada ya kusogea hatua chache karibu na msaidizi, ghafla aliona madoa ya damu kwenye miguu ya yule msaidizi.
Ghafla, Matthew alikuwa na hali ya kutatanisha. Wakati huo huo, kitu kilitupwa kwake kutoka nyuma. Matthew aliinamisha mwili wake upande mmoja na kukwepa. Baada ya hapo, alikimbia haraka kuelekea upande mwingine.
Hata hivyo, gari mbili nyeusi zilienda kasi na kumsimamisha upesi. Baadaye, watu wanane waliruka nje ya magari wakiwa na visu mikononi mwao. Matthew alizingirwa kutoka pande zote.
“Nyie ni akina nani?” Maneno ya Matthew yalikuwa ya wasiwasi. Licha ya kuwa amekumbana na hatari nyingi tangu akiwa mdogo, siku zote alikuwa na mlinzi wake mahiri kando yake. Ilikuwa mara yake ya kwanza kukumbana na hali kama hii.
Badala ya kujibu swali lake, kundi hilo la watu lilimshambulia moja kwa moja. Ingawa Matthew alikuwa stadi, hakuwa na silaha yoyote pamoja naye, hata hivyo. Kwa kuzingatia kwamba alikuwa akikabiliana na watu wengi, hakuna kitu ambacho angeweza kufanya. Muda si muda, mwili wake, miguu na mikono vilijeruhiwa vibaya sana. Mwishowe, alishindwa wakati mtu alipomwangusha kwa siri kutoka nyuma.
Baada ya kuzimia, wale watu walimtupa kwenye gari moja kwa moja, na kiongozi huyo akapiga namba moja kwa moja. "Bwana Mushi, tumeshughulika naye."
“Jificheni sasa hivi. Msiruhusu mtu yeyote awapate,” Kelvin alisema kwa ukali.
“Sawa.”
Mara baada ya kukata simu, Kelvin akampigia Lina kwa haraka. “Matthew ameanza kukushuku.”
"Nini?" Lina alishtuka. Kwa sauti ya chini, alisema, "Lazima Lisa alimwambia jambo fulani."
“Matthew alienda Dar es Salaam leo ili kujua kuhusu mambo yako. Watu wengi wanajua mambo ya kijinga uliyofanya zamani. Kwa bahati nzuri, niliitayarisha na kupandikiza mpelelezi huko Dar es Salaam mapema. Nimemkamata Matthew, na msaidizi wake amekufa.”
Hatimaye Lina alishusha pumzi ya raha. Alifurahia kufanya kazi na Kelvin haswa kwa sababu alikuwa mkali. “Bwana Mushi, una uwezo. Lakini kwa nini unamweka Matthew hai? Ni salama kumuua. Katika hali hiyo, ninaweza kuelekeza lawama kwa Lisa na Alvin.”
“Huenda Sheryl amechanganyikiwa—akiwa anaongozwa na dawa hiyo, lakini je, unafikiri kwamba Titus ni mjinga? Yeye ni mwerevu. Ikiwa hali ya Sheryl itaendelea hivyo, atagundua hivi karibuni, na wewe ndiye wa kwanza atakayekushuku. Iwapo sote tunataka njia ya kutokea, ni lazima tubaki na Matthew ili kulinda maisha yetu,” Kelvin alijibu kwa ubaridi.
Mara moja Lina alielewa hoja yake.
“Lakini...” Kelvin alicheka ghafla. "Kwa kweli, unaweza kumpakazia Lisa na Alvin kuhusu kutoweka kwa Matthew. Sheryl anapoteza udhibiti, na Lisa ni kwake ni mkatili. Ikiwa Sheryl atamuumiza mtu yeyote karibu na Lisa, Lisa atamchukia ingawa yeye ni mama yake mzazi. Tuwaache wawili hao wauane.”
"Wewe ni mkatili kweli." Lina alitabasamu.
“Na wewe pia. Fikiria njia za kubana pesa za Sheryl kwa muda mfupi iwezekanavyo, au bora zaidi, kuiba pesa nyingi zaidi kutoka kwenye mabenki yake.” Kelvin alimkumbusha, “Bila shaka, kabla ya kufanya haya yote, unahitaji kumfanya Sheryl ahisi kana kwamba kila mtu amemwacha. Kisha, atakuwa na mzozo mkali na Titus.”
Punde, wazo likaibuka kichwani mwa Lina. “Hili linawezekana. Sheryl na Titus tayari wanalala katika vyumba tofauti. Suala la Matthew linaweza kuliongezea nguvu.”
•••
Katika nyumba ya familia ya Kimaro.
Lisa alikuwa amevaa aproni, akipika nyama ya nguruwe jikoni. Kwa vile Alvin hakwenda kazini siku hiyo, aliongozana na watoto kukamilisha fumbo sebuleni.
“Hii ni makosa. Mrengo unapaswa kuwa hapa ... "
"Umeiweka mahali pabaya, kilaza wewe..."
“Baba, Lucas ananionea tena. Hata aliniita kilaza.” Suzie alifoka na kumlalamikia.
“Yeye ni kilaza tu. Kipande hiki kinapaswa kuwa hapa."
Kichwa cha Alvin kilimuuma usoni kwa manung'uniko ya bintiye. Suzie aliiweka vibaya kipande cha fumbo, lakini hakukubali kukosea akaanza kulia. Mara tu alipolia, angezingatiwa kuwa sawa kwa kila kitu ulimwenguni.
“Sawa, sawa. Uko sahihi. Wewe si kilaza. Tuyaache hapa.”
“Angalia. Hata baba alisema niko sawa.” Suzie aliacha kulia papo hapo na akawa mbishi juu ya hilo.
Lucas alikosa la kusema. “Hii inachosha. Sitaki kucheza na nyinyi, au itapunguza kiwango changu."
"Pfft. Sitaki kucheza na wewe pia. ” Suzie alikasirika.
Alvin alishindwa cha kusema. Lisa alipoleta nyama ya nguruwe kwenye meza, aliona sura ya Alvin yenye mgongano. Alicheka kabla hajapunga mkono na kusema, "Jitayarishe kwa chakula cha jioni."
“Haya! Hatimaye ni wakati wa chakula cha jioni.”
Baada ya kunawa mikono yao kwa hiari yao wenyewe, Suzie alichukua ubavu wa nguruwe na kuula kwa raha huku Lucas akimenya kamba. Baada ya Alvin kuketi, alikula nyama za nguruwe na binti yake.
Lucas alimtazama na baadae akageuka kumtazama Suzie. Kwa ghafla, alisema kwa dharau, “Hatimaye ninajua Suzie anamfuata nani.”
Lisa alicheka huku Alvin akiwa hana la kusema. "Suzie na mimi tunashiriki ladha sawa katika suala la chakula. ”
“Suzie, anakudharau kwa sababu ya kiwango chako” Lucas alitania.
"Hapana." Kichwa cha Alvin kilianza kumuuma.
“Kwanini hukusema Suzie anakufuata katika kila kitu badala yake?” Lucas aliweka uso uliopoa huku akijaribu kumuweka Alvin kwenye mkengeuko wa mawazo.
Alvin hakujua la kusema. Kwa bahati nzuri, simu yake iliita wakati huo, ambayo ilimuokoa kutoka kwa makucha ya wale wasumbufu wawili watoto.
Baada ya kuona taarifa ya simu inayoingia, alisita kwa sekunde mbili kabla hajapokea simu. "Mjomba ..."
"Alvin, umekula chakula cha jioni?" Spencer aliuliza, “Je, unapatikana usiku wa leo?”
"Kuna nini?"
“Mimi na shangazi yako tutampeleka Willie India kutibu ugonjwa wake, na hatuna uhakika ni lini tutarudi. Kuna jambo hapa ambalo tungependa ulipitishe kwa babu na bibi yako. Nilitaka kuwafahamisha kibinafsi mwanzoni, lakini wamekataa kukutana nami tangu majuzi,” Spencer alisema kwa sauti ya hovyo.
"Nini kile? Nitamwomba Hans. aje achukue...”
“Ni urithi wa familia ya Kimaro ambao babu yako alinipa. Unapaswa kuuchukua mwenyewe kwa sababu ni wa thamani sana,” Spencer alijibu.
“Sawa, nitakuja baada ya muda mfupi.” Alvin akaweka simu yake chini.
"Unaenda wapi?" Lisa aliuliza.
“Mjomba ameniomba niende kwake kuchukua kitu. Unaweza kukaa nyumbani na watoto."
Baada ya kumaliza chakula chake cha usiku, Alvin alisimama na kuondoka nyumbani.
Sura ya: 803
Ni baada tu ya gari lake kuondoka kwenye nyumba ya familia ya Kimaro ambapo Alvin aliwasiliana na Shani. "Peleka watu wengine wavizie kwa siri nyumba ya mjomba wangu na kuchukua hatua baadae."
Shani alipigwa na butwaa. "Unashuku kuwa kuna kitu kilitokea katika nyumba ya Spencer Kimaro?"
“Mmh.” Alvin hakufafanua hilo. "Ikiwa sitawasiliana nawe ndani ya nusu saa, unaweza kuingia mara moja."
“Sawa.” Shani aliweza kuhisi jinsi Alvin alivyokuwa makini kutokana na sauti yake. “Unahitaji nipige simu polisi?”
"Hakuna haja. Ninashuku Willie ametekwa nyara.”
Alvin alifanya nadhani hii kulingana na maneno ya Spencer ambayo yalikuwa yamejaa mianya. Ingawa Spencer alikuwa mwana pekee wa kiume wa Mzee Kimaro, urithi wa familia haujawahi kupitishwa kwake. Kwa kuwa Spencer alitaka aende zake kwa ghafla sana, ilikuwa na uwezekano mkubwa kwamba alitishwa. Kwa kweli, Alvin angeweza tayari kukisia ni nani aliyemtisha Spencer.
Dakika 40 baadaye, Alvin aliendesha gari hadi kwenye jumba la mjomba wake. Wakiwa wamesimama uani, Iveta na Spencer walikunja midomo yao kwa busara. Spencer alikuwa wa kwanza kusema, "Alvin, samahani kwa kukufanya uje saa za usiku hivi."
Alvin alimtazama Spencer bila kujali hata Spencer akatetemeka sana. "Mjomba, kwa kuwa sasa umenidanganya kuja hapa, ni wakati wa kuniambia sababu halisi."
Midomo ya Spencer ilitetemeka kwa aibu. Iveta alimkodolea macho Alvin na kusema kwa meno ya kusaga, “Ndio. Tulikudanganya kuja hapa. Baada ya yote, familia yetu iliingizwa kwenye matatizo kwa sababu yako na Lisa. Maskini Willie. Tayari ni zuzu, lakini bado hawataki kumwacha. Hakika ya imetosha…”
Hatimaye Alvin alipata picha. “Nani alifanya hivyo?”
"Kelvin anasema anataka kukuona." Spencer alionesha ishara sebuleni na kidevu chake. “Usijali. Hakumleta mtu mwingine yeyote hapa. Katibu wake wa kike tu ndiye yuko naye. Alvin, kwa kweli sijui anapanga kufanya nini, lakini lazima umwokoe Willie. Huyo mwanaharamu alimdanganya Willie aondoke naye nilipokuwa mjini kununua kitu na shangazi yako.”
Alvin alikunja uso. Hakuwa na hakika na nia ya Kelvin. Ikiwa Kelvin alitaka kushughulika naye, angewezaje kumleta mtu mmoja tu hapa? Kelvin alikuwa anapanga nini duniani?
“Lazima umuokoe Willie. Kelvin alikuja kututafuta sote kwa sababu yako.” Alipogundua kwamba Alvin alikuwa amenyamaza, Ivete alipiga kelele kwa haraka, “Nadhani anachotaka ni kuzungumza nawe jambo fulani. Tii tu chochote anachoomba. Willie ni binamu yako. Sasa kwa kuwa tayari ni mjinga hawezi kupoteza maisha yake.”
“Inatosha.” Spencer alimzuia.
"Ninafanya hivi kwa ajili ya Willie. Ikiwa jambo fulani litatokea kwa Willie, ninaweza hata kujiua. Nimechoshwa na mambo kama haya kutoka kwa familia ya Kimaro." Ivete akapiga kelele,
“Mwambie atoe simu yake.” Sauti kutoka ndani iliamuru.
Spencer aliona aibu. Alitamani ajizike kwenye shimo. "Alvin, Kelvin anaogopa kwamba utarekodi mazungumzo yako na yeye, kwa hivyo anataka utoe simu yako."
Midomo myembamba ya Alvin ilijikunja kwa huzuni. Kwanini Kelvin aliogopa kurekodiwa? Aliogopa wazi kwamba Alvin angeomba msaada.
Baada ya kuona Alvin ametulia tuli, Spencer alianza kuingiwa na hofu. “Alvin, sisemi uongo. Ni Kelvin tu na sekretari wake waliomo ndani, naapa. Alisema usipofuata maagizo yake, Willie hatarudi tena.”
Spencer alikuwa karibu kumwaga machozi.
“Mjomba, ninakubali kwamba Kelvin alimtishia Willie yote kwa sababu yangu. Lakini hii ni mara ya mwisho ninaenda kumuokoa. Siwezi kumlinda milele.”
Alvin akaitupa simu yake mkononi mwa Spencer. Ingawa hakujua ni nini Kelvin alikusudia kufanya, Shani angeingia baada ya dakika 2o hata kama hakuwa na simu yake. Kwa kuwa dakika 1o zilikuwa zimepita, alipaswa kuwa na uwezo wa kushughulika na watu kumi au hivyo kuzingatia ujuzi wake.
Alipomaliza kuongea, alipiga hatua kuelekea ndani kwa miguu yake mirefu. Alipoingia ndani ya jengo hilo, taa zote zilizima ghafla. Hata madirisha yalifungwa kwa nguvu bila mwanga kupenya ndani. Aligeuka, akakuta mlango wa nyuma yake ukigongwa kwa nguvu.
Hasira iliangaza machoni mwa Alvin. Hapo awali alifikiri kwamba walimnyang'anya simu ili kumzuia kuwasiliana na mtu yeyote nje. Hata hivyo, kwa mwonekano wa mambo, walitaka kumzuia asitumie tochi kwenye simu.
Kwa hivyo ni nini ikiwa asingeweza kuona chochote? Bado angeweza kumtambua Kelvin kulingana na sauti yake.
"Kelvin Mushi, ukiweka ubaya wako kando, hauthubutu hata kuacha taa ikiwaka. Je, unaona aibu kukutana nami kwa sababu ya hayo machafu uliyoyafanya?”
Alvin alisimama palepale huku sauti yake ikiwa imejawa na uchochezi na dharau. Hata hivyo, swali lake lilipokelewa na ukimya. Ghafla, kipande cha muziki wa ajabu kilisikika kwenye vnyumba. Hakujua ni nchi gani muziki huo ulitoka, lakini ilionekana kama wimbo wa Sanskrit, India ya zamani. Ingawa hakuielewa, kwa namna fulani alipata kuifahamu. Alionekana kuwa ameusikia mahali fulani hapo awali. Aliusikiliza muziki kwa muda, akijaribu kuukumbuka. Hata hivyo, kichwa chake kilianza kumuuma ghafla.
Kisha, mwanga wa ajabu uliofanana na nyota ulitokea ghafla kwenye ghorofa ya pili. Wakati Alvin akielekea kwenye mwanga, mwanga mwingine wa ajabu ukawaka pembeni. Taa hizo mbili zilikuwa zikiwaka kwa wakati mmoja bila kukoma, na akaanza kuchanganyikiwa. Alipogundua kinachoendelea, Alvin alifumba macho.
Baadaye, sauti ya mwanamke ilisikika kutoka ghorofa ya pili. "Alvin, kumbuka kuwa Sarah ndiye mwanamke unayempenda zaidi. Mwanamke unayempenda zaidi ... "
Sauti hii… Kichwa cha Alvin kilizidi kumuuma. Ni kana kwamba kuna kitu kilikuwa kikiunguruma kichwani mwake, ambacho kilikuwa kinakaribia kulipuka. Hapana, haikuwa hivyo. Lisa ndiye mwanamke aliyempenda zaidi. Hapana!
"Sarah Njau, hivi ndivyo unavyofanya?" Alvin alifuata uelekeo wa sauti ile na kusogea mbele gizani. Lakini, hakuweza kupata njia yake. Hata aliteleza juu ya kitu.
Sauti hiyo tambarare iliendelea, “Mtu unayemchukia zaidi ni Lisa. Ni Lisa. Ni Lisa. Yeye ndiye aliyekutongoza. Alikutongoza, akakutongoza...”
Kuna kitu kilionekana kuamsha kumbukumbu yake. Kichwa cha Alvin kilianza kumuuma sana. Kutokana na maumivu hayo, uso wake mzuri ulipauka. Kwa ufahamu wake mdogo, alikuwa anafahamu vyema nia halisi ya Kelvin. Kadiri alivyokataa kuisikiliza ile sauti, ndivyo ilivyopenya masikioni mwake kama sauti ya shetani. Zaidi ya hayo, sauti nyingi zilitoka kichwani mwake. Sauti hizi katika kumbukumbu zake zilikuwa za kawaida lakini za kushangaza.
"Unaweza kunitaliki, lakini unahitaji kunipikia kwa miaka mitatu, na nitakubali ombi lako."
"Lisa, ulinipenda kweli?"
“Hata kama haujali, mimi hunijali. Lisa, najua unanichukia, lakini nifanye nini? Ninahisi kama umenidanganya, lakini siwezi kuvumilia kukuacha uende. Nimewekewa sumu aina ya Lisa.”
Nani alikuwa akizungumza? Hapana. Hakuweza kuruhusu sauti ziendelee.
Wakati Alvin akiendelea kujikongoja kuelekea upande wa sauti ile gizani, alikosea kunyanyuka na kutereza kwenye ngazi. Sauti zikaacha kuita pia....... ITAENDELEA.....
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA...
