JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................762-763

Sura ya: 762

'Joel Ngosha...'
Hayo ni maneno mawili ambayo yalijitokeza mara moja kwenye akili ya Sheryl. Alipogundua kuwa alikuwa na kipindi cha nyuma na Joel, alitafuta habari za Joel kwenye mtandao nyuma ya mgongo wa Titus. Picha kwenye mtandao zilifanana sana na mtu aliye mbele yake. Alionekana mdogo tu kwenye picha.

"Samahani. Sikujui wewe. Umenifananisha." Usemi wa Sheryl ulikuwa baridi. Kwa kuwa alisikia habari mbaya za mwanaume huyo kutoka kwa Lina hapo awali, hakuwa na mawazo mazuri juu yake wala hakutaka kuwa na maingiliano yoyote naye.

Joel alishikwa na butwaa. Kisha, akatikisa kichwa. “Haiwezekani. Nakumbuka jinsi unavyoonekana. Sherry, nilidhani umekufa...” Hata alishindwa kujizuia na kuushika mkono wa Sheryl kwa fadhaa.

Hata hivyo, alipomgusa tu, mwanamume, pengine mlinzi, alisogea mbele na kuusukuma mkono wa Joel. Baada ya hapo, mlinzi alitumia mkono wake kumkinga Sheryl haraka. "Bibi, tafadhali ingia kwenye gari."

Sheryl alitembea kuelekea kwenye gari mara moja. Lina, ambaye alikuwa pembeni, mara moja akaingia kwenye gari kwa woga. Hakutarajia wangegongana na Joel haraka namna ile. Kwa bahati, Joel hakuwahi kumuona Lina hapo awali.

“Sheryl, sijakokosea. Wewe ni Sheryl Jones.” Joel alimfuata kwa hasira, lakini alisukumwa mbali na mlinzi tena.

Akiwa amekosa kuridhika, alisema kwa macho yenye damu, “Sheryl, najua unanichukia, na hutaki kunikubali. Lakini si unamkumbuka Lisa? Yeye ni binti yako.”

Sheryl hakumjali na kuingia kwenye gari moja kwa moja. Haikuwezekana kuona kilichokuwa kikiendelea ndani ya gari mara mlango wa gari ulifungwa na vioo vilikuwa tinted.

Baada ya mlinzi huyo kuingia ndani ya gari, muda si mrefu gari liliondoka.
Joel alitaka kuifuata, lakini polisi wa trafiki walikimbia na kumzuia. “Bwana, naomba uwe makini na magari. Unachofanya ni hatari.”

Joel alikuwa ameduwaa. Wakati huo huo, ni kana kwamba roho yake ilikuwa imepagawa. Je, alikosea? Lakini, mtu huyo alionekana kama Sheryl. Ingawa zaidi ya miaka 2o ilikuwa imepita, alionekana kama alikuwa na umri wa miaka thelathini tu. Mbali na hilo, watu wanaweza kuonekana sawa, lakini kufanana kwa tabia hakuwezi kuwa bandia, sivyo? Alihisi kana kwamba yuko ndotoni na bado hajaamka.

Katika sedan, Lina alihisi woga sana hivi kwamba moyo wake ulikuwa umezunguka kila mahali. Muda si mrefu, Joel alikuwa amepaza sauti akisema, “Humkumbuki Lisa? Yeye ni binti yako.”

Wakati huo, Lina karibu ashindwe kupumua. Kwa bahati nzuri, alisema uwongo na kusema kwamba Lisa alijifanya kuwa binti wa Sheryl na Joel. La sivyo, mambo yangekuwa magumu. Ilikuwa ni bahati kwamba Sheryl hakumkubali Joel au kubishana kuhusu binti yao pia.

Lina alitulia na kukunja ngumi. Hapana, asingeweza kuruhusu Sheryl kupata nafasi ya kumshuku.

"Mama, sasa hivi... huyo alikuwa ... baba yangu?" Lina alisema huku akijifanya kuwa na uchungu.

“Najua.” Sheryl bado alikuwa amepigwa na butwaa, lakini alirudi kwenye fahamu zake haraka. Dharau ilikuwa imeandikwa usoni mwake. "Yeye ni mjinga ambaye anaweza hata kumkosea binti yake wa kumzaa." Baada ya kuongea, alipiga piga nyuma ya mkono wa Lina. “Usijali kuhusu yeye. Hastahili kuwa baba yako.”

Lina alitikisa kichwa. Alijifanya kuwa na akili iliyofunguka na kusema, “Nilikuwa nimekasirishwa sana na jambo hilo, lakini nimefikiria vizuri. Niko sawa maadamu uko hapa, Mama. Isitoshe, sidhani kama Uncle Titus hataki uwasiliane na Joel tena. Uncle Titus anakutendea mema, na ananikubali pia. Sitaki nyinyi wawili mgombane juu yake. Hata kama Joel anamkosea Lisa kama binti yake, ni sawa. Nitalipiza kisasi kwa Lisa hata hivyo. Sihitaji toba yake na msamaha pia. Atatusumbua zaidi tu.”

Sheryl aliitikia kwa kichwa, akajihakikishia. Wakati huo huo, maneno ya Lina yalimkumbusha kwamba anapaswa kukaa mbali na Joel ikiwa angemuona tena. Hakutaka migogoro itokee kati yake na Titus pia.

Baada ya kufikiria kidogo, alimwambia mlinzi aliyekuwa kwenye kiti cha abiria, “Usimwambie Titus kuhusu tukio la leo.”

“Sawa.” Mlinzi alitikisa kichwa kwa heshima.

Hata hivyo, Lina alisema, “Mama, hutaki kumtambua Joel, lakini atakuchunguza. Nadhani bado ana hisia na wewe. Kwa kuongezea, ana ushawishi fulani hapa Nairobi. Akigundua... Itakuwa tabu sana. Labda atajitokeza mbele ya Uncle Titus. Kwanini tusiwe na mtu wa kufuta picha za usalama kando ya barabara na maduka?"
Alipokumbuka kuwa Titus alikuwa mtu mwenye wivu, Sheryl alikubaliana na Lina. Kwa hivyo, mara moja aliamuru mlinzi afute picha zake zote kwenye duka siku hiyo.

Kwa upande mwingine, baada ya Joel kuingia ndani ya gari kwa wasiwasi, dereva alimtupia jicho la woga. "Bado tunaenda kwenye ghala jipya kwa ukaguzi?"

"Hapana." Joel alirudi kwenye fahamu zake na mara moja akampigia simu Lisa. “Uko wapi?”

"Baba, niko ofisini, Mawenzi."

“Rudi kwenye makazi ya familia leo. Nina jambo la kukuambia.” Joel alikata simu baada ya kuongea.

Lisa alikuwa hajasikia sauti nzito kama hiyo kwa muda mrefu. Kwa hali hiyo, hakuthubutu kuchelewa akarudi kwenye makazi ya baba yake baada ya kumaliza kazi yake.

Katika sebule pana Joel alikaa kwenye sofa. Alikuwa na picha mkononi mwake. Alikuwa amezama kwenye picha hiyo hata hakuona kuwa Lisa alikuwa amerudi.

Lisa akatembea. Aliona ni picha ambayo Joel alipiga na Sherry alipokuwa mdogo. Ilikuwa ni picha tamu ya wote wawili wakiwa wamekumbatiana pale uwandani.

"Baba, kweli unayo picha na mama yangu?" Lisa alitabasamu na kumtania. "Sijawahi kukuona ukiitoa hapo awali."

“Siku zote nimekuwa nikiiweka kwenye sefu. Hii ni picha ya mama yako na mimi tukiwa safarini kwenye mbuga ya wanyama alipokuwa na umri wa miaka 20.” Joel akamgusa Lisa usoni kwa uchungu. “Inafanana. Inafanana kabisa.”
"Baba, ni nini kinachofanana? sijakuelewa.” Lisa akaketi kando yake. Hapo ndipo alipogundua kuwa macho ya Joel yalikuwa mekundu. Alipigwa na butwaa.

“Lisa, nadhani nimemuona mama yako leo, lakini hakukubali. ” Joel ghafla alidondosha ukweli wa kushtua.

Lisa alishtuka. "Mama yangu hakuwa amekufa muda mrefu uliopita?"

"Ndio, nilifikiri alikuwa amekufa wakati wote pia." Joel alisema hivi kwa hisia, “Lakini mtu huyo alifanana sana na mama yako. Macho yake, pua na midomo. Nisingekuwa nimekosea. Zaidi ya hayo,” akifikiria juu yake kwa uangalifu, Joel alisema, “mama yako alikumbana na kimbunga mwaka huo, lakini familia ya Jones haikupata mwili wake.”

Moyo wa Lisa ulitetemeka baada ya kusikia maneno yake. Hakika hawakuupata mwili wa Sheryl mwaka huo. Bila maiti, isingeweza kuwa na uhakika wa asilimia 1oo kwamba mtu huyo alikuwa amekufa.

Lisa aliuliza kwa haraka, "Baba, ulizungumza naye?"


“Nilichanganyikiwa sana wakati huo na kumuuliza ikiwa yeye ndiye Sherry. Lakini, alionekana kana kwamba hanijui mimi na kusema nilimchanganya na mtu mwingine. Baada ya hapo, mlinzi alijitokeza na kunisukuma.” Joel alisema kwa uchungu, “Hata hivyo, ilikuwa imepita zaidi ya miaka 20. Niliogopa kuwa huenda nimechanganyikiwa, kwa hivyo niliitafuta picha ya mama yako. Kadiri ninavyoitazama, ndivyo nadhani wanafanana. Tofauti pekee ni kwamba anaonekana mzee na amekomaa zaidi.”

Lisa alishindwa kujizuia kutokana na hisia pia. Ingawa hakuwahi kukutana na Sheryl hapo awali, Sheryl ndiye aliyeanzisha Mawenzi Investments.
Mama yake ndiye mwanamke aliyemvutia zaidi.

 Sura ya: 763

Hata hivyo, Lisa alikuwa mtulivu ikilinganishwa na Joel. “Baba, kwa kuwa unadhani anafanana, hebu tuchunguze. Labda ni kama matukio yale kwenye televisheni ambapo mama yangu anaweza kuwa amepoteza kumbukumbu zake. Kwani, ikiwa angali hai, angewezaje kuwaacha babu na nyanya yangu na familia yake?”

Joel alipigwa na butwaa. “Uko sahihi. Sheryl alikuwa mtu muungwana sana. Ikiwa alikuwa hai lakini hakurudi, lazima kuwe na sababu fulani.

"Jambo la dharura zaidi sasa ni kumpata mwanamke huyo. ” Lisa akauliza, “Ulimuona wapi? Angalia picha za usalama. Alipanda gari gani wakati anaondoka? Alienda wapi?” Aliamini kwamba kwa uwezo wa Joel, kuchunguza mambo hayo ingekuwa rahisi sana.

Joel aliitikia kwa kichwa. Alisimama mara moja. “Nilikutana naye kwenye maduka. Lazima amekuwa akinunua vitu. Nitaenda dukani mwenyewe sasa hivi.”

“Nitakwenda nawe.” Lisa akaenda naye.

Joel aliwasiliana na meneja mkuu wa duka hilo na kumtaka aangalie picha za usalama za jioni hiyo. Lakini, walipokuwa kwenye chumba cha usalama, mfanyakazi huyo alisema, "Picha za usalama za jioni hii zimefutwa."

Joel na Lisa walipigwa na butwaa. Joel aliuliza kwa haraka, “Vipi kuhusu picha za mlango wa duka hilo?”

"Zote hazipo pia." Mfanyakazi akatikisa kichwa. "Sijui ni nini kilitokea, lakini picha za usalama kutoka saa 3:00 alasiri hadi 5:00 jioni zote zimepotea."
Meneja mkuu alimkazia macho mfanyakazi huyo kwa ukali. "Unafanya kazi hapa, na bado hujui kuwa picha zimefutwa?"

Mfanyakazi huyo aliaibika kwa kukosolewa. “Kwa kweli sijui. Nilienda bafuni hapo katikati, na niliporudi sikukuta kitu.”
.
"Naweza kuangalia kompyuta yako? ” Lisa aliuliza kwa upole.

“Bila shaka.” Mfanyikazi huyo mara moja alitoa nafasi kwa Lisa.

Baada ya Lisa kuketi, aliangalia taarifa za mfumo na kusema, “Meneja Mkuu, usimlaumu. Inaweza kuwa ni mdukuzi ndiyo amefanya. Wadukuzi hao waliweka virusi kupitia mtandao wa umma wa duka hili, wakavamia kompyuta ya chumba cha usalama, na kufuta picha hizo.”

Meneja mkuu alishtuka. "Huyu mdukuzi asingeweza kudukua akaunti ya kampuni, sivyo?"

“Usijali. Mdukuzi huyu alitaka tu kufuta picha za usalama. Zaidi ya hayo, mdukuzi kama huyu anapaswa kuwa mmoja wapo wa juu kimataifa. Mshindani wa duka lako bado hana uwezo wa kuajiri mtu kama huyo.”

Joel na Lisa walitoka nje baada ya kumshukuru mkurugenzi mkuu. Uso wa Joel ulikuwa mzito. “Lisa, inawezaje kuwa bahati mbaya? Kufikiria tu picha za usalama tumekuta zilifutwa kwa wakati kama huo?”

Lisa hakusema chochote. Alikuwa na mengi akilini mwake.

Hata hivyo, Joel hakuwa tayari kukata tamaa. Alisema, "Lazima kuwe na kamera za usalama kando ya barabara. Twende kwa idara ya polisi wa trafiki.”

“Baba, huoni kwamba upande mwingine umefikiria hivyo pia? Nadhani hata ukienda, zinaweza kuwa zimefutwa pia." Lisa alimtazama baba yake kwa kutojiweza na kukata tamaa. “Ulichosema sasa hivi kilikuwa sawa. Hakuna bahati mbaya, ni mchezo dhahiri.”

Ingawa Joel alikuwa amekata tamaa, haikumaanisha kuwa alikuwa mpumbavu. Uso wake wa kifahari ulijawa na mkanganyiko na tamaa.

Lisa pia alikata tamaa. Lakini, alisema, "Kwa kweli, ikiwa tulikuja kuchunguza na picha za usalama zingekuwa bado zipo, hiyo ilimaanisha kuwa mtu huyo anaweza kuwa sio mama yangu. Lakini, kwa kuwa picha za usalama zimetoweka, inamaanisha kuwa hawataki uendelee kuzichunguza. Kwanini hivyo? Labda ni kwa sababu ... mashaka yako ni sawa. Huyo mwanamke ni mama yangu kweli. Alikutambua jioni ya leo lakini hakutaka kuwa na uhusiano wowote na wewe au kukuruhusu uchunguze suala hili.”

Joel alionekana kushindwa. Alikuwa mpweke sana na katika uchungu. “Uko sahihi. Nilichofanya wakati huo kilikuwa cha kinyama. Ukweli kwamba Nina alikuwa akinidanganya hata ikawa habari kwa umma. Kila mtu ananidhihaki na kunikemea kama mjinga. Mama yako ni mtu mwenye kiburi, hivyo lazima anidharau na kunichukia. Ni sawa ikiwa hatanitambua, lakini wewe ni binti yake wa kumzaa. Je, hataki kukukubali?”

Maneno yake yaliuchoma moyo wa Lisa.
Alikuwa akifikiri John Jones na mkewe walikuwa wazazi wake, lakini ikawa sivyo. Lisa alijifariji kuwa mama yake hakumtelekeza makusudi. Mama yake alikuwa amekwenda kwa sababu ya ajali. Hata hivyo, je, hakutamani upendo wa kimama pia? Yeye pia aliutaka! Lakini, baada ya makumi ya miaka ya kwenda bila upendo wa mama, asingeweza kulazimisha ikiwa mtu mwingine hataki. Baada ya yote, Lisa alikuwa amepitia zaidi ya miaka 20 bila mama, na alikuwa na ujasiri zaidi kuliko wasichana wa kawaida wa umri wake.

"Baba, mama amepotea kwa zaidi ya miaka 20, sio miaka mitano au sita, au mwaka mmoja au miwili. Mambo mengi yanaweza kutokea katika miaka 20, kama vile kujenga familia na kazi na kuzaa mtoto. Ulisema mwenyewe kuwa alikuwa na mlinzi naye, kwa hivyo lazima awe na utambulisho usio wa kawaida. Aidha, hujawahi kukutana naye kabla licha ya kuwa umeishi Nairobi kwa muda mrefu. Hii inamaanisha kuwa amekuja Nairobi hivi majuzi. Labda amekuwa akiishi ng’ambo muda wote.” Lisa bila huruma alifichua mambo fulani.

Joel alicheka kwa uchungu. “Uko sahihi. Hata nilioa na kuachwa pia. Ikiwa mama yako bado yu hai, anawezaje kuwa bado hajaolewa? Nakumbuka nilipokutana naye jioni, kulikuwa na msichana kando yake. Sikumuangalia kwa uangalifu, lakini msichana huyo alionekana kama yeye. Labda huyo alikuwa binti yake.”

“Je! Basi hakika ni binti yake.” Lisa alitabasamu kwa utulivu. Lakini, kwa kweli, alijisikia vibaya sana. Alikuwa na mama pia, lakini mama yake alikuwa na familia nyingine na mtoto.

Angewezaje kuliweka kwa maneno? Ikiwa angetokea ghafla na kumwita mama yake 'Mama', anaweza kuwa 'mzigo wa ziada' ambao watu walimaanisha, sivyo?

“Baba, sahau. Labda hataki kuwa na mahusiano zaidi na maisha yake ya zamani. Je, ikiwa tunasisitiza kuchunguza na kuishia kukutana na mumewe? Hakika angesumbuliwa na ukweli kwamba alikuwa na mtoto hapo awali. Labda hiyo ingeathiri hata ndoa yake ya sasa. Wacha tuichukue kama vile mama yangu alikufa zaidi ya miaka 20 iliyopita.”  
Ni kwa kufikiria hivyo tu Lisa angeweza kushinda.

Moyo wa Joel ulimuuma sana, akajiona mwenye hatia. Binti yake alikuwa na akili sana. Asingeweza kamwe kuwasumbua wazazi wake, na pia hakuomba chochote kutoka kwa wazazi wake. Hata hivyo, hilo lilimfanya ahisi kuwa ana deni lake zaidi.

“Lisa, mama yako si mtu wa aina hiyo. Hakika anakupenda. Labda ni kama vile ulivyosema. Hakumbuki.”

"Ikiwa hatukumbuki, kwanini arudi na kufuta picha za usalama?" Midomo ya Lisa ilipinda. "Baba, watu wanabadilika."

Ghafla Joel hakujua la kusema. Alikuwa amepotea tu. Je, ni kweli Sheryl alikuwa ameolewa? Ili kuficha maisha yake ya zamani kwa ajili ya familia yake nyingine, angependelea zaidi kutomtambua mtoto wake na familia ya akina Jones?

Akitazama sura ya baba yake iliyopotewa na akili, Lisa alisema, “Kwa kweli, bado kuna njia ya kuthibitisha kama yeye ni mama yangu au la. Ni rahisi sana. Kwa kuwa amerudi, labda ataenda Dar es Salaam kutembelea na kusafisha kaburi la babu na bibi yangu ikiwa bado ana dhamiri fulani. Tutajua kama kuna dalili kwamba kaburi limesafishwa.”

Macho ya Joel yalimtoka na kukaa kimya. Lisa hakuzungumza pia. Kwa kweli, hakutaka kujua. Ikiwa angejua zaidi, angehisi kwamba mama yake alikuwa amemtelekeza.

Lakini, Lisa hakumlaumu pia. Kama mama, Sheryl tayari alikuwa ameunda na kuirithisha Mawenzi Investments kwa Lisa na kutimiza majukumu yake. Lisa hakuweza kuomba sana kutoka kwake..... ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA...