AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................752-753
Sura ya: 752
"Mbona unashobokea sana?" Pamela alipiga kelele. “Una wivu?”
"Pfft. Nina wivu?" Rodney alipandwa na hasira. “Kwani nina ubaya gani mimi kuwa na wivu? Siwezi kupata wivu kwa sababu ya mke wangu?”
Pamela alipigwa na butwaa. Hii ilikuwa kinyume na matarajio yake. Alifikiri Rodney angekataa vikali, lakini ...Uso wake ulikuwa ukiwaka kwa aibu badala yake.
Rodney alihisi kufedheheshwa mwanzoni, lakini mara tu alipomuona akiona haya bila kusema neno, hisia ya unyonge ndani yake ikatoweka mara moja. "Hata hivyo, kumbuka maneno yangu. Hili likitokea tena, nitamtafuta Patrick na kumwambia kwamba unamtumia.”
Pamela alihisi kuongezeka kwa hisia kifuani mwake. " Vyovyote vile. Nenda huko. Ninataka kumpigia Lisa.”
“Siondoki. Nani anajua kama utachukua nafasi hiyo kumpigia simu Patrick nikigeuka.” Rodney moja kwa moja akavuta kiti na kuketi juu yake.
Alikumbuka kusikia Pamela akiongea na Patrick kwa upole kwenye simu muda si mrefu, lakini kwake, alipiga kelele au kufoka. Ni tofauti gani kubwa katika jinsi alivyowatendea.
“Utajua mwenyewe. ” Pamela alikata tamaa nae. Kwa hiyo, alimfumbia macho na kumpigia simu Lisa. “Patrick alinipigia simu tu na kusema kwamba Linda alienda Zenith Club. Muda mfupi baadaye, Lina na Cindy walijitokeza pamoja.”
"Kweli ni yeye." Lisa alizidiwa na dhiki. Alitumaini dhana yake haikuwa sahihi, lakini ikawa kwamba alikuwa sahihi. "Cindy alienda pia?"
“Cha ajabu nini hapo? Lina amekuwa karibu na Cindy tangu walipokuwa Dar.” Pamela alisema kwa mkoromo, “Lina hakika anajua kwamba Cindy ataolewa na Chester, kwa hiyo anataka kumweka karibu kwa vile atakuwa na nguvu kubwa.”
“Tayari tuna chuki na watu hawa watatu. Sarah akiungana nao pia...” Lisa kichwa kilimuuma.
“Una mpango gani? Kwanini tusiende kwenye Zenith Clabu na kumkamata Lina ili kumchunguza? ” Pamela alipendekeza kawaida.
“Sawa.”
“Huh?” Pamela alishtuka, akidhani kwamba amesikia vibaya. “Nilikuwa natania. Nilidhani usingetaka kupiga kengele sasa.”
“Kwa kweli sikutaka. Lakini nilipoweka watu wa kuwafuatilia Mzee Jones na Mkewe mara ya mwisho, Logan na Austin waliishia kujeruhiwa. Je, ikiwa kitu kitatokea kwa watu wanaomfuatilia tena wakati huu? Sitaki kutoa kafara mwanachama yeyote wa ONA. Ningeweza kwenda kukutana na Lina sasa. Kwa sasa, ninaweza pia kujua jinsi alivyo na nguvu.”
Lisa aliongeza, “Malizia upesi mlo wako. Tutaelekea huko pamoja baadaye.”
"Sawa."
Pamela alitikisa kichwa mara moja.
“Mwelezee hili Rodney. Sikutaka kukuingiza kwenye hili mwanzoni kwa sababu wewe ni mjamzito, lakini ... nina wasiwasi kwamba ikiwa sitakwenda pamoja na wewe, huenda nisiweze kuondoka mahali hapo nikiwa mzima, " Lisa alieleza kinyonge.
"Naelewa."
Baada ya kukata simu, Pamela alielekeza macho yake kwa Rodney kwa shida.
Rodney alionekana kuwa na huzuni kwani pengine alikuwa ameupata ujumbe huo. "Unapanga kuelekea Zenith Club na tumbo lako linalochomoza?"
“Mimi ni mtoto wa kike wa Rais mtarajiwa. Kwa hadhi yangu, hakuna mtu ambaye atathubutu kunifanyia chochote,” Pamela alieleza huku akikunja uso. "Lazima niende huko usiku wa leo."
“Sikuelewi. Hii ni biashara ya Lisa. Kwanini unalazimisha kujiingiza kwenye fujo hili?” Rodney hakuweza kujizuia kulalamika.
“Alvin ni rafiki yako. Sasa kwa kuwa Lina anataka kumlenga, utamtazama anaposhuka tena na kupotea?” Pamela aliuliza.
Rodney mara moja akanyamaza. Ni baada tu ya Pamela kuingia nyumbani na kumaliza chakula chake ndipo aliposema bila msaada, "Unaweza kwenda, lakini lazima nikufuate." Pamela alimtupia jicho na kutikisa kichwa mwisho.
Dakika 4o baadaye, Lisa aliendesha gari hadi nyumbani kwa Pamela.
Baada ya kuingia ndani ya gari, Rodney aliinua uso wake. “Mbona uko peke yako? Je, Alvin haendi?”
"Polisi wako KIM International tena, na amefungwa kwa sasa. Sikumwambia, asije akahangaikia hilo,” Lisa alijibu.
"Usipomwambia, atakuwa na wasiwasi zaidi ikiwa kitu kitatokea," Rodney alisema kwa mshtuko.
“Sawa, nina ninyi wawili pamoja nami.” Lisa alitabasamu. "Haijalishi Lina anaenda umbali gani, naamini hatakuwa na ujasiri wa kutosha kushambulia familia ya Shangwe. Zaidi ya hayo, amelala chini kwa muda mrefu kabla ya kurudi. Nadhani anapanga kunitesa kidogo kidogo na kunivua kila kitu kabla hajanisukuma shimoni. Haitakuwa na maana kwake kuniua mara moja.”
Rodney alimpiga Lisa sura ngumu. Alihisi kuwa Lisa amekuwa hatabiriki na kuwa mjuzi wa kufahamu kilichokuwa kwenye akili za watu sawa na Alvin.
Alipofika Zenith Clubhouse, Rodney aliangaza kadi yake ya uanachama. Kisha, walipitia ukaguzi kadhaa wa usalama kabla ya kupanda lifti hadi ghorofa ya juu.
"Ni mara yangu ya kwanza hapa, lakini pana ulinzi mkali sana." Pamela alipumua na kumwambia Rodney, “Wewe pia una jumba la klabu, sivyo? Haionekani kuwa kali kama mahali hapa."
Rodney alijibu kwa hisia tofauti, “Kwa sababu mmiliki wa jumba hili la klabu si mtu wa kawaida.”
“Ni nani?” Lisa aliuliza kwa udadisi.
"Mjukuu wa Rais wa sasa, Brian Zalongwa." Rodney alisema, "Ingawa yeye ni mdogo wangu wa miaka miwili, yeye sio mtu wa kawaida. Alitaka hata kushindana na ba’mdogo wangu kugombea uRais mwanzoni, lakini
kwa bahati mbaya, yeye ni mdogo sana kikatiba. Baada ya ba’mdogo wangu kujiuzulu, Brian na Ian bila shaka watagombea wadhifa huo katika uchaguzi ujao.”
Pamela alipigwa na butwaa. Alipata jambo hili tata. Rodney aliendelea bila kujali, "Kwa Shangwe Corporation kama msaada mkubwa, familia ya Shangwe ina makali juu ya Brian. Baada ya kusema hayo, Brian anajishughulisha na watu wengi matajiri, na hii ndiyo klabu ambayo anawahudumia. Ndiyo maana sisi huja hapa mara chache sana.”
"Lakini Lina na Cindy walikuja hapa pia," Lisa alisema ghafla, "Je, Lina angewezaje kufahamiana na Brian?"
Rodney akatikisa kichwa huku amekunja uso. “Kutokana na kwamba Brian ni msiri sana, hatajisumbua kuchangamana na watu ambao anawaona hawana thamani. Hatatenda kwa msukumo kwa ajili ya mwanamke pia. Mbali na hilo, amejaribu kufanya urafiki na Alvin hapo awali. Ingawa Alvin amekuwa vuguvugu kwake, hatakuwa mjinga kiasi cha kumshambulia Alvin.”
Lisa alikataa maoni yake. "Itakuwaje ikiwa Brian atavutiwa na nguvu iliyo nyuma ya Lina?"
Rodney alinyamaza papo hapo.
Mara lifti ilipofika kwenye ghorofa ya juu, wote watatu wakatoka nje. Hii ilikuwa ni ghorofa ya juu kabisa katika Nairobi yote, na Lisa alionekana kuwa alielewa kwanini mahali hapo pakaitwa Zenith Club. Kusimama hapa kulimfanya ahisi kana kwamba alikuwa kwenye kilele cha anga. Vyombo vyote hapo vilikuwa na thamani ya mamia ya mamilioni ya pesa.
"Bwana Shangwe, ni nini kinakuleta Zenith Club?" Meneja wa kike mrembo alimsogelea Rodney huku akitabasamu. Alipowaona Pamela na Lisa, alipigwa na butwaa. "Hata ulimleta Madam Shangwe na Bi Jones pia?"
Lisa alishangaa kwa siri. Meneja huyu wa kike hakuwa mtu rahisi, ikizingatiwa kuwa angeweza kuwatambua mara moja.
Rodney alishika kiuno cha Pamela na kusema kwa tabasamu, “Tulikuwa tunapita eneo hili. Mke wangu alisema hajawahi kuingia Zenith Club, na angependa kufurahiya na rafiki yake wa karibu, kwa hivyo nikawaleta hapa.”
Sura ya: 753
Pamela alijisikia vibaya kwa jinsi Rodney alivyokuwa akimkumbatia hadharani. Hata hivyo, alijua tabia ya Rodney ilikuwa ya kujionyesha tu, hivyo hakumsukuma.
“Unampenda sana mke wako, Bwana Shangwe.” Meneja wa kike alikuwa mtu mwerevu. Alisema huku akimsifia, “Umebarikiwa sana, Bibi Shangwe.”
Pamela alipumzika bila kusema neno lolote. Watu kama vile meneja wa kike wangefahamu kilichotokea kati ya Rodney na Sarah hapo awali, lakini bado alizungumza kwa utamu na Pamela. Pamela asingeweza kuwajali sana.
“Halafu, niliona gari la Bwana Zalongwa chini. Kwa kuwa nipo hapa, naomba niende nikamsalimie. Yuko wapi?” Rodney alidanganya, akijaribu kumchunguza meneja. Kwa kweli hakuiona gari ya Brian.
Meneja wa kike alisema huku akitabasamu, “Baadhi ya marafiki zake wapo hapa, kwa hiyo amekwenda kuwasalimia.”
“Oh, sawa. Huenda nawafahamu marafiki zake pia,” Rodney alijibu huku akitabasamu.
Lisa ghafla alisema kwa upole, "Tusiwasumbue."
"Ndio," Pamela alinong'ona, "nilitaka kutazama pande zote."
“Hujui chochote. Huu ni uungwana wa kawaida.” Rodney alisema kwa mkoromo, “Unajua Bwana Zalongwa ni nani? Ni mjukuu wa Rais.”
Sura ya butwaa iliangaza usoni mwa Pamela. "Basi tungeweza kumsalimia."
Baada ya kufikiria kidogo, meneja wa kike alitikisa kichwa. "Yuko kwenye ghorofa ya pili. Ngoja niwapeleke huko.” Alipomaliza kusema tu, alitangulia mbele.
Rodney alisogea karibu na sikio la Pamela kutoka nyuma na kumnong'oneza kwa tabasamu, "Haya, huoni kwamba tunafanya kazi pamoja vizuri?" Akauweka mkono wake kiunoni mwake na kunong’ona maneno yale ya kichochezi sikioni mwake.
Wakati huo, Pamela alihisi kutetemeka. Kadiri alivyojaribu kujinasua kutoka kwake, Rodney alikuwa ameshika kiuno chake. “Acha kuzunguka. Tusipoigiza kama njiwa, watu wengine wanaweza kutushuku.”
Pamela alimwangazia kwa siri. Hakuweza kuelewa ni kwanini ilimbidi aigize mapenzi naye kana kwamba alikuwa jasusi wakati, kwa kweli, alikuja tu kwenye klabu ya usiku kwa ziara.
Muda si muda, meneja huyo wa kike alisimama mbele ya chumba cha faragha na kubisha hodi kwa urahisi.
Mwanamume aliyeonekana kama mlinzi haraka akafungua mlango. “Unamtafuta nani?”
“Namtafuta Bwana Zalongwa. Mimi ni rafiki yake.” Rodney alimsukuma mlinzi na kuingia ndani. Alikimbia moja kwa moja hadi kwa mtu aliyekuwa ameketi katikati ya kochi na kumsalimia kwa shauku, "Hi, BwanaZalongwa. Ni muda umepita tangu tukutane.”
Alipogundua kuwa Rodney alikuwa marafiki na Bwana Zalongwa, mlinzi alishusha ulinzi wake. Lisa na Pamela pia walichukua fursa hiyo kuingia kwenye chumba cha faragha. Kulikuwa na watu wanne tu ndani ya chumba hicho kikubwa. Kati ya watu hawa wanne, Lisa alimjua kila mtu isipokuwa Bwana Zalongwa. Watu watatu aliowafahamu ni Cindy, Linda, na... Lina.
Siku hiyo, Lina alikuwa amevaa mavazi ya maxi nyekundu na yalimtoa vizuri zaidi kuliko miaka mitatu iliyopita. Uso wake ulikuwa bado uleule kwa mtazamo wa kwanza,lakini, ukiangalia kwa karibu, alikuwa tofauti kabisa na hapo awali. Ni wazi kwamba alikuwa amefanyiwa upasuaji wa plastiki. Ingawa alionekana mrembo mwenye kidevu kilichochongoka kama ncha ya yai, alionekana mkaidi na asiye wa kawaida ikilinganishwa na Cindy aliyekuwa kando yake.
Lina alielekeza macho yake kwa Lisa, na sura yake ikabadilika kidogo.
Hata hivyo, midomo yake myekundu punde ilijikunja na kutabasamu. Hakutarajia Lisa angegundua mahali alipokuwa mapema namna ile. ilimfanya kushangaa kidogo, lakini haikumuathiri sana.
Kinyume chake, Cindy na Linda walionekana kushangazwa na ujio wa Lisa na Pamela.
"Bwana Mdogo Shangwe, ni nini kinakuleta Zenith leo?" Brian alimpiga Rodney begani kwa tabasamu. Walionekana kuwa wa kirafiki.
"Nadhani Bwana Shangwe na mkewe walikuja hapa kunitafuta."
Midomo ya Lina ilijikunja na kutabasamu. Akiwa ameshika glasi ya mvinyo mwekundu, alimtazama Lisa kwa dharau na kumpandisha. "Nashangaa jinsi ulivyojua kuwa niko hapa."
Uso wa Brian uliganda. Kisha, akahamishia macho yake ya kuchanganyikiwa kwa Rodney. "Bwana Mdogo Shangwe, huyu ..."
"Bwana Zalongwa, inaonekana kama rafiki yako anamjua mke wangu." Rodney alijifanya anaonekana kushangaa.
“Bwana Shangwe, acha kujifanya. Sio tu kwamba tunafahamiana, lakini pia tumejuana muda mrefu sana.” Hakuweza kujisumbua kucheza naye, Lina alisema bila kuficha, “Binamu yangu mpendwa, umepokea barua niliyomwomba mtu akutumie?”
“Ndio. Sikutarajia ungekuwa muovu kiasi hicho kuharibu kaburi la shangazi yako wa damu.” Lisa akamsogelea Lina. Tabasamu lilitanda usoni mwake huku akimwangalia Lina. "Umekua mkatili zaidi katika miaka minne ambayo umekuwa mbali. Bado wewe ni mbaya kama zamani."
Uso wa Brian ulitiwa giza, kisha akanguruma, "Afadhali uangalie maneno yako."
Lisa alikunja uso, na Rodney mara moja akauliza, “Bwana Zalongwa, kuna nini? Huyu ni mwanamke mpenzi wako?"
"Ninajaribu kumfanya awe mpenzi wangu." Brian akajibu kwa tabasamu lisilo na furaha, “Ndiyo maana nyinyi watu mnapaswa kumtendea kwa heshima.”
Aliposikia hivyo, Lina alicheka kwa hasira. Mara moja Linda alitabasamu na kusema, “Lisa, unafikiri bado unaweza kumdhulumu Lina kama ulivyokuwa unamfanyia? Bwana Zalongwa, ikiwa kweli una nia ya kumchumbia Lina, unahitaji kushughulika na Miss Jones usiku wa leo. Kama si yeye, Lina asingelazimika kujificha ng'ambo.”
Lina alinyamaza kimya akimaanisha kukubaliana na maneno ya Linda. Brian alijibu kwa tabasamu, "Hicho ni kipande cha keki."
Kwa hivyo, sauti yake iligeuka kuwa baridi. "Walinzi..."
"Bwana Mkubwa Zalongwa." Baadaye, walinzi wachache waliingia.
Brian alimwelekezea Lisa kwa kidevu chake. "Mtendeeni vizuri Bi Jones."
"Bwana Zalongwa, unajaribu kufanya nini?" Rodney alisimama mbele ya Lisa, uso wake ukigeuka kaburi. "Wacha nikukumbushe kuwa yeye ni mwanamke wa Alvin Kimaro."
“Alvin Kimaro?” Brian alitoa dharau. "Familia ya Kimaro itatoweka kutoka eneo la Kenya kwa muda mfupi. Kwa nini nimjali?”
“Lakini unaamini kwamba nitakufanya utoweke kabla hajatoweka?” Lisa aliuliza kwa sauti ya kutojali, lakini, macho yake yalikuwa baridi na ya kutoboa.
Pamela alishtuka kwa hofu. Lisa anathubutu vipi kusema maneno kama haya mbele ya Brian? Alikuwa akichukua maisha yake mikononi mwake.
Hata Rodney hakuweza kujizuia kuinua kidole gumba kana kwamba anasema, “Unashangaza.”
"Ulisema nini?" Brian alicheka mara moja.
Hata hivyo, kicheko chake kilijaa uovu na mshangao.
Lisa alimtazama Lina aliyekuwa akitazama tamthilia hiyo. "Ingawa sijui ni kwanini mjukuu wa Rais amechagua kupendelea mwanamke huyu ambaye amefanyiwa upasuaji wa plastiki, nadhani inahusiana na mtu aliye nyuma yake. Nina hakika mtu huyu si MKenya wala Mtanzania. Lakini, unahitaji kuwa wazi kuwa hii ni Kenya. KIM International inaweza kuchunguzwa wakati huu, lakini halijasambaratika wala kushtakiwa kwa lolote. Bado ninaweza kushughulika nawe mradi KIM International iko karibu. Ikiwa unataka kushughulika nami, endelea. Lakini hakuna haja ya haraka kuchukua muda wako. Sio lazima uifanye leo. Vinginevyo, unaweza kuishia kupoteza kila kitu huku mtu mwingine akifurahishwa nacho.”
Brian alikuwa amezoea kuwa na watu wanaompambapamba na kujipendekeza kwake. Lisa alichukuliwa kuwa mtu wa kwanza ambaye alikuwa na ujasiri wa kumkasirisha kwa njia hii. Uso wake ulikunjamana kwa hasira. Alitamani ampige kofi la kifo pale pale. Hata hivyo, maneno ya Lisa yalikuwa tishio sana kwake....... ITAENDELEA......
Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA...
