JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU YA................................682-683

Sura ya: 682

Kwa hofu, Sarah akampiga jicho kali na kumtazama kwa haraka. Kwa kadiri alivyojua, Kelvin kwa sasa alikuwa chini ya huruma ya familia ya Choka na kwenye kona kali. Je, angefanya nini ambacho kinaweza hata kumfanya Chester ashindwe kukabiliana naye?
Alifungua kinywa chake kwa kusitasita. "Huenda usijue uwezo wa kweli wa familia ya Choka. Hata kama Mason atakabiliana na familia ya Choka, hatakuwa na makali juu yao...”
“Najua. Hivi karibuni, utaelewa. ” Kelvin alitoa tabasamu baridi.
Akiwa ameingiwa na mawazo, Sarah akauliza ghafla, “Ulisema mimi ni mwanamke wa pili katili zaidi uliyekutana naye, kwa hiyo unamaanisha kwamba kuna mwanamke mwingine ambaye ni mkatili kuliko mimi?
"Nadhani nyote wawili hamna huruma sawa. Pia... Kwa bahati mbaya, anawachukia Alvin na Lisa pia,” Kelvin alijibu kwa tabasamu lisilo na furaha.
Sarah mara moja akanyamaza. Mwanamke huyu anaweza kuwa nani? Lakini, kwa kuwa walikuwa na maadui sawa, wangeweza kufanya kazi pamoja katika siku zijazo.
•••
Lubumbashi Kongo. Casino Royale Resto Terrasse.
Zamani likiitwa jiji la Elisabethville, Lubumbashi ni jiji la pili kwa ukubwa nchini Kongo, na pia ni bandari ya nchi kavu. Mtu tajiri zaidi aliyekuwa anayedhibiti jiji hili aliitwa Titus Tshombe. Sio tu kwamba familia ya Tshombe ilikuwa na udhibiti wa mauzo ya madini ya Colbat ulimwenguni, lakini pia ilidhibiti migodi ya chuma, copper na Zinc huko Katanga, walimiliki mahoteli makubwa ya kifahari karibu miji mikubwa yote nchini Kongo, na mnyororo wa mabenki yao pia ulikuwa na matawi hadi Ulaya.
Kwa wakati huo, mwanamke wa Kitanzania tayari alikuwa ameshinda pesa nyingi kwa kucheza kamari siku tatu mfululizo kwenye kasino kubwa zaidi ndani ya jiji la Lubumbashi, Casino Royale Resto Terrasse, iliyomilikiwa na familia ya Tshombe.
Nywele nene, za rangi ya hudhurungi na sifa nzuri za mwanamke huyu zilisababisha wanaume wengi kutoka sehemu mbalimbali za dunia waliokuwa wakicheza kamari ndani ya Casino hilo kumlemea. Mwanamke huyu hakuwa mwingine ila Lina Jones, ambaye alikuwa ametoweka kwa miaka mingi.
"Samahani, nimeshinda tena." Lina alifungua kadi yake ya mwisho kwa namna ya moyo mwepesi. Chini ya macho ya umati wa watu, alijikongoja na sura yake iliyopinda.
Alikuwa hapo kwa wiki moja. Kabla hajaja, alikuwa ametumia pesa nyingi kumwajiri mcheza kamari mmoja ili kumfundisha ustadi fulani wa kucheza kamari ili tu ashinde. Lakini, ikiwa angeendelea kufanya hivi, hakika asingeweza kushinda tena kesho yake.
Kwanini mtu huyo alikuwa bado hajajitokeza? Je, Kelvin angeweza kumdanganya? Hapana. Hata kama angeachwa na nafasi ya mwisho, ilimbidi atende kulingana na mpango. Hakuweza kumudu kufanya makosa.
Lina hakujua kwamba kulikuwa na mtu amesimama nyuma ya dirisha la kioo kwenye ghorofa ya tano, akimwangalia akiondoka. Mtu huyo aliingiza mikono yake mfukoni kwa utulivu. Taa zilizokuwa juu yake ziliangazia nywele zake za mtindo wa Ras zilizoanguka juu ya mabega yake. Wanaume wengi walimtazama, hakuwa na mvuto mwenye nywele zake ndefu zilizosokotwa, lakini alikuwa na sura ya kuvutia iliyofanana na ya shetani.
Hata hivyo, mtu yeyote ambaye angemwona angejawa na woga kwa sababu ya macho yake ya ajabu ya ukungu. Macho yake yangeweza kupelekea mtu kuwa na baridi hadi kwenye uti wake wa mgongo.
Kila mtu alijua kwamba tajiri mkubwa wa Lubumbashi, Titus Tshombe, alikuwa na aina hiyo ya macho. Mtu huyo alikuwa mwana wa Titus, Matthew Tshombe—mrithi wa baadaye wa familia ya Tshombe.
“Bwana Mkubwa..” Mhudumu alitembea. “Nimeulizia kuhusu hilo. Jina lake la mwisho ni Jones, na alitoka Tanzania.
“Jones?” Mathew alikodoa macho taratibu. "Hufikirii ... anafanana na mama yangu?"
Baada ya kukaa kimya kwa muda, msaidizi alijibu, "Baada ya kumtazama kwa karibu, nadhani alifanyiwa upasuaji wa plastiki hapo awali. Pengine aligundua sura ya Madam na kufanyiwa upasuaji wa plastiki ili kufanana naye.”

"Mama yangu haonyeshi uso wake hadharani, hakuna mtu aliyewahi kumuona. Isitoshe, maneno na tabia yake ni kama ya mama yangu pia.” Matthew alisema kwa sauti ya kutatanisha, “Mama yangu aliniambia kwamba alijifungua mtoto kabla hajafika Kongo. Hii inamaanisha kuwa nina dada wa kambo huko Tanzania ambaye anashea mama mmoja na mimi.”
“Unashuku kuwa ni yeye?” Mhudumu alishangaa.
“Waambie wafanyakazi wa hoteli watafute njia ya kupata nyuzi mbili za nywele zake. Ninataka vipimo vya DNA vifanyike kwa ajili yake na mama yangu haraka iwezekanavyo. Nataka kujua matokeo kesho asubuhi.”
Baada ya Mathew kutoa agizo hilo, aligeuka na kuondoka.
Kulipopambazuka asubuhi iliyofuata, msaidizi alimwendea na matokeo. “Bwana Mkubwa, ikawa kweli ana uhusiano na wewe. DNA yake ni sawa na asilimia 90 na ya mama yako. Hii pia inamaanisha kuwa hakika una uhusiano naye. ”
Mathew alichukua ripoti ili kuangalia. Macho yake yalionyesha sura ya furaha. Ikiwa mama yake angejua kwamba alikuwa amempata binti yake aliyepotea kwa muda mrefu, angefurahi sana. Mara moja alichukua ripoti na kuchukua ndege ya haraka hadi Paris Ufaransa, jiji ambalo wazazi wake waliishi kwa miaka mingi.
Baada ya kujua mahali alipo mama yake, mara moja alielekea kwenye bwawa lililo nyuma ya jumba.
Wenzi hao wa ndoa walikuwa wakivua samaki kando ya bwawa. Licha ya kuwa katika umri wao wa makamo, wawili hao walidumisha sura ya ujana. Mwanamke huyo alikuwa mzuri, wakati mwanamume alikuwa mtanashati sana. Wote wawili walionekana kana kwamba walikuwa na miaka 30 tu licha ya kwamba walikuwa wakikaribia kuingia miaka ya 5o.
“Mpenzi, usiweke macho yako kwenye fimbo ya kuvulia samaki. Niangalie." Kwa wakati huu, Titus, tajiri mkuu wa Lubumbashi, alikuwa mbali na kiburi na kutawala kama jinsi wengine walivyomwona kuwa. Alimng'ang'ania mke wake kama kupe na ng’ombe.
“Nyamaza na ukae kimya. Usiongee samaki wangu atakimbia.” Sheryl alimpiga Titus mng’ao mkali.
Titus alipepesa macho kwa huzuni. "Wewe, unanipenda mimi au samaki zaidi?"
Sheryl alikosa la kusema. “Wewe bado ni mtoto katika uzee huu. Acha ujinga."
“Mimi ni mzee hivyo? Ninahisi nina umri wa miaka 30 tu,” Titus alijibu kwa tabasamu.
Sheryl alishindwa cha kusema.
“Mama...” Mathew alimkimbilia kwa haraka.
Titus alimtupia jicho la dharau. “Mbona umerudi? Si tulikuambia ubaki Kongo usimamie biashara ya familia yetu? Siku zote unasafiri kwenda na kurudi.”
Kwa kudharauliwa na baba yake, Mathew alikosa la kusema. Alijihisi kana kwamba ni zawadi ambayo mama yake alimpa baba yake na hakukaribishwa hata kidogo.

Kwa mawazo kwamba baba yake angejisikia vibaya baadaye, Matthew alifurahi sana.
"Mama, nina kipande cha habari ya kushangaza kwa ajili yako wakati huu." Uso wa Matthew ulijawa na msisimko.
"Habari gani?" Sheryl alimtazama kwa mshangao.
“Nilimpata mtoto uliyemzaa hapo awali. ” Mathew alipomaliza kusema tu, Titus alimvuta kola.
“Umesema nini?” Macho ya Titus yalimfanya aonekane kuwa anataka kummeza Mathew.
“Shoo! ” Sheryl alimsukuma Titus. “Uliponioa, uliahidi kwamba utamkubali mtoto wangu mwingine ikiwa nitampata baadaye.”
Mdomo wa Titus ulining’inia, na uso wake ulionyesha masikitiko yake.
“Usijali, nitamkubali mtoto tu na sitakuwa na uhusiano wowote na mpenzi wangu wa zamani,” Sheryl alisema kwa sauti laini.

Sura ya: 683

Hapo ndipo uso wa Titus ulipolainika. “Sawa basi. Huwezi kuwasiliana na mtu huyo, ama hakika nitaharibu familia yake.”
Sheryl alimuangalia Mathew kwa shauku bila kusumbuliwa na Titus.
"Mama, angalia." Mathew alimkabidhi ripoti mbili za vipimo vya DNA. “Hivi majuzi, kulikuwa na mwanamke ambaye alitembelea kasino kwenye hoteli yetu na kushinda siku tatu mfululizo. Yeye ni kipaji kabisa. Nilipoenda kukagua, nilimwona na mara moja nikafikiri kwamba anafanana na wewe. Kwa hiyo nilimwomba mtu achukue nywele zake kwa kipimo cha DNA.”
Baada ya kuangalia taarifa hizo, Sheryl alifurahi sana. "Ilitokea kwamba nilizaa binti wakati huo. Fanya haraka umlete, Mathew.”
“Subiri, wifey. Ninaona ni ajabu kidogo," Titus alisema, "Kwanini alijitokeza kwenye kasino na kucheza kamari kwa siku tatu mfululizo? Inaonekana alikuwa anajaribu kuvutia umakini wa mtu.”
“Lakini matokeo ya uchunguzi wa DNA hayawezi kuwa na makosa. Hata ikiwa ana nia mbaya, tunaweza kujua kwa kumuuliza.” Sheryl hakuweza kusubiri kukutana na binti yake. “Hubby, natumai unaweza kuelewa. Yeye si tu binti yangu wa damu bali pia daraja pekee kati yangu na wazazi wangu. Wakati huo, mawimbi ya ziwa Tanganyika yalinisomba hadi Kwenye kisiwa kidogo cha Lupita. Sikuelewa kabisa nilikotoka. Nilichokuwa nacho ni kipande cha mbao kilichochongwa kikiwa na jina 'Sheryl' mkononi mwangu. Sijui wazazi wangu ni akina nani, kama nina ndugu na dada zangu, na ninaishi wapi, sijui chochote.”
“Sawa, Sheryl. nitakuunga mkono.” Titus alishusha pumzi na kumkumbatia. Kwa kuwa alianguka kwa ajili yake mara ya kwanza, yeye pi alikuwa na lawama.
Muda mfupi baadaye, Mathew alimleta Lina. Akiwa njiani kuelekea huko, Lina alifadhaika, mwenye woga, na mwenye furaha kupita kiasi. Kamwe katika ndoto zake kali hakuwahi kufikiria kuwa mpango wake ungefanya kazi.
Nywele alizopata Mathew kwa kipimo cha DNA zilikuwa za Lisa. Kelvin alikuwa amekusanya nywele zote za Lisa ambazo zilianguka wakati wote wa kukaa kwake na kumpatia Lina. Lina aliziacha kwa makusudi nywele za Lisa kwenye sega yake na sakafu ya hoteli. Wafanyakazi wa hoteli walikuwa wamechukua nywele za Lisa wakati Lina hayupo.
Kwa hiyo. Lina angekuwa binti wa tajiri mkubwa wa Lubumbashi na vile vile dada wa mmiliki wa baadaye wa familia tajiri ya Tshombe. Kufikia wakati huo, kuwaangamiza Alvin na Lisa kungekuwa rahisi kama kukandamiza chungu. Alitumaini tu kwamba kumbukumbu ya Sheryl isingerudi kamwe.
Mathew alimpeleka kwenye chateau (kwa maana ya jumba la kifahari kama wanavyoita huko Ufaransa). Baada ya muda mfupi, wenzi wa ndoa walishuka ngazi.
Lina alikuwa amemwona Sheryl kwenye picha ya familia ya Jones. Alipokutana na Sheryl ana kwa ana ndipo alipogundua kuwa alionekana bora zaidi katika maisha halisi. Sheryl alionekana mtu mzima na mwenye haiba. Kama waridi linalochanua, alionekana maridadi na mtukufu.
Baada ya kupigwa na butwaa, mara Lina aliita. “Mama...”
Uso wa Mathew ulibadilika kidogo, huku Sheryl akimtazama Lina kwa mshangao. “Umejuaje kuwa mimi ni mama yako?”
"Nimekuona kwenye picha ya Bibi." Lina alianza kuigiza. "Kuna kitu kilikutokea mara tu baada ya kunizaa."
"Nini kilitokea?" Sheryl aliuliza kwa upole, lakini macho yake yakawa makali bila mtu yeyote kugundua.
Kwa hadhi na cheo alichokuwa nacho, ilimbidi awe macho sasa wakati binti ambaye alionekana kuibuka ghafla alidai yeye ni mama yake.
"Ulifagiliwa na kimbunga." Lina aliuma mdomo wake. "Nilikuwa mdogo sana zamani, kwa hivyo sina uhakika sana. Nilipata tu kujua kuhusu tukio hilo wakati Bibi alipolitaja katika dakika zake za mwisho miaka michache iliyopita. Alisema kuwa ghafla ulielekea Kigoma baada ya kupigiwa simu. Wakati huo, kulikuwa na kimbunga na ulipotea baada ya hapo. Polisi walisema huenda kimbunga hicho kilikusomba ziwani na hukunusurika..”
Kifua cha Sherly kilikuwa kigumu. Alikuwa ameokolewa kutoka ziwani. Mbali na mmiliki wa kisiwa hicho na wasiri wake wachache, hakuna mtu mwingine aliyefahamu kuhusu tukio hilo. Sasa wale washika siri walikuwa wameshafariki, ni Titus na Mathew pekee ndio walijua hilo.

"Kwa hiyo mama yangu tayari amekufa?" Sherly alichanganyikiwa, na moyo wake ulimuuma.
"Siyo tu kwamba Bibi amekufa, lakini babu pia ameaga dunia kwa muda mrefu. Tayari walikuwa katika miaka ya 80.” Lina akahema kwa macho mekundu. “Pia una kaka mkubwa anayeitwa John Jones, na Mjomba alinitendea vizuri sana.”
“Kweli?” Sura ya dhiki iliosha uso wa Sherly.
Licha ya kupoteza kumbukumbu, alikumbuka kwamba ni wazazi wake waliomlea tangu kuzaliwa. Alitakiwa kutimiza wajibu wake wa kimwana kwa wakati huo, lakini aliishia mahali pa mbali. “Kaka yangu anaendelea vizuri?”
"Hapana, yuko gerezani." Lina akahema.
Sheryl alipigwa na butwaa, Kisha, akafinya macho yake mazuri. "Nini kilitokea?"

"Ni jambo gumu sana." Lina akainua midomo yake. Baada ya kusitasita kwa muda, alisema, “Inahusiana na binti yake. Lo, hebu tuache. Mama, kwa kweli nilienda Kongo wakati huu kukutafuta. Sikuwa na uhakika kama bado ulikuwa hai. Lakini mwaka mmoja uliopita, nilikutana na mtu ambaye aliniambia kwamba aliona mtu fulani huko Lubumbashi ambaye anafanana nami. Nilidhani unaweza kuwa bado uko hai, kwa hivyo nilienda huko na kusudi. Nilijaribu tu bahati yangu, lakini sikutarajia...” Machozi yakamtiririka tena. “Sikujua ni jinsi gani ningeweza kukupata. Nilishinda siku tatu mfululizo kwenye kasino, nikitumaini kuvutia watu wa Lubumbashi. Labda ungenifahamu na kuona kufanana kwetu…”
“Inatosha. Ninaelewa kila kitu.” Sheryl alimwendea Lina na kumkumbatia kwa upole. Mashaka yake ya awali kuhusu Lina kwenda Kongo yalikuwa yametoweka kwa wakati huu. "Lazima umekuwa na wakati mgumu zaidi ya miaka, msichana wangu."
"Hapana, nina furaha zaidi kuweza kumuona mama yangu mzazi katika maisha yangu," Lina alisema huku akilia.
Titus aliyekuwa kando yao aliunganisha mawazo yake. Kisha akauliza kwa sauti ya baridi, yenye kina kirefu, “Ni mtu gani aliyekuambia kuhusu hilo? Anaonekanaje?"
Titus alikuwa mrefu na mwenye umbo la nguvu. Kwa hiyo, uwezo wake wa mamlaka mara moja ulimfanya Lina kuwa na wasiwasi na woga.
“Mimi... sina wazo pia. Alikuwa ameketi kando yangu katika kiti cha daraja la kwanza cha ndege.”

“Sawa, mume. Yeye ni binti yangu. Matokeo ya uchunguzi wa DNA hayawezi kuwa na makosa.” Sheryl alimpa Titus sura mbaya.
Titus alikoroma. "Amefanyiwa upasuaji wa plastiki hapo awali. ” Kwa macho yake makali, alitambua hilo mara ya kwanza. Alichukia wanawake ambao walikuwa wamefanyiwa upasuaji wa plastiki kwa vile walikuwa walaghai na wakaidi. Uso wa Lina haukuwa wa asili hata nusu kama wa Sheryl.
Kwa kuzingatia kwamba Titus alikuwa amempenda Sheryl, papo hapo, hakutakiwa kumchukia binti yake. Kwa sababu fulani, hata hivyo, alihisi bila kujua kwamba Lina hakuwa na sura aliyokuwa nayo Sheryl alipokuwa mdogo ingawa walikuwa na mfanano wa kawaida.
Uso wa Lina ulikuwa mgumu. "Sikuwa na nia ya kufanyiwa upasuaji wa plastiki. Niliwaudhi baadhi ya watu wenye nguvu huko Kenya miaka michache iliyopita, kwa hiyo sikuwa na budi ila kufanyiwa upasuaji wa plastiki ili kujificha. Hii ni picha yangu ya zamani."
Aliwasha simu yake na kutafuta picha ya zamani kabla ya kuwakabidhi.
Kwa bahati nzuri, alionekana zaidi kama John Jones Masawe. Muonekano wake wa zamani ulifanana kidogo na Lisa na Sheryl.......ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo, maana simulizi inazidi kuwa tamu kila siku lakini sina budi kuhitimisha kipande hiki ila niwasihi tukutane katika episode zijazo ili kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuelimisha unaokwenda kwa jina la LISA...