JINA LA SIMULIZI............................LISA

AUTHOR...........................JOMBA WAJO

SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY

WHATSAPP.........................0628924768

SEHEMU YA...............................126, 127


Sura ya 126


“Usifanye, usifanye.” Kwa kufikiria onyo la Alvin jana yake, Willie alimzuia Lisa mara moja. “Alikataa kuniruhusu nikuambie kuhusu hilo. Kwa kuzingatia kwamba nimeshiriki video zangu za faragha na wewe, tafadhali unaweza kujifanya kuwa hujui lolote, Bi Jones?”


Lisa alishangaa kusikia hivyo kutoka kwa Willie. Alvin alikuwa kweli mtoto wa familia tajiri ya Kimaro? Kwa kuwa Willie alikuwa akimheshimu na kumuogopa sana Alvin, inawezekana kwamba Alvin alikuwa na nguvu kubwa kuliko Willie? Inawezekana kuwa yeye ndiye mrithi wa familia ya Kmaro? Asingeweza kamwe kufikiria kuichokoza familia ya Kimaro. Familia ilikuwa ngumu sana kwa mtu wa kawaida kama yeye kufikiria.


“Sawa, nakuahidi, lakini naweza kujua Lina alikufahamu vipi?” Lisa aliuliza huku akijilazimisha kutulia.


"Ni Stephen ambaye alimtambulisha kwangu," Willie alidhihaki, "Msaidizi wangu anafahamiana na familia ya Kileo. Stephen alitaka kuanzisha uhusiano nami, kwa hiyo akamtuma mpenzi wake kwangu.”


Lisa alishangaa “Unafurahia kulala na rafiki wa kike wa rafiki yako?”


Willie alitoa kikohozi kidogo. “Kweli, mke si mtamu kama mchepuko. Inavutia zaidi kulala na mpenzi wa mtu mwingine.”


Lisa alikosa la kusema. Alikuwa na shauku kubwa ya kumuuliza ikiwa yeye ndiye pekee mwenye tabia mbovu katika familia nzima ya Kimaro au ikiwa kuna wengine wote walikuwa hivyo, ikiwemo Alvin, lakini hakufanya hivyo.


Baada ya kurudi ofisini, Lisa alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa. Hapo awali aliolewa na Alvin kwa kudhani kuwa alikuwa mjomba wa Ethan. Baadaye, aligundua kwamba alikosea na akafikiri kwamba Alvin alikuwa wakili tu. Nani alijua kuwa yeye alikuwa mtoto wa familia tajiri na maarufu zaidi nchini?


Naam, haikumshangaza. Badala yake, aliona kuwa ilikuwa na mantiki. Huenda Alvin alikuwa akimpima. Ikiwa angekutana na Alvin akajiweka wazi utambulisho wake, angehisi kwamba amempenda kwa ajili ya mali zake. Vilevile Alvin angempeleka kumtambulisha nyumbani kwao, familia yake labda isingemkubali.


Ghafla, alihisi kuchoka. Ili kujizuia kuwaza kupita kiasi, alibofya kipande kimojawapo cha video ambazo Willie alimtumia. Mwanzoni, alikuwa akijaribu tu kuangalia juujuu. Kinyume na matarajio yake, video hiyo iligeuka kuwa ya kufurahisha sana hivi kwamba Lisa ambaye alikuwa hajakomaa kama Lina aliguna.


Alipotambua kwamba alikuwa amezama katika video hiyo, Shani alimkumbusha hivi kwa uchungu, “Bi Jones, ulisema hutaitazama, sivyo? Zaidi ya hayo, Bwana Kimaro hatakuruhusu kutazama aina hii ya mambo.”


"Lo... Hatajua kama utatunza siri." Lisa alitoa tabasamu la aibu. Kwa kuwa Alvin asingemruhusu hata kutazama picha zisizofaa za Willie, bila shaka angemchuna akiwa hai iwapo angejua kuhusu jambo hili. Shani alishindwa cha kusema. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulifumbia macho.


Lisa alipokuwa akiitazama video hiyo, wazo zuri lilimjia. Alimwita msaidizi wake haraka. “Nakumbuka mjukuu wa Amiri alisema kwamba kuna mnada unakuja?”


“Ndiyo, ni usiku wa leo. Mratibu wa manada amekualika pia kwenye tukio. Watu wengi matajiri wa hapa Dar na mikoa mingine watahudhuria.”


“Sawa. Hata mimi nitaenda.” Lisa alicheka. Leo itakuwa siku ya giza zaidi katika maisha ya Lina.

•••

Hotelini Baada ya kutoka kwenye ofisi za Mawenzi Investments, Willie alikuwa tayari kufungasha vitu vyake na kuondoka Dar. Kukaa katika jiji moja na Alvin kulitisha maisha yake. Alipousukuma tu mlango wa chumba, alimuona mtu mrefu akiwa ameketi kwenye kochi la ngozi, akifanana na mfalme. Miguu yake iligeuka kuwa milegevu kama mlenda, na midomo yake iliendelea kutetemeka. “Kaka Alvin, umekuja kwa wakati ufaao. Nilikuwa karibu kukuambia kuwa nilienda Mawenzi Investments na kusuluhisha suala hilo. Hakuna mtu atakayethubutu kumsababishia Lisa matatizo tena.”


“Najua. Umefanya vizuri sana.” Alvin alikaa pale bila wasiwasi huku hisia za heshima kubwa zikitoka kwenye uso wake mzuri. Willie alijawa na furaha moyoni kusikia hivyo. Kabla hajaongea, midomo myembamba ya Alvin ilianza kusonga. "Lakini ... hakushuku chochote?"


Mara tu Alvin alipomaliza kuongea, hali ya wasiwasi na hofu ilitawala mazingira. Moyo wa Willie ulionekana kuganda.


“Usinidanganye, Willie,” Alvin alionya kwa upole, “unakumbuka kilichotokea ulipokuwa na umri wa miaka 18 baada ya kunidanganya, sivyo?”


Willie akatetemeka. Mwaka aliofikisha miaka 18 ulikuwa mwaka wake wa giza kuwahi kutokea.


"Yeye ... alishuku." Huku akitetemeka kama jani linalopigwa na upepo, Willie aliogopa sana kumficha. "Sasa anajua kwamba unatoka katika familia ya Kimaro, lakini sikumwambia makusudi kuhusu hilo. Yeye ndiye aliyenitega, na nilifanya makosa. Zaidi ya hayo, majina yetu ya mwisho ... "


Alvin akasugua macho yake. Alijua mapema kwamba Willie, mpuuzi yule kijana, angeshindwa kufanya kulingana na maagizo yake na kuishia kumuumbua zaidi.


Willie alisema kwa kigugumizi, “Kaka Alvin, una wasiwasi kwamba atajikombakomba kwako na kukusumbua baada ya kukujua wewe ni nani? Kwa kweli, hii ni kawaida sana kwetu. Haijalishi tunaenda wapi, wanawake wengi humiminika kwetu. Hata hivyo, hadhi yake ni ya chini sana kuwa mpenzi wako.


"Nyamaza." Macho makali ya Alvin yalimkumba. "Ondoka Dar mara moja."


“Sawa, sawa. naondoka sasa hivi kaka.” Willie pia hakujisikia kubaki mahali hapo pabaya palipomchachia. Mara moja akafungasha vitu vyake na kuondoka kama anayefukuzwa.


Alvin aliinuka na kuelekea kwenye dirisha lililokuwa ndani ya chumba hicho. Akili yake sasa ilikuwa imevurugika kabisa Alikuwa mtu mwenye shaka. Alipokuwa akiishi katika neema ya utajiri wa familia ya Kimaro tangu alipokuwa mdogo, wanawake wengi walikuwa wamemtumia kwa kisingizio cha kumpenda kwa sababu ya utambulisho wake, jambo ambalo lilimjaza chuki. Kwa hiyo, hakuwahi kumwambia Lisa kuhusu utambulisho wake halisi, akitumaini kwamba angempenda yeye kama yeye na si kwa utajiri wake. Hata hivyo hakuna marefu yasiyo na ncha. Hatimaye Lisa alikuwa amejua kuhusu utambulisho wake. Angemwonaje?


Hans alimwambia kwa upole, “Usijali, Bwana Kimaro. Lisa alikupenda tangu alipokutana nawe kwa mara ya kwanza kwenye baa. Wewe ndiye anakupenda, na haihusiani na utambulisho wako.”


"Hiyo ni sawa." Alvin alijisikia raha. Kweli, kwa nini alikuwa anafikiria kupita kiasi? Alikuwa ameanguka kwa ajili yake bila matumaini, kama yeye mwenye alivyosema.

•••

Saa kumi na moja jioni, gari jeusi lililoonekana kuwa la gharama kwa mwonekano wake lilikuwa limeegeshwa nje ya mlango wa jengo la Mawenzi Investments. Muda mfupi baadaye, Lisa alishuka kwenye gari huku yule aliyekuwa kwenye kiti cha dereva akivua koti lake. Alionekana akiwa amevalia shati jeupe chini ya fulana, ambayo ilisisitiza umbo lake refu. Akiwa na sura nzuri ya kuvutia, alitoka kama mhusika kutoka kwenye kitabu cha hadithi za kubuni.


Ingawa alimuona kila siku, sura yake ya kuvutia haikukosa kumshangaza. Hakika asngechoshwa na sura ya mwanaume huyo.

Alipojua kuhusu utambulisho wake siku hiyo, alikuwa akipingana na mawazo yake kila mara. Hata hivyo, wakati huo, alikuwa na hakika kwamba asingeweza kuvumilia kumwacha mwanamume huyo.

Siku zote alikuwa mtu ambaye alikaa karibu naye katika nyakati ngumu zaidi. Siku hiyo, alimsaidia kukabiliana na dhoruba tena. Haijalishi jinsi gani safari yao ya mbele ingekuwa ngumu, alisisitiza kuwa pamoja naye.


“Mbona unanitazama?” Alvin alibana ncha ya pua yake, alikuwaakijshtukia.


Lisa aliitazama saa iliyokuwa kwenye mkono wake, jambo ambalo lilimkumbusha jinsi alivyokuwa akimshangaa kwa aina ya nguo zake. Ikamjia akilini kwamba huenda nguo hizo zilikuwa zikificha utambulisho wa Alvin kwa makusudi.


“Ninautazama uso wako mzuri. Pia, niko katika hali nzuri leo. Uliona jinsi Jones na Lina walivyofedheheka? Lina siku zote alijifanya kuwa safi na aliishi kwa unafiki wakati huo. Sasa, kila mtu anamdharau.”


“Ndiyo.” Baada ya kumsikia akipiga kelele, Alvin aliinua macho yake na kuuliza, "Kuna chochote unachotaka kuniuliza?"


Sura ya 127


Lisa alipigwa na butwaa. Alikuwa amepanga kumuuliza Alvin kuhusu utambulisho wake halisi. Hata hivyo, uhakika wa kwamba alimwomba Willie afiche utambulisho wake ulionyesha kwamba hakutaka kumfunulia. Katika hali hiyo, hakujisumbua kumuuliza.


"Hapana." Alvin taratibu akadondosha macho yake. Lisa alimtazama wakati huo na kusema, “Nitahudhuria mnada usiku wa leo, kwa hivyo sitakuwa nyumbani kwa chakula cha jioni. Unataka… kwenda pamoja nami?” Aliuliza kwa tahadhari ingawa alihisi kwamba Alvin asingekubali kwenda pamoja naye. Kwa kuzingatia tabia yake ya kiburi na dharau, asingependezwa na tukio la aina hiyo.


“Sawa.” Alvin akakubali.


“Huu?” Lisa aliduwaa, akifikiri kwamba alimsikia vibaya.


“Nimesema sawa. Mbona unashangaa?” Alvin alitazama sura yake iliyopigwa na tabasamu.


"Lakini hupendi kushiriki katika hafla zinazofanyika Dar se salaam, leo imekueje?"


"Ninakuja ili kuzuia wanaume wowote wasikucheze." Alvin alijibaraguza. Aliendesha gari kwa umakini huku macho yake yakiwa yametazama barabara iliyo mbele. Lisa aligeuza kichwa chake na kutazama wasifu wake kamili kwa muda. Hakuweza kujizuia kumpa busu la shavuni. Usukani uliokuwa mikononi mwake ulitetemeka, kisha akamwambia kwa utani, “Usinichezee kimapenzi ninapoendesha gari.”


Sentensi hiyo ilionekana kuwa ya kawaida. Lisa alicheka na kujibu, “Najua. Itasababisha ajali mbaya sana, si ndiyo?"


"Hapana." Akamtazama. "Itasababisha moyo wangu kuruka."


Mapigo ya moyo wa Lisa yakagongana na kifua. Hali isiyoeleweka ilionekana kujaa kwenye mishipa ya mwili wake mzima. Moyo ulimwenda mbio zaidi baada ya kumbusu. Wakati huo, alikuwa na hamu kubwa ya kumbusu kwa mapenzi. Hata hivyo, alitilia maanani zaidi usalama barabarani.


Saa moja na nusu usiku, Mnada ulikuwa karibu kuanza katika jumba la mikutano la Karimjee. Watu mashuhuri kutoka Dar es Salaam na mikoa jirani waliingia ukumbini mmoja baada ya mwingine. Kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, Lisa alionekana kuwa kivutio cha tukio hilo. Umati ulimsonga mara tu alipoingia ndani.


Ethan naye alikuwepo. Alivyoona jinsi Lisa anafuatwa sana na watu kwa mbali, Ethan alijawa na uchungu. Kamwe katika ndoto zake hakutarajia kuwa mpenzi wake ambaye awali alimwacha kwa ajili ya Lina angekuwa mwenyekiti mpya wa Mawenzi Investments ndani ya muda mfupi. Wakati huo watu wengi walimwona mpumbavu. Kwa kweli, Ethan alikuwa mpumbavu. Alimkosea kipumbavu sana Lisa na kwa hivyo akakosa nafasi ya kuwa naye. Akiwa na mwanamume bora kando yake sasa, aliona kwamba asingekuwa na nafasi yoyote kwake.


Mchumba wake mpya, Tracy Laizer, alikuwa ameketi kando yake na kuubana mkono wake. "Nilisikia kwamba yeye ni mpenzi wako wa zamani, ni kweli?"


'Yote ni ya zamani." Ethan alilazimisha tabasamu. Alijua kwamba angeweza tu kufanya kazi kwa bidii ili kuifurahisha familia ya Laizer kwa sasa.


“Ni vizuri kwamba unajua. Maadamu unanipenda sana, familia yangu itakutegemeza,” Tracy alisema kwa upole.


Upande mwingine, Lisa naye alimwona Ethan pia kwa sababu ya suti yake nyeupe iliyovutia. Mwanamke wa ajabu kutoka familia mashuhuri alisimama kando yake. Moyoni mwake, Lisa alihema huku akimfikiria mwanaume ambaye aliyemuona kuwa mkamilifu wakati ule. Kinyume na matarajio yake yote, mwanamume huyo aligeuka kuwa mtu ambaye angemsaliti kwa ajili ya mamlaka na umaarufu.


“Unamtazama Ethan?” Ghafla sauti ya Alvin ya kuonya ilisikika.


"Nilikuwa nikifikiria juu ya jambo fulani."


“Ulikuwa unafikiria nini?” Alvin alikasirika.


"Yajayo yanafurahisha. Onyesho nzuri inakuja. Utajua baada ya muda mfupi.” Lisa aliinua uso wake, macho yake angavu yaking'aa kwa ucheshi. Uso wa Alvin ukalegea taratibu.


Wanawake kadhaa ambao waliolewa na wafanyabiashara matajiri walimzunguka Lisa na kumpongeza.


“Mwenyekiti Jones, hili gauni umenunua wapi? Ni nzuri!"


"Mkufu uliovaa umetoka kwa Tiffany na ndio muundo mpya zaidi, sivyo?"


"Habari za jioni, the bosy lady?"


Ghafla Janet alishika glasi ya mvinyo mwekundu na kumsogelea Lisa kwa nia mbaya. “Ah, Mwenyekiti Jones, sikutarajia kwamba ungekuwa na jeuri ya kushiriki katika mnada. Subiri kidogo, sina uhakika kama bado nitakuita Mwenyekiti Jones sasa hivi.”


"Unamaanisha nini, Bi Kileo?" mmoja wa wanawake hao, Madam Clark, aliuliza huku akihema.


Janet akahema. “Pengine ninyi nyote hamfahamu kilichotokea. Nilisikia kwamba Mwenyekiti Jones alimpiga Willie Kimaro aliyetoka Nairobi wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya Mawenzi Investments jana usiku.”


"Nini? Unamaanisha huyo Willie kutoka familia ya Kimaro?"


"Ndio, ni yeye." Janet akaitikia kwa kichwa. “Rafiki yangu aliniambia kwamba Mwenyekiti Jones alisababisha uso wa Bwana Kimaro kuvimba, na Bwana Kimaro alikasirika sana. Sijui hata atafanya nini! Hiyo ilikuwa ni sawa na kujitakia matatizo makubwa sana kwako, Mwenyekiti Jones. Hivi mtu kama wewe unawezaje kuichokoza familia ya Kimaro? Natumai utakuwa uko salama na unaendelea vizuri nitakapokuona tena.”


Wanawake wote walishtuka na kurudi nyuma mmoja baada ya mwingine.


"Halo, mume wangu ananiita."


"Imekuwa muda tangu tulipokutana mara ya mwisho, Madam Ngololo."


Muda mfupi baadaye, kundi la wanawake lilitoa visingizio na kuondoka mahali hapo mara moja. Hawakuwa tayari kukaribiana na mtu aliyeiudhi familia ya Kimaro. Tukio hilo halikuwa la mzaha. Walijua kuwa kwa kuwa Lisa alikuwa ameichokoza familia ya Kimaro, alikuwa amejihukumu kifo. Ingekuwa haina maana kumsogelea.


Bila kujisumbua kuliweka wazi jambo hilo, Lisa alimkazia macho Janet kana kwamba ni mlemavu wa akili. Ikizingatiwa kuwa alikuwa na uhusiano wa kirafiki na Lina, kwa nini Lina hakumwambia ukweli?


"Lazima uwe na hofu, sawa? Pengine hukutarajia kwamba utapoteza nafasi ya mwenyekiti wakati ndio kwanza umeanza kuifurahia.” Janet alitabasamu kwa kuridhika kisha akageuka kumtazama Alvin. "Bwana. Kimaro, nakushauri ujiepushe naye ili usije ukaingizwa kwenye matatizo haya.”


Alvin alimwangalia tu bila kujali alichosema. Janet alifikiri kwamba maneno yake yalikuwa yameamsha kupendezwa kwake, hivyo mara moja akasema, “Msaidizi mkuu wa Willie ni jamaa yangu. Ukija na kuniomba msaada, hakika nitakuunganisha naye.”


Kwa namna fulani, Lisa alihisi kucheka. Hata Willie alimuogopa sana Alvin. Kwa wazi, msaidizi maskini asingekuwa na maana yoyote kwake.


“Alvlisa, mpuuze tu huyu kichaa. Hebu tutafute nafasi tukae.” Alisonga mbele huku akimshika mkono Alvin. Hakuwa hata na muda wa kupoteza kumwambia Janet ukweli.


Akiwatazama wanaondoka, Janet alicheka nyuma yao. Aliweza kuwa ameridhika kwa muda huo, lakini kile ambacho kingefuata kingemwacha akilia baadaye.


Mara baada ya kuketi, Alvin alimtazama mwanamke aliyekuwa kando yake kwa namna ya kinyonge. “Kwanini usingelifafanua sasa hivi hilo jambo lako? Au lina uhusiano wowote na madai yako kwamba yajayo yanafurahisha?”


"Unanielewa vizuri, Alvilisa." Lisa alitabasamu.


Alvin aligundua kuwa tangu Lisa awe mwenyekiti, alikuwa na ujuzi zaidi wa kucheza na wengine. Baada ya kusema hivyo, halikuwa jambo baya hata kidogo. Ilibidi awe mwovu na mkatili zaidi ili ahitimu kuwa mke wake katika siku za mbeleni.


Mnada ulianza muda mfupi baadaye. Kwa kweli, mnada wa usiku huo ulikuwa tukio la kuchangisha harambee fulani. Lisa aliinua kadi yake ya zabuni kwa picha mbili za uchoraji zenye thamani ya shilingi milioni kadhaa. Bidhaa ya mwisho ilikuwa 'Mkufu wa Malkia'.


Ulikuwa ni mkufu unaometa na kishaufu cha almasi ya rubi inayong'aa ukiwa umeketi juu ya satin nyeusi. Mkufu huo uliundwa kwa ustadi. Hata mnyororo huo ulipambwa kwa almasi ndogo, ambayo ilifanana na safu ya nyota.

Wanawake wote walishangaa kuuona ule mkufu, na pia ulikuwa umemvutia Lisa.


Alvin alimtazama Lisa kwa macho ya kina. Kwa wakati huo, mwendesha mnada alianzisha kwa shauku, "Sasa ni wakati wa kuvutia zaidi. Hapo awali, mfalme wa zamani wa nchi fulani alipata mbunifu mzuri zaidi wa kuunda mkufu, na ilimchukua miaka miwili kuukamilisha. Kito hiki kina karati 383.4 za almasi. Kuna uvumi kwamba ikiwa mtu atampa mwanamke wake mpendwa Mkufu huu wa Malkia, watakuwa pamoja milele. Huu ndio mkufu ambao kila mwanamke anauota. Zabuni ya kuanzia kwa bidhaa hii usiku wa leo ni shilingi bilioni 1.6.”


Bei hiyo ya ajabu ilizua taharuki ukumbini. Hata hivyo, upesi mtu fulani akapaza sauti na kusema, “bilioni 1.7.”


Kwa udadisi, Lisa alitazama upande ule, na kugundua kuwa alikuwa ni Ethan.....ITAENDELEA...

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.